Kimenuka Dodoma, magamba yapata moto

Kimenuka Dodoma, magamba yapata moto

quote_icon.png
By Mzee Mwanakijiji Kwanini watu wanafikiri Lowassa ana clout ya kuwashawishi wananchi wa Tanzania kuwa hayuko jinsi anavyodhaniwa au kujulikana? NI KWA SABABU EL hajawahi wala hakufaidika na Richmond, ukweli ambao unajulikana na alijiuzulu u PM kwa uwajibikaji na sio muhusika. Pia mpaka mtu ahukumiwe ni ngazi ya mahakama tuu ina uwezo huo na sio MAGAZETI. Ni kweli wapo watu wanaoweza kuapa kwa Lowassa lakini kweli hivi akisimama na kuanza kampeni ataahidi nini Watanzania ambacho hakijawahi kuahidiwa na viongozi wenzake wa CCM waliopo au waliopita? Akipewa nchi EL atahaidi yaleyale waliyowahi kuhaidi viongozi waliopita.Naombeni kitu japo kimoja tu ambacho EL anaweza kusema ambacho hakijawahi kusemwwa na CCM. Hakuna ambacho anaweza kusema EL ambacho CCM haijawahi kukisema. Tofauti ya EL na wengine ni UTHUBUTU na uwezo wa kufanya MAAMUZI magumu. Pia EL ni MTENDAJI na na mtekelezaji
quote_icon.png


Nadhani unakumbuka staili ya BWM na ya Mwinyi, Mkapa alikua anaongea kidogo na kutenda kwa wingi. Just to give you an example.
 
Huyo unaemsema mchapakazi he has been there, and he has done nothing!! Ebu nipe mfano wa uchapakazi wake na faida kwa taifa nzima.

Ulikuwepo Tanzania wakati EL alipokuwa waziri mkuu? Upo Tanzania na unafuatilia siasa?
 
Ccm hawawezi wakawa na Moral Authority ya kuwawajibisha Chenge na Lowasa pia hata Rostam asingekuwa kaondoka.
Suala linalomwandama Chenge,halimwandami Chenge kama Chenge,ufisadi huo ulifanyika katika kipindi alichokuwa Mwanasheria mkuu waSerikali na Mjumbe wa Baraza la Mawaziri,kila alichokifanya alikifanya chini ya maamuzi ya Baraza la Mawaziri ambalo Mkt wake ni Rais wa Jamhuri ya Muungano,kipindi hicho akiwa Mkapa.
Pia vyombo vya Usalama Vilikuwapo kwasababu Rada ilikuwa ina mahusiano ya kiusalama wa Taifa,Pia waziri wa Mambo ya nje alikuwepo ambaye ni ndg Jakaya[Rais] hawezi kukwepa katika hili pia.Hivyo kumwadhibu Chenge pekee ni kumwonea,wotewalio husikakuanzia na Mkapa pamoja na Jakaya inabidi wafukuzwe na kuwajibika kisheria.
Upande wa Lowasa pia ni kumwonea kwasababu,hakufanya kama Lowasa ktk suala la Richmond,Yeye alifanya kama waziri mkuu.,yeye alipeleka Ripoti kila hatua ya utekelezaji ilipofikia aliwasilisha kwa Baraza la Mawaziri,ambalo Jakaya ni Mkt,Pia vyombo vya Usalama vilikuwepo kwasababu nchi ilikuwa imetumbukia gizani,lakini pia Waziri wa mambo ya nje ambaye ni Membe,alishindwaje kugundua uwapo wa kampuni iliyosemekana ipo Marekani wakati haipo?nini ni kazi yake?
Pia CCM katika Ripoti ya Wataalam wao Prof Luhanjo na Mkama kabla hajawa katibu mkuu waliainisha juu ya Sababu ya CCM kukosa Mvuto ni Suala la UFisadi,sidhani kama walitaja majina ya mafisadi?zaidi ya kuainisha dhana ya ufisadi.
Kama ripoti inaongelea mfumo wa CCM unaodharisha Mafisadi ili bidi waujadili mfumo na miiko ya uongozi,wakaacha kujadili ufisadi,wakajadili majina,hakika wakakwepa hoja.

Hakuna atakaye nusurika ndani ya CCM juu RICHMOND AU JUU YA RADA nk.Akina mkapa wametajwa pahala pengi mbona hawavuliwi?huu ni mkakati wa urais 2015 na siyo juu ya kukisafisha chama chao.
Hivyo basi CCM kama wana nia ya dhati ya kurejesha heshima kwa jamii,wawashughulikie wote waliojaribu kutajwa tuu kwenye vyombo vya habari kama Nape alivyowahi kusema kwamba kama jamii imekuhisia au umetajwa hata hukutenda tutakuondoa,Jk na PPTL vp.
 

