Kikwete to USA (May 2009)

Kikwete to USA (May 2009)

Invincible,
Mkuu watamwabia kitu gani?.. kama ni Tanzania imekabidhi rasilimali zake kwa wezi na waporaji wazilinde...Atawaomba ushahidi kwa sababu it's Only in Tanzania Ushahidi hukusanywa na wananchi..
 
Na nyinyi watanzania ambao mtabahatika kukutana na huyu mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, mwelezeni haya tunayolalamikia.

Sio kwamba hapa tunaonyesha ujasiri, halafu mbele yake tunaufyata.

Naam hili ni muhimu sana kumuweka kiti moto kila Watanzania walio nje wanapokutana naye, lakini pia kuna ufisadi ambao umenaza kufanyika ambapo Watanzania wachache ambao wanaonekana 'si wakorofi' na balozi zetu huchaguliwa ili wakakutane na Rais. Hawa huishia kukenuakenua tu na kupiga picha nyingi na Rais bila kuuliza maswali yoyote ya muhimu kuhusiana na 'uongozi' wake.
 
Ni kweli, kama kusikia angekua kasha sikia na kuji rekebisha. Kilicho baki ni vitendo tu. 2010 wananchi kazi kwetu. Ila tatizo kabla hajaondoka huyu lazima apatikane kiongozi thabiti wa kuchukua nafasi yake siyo tunaondoa "papa" tunaingiza "nyangumi".


Ile thread iliyoanzishwa ya kupendekeza mtu mbadala wa kuchukua nafasi ya Jakaya mwaka 2010 ndio ingekuwa dira yetu wanaJF; lakini wapambe wa chama tawala waliitoa kabla ya majority hawajapendekeza!!
 
Yaani rais anakuja kuzungumza na viongozi wa IBM? Tanzania hatuna wizara ya elimu na teknolojia since msaada wao wameutoa kwa chuo kikuu cha Dodoma?
I think it belittle the presidency. Na huyo Mwethiopia wa Los Angeles anajijenga kwa kutumia majina ya wakubwa. Hata ule mkutano alioshiriki Mrs. Kikwete nilishangaa Mrs. Obama hakuwepo. Mwawado, thanks for the details. Nilijua tu kwamba utatumwagia details.
 
...kuna swine flu huko, zama hizi wala sio za kupendelea kusafiri safiri kwenye haya madege jamani...
 
Muheshimiwa anaweza kuwa anawahi Draft ya Hashim Thabit maana ni jumanne. Si unajua Ze-comedy anavyopenda basketball na mashindano ya umiss.
Go JK, Goo Hashim
 
Ha ha ha haaaaaaa....Kwa kweeeli Steve D umeniacha hoi...kwenye hizo Youtube...Nimecheka sana...
 
Last edited:
Yaani rais anakuja kuzungumza na viongozi wa IBM? Tanzania hatuna wizara ya elimu na teknolojia since msaada wao wameutoa kwa chuo kikuu cha Dodoma?
I think it belittle the presidency. Na huyo Mwethiopia wa Los Angeles anajijenga kwa kutumia majina ya wakubwa. Hata ule mkutano alioshiriki Mrs. Kikwete nilishangaa Mrs. Obama hakuwepo. Mwawado, thanks for the details. Nilijua tu kwamba utatumwagia details.

Hakuna cha ku belittle the presidency wala nini. Vi raisi vyote vya Afrika viko vidogo vidogo tu....havina lolote zaidi ya kujipendekeza pendekeza na kukenua kenua vikipata photo op na viongozi wa Marekani...
 
JK TO MEET OBAMA:

MUHIDIN ISSA MICHUZI in San Francisco, 18th May 2009

President Jakaya Kikwete is expected to be the first African head of state to meet US President Barack Obama since his inauguration.President Kikwete and his delegation arrived here on Saturday, for a week-long official tour and is scheduled to visit President Obama at the White House on Friday.

