View attachment 2184447
Nimeangalia na kusona sehemu ya maandiko kuhusu mmea aina ya Canola au Rapeseed, ambao unaweza kuzalisha mafuta ya Kula zaidi ya Alizeti.
Wenzetu Kenya wenye mashamba makubwa wameanza kulima, licha ya kuwapatia faida lakini kimekuwa ni kama kilimo cha muda kusaidia kurutubisha ardhi au kubadilisha mazao wakati wa kulima Ngano.
View attachment 2184452
Imeelezwa kuna aina mbili kuu za mafuta yanayopatikana kutoka na mmea huu wa Rapeseed. Ipo inayotoa mafuta kwa ajili ya kupikia na mafuta ya tasnia ya kemikali za magari.
Kwa upande wa Kenya inaelezwa kuwa bei ya jumla ya mbegu za Rapeseed (canola) kwa mwaka huu 2022, inakadiriwa kuwa Kati ya US$ 5.2 na US$ 9 kwa kilogram au Kati ya US$ 2.36 na US$ 4.08 kwa pound(lb). Bei hii kwa Kenya ni sawa na Shilingi ya Kenya (KES) 566.45 kwa kilogram kwa Mombasa and Nairobi.
View attachment 2184442