Acha hasira za kitoto wewe, umwombe Mungu akusamehe dhambi zako, kisha akurehemu upate mume, unapoomba uwe unataja mistari ktk Biblia.
Mungu huwa anapenda kuombwa kwa ushahidi, kuhusu kuomba rehema soma Kutoka 34:7 na Zaburi 78:38.Kuhusu kuvunja falme za giza zinazokuzuia kuolewa, soma Amosi 9:1-4.na Yeremia 51:20-24.
Ukiingia kwenye maombi hakikisha unatamka mistari hiyo, Mungu haombwi kwa mazoea kama binadamu, na usiombe maombi ya kiroma hayana upako wa Mungu.
Tafuta watumishi wa Mungu wakufundishe kuomba ila wasiwe waroma hao hawajui kumwomba Mungu, na pia uache dhambi maana maombi ya mwenye dhambi ni kelele mbele za Mungu.