P Upande wa Lowasa pia ni kumwonea kwasababu, hakufanya kama Lowasa ktk suala la Richmond, Yeye alifanya kama waziri mkuu. Yeye alipeleka Ripoti kila hatua ya utekelezaji ilipofikia aliwasilisha kwa Baraza la Mawaziri; ambalo Jakaya ni Mkt. Pia vyombo vya Usalama vilikuwepo kwasababu nchi ilikuwa imetumbukia gizani,lakini pia Waziri wa mambo ya nje ambaye ni Membe alishindwaje kugundua uwapo wa kampuni iliyosemekana ipo Marekani wakati haipo? nini ni kazi yake?

Kamanda umeongea
 
Lowasa aliponzwa na uchapakazi wake, katika sakata la richmond, aliingizwa kwa sababu ya Memo aliyomunadikia msabaha akimtaka awaulize richmond juu ya uwezo wao wa kuleta umeme, alikuwa waziri mkuu na alikuwa anahakikisha kuwa umeme unapatikana. Tunakumbuka akiwa waziri mkuu baada ya clouds kutangaza mashimo ya bara bara ya Shekilango alikwenda pale na kuagiza barabara ijengwe na ilijengwa. Akiwa waziri mkuu aliagiza vibanda vyote vilivyokuwa mjini Posta na kariakoo vivunjwe na vilivunjwa mji ukawa safi. Akiwa Premear aliguswa na suala la foleni na alianza kulifanyia kazi kwa kujaribu njia tatu, Akiwa Premier Lowasa alikuwa naogopwa na wakurugenzi wa halmashauri na wizi ulipungua sana,need I say more?
 
Huyo unaemsema mchapakazi he has been there, and he has done nothing!! Ebu nipe mfano wa uchapakazi wake na faida kwa taifa nzima.
Uchapakazi wa EL unajulikana umejadiliwa sana tena kwa kina thread zake zipo usiwe mvivu kuzipitia, iliyobaki ni counterpart yake mtuambie kwanini hawezi.
 
Lowasa aliponzwa na uchapakazi wake, katika sakata la richmond, aliingizwa kwa sababu ya Memo aliyomunadikia msabaha akimtaka awaulize richmond juu ya uwezo wao wa kuleta umeme, alikuwa waziri mkuu na alikuwa anahakikisha kuwa umeme unapatikana. Tunakumbuka akiwa waziri mkuu baada ya clouds kutangaza mashimo ya bara bara ya Shekilango alikwenda pale na kuagiza barabara ijengwe na ilijengwa. Akiwa waziri mkuu aliagiza vibanda vyote vilivyokuwa mjini Posta na kariakoo vivunjwe na vilivunjwa mji ukawa safi. Akiwa Premear aliguswa na suala la foleni na alianza kulifanyia kazi kwa kujaribu njia tatu, Akiwa Premier Lowasa alikuwa naogopwa na wakurugenzi wa halmashauri na wizi ulipungua sana,need I say more?

Mbona hizo sio kazi za waziri mkuu? Kama ndio ulikua uchapakazi wake huo I doubt kama alikua akielewa majukumu ya uwaziri mkuu!!
 
Lowasa aliponzwa na uchapakazi wake, katika sakata la richmond, aliingizwa kwa sababu ya Memo aliyomunadikia msabaha akimtaka awaulize richmond juu ya uwezo wao wa kuleta umeme, alikuwa waziri mkuu na alikuwa anahakikisha kuwa umeme unapatikana. Tunakumbuka akiwa waziri mkuu baada ya clouds kutangaza mashimo ya bara bara ya Shekilango alikwenda pale na kuagiza barabara ijengwe na ilijengwa. Akiwa waziri mkuu aliagiza vibanda vyote vilivyokuwa mjini Posta na kariakoo vivunjwe na vilivunjwa mji ukawa safi. Akiwa Premear aliguswa na suala la foleni na alianza kulifanyia kazi kwa kujaribu njia tatu, Akiwa Premier Lowasa alikuwa naogopwa na wakurugenzi wa halmashauri na wizi ulipungua sana,need I say more?

Uchapakazi wa EL unajulikana umejadiliwa sana tena kwa kina thread zake zipo usiwe mvivu kuzipitia, iliyobaki ni counterpart yake mtuambie kwanini hawezi.

