Nimekuta mmoja wa wafuasi Lowassa, ambaye toka jana amekua akilalamika kupambana, Ally Bananga, amebandika maneno haya katika kundi la Tanuri la Fikra ndani ya Facebok;
"Ally Bananga Mwatiga5:29pm Nov 21
eti wanataka kuivunja UVCCM, tumewakosea nn?"
Taarifa zinasema huenda Jumuiya hiyo na nyingine zikavunjwa kwa muda. Hiyo ni wakati sasa hali ikiendelea kufukuta mjini Dodoma ambako mabilioni ya fedha yamemwagwa kwa wajumbe wa NEC kuhakikisha kila azimio linapigiwa kura ili azimio la kuvua gamba lipingwe.
Tayari waraka wa mmoja wa wajumbe wa Kamati Kuu uliokua na mambo mengi mazuri ulishaingia dosari kwa kuchomeka hoja ya kuwasamehe mafisadi kwa lengo la "kunusuru chama"... Mwenyekiti akapinga kwa kusema, "chama kitanusurikaje kwa kulinda uvundo?" Sasa kazi ipo. Magamba yanazidi kuwaka moto, hadi yatapasuka.