Kujua tunataka ndio maana tunadadisi... lakini majibu tunayopewa ndio yanapelekea tusiyaelewa... (jambo lenye kueleweka halihitaji nguvu kubwa).
Ndio maana hauwezi kumuelezea mtoto mdogo maumivu yakoje kama hajawahi-experience hiyo hali... huenda suala la Mungu lipo kwenye personal experience ya mtu mmoja mmoja hivyo linakosa sifa ya kuwa compulsory kwa kila binadamu...
Manake tukiliweka kwenye elimu ndio linafeli vibaya kabisa... kwasababu binadamu anakuwa na uelewa zaidi na jambo analokuwa na interest nalo... kila ambacho ni compulsory kwa binadamu kinafanyika bila kuhitaji mahubiri... Tatizo langu kubwa na God believer ni kitendo cha kuwaambia hata wale wanaokanusha uwepo wa Mungu kwamba wanatenda makosa hivyo wataadhibiwa na huyo Mungu kwa kufanya hivyo... kwa mtazamo wangu Mungu huyo kama yupo basi atakuwa wa ajabu kuliko hata binadamu mwenyewe.
Kwa maoni yangu Mungu wa kwenye biblia na wa kwenye quran... sijawahi kumuelewa... kama yupo tuna haki zote za kumuwajibisha.
Sent using
Jamii Forums mobile app