Hakika kama huu hapo juu ndio uchapakazi wake, I need not to say more​!!!!
 
Ccm hawawezi wakawa na Moral Authority ya kuwawajibisha Chenge na Lowasa pia hata Rostam asingekuwa kaondoka.
Suala linalomwandama Chenge,halimwandami Chenge kama Chenge,ufisadi huo ulifanyika katika kipindi alichokuwa Mwanasheria mkuu waSerikali na Mjumbe wa Baraza la Mawaziri,kila alichokifanya alikifanya chini ya maamuzi ya Baraza la Mawaziri ambalo Mkt wake ni Rais wa Jamhuri ya Muungano,kipindi hicho akiwa Mkapa.
Pia vyombo vya Usalama Vilikuwapo kwasababu Rada ilikuwa ina mahusiano ya kiusalama wa Taifa,Pia waziri wa Mambo ya nje alikuwepo ambaye ni ndg Jakaya[Rais] hawezi kukwepa katika hili pia.Hivyo kumwadhibu Chenge pekee ni kumwonea,wotewalio husikakuanzia na Mkapa pamoja na Jakaya inabidi wafukuzwe na kuwajibika kisheria.

Upande wa Lowasa pia ni kumwonea kwasababu,hakufanya kama Lowasa ktk suala la Richmond,Yeye alifanya kama waziri mkuu.,yeye alipeleka Ripoti kila hatua ya utekelezaji ilipofikia aliwasilisha kwa Baraza la Mawaziri,ambalo Jakaya ni Mkt,Pia vyombo vya Usalama vilikuwepo kwasababu nchi ilikuwa imetumbukia gizani,lakini pia Waziri wa mambo ya nje ambaye ni Membe,alishindwaje kugundua uwapo wa kampuni iliyosemekana ipo Marekani wakati haipo?nini ni kazi yake?

Pia CCM katika Ripoti ya Wataalam wao Prof Luhanjo na Mkama kabla hajawa katibu mkuu waliainisha juu ya Sababu ya CCM kukosa Mvuto ni Suala la UFisadi,sidhani kama walitaja majina ya mafisadi?zaidi ya kuainisha dhana ya ufisadi.
Kama ripoti inaongelea mfumo wa CCM unaodharisha Mafisadi ili bidi waujadili mfumo na miiko ya uongozi,wakaacha kujadili ufisadi,wakajadili majina,hakika wakakwepa hoja.

Hakuna atakaye nusurika ndani ya CCM juu RICHMOND AU JUU YA RADA nk.Akina mkapa wametajwa pahala pengi mbona hawavuliwi?huu ni mkakati wa urais 2015 na siyo juu ya kukisafisha chama chao.
Hivyo basi CCM kama wana nia ya dhati ya kurejesha heshima kwa jamii,wawashughulikie wote waliojaribu kutajwa tuu kwenye vyombo vya habari kama Nape alivyowahi kusema kwamba kama jamii imekuhisia au umetajwa hata hukutenda tutakuondoa,Jk na PPTL vp.

Kamanda umeongea

Hakika FairPlayer is not fair!!! Yaani katika yote yalizungumzwa na Mwakajilae, wewe umeona hicho kipande tu!! Mbona ujumbe wa hiyo post unamweka Lowassa katika losing side?!?!
 
leo mchana nikijadiliana na mbunge mmoja wa ccm kutoka mkoa wa dar, aliniambia wazi kwamba, lowassa hawezi kufukuzwa chamani, kwani ndiye anayeunganisha chama. Kabla ya el kungo'lewa gamba, mwenyekiti atakuwa wa kwanza kwani matatizo lukuki ndani ya chama na taifa yametokea katika utawala wake. Amesema udini, ufisadi, umasikini, siasa ya makundi yameendelezwa na mwenyekiti wa chama na siyo lowassa, kwa maana hiyo gamba kubwa ni rais mwenyewe na siyo el.

El akingo'lewa basi tutaelekea kwenye uchaguzi mara moja na ccm itakufa kwa maana 70% ya wabunge ccm wanamuunga mkono el. Jk hawezi kumgusa el na anajua hilo


mkuu el anangolewa tu vizuri wala hana hata ujanja wowote,ila watachelewa.
 
