Kimenuka Dodoma, magamba yapata moto

Kimenuka Dodoma, magamba yapata moto

Hivi EL akingolewa CCM ndo kitakuwa chama bora? Kitaacha kutuburuta kwenye katiba? Kitaacha Kulea Uzembe? Serikali yake itaacha Ubabe?
 
Hajui kuwa waziri mkuu ndio ana mamlaka na serikali za mitaa Tanzania nzima. Hii ndo tatizo la ku discuss siasa na wasioelewa siasa
 
Naona wafuasi wa mafisadi presha inapanda, presha inashuka. Mmenusa nini huko? Maana naona mnajitahidi kutoa povu mdomoni na kujitoa akili kumtetea ENL.

Hivi kweli mnataka kusema kwa dhati ya nafsi yenu hamjui ufisadi wa ENL. Mnataka kusema hata Mwalimu Nyerere alikua anamuonea wivu au anautaka Urais baada ya kuwa kastaafu kwa hiari yake. Hebu acheni uvivu, fuatilieni humuhumu kuna thread zinamchambua madudu ya kila wizara aliyowahi kupewa na kote huko ameacha footprints za ufisadi, kuanzia kipindi yuko ofisi ya waziri mkuu-maafa, ardhi, maji na maendeleo ya mifugo, uwaziri mkuu ndo ikatokea the straw that broke the camels back.

Acheni ujuha kwenye masuala ya msingi ya taifa. Rwanda wanapaa sababu ya zero tolerance kwa corruption halafu hapa anakuja mtu kumpigia debe fisadi mchafu!!! Kisa nawewe umeahidiwa kijipost akiula, na bila aibu unakuja na disclaimer kuuubwa baada ya kujistukia unajitia ujuha kwenye kadamnasi.
 
CCM YA WASANII HAKUNA JIPYA, ZAIDI YA USANII..!

cku hizi sio enzi za CCM ya Hayati Mwalimu....,
enzi hizo ndiyo tungeweza kujua litatokea nn hasa pale wanapokuwepo wanachama ambao co waadilifu,na wamefanya makosa yanayoligharimu Taifa na Utu wake....,

Cku hizi kuanzia CCM ni ya usanii, makada na viongozi wake ni wasanii, Govt nzima ni ya wasaniii...., wabunge wa CCM ni wasanii pia...! je tunategemea nn toka katika Jumba la wasaniii zaidi wa Maigizo, ngonjera, utunzi nk...
Just wishing wangekuwa wanacheza sarakasi pia, maana mchezo wa sarakasi wahitaji ujasiri na ukomavu wa kimwili na kiakili...! mtu goi goi asiye weza kufikiri awezi cheza sarakasi...!

Ukiangia usanii unavyoiharibu nchi yetu nzuri, hata Joti na kundi lao ze Comedy wakipata nafasi ya kukaa ikulu wataweza tuu kuiongoza govt ya CCM! maana waliopo ikulu, hakuna tofauti yeyote na wakina Joti na wenzie..!

Hapa Dodoma hakutakuwa na jipya na uongozi wa kisaniii, ni yale yale tuu, hakutakuwa na jipya!
nilitegemea alipokuwa anawahutubia wazee wa CCM Dar, atleast angetoa mwelekeo ktk mazungumzo yake, yatakoyojiri Dodoma toka juzi, but wapi???
toka 2005 hakuna aliye seroius na umaskini wa Tanzania na wananchi wake...,

Kucheka kucheka na maneno ya mtaani toka 2005, hayataleta mabadiliko ya kiuchumi na kisiasa ndani ya CCM yao na Taifa kwa ujumla...!

 
Naona wafuasi wa mafisadi presha inapanda, presha inashuka. Mmenusa nini huko? Maana naona mnajitahidi kutoa povu mdomoni na kujitoa akili kumtetea ENL.

