Sijui ni kivipi mtu anapofika kwenye level fulani ya maisha hutaka kuilazimisha akili yake kuwa na wengine wote wako kama yeye
Badala ya kurudisha akili zake kule alikotoka ili ayapime maisha aliyopitia na hatimaye aone pia wale ambao bado wako huko wanapitia ugumu uleule aliowahi kuupitia yeye kabla hajafika hapo alipo, hata akichaguliwa/bahatika kuwa katika nafasi Fulani ya uongozi, Aumize kichwa chake jinsi ya kuisaidia jamii masikini,
Kusaidia Jamii kama kiongozi, hauhitaji utoe pesa mfukoni mwako
Ni kuweka sera wezeshi ambazo zitaifanya jamii hii masikini kufikia uwalau maisha ya kufurahia uwepo wao hapa duniani
Jamii yetu bado masikini sana, bahati mbaya kabisa, tunao baadhi ya viongozi ambao tangu kuzaliwa hawaijui shida, na ndiyo maana imekuwa ni rahisi kwa viongozi kama hao kupiga makofi kwenye mijadara mingine inayoumiza walala hoi, Lakini Kuzaliwa kwetu katika jamii ambayo haikuwahi kuona shida, isitufanye kutotambua kwamba masikini wa masikini wapo, na shida zipo
Kinacho kwenda kufanyika sasa kwenye sera ya makato ya miamala ya simu, ni kwenda kuzidisha ukali wa maisha kwa jamii kubwa ya watu wa maisha ya chini na kuathiri uchumi wao mdogo unaotegemea jasho jingi ili mtu apate mlo wa siku
Naishauri serikali, Kwa sababu tunajamii kubwa ambayo inaishi kwa kutegemea maisha ya kubangaiza, na kwa sababu tozo hiyo ya miamala na laini ya simu ni mpango wa serikari ipate kodi ili kuendeleza miradi na ujenzi wa barabara vijini
Badala ya kodi hiyo kuingizwa kwenye huduma hizi mhimu na kuifanya huduma hii iwe na makato makubwa kiasi cha kufanya wazee wetu kule vijini wakose msaada kutoka kwa vijana wao wanaowatumia vijisenti vya kujipatia mahitaji yao
Kodi hii ihamishiwe upande wa abiria wanaosafiri kwa mabasi kwenda mikoani, usafiri wa Treni, meli, na ndege, na kodi yake iwe ni kila abilia atakatwa kodi ya sh 1,000 tu kwa kila abiria anayetumia usafiri wa basi kwenda mkoani,
Serikali itafute namna ya kulipa hiyo kodi, ni au iunganishwe kwenye tiketi, msafiri badala ya kulipa 10,000 alie 11000,
Itawaokoa wengi ambao hata hawajui ni lini watapanda basi, ndege, meli wala treni kwa maana hawana huo uwezo, lakini wanasimu na hawapigi simu wao, zaidi husubiri wapigiwe tu na kutumiwa pesa kidogo
Badala ya kurudisha akili zake kule alikotoka ili ayapime maisha aliyopitia na hatimaye aone pia wale ambao bado wako huko wanapitia ugumu uleule aliowahi kuupitia yeye kabla hajafika hapo alipo, hata akichaguliwa/bahatika kuwa katika nafasi Fulani ya uongozi, Aumize kichwa chake jinsi ya kuisaidia jamii masikini,
Kusaidia Jamii kama kiongozi, hauhitaji utoe pesa mfukoni mwako
Ni kuweka sera wezeshi ambazo zitaifanya jamii hii masikini kufikia uwalau maisha ya kufurahia uwepo wao hapa duniani
Jamii yetu bado masikini sana, bahati mbaya kabisa, tunao baadhi ya viongozi ambao tangu kuzaliwa hawaijui shida, na ndiyo maana imekuwa ni rahisi kwa viongozi kama hao kupiga makofi kwenye mijadara mingine inayoumiza walala hoi, Lakini Kuzaliwa kwetu katika jamii ambayo haikuwahi kuona shida, isitufanye kutotambua kwamba masikini wa masikini wapo, na shida zipo
Kinacho kwenda kufanyika sasa kwenye sera ya makato ya miamala ya simu, ni kwenda kuzidisha ukali wa maisha kwa jamii kubwa ya watu wa maisha ya chini na kuathiri uchumi wao mdogo unaotegemea jasho jingi ili mtu apate mlo wa siku
Naishauri serikali, Kwa sababu tunajamii kubwa ambayo inaishi kwa kutegemea maisha ya kubangaiza, na kwa sababu tozo hiyo ya miamala na laini ya simu ni mpango wa serikari ipate kodi ili kuendeleza miradi na ujenzi wa barabara vijini
Badala ya kodi hiyo kuingizwa kwenye huduma hizi mhimu na kuifanya huduma hii iwe na makato makubwa kiasi cha kufanya wazee wetu kule vijini wakose msaada kutoka kwa vijana wao wanaowatumia vijisenti vya kujipatia mahitaji yao
Kodi hii ihamishiwe upande wa abiria wanaosafiri kwa mabasi kwenda mikoani, usafiri wa Treni, meli, na ndege, na kodi yake iwe ni kila abilia atakatwa kodi ya sh 1,000 tu kwa kila abiria anayetumia usafiri wa basi kwenda mkoani,
Serikali itafute namna ya kulipa hiyo kodi, ni au iunganishwe kwenye tiketi, msafiri badala ya kulipa 10,000 alie 11000,
Itawaokoa wengi ambao hata hawajui ni lini watapanda basi, ndege, meli wala treni kwa maana hawana huo uwezo, lakini wanasimu na hawapigi simu wao, zaidi husubiri wapigiwe tu na kutumiwa pesa kidogo