[TABLE="width: 879"]
[TR]
[TD="bgcolor: #ffffff"][TABLE="width: 599"]
[TR]
[TD]
• LOWASSA, CHENGE WAIVURUGA CCM

na Mwandishi wetu

[/TD]
[/TR]
[/TABLE]
[/TD]
[TD="width: 140, bgcolor: #FFFFFF"][/TD]
[/TR]
[TR]
[TD][TABLE="width: 599"]
[TR]
[TD]
HATIMA ya Chama cha Mapinduzi (CCM), sasa inaonekana kuwa mikononi mwa vigogo wawili wa chama hicho, Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa, na Andrew Chenge, ambaye ni Mbunge wa Bariadi Magharibi, baada ya kubainika kuwepo kwa kundi kubwa la viongozi na makada maarufu walio tayari kuwaunga mkono katika jambo lolote watakaloamua.


Habari za uhakika zilizolifikia Tanzania Daima, zimeeleza kuwa kundi hilo ambalo ndani yake wamo wenyeviti kadhaa maarufu wa CCM wa mikoa, limekuwa kwa siku mbili likifanya mikutano ya siri na kuonana na baadhi ya wajumbe ambao wanaonekana kukosa msimamo wa dhati katika kuamua kuwaondoa wabunge hao katika uongozi wa juu wakidaiwa kuwa magamba yanayotakiwa kuvuliwa.

Mmoja wa viongozi wanaowaunga mkono wabunge hao ameliambia Tanzania Daima kuwa wataungana na wabunge hao katika maamuzi yao, kwa madai kwamba wako viongozi wengi wanaotakiwa kuwafukuza kwa kukivuruga chama hicho.

“Ubovu ndani ya chama chetu hauwezi kubebeshwa watu wawili tu, kana kwamba wao ndio waamuzi wa mwisho. Kama ni kutota tutatota nao, na wala hatuoni aibu katika hilo,” alisema kada huyo ambaye jina lake linahifadhiwa.

Taarifa zimebainisha kuwa mbali na ajenda nyingine zinazotarajiwa kujadiliwa, inayoonekana kukamiwa kwa nguvu kubwa ni ile ya utekelezaji wa dhana ya kujivua gamba ambayo Katibu wa Halmashauri Kuu ya Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, amesikika mara nyingi akiwalenga wabunge Lowassa, Chenge na Rostam Aziz kama magamba yanayotakiwa kuvuliwa.


Ni kauli hiyo iliyomfanya aliyekuwa mbunge wa Igunga na mjumbe wa Kamati na Halmashauri Kuu ya CCM, Rostam Aziz, kujivua nyadhifa zote za uongozi pamoja na ubunge baada ya kuchoshwa na kile alichokiita ‘siasa za maji taka’ alizodai zinafanywa na Nape na Naibu Katibu Mkuu (bara), John Chiligati.


Hata hivyo, taarifa za kina zinaonyesha kuwa kundi linalotaka wabunge hao kuondoka limeapa kupigana kwa nguvu zote kuhakikisha watuhumiwa wote wa ufisadi wanaodaiwa kuchafua jina na heshima ya CCM, wanavuliwa nyadhifa zao hata kama hatua hiyo itasababisha chama hicho kugawanyika.


“Nani kakuambia maneno hayo…sisi hatujapanga kumwondoa Lowassa wala Chenge…hizo ni njama zenu waandishi wa habari,” alisikika akisema mjumbe mmoja wa Halmashauri Kuu ya CCM kwa mwandishi wa habari hizi alipotakiwa kutoa maelezo ya yeye na wenzake kuwa miongoni mwa watu walio katika kundi linalotaka wabunge hao watimuliwe.


Hata hivyo, bila kujua kuwa alikuwa akifuatiliwa kwa makini, mjumbe huyo dakika chache baadaye alisikika akizungumza na mtu mwingine kwa njia ya simu, akimtaka kuwa makini na waandishi wa habari kwa madai kuwa ‘siri zao zinavuja hovyo’ kwani habari zinasema kuwa kundi linalotaka Lowassa na Chenge wang’olewe limeamua kutumia kwanza njia za kistaarabu za kuwatuma wazee mashuhuri wa CCM kuonana na wabunge hao na kuwaomba waondoke kistaarabu ili kunusuru uhai wa chama hicho.


Hoja nzito inayotakiwa kutumiwa ni kuwataka watambue hali ngumu ya kisiasa ilivyo nchini, hususan upinzani mkubwa unaokipata kutoka Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ambacho kimekuwa kikiwanyima usingizi.


Jana wajumbe wa Kamati ya Maadili walikutana kwa siku nzima katika kikao cha siri kilichoketi makao makuu ya chama hicho maarufu kama White House chini ya Mwenyekiti wa Chama hicho, Rais Jakaya Kikwete.