Hivi kweli mnataka kusema kwa dhati ya nafsi yenu hamjui ufisadi wa ENL. Mnataka kusema hata Mwalimu Nyerere alikua anamuonea wivu au anautaka Urais baada ya kuwa kastaafu kwa hiari yake. Hebu acheni uvivu, fuatilieni humuhumu kuna thread zinamchambua madudu ya kila wizara aliyowahi kupewa na kote huko ameacha footprints za ufisadi, kuanzia kipindi yuko ofisi ya waziri mkuu-maafa, ardhi, maji na maendeleo ya mifugo, uwaziri mkuu ndo ikatokea the straw that broke the camels back.

Acheni ujuha kwenye masuala ya msingi ya taifa. Rwanda wanapaa sababu ya zeto tolerance kwa corruption halafu hapa anakuja mtu kumpigia debe fisadi mchafu!!! Kisa nawewe umeahidiwa kijipost akiula, na bila aibu unakuja na disclaimer kuuubwa baada ya kujistukia unajitia ujuha kwenye kadamnasi.

Toa point. UFISADI wa Lowassa ni nini? lete evidence.

Mwalimu kasema, shehe Yahaya Kasema Mfaume kasema (all RIP) au Sitta kasema haitosaidia. Who are they anyway? Saints, Angels?

Tupe evidence acha blah blah. Nikisema wewe ni Mwizi kwa kua hapo unapofundishia unaiba vitabu inakufanya uwe Mwizi?. Lazima niwe na EVIDENCE.

Acheni kucheza ngoma ya watu msioijua.
 
Lowasa aliponzwa na uchapakazi wake, katika sakata la richmond, aliingizwa kwa sababu ya Memo aliyomunadikia msabaha akimtaka awaulize richmond juu ya uwezo wao wa kuleta umeme, alikuwa waziri mkuu na alikuwa anahakikisha kuwa umeme unapatikana. Tunakumbuka akiwa waziri mkuu baada ya clouds kutangaza mashimo ya bara bara ya Shekilango alikwenda pale na kuagiza barabara ijengwe na ilijengwa. Akiwa waziri mkuu aliagiza vibanda vyote vilivyokuwa mjini Posta na kariakoo vivunjwe na vilivunjwa mji ukawa safi. Akiwa Premear aliguswa na suala la foleni na alianza kulifanyia kazi kwa kujaribu njia tatu, Akiwa Premier Lowasa alikuwa naogopwa na wakurugenzi wa halmashauri na wizi ulipungua sana,need I say more?

Hajui kuwa waziri mkuu ndio ana mamlaka na serikali za mitaa Tanzania nzima. Hii ndo tatizo la ku discuss siasa na wasioelewa siasa

Sasa mbona hizo kazi zingefanywa na mkurugenzi wa halmashauri tu? Kwanini waziri mkuu aende kusimamia ufukiaji wa mashimo ya barabara? Kwanini waziri mkuu aagize suala la njia tatu? Je, maagizo na kuogopwa kwake na wakurugenzi kulileta tija gani kwa taifa? Hizo njia tatu zilipunguza foleni? Je, hayo mashimo ya Shekilango leo hayapo?

Lowassa kutokana na mipango yake ya kutaka kuwa rais, alikua anajaribu kuonekana mchapakazi kwa kufanya yale ambayo hakupaswa kuyafanya kama waziri mkuu; alipenda kucheza na jukwaa kama Mrisho Ngasa, badala ya kuhakikisha anaichezesha timu yake vizuri ili timu ipate ushindi!!
 
Toa point. UFISADI wa Lowassa ni nini? lete evidence.
Mwalimu kasema, shehe Yahaya Kasema Mfaume kasema (all RIP) au Sitta kasema haitosaidia. Who are they anyway? Saints, Angels?
Tupe evidence acha blah blah. Nikisema wewe ni Mwizi kwa kua hapo unapofundishia unaiba vitabu inakufanya uwe Mwizi?. Lazima niwe na EVIDENCE.
Acheni kucheza ngoma ya watu msioijua.