The US President, who recently marked 100 days in office, is reportedly under tremendous pressure from African nations and their diplomatic representatives in Washington to leaders from the continent.According to a programme released by the Ministry of Foreign Affairs and International Co-operation, the President will also meet with the US Secretary of State, Hilary Clinton and the IMF Managing Director, Dominique Strauss-Kahn, in Washington DC on the same day.

The president is accompanied by the Minister for Foreign Affairs and International Co-operation, Mr Bernard Membe and Zanzibar Minister for Labour, Youth, Women and Children Development Affairs, Ms Asha A. Juma.

On Monday, President Kikwete will visit Stanford University and later Google headquarters, as well as the IBM University where he is to be briefed on the firm's activities in Africa, cognitive computing project and IBM BlueGene Supercomputer.

On the following day, President Kikwete will tour the Sillicon Valley, where he is scheduled to hold talks with CISCO, Google and IBM executives.On Wednesday, President Kikwete flies to Los Angeles for a number of activities, including the Global Water for Life Event hosted on Thursday by the House of Mohans.

Source: Daily News.
 
na haya ndiyo aliyoandika salva. Je, nyie wa san Francisco, haya ndiyo mliyomuuliza rais?



Na Mwandishi Maalum, San Francisco, California, Marekani

Baadhi ya Watanzania wanaoishi mjini San Francisco, Jimbo la California, Marekani, wamezilaumu baadhi ya taasisi zisizokuwa za kiserikali (NGO’s) zinazofanya kazi katika Tanzania kwa kujinufaisha tu binafsi baadala ya kuelekeza misaada ambayo zinaipata kwa walengwa.

Watanzania hao wamesema kuwa taasisi hizo zinatakiwa kulenga kuwasaidia walengwa wao na siyo kushibisha matumbo yao kama ilivyo sasa kwa NGO’s zilizoko nyingi. Watanzania hao hawakutoa mifano yoyote ya taasisi za namna hiyo.

Lawama na mjadala kuhusu taasisi hizo zimetolewa na kuanzishwa na Mjumbe wa Bodi ya Chama cha Watanzania wanaoishi mjini San Francisco, California, Mama Christine Chacha katika mkutano kati ya viongozi wa chama hicho na Rais Jakaya Mrisho Kikwete.

Mama Chacha alikuwa mmoja wa kundi la viongozi wa chama hicho ambao walimpokea Rais Kikwete baada ya kuwa amewasili mjini San Francisco kuanza ziara yake ya siku nane katika Marekani. Chama hicho kinachoongozwa na Bwana Mwesigwa kina wanachama 100.

Katika mkutano wao na Rais Kikwete kwenye Hoteli ya Four Seasons, mjini humo, Mama Chacha amesema wajibu mkubwa wa taasisi zisizokuwa za kiserikali ni kuwatumikia walengwa wao na siyo kuendesha magari ya kifahari ya Land Cruiser kama ilivyo sasa.

Akitoa kauli yake kwenye mjadala huo, Rais Kikwete amesema kuwa siyo kazi ya Serikali kuingilia shughuli za NGO’s kwa sababu hizo ni taasisi za kijamii ambazo ni muhimu katika ujenzi wa demokrasia.

“Kazi yetu ni kuzijengea taasisi hizo mazingira mazuri ya kufanya kazi. Siyo kazi ya Serikali kuingilia kazi ya taasisi hizo. Ni taasisi muhimu…hata nyingine zinadai kupewa madaraka kama ya viongozi waliochanguliwa na wananchi,” amesema Rais Kikwete.

Katika mkutano huo, viongozi hao wa chama cha Watanzania pia wameiomba Serikali kuangalia uwezekano wa kubadilisha sheria, ili kuruhusu Watanzania, wanaopenda, kuwa na uraia wa zaidi ya nchi moja.

Rais Kikwete amewaambia Watanzania hao kuwa suala hilo lina taratibu ndefu kwa sababu litahitaji mabadiliko ya Katiba.