Rais Kikwete, aliwasili eneo hilo majira ya saa tano na kuungana na viongozi wenzake kuanza kikao hicho, na zilikuwepo taarifa zisizo rasmi za kuhojiwa kwa baadhi ya makada wakongwe wa chama hicho pamoja na wale wa Umoja wa Vijana (UVCCM), wanaotuhumiwa kuzua mtafarufu wa ndani uliokigawa chama katika makundi ambayo sasa yanapingana hadharani.


Makada wengine waliotarajiwa kuhojiwa na kamati hiyo kwa mujibu wa chanzo chetu ni watuhumiwa wa ufisadi ambao wameshindwa kutekeleza maagizo ya NEC ya kujivua gamba kwa kuachia nyadhifa zao kwenye chama ndani ya siku 90 ambazo kimsingi zimehitimishwa kwa kada mtuhumiwa mmoja, Rostam Aziz, kuachia ngazi zote ukiwemo ubunge wa Igunga.


Tayari kumekuwa na lawama kutoka kwa vigogo wengi wa chama hicho za kumshtumu Nape na Naibu Katibu Mkuu, Kapteni mstaafu John Chiligati, kuwa walibeba na kutekeleza agizo hilo la falsafa ya kujivua gamba kwa malengo yao binafsi.


Akizungumza kwa kifupi majira ya saa 11 jioni wakati wa mapumziko, Naibu Katibu Mkuu wa CCM Tanzania Bara, Chiligati, alisema Kamati ya Maadili ni sehemu ya CC na hivyo walikuwa wakiandaa ajenda za mkutano wa leo. “Hapa tunapumzika hadi saa moja jioni, tutarudi kuendelea na kikao chetu.”

Hata hivyo, alipobanwa zaidi kuhusu taarifa za baadhi ya makada kuhojiwa na kamati hiyo, Chiligati alionekana kusita na kukwepa kulitolea ufafanuzi wa kukiri ama kukataa.

“Wewe hata kama kuna watu waliohojiwa na kamati...tusubiri maamuzi yatatolewa kwenye kikao cha NEC,” alisema Chiligati kwa kifupi.
[/TD]
[/TR]
[/TABLE]

[/TD]
[/TR]
[/TABLE]
 
Tupeni kinachoendelea dodoma na si porojo za lowassa, mnatuzingua hapa.
 
Kamanda wangu kwanza niweke disclaimer. Eddo Lowassa simfahamu, hanifahamu wala simfahamu ndugu wake wa karibu wala wa mbali. Mara ya mwisho kuwa naye karibu ilikua December kati ya 27 mpaka 29 nadhani ilikuwa ni Serengeti.

Kwahiyo kila nikiandikacho hapa najaribu kuandika kwa manufaa ya umma kadri ya uelewa wangu. I am very fair.

Tatizo ni upande wa pili tumeomba ushahidi wa UFISADI wa Lowassa wameingia mitini au kuja na hadithi za magazeti ya udaku.

Nimemjibu mwanakijiji. Na mimi pia inatakiwa unijibu maswali yangu hapo juu.
 
Nayezingua ni HALISI alieanzisha mada inayohusu Dodoma lakini anamsiliba Eddo wa watu
 
Lowasa aliponzwa na uchapakazi wake, katika sakata la richmond, aliingizwa kwa sababu ya Memo aliyomunadikia msabaha akimtaka awaulize richmond juu ya uwezo wao wa kuleta umeme, alikuwa waziri mkuu na alikuwa anahakikisha kuwa umeme unapatikana. Tunakumbuka akiwa waziri mkuu baada ya clouds kutangaza mashimo ya bara bara ya Shekilango alikwenda pale na kuagiza barabara ijengwe na ilijengwa. Akiwa waziri mkuu aliagiza vibanda vyote vilivyokuwa mjini Posta na kariakoo vivunjwe na vilivunjwa mji ukawa safi. Akiwa Premear aliguswa na suala la foleni na alianza kulifanyia kazi kwa kujaribu njia tatu, Akiwa Premier Lowasa alikuwa naogopwa na wakurugenzi wa halmashauri na wizi ulipungua sana,need I say more?


Kama kweli unahisi EL ni mzuri na aliyoyafanya ni mazuri kwa watanzania, mshauri either aanzishe chama chake au ajiunge na chama kingine. Kama ni mzuri atakuwa mpinzani wa kweli na kama ni garasa itakula kwake. Kwa uzuri unaousema haina haja ya yeye kung'ang'ania CCM kwani KIZURI CHAJIUZA KIBAYA CHAJITEMBEZA.
 
Back
Top Bottom