Hafai kuwa kiongozi mkubwa wa nchi hii kwani ameshakuwepo toka zamani na hakuna alilolifanya na kumfanya awe na moral authority ya kuomba kura kwa watanzania wa sasa!! Nimekuuliza nipe mifano ya uchapakazi na utendaji wake mzuri toka awe waziri enzi zile hadi uwaziri mkuu juzi juzi.
 
Kuna taarifa kwamba, vikao vya awali vya CCM mjini Dodoma vimeanza kwa kuwahoji vijana kadhaa wa UVCCM wanaotajwa kuwa karibu na Watuhumiwa wa ufisadi walotakiwa kujivua gamba.

Haijafahamika kama vijana hao watakua kafara la baba zao ama ndio kipima joto cha maamuzi magumu yanayotarajiwa kufanywa wiki hii. Hakika mwandishi mahiri wa makala katika Raia Mwema alisema, "mbele giza nyuma kaburi" na sasa uamuzi wa kurudi nyuma ni CCM kuingia kaburini na kwenda mbele ni gizani maana magamba yana nguvu za ajabu na kila kukicha yanakua magumu.

Je, CCM itaamua kuingia gizani kuvua magamba ama kurudi nyuma na kuyaacha iwe ni kaburi la CCM?

Taarifa zaidi baadae.

attachment.php
Mbona sehemu aliyokaa Kikwete inaonekana mtu ametoka!!!!!!!!????
 
Toa point. UFISADI wa Lowassa ni nini? lete evidence.

Mwalimu kasema, shehe Yahaya Kasema Mfaume kasema (all RIP) au Sitta kasema haitosaidia. Who are they anyway? Saints, Angels?

Tupe evidence acha blah blah. Nikisema wewe ni Mwizi kwa kua hapo unapofundishia unaiba vitabu inakufanya uwe Mwizi?. Lazima niwe na EVIDENCE.

Acheni kucheza ngoma ya watu msioijua.

Mimi ninasimamia nilichokisema ENL ni FISADI Period.

Hapa kwenye Jukwaa la Siasa kuna topics 26,082. Huyu unayempenda unconditionally nakuhakikishia ameshajadiliwa na kwa ushahidi wa kutosha tu. Upo ushahidi wa kinyaraka ziliwekwa humu, upo ushahidi wa kimazingira na upo ushahidi wa simulizi za first hand wazee wanaoheshimika. Kama kweli uko passionate na huo utetezi mfu wako, take time peruse topics zote NINAHAKIKA utakutana na hizo evidence.

Sasa kama wewe kutokana na mapenzi yako hayo utataka ushahidi wa kukuta kitu kimezama kwa mkeo wakati watu wamekupa all the evidence ya kwamba kuna jamaa anakumegea mkeo, hiyo ni hiari yako.

After all ukipenda hata chongo utaliita kengeza.
 
Mbona Mwalimu aliwahi kutuambia Mkapa ni Mr Clean, does that hold now?
 
Mbona Mwalimu aliwahi kutuambia Mkapa ni Mr Clean, does that hold now?

Mpaka Mwalimu anafariki dunia YES ilikua ina still hold. Huwezi kujudge statements retrospectively. Pale alipokua anatoa huo ushuhuda ni kweli Mkapa alikua CLEAN, yaliyotoeka baada ya yeye kufariki si sawasawa kuhusisha na kauli ya kumsafisha Mkapa 1995' tusipotoshane kwa vile mnataka kumsafisha Fisadi. Mwalimu alishampa a big NO, mnatwanga maji kwenye kinu tu.
 