Ameongeza pia kuwa mchakato mzima wa kuanzisha utaratibu wa uraia wa zaidi ya nchi moja unahitaji wananchi kuelimishwa na kuhamasishwa ili wayakubali mabadiliko hayo.

Kuhusu swali kuwa kwa nini makampuni ya madini nchini yanauza hisa zao kwa makampuni mengine baada ya muda mfupi, Rais Kikwete amesema kuwa hayo ni makampuni binafsi yenye uhuru wa kuunza hisa wakati yanapotaka, na wala Serikali haiwezi kuyazuia kuuza hisa na umiliki wa makampuni yao.

“Katika mfumo wa biashara huria, ni jambo la kawaida kabisa kwa mwekezaji binafsi kuuza hisa zake wakati wote akipenda ama akiona kuwa akiuza atapata faida. Serikali haiwezi kumzuia kufanya hivyo.”

Ends
 
n

Mama Chacha alikuwa mmoja wa kundi la viongozi wa chama hicho ambao walimpokea Rais Kikwete baada ya kuwa amewasili mjini San Francisco kuanza ziara yake ya siku nane katika Marekani. Chama hicho kinachoongozwa na Bwana Mwesigwa kina wanachama 100.

.......



Watanzania wanaoishi Marekani ndio wenyeji wa Rais JMT Jimboni, Carlifornia.
 
Watanzania wanaoishi Marekani ndio wenyeji wa Rais JMT Jimboni, Carlifornia.
Hivi rais anapokuwa na working visit kama hii nchi mwenyeji hata haitambui 'udiplomasia' wake na kumtoa angalau gavana kwenda kumpokea?
 
Hivi rais anapokuwa na working visit kama hii nchi mwenyeji hata haitambui 'udiplomasia' wake na kumtoa angalau gavana kwenda kumpokea?


Kikwete kasahau msemo wa akufukuzae hakwambii toka.

Apate funzo, labda atatulia.
 
I do pay taxes through different means which am not interested in discussing them with you.
True, he has a gorgeous smile. We unataka Rais wako awe havutii?

Discuss issues not tissues!

Kui, what a nonsense!!!! kwako wewe kuwa na gorgeous smile ndio issue???
 
Anaenda kujitambulisha nini? Maana trip zote alizoenda ni maumivu tu kwani hela zimeisha huko kwenye hazina. Benefit NIL to Tanzanians. Jamaa hata wakikutana naye hakuna jipya atajichekechekesha hapo then basi huyo anaondoka zake. Waendelee na shughuli zao hana jipya unless kama sikijui hicho kipya nielimishwe....
 
Mimi nikifikiri na kutafakari na kumwangalia usoni vizuri akiwa anaongea, naona mheshimiwa wetu aliutaka uongozi ili tu na yeye awe raisi, apigiwe ving'ora na heshima zote kama raisi wa nchi. Lakini hakuwa na mkakati wowote wa maana wa namna ya kuipunguzia nchi yetu mzigo wa umasikini.
 
Hii ziara ni ya kutalii au kaenda kujionyesha kule?
 
Mimi nikifikiri na kutafakari na kumwangalia usoni vizuri akiwa anaongea, naona mheshimiwa wetu aliutaka uongozi ili tu na yeye awe raisi, apigiwe ving'ora na heshima zote kama raisi wa nchi. Lakini hakuwa na mkakati wowote wa maana wa namna ya kuipunguzia nchi yetu mzigo wa umasikini.
He nimestuka sana na ni hoja nzito kweli umetoa hapo.
Inabidi tumsaidie muungwana kwa kumpunzisha next term kwani akiendelea nadhani itakuwa balaa zaidi.
 
Hivi kweli 8 day Marekeni wala bila kualikwa anafanya nini. Mimi nafikiri ni haki yetu wananchi kujua rais wetu anafanya nini huko. Sasa inafikia NGO za watanzania ndiyo wanakuwa wenyeji wake. Au jamaa ameamua kuiba kiana aina kwa kutumia safari badala ya kujiuzia makampuni kama akina Mkapa.
 
Back
Top Bottom