Ha ha ha!Why Chenge doesn't clap for the chairman?Anaonekana anayo Gazabu...
d26.jpg


Nape vipi??Magamba yanavuka hayavuki?
d18.jpg


Awkward position?Kikao hiki ni cha watu nane?Kwa haraa niliowatambuwa ni EL,Pinda,JK,Msekwa,Makinda,Makamu wa Rais,Msekwa,mwingine sijamtambua,hata hivyo ni kikao cha watu nane hapo chini...
d14.jpg

Picha:Kwa hisani ya Haki Ngowi.
Mbona Nape na Chenge hawana furaha????
 
Ndugu yangu Halisi,

Tumeshajadiliana sana kuhusu EL. Mie kila ninapokuona una comment kuhusu EL huwa najiuliza. EL kafanya UFISADI upi?. Tupeni ushahidi. Sijawahi kupewa bali kila siku utasikia hooo Richmond mara sijui nyumba London ya mwanae, sasa Key question ni kuwa Richmond ni kampuni na mikataba EL hakusaini sasa anahusikaje mpaka kupewa jina baya?

Andrew C anahusika sana na mikataba mingi lakini hasikiki kutajwa tajwa hata alipokutwa na visenti pia hajatajwa tajwa.

Why EL all the time? Are paid to make sure that EL is seen as a menace to society?, am sure you are not!, but why?

Naomba uje na EVIDENCE kuwa EL ni Fisadi. acha ngojera za magazeti tumeyazoea.

Mkuu FairPlayer,
Namheshimu sana Halisi na michango yake mingi ni very constructive hapa JF lakini sio plae inapohusu Lowassa.

Yuko biased na ni kama ana chuki fulani na huyo bwana. Binafsi naona suala kubwa ni ugomvi wa Mengi na Lowassa. Lakini jana
kaniita nina mawazo mgando. Well, sitegemei mwandishi wa habari atumie lugha kama hiyo maana hapa duniani ni mjinga tu anaweza kufikiri kuna mawazo mgando. Hakuna mawazo ya kijinga wala mawazo mgando hata kama yangetoka kwa kichaa.

Labda yeye hajijui lakini michango yote ya Halisi kuhusu Lowassa inakuwa ni kama imetawaliwa na chuki zaidi ya facts. Mimi ndivyo ninavyoona ninaposoma. Naweza kuwa wrong lakini ndivyo inavyoongia kichwani.

Simtetei Lowassa na wala sina mapenzi naye lakini ninaposhangaa ni pale watu wanapotumia nguvu kubwa kumtenganisha Lowassa na JK. kwa ninavyoona mimi hao ni wamoja na kama kuna makosa basi wote wameshirki kwa kiasi kikubwa kutufikisha hapa tulipo. Aidha siamini kabisa Lowassa anaweza kuwa rais wa nchi; watanzania wa 2015 sio wajinga kiasi hicho. tayari ameshachafuka kwa ufisadi au hisia za ufisadi na kwa mwaka 2015 hiyo sio sifa ya mtu anayetaka kuwa rais.

Wacha tukae kimya maana hii movie inajirudia kila siku na wachezaji ni wale wale. 2010 tuliambiwa atachukua fomu ya urais nk. Ghafla ikawa kimya. Tukaambiwa anaandaa mipango ya kumpindua rais, ghafla kimya. Tukaambiwa anataka kuwa mwenyekiti wa CC, ghafla kimya. Jamani si ifike mahali tusubiri na kuona nini kitaendelea?
 
n1.JPG


Nape Mnauye wakati akiongea na vyombo vya habari mjini Dodoma leo ambako vikao vya Chama cha CCM vikiendelea amebadilisha kuali mbiu ya awali aliyokuwa akizunguka nchi nzima kutangaza majina ya wanaotakiwa kuachia ngazi . Leo kaja na mpya kwamba vyombo vya habari vilipotosha ukweli wa maana ya kuvua magamba kwa maana ya kubadilika na wala si kuwafukuza watu. Hii imekaaje?
 
ukiona nape anageuka hivyo ujue lowasa kasafishwa.....haya majitu hayafai
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom