Kiingereza cha Mlimani City

Kiingereza cha Mlimani City

Jamani kwa nini kila mtu akikanyaga tu lango la kuingilia mlimani city anaanza kuongea kingereza? Utasikia cha kuungaunga mara IS na WAS kibao. Kwani mkiongea Kiswahili chenu mtakuwaje? Acheni uzuzu ubitozi na usister duu!

Mbona huwa naenda pale mara nyingi tu na huwa siongei Kiingereza?
 
jamani kwa nini kila mtu akikanyaga tu lango la kuingilia mlimani city anaanza kuongea kingereza? Utasikia cha kuungaunga mara is na was kibao. Kwani mkiongea kiswahili chenu mtakuwaje? Acheni uzuzu ubitozi na usister duu!
sehemu za heshma twatumia lugha ya heshma.
 
' you know, am like let's go n watch a movie au twende kwa samaki² n have fun then we'll keep surveying the shops.. ''''
hahaha, hapo na #selfie kibaos za kupost IG ili mtu ale likes za kutosha. mwanawane cc wengine ingirishi izi noti richabo ndomana we always sit back lay low tuwaangalie wazungu weusi wa mcity
 
Kwani wakiamua kuongea Kiingereza wao wanakupunguzia nini wewe?

mkuu Kiranga, tatizo wanakosea sana hiyo lugha. Mfano last week nilikuwa nimepumzika namsubiri mwanangu achorwe usoni

kwenye bench wamekaa mabinti wawili, mmoja anasema "am listening to Diamond musics, they are delicious"
 
Last edited by a moderator:
mkuu Kiranga, tatizo wanakosea sana hiyo lugha. Mfano last week nilikuwa nimepumzika namsubiri mwanangu achorwe usoni

kwenye bench wamekaa mabinti wawili, mmoja anasema "am listening to Diamond musics, they are delicious"

Kuna mtu anayejifunza lugha ya kigeni bila kukosea?

Wasipojifunza mnawasema kwamba wabongo kiingereza kituo cha polisi, wakijifunza mnawasema wanakosea.

Mimi mtu anayejifunza lugha ya kigeni nategemea akosee, si lugha yake ati.

Hao ni wa kupongezwa kwa kujitahidi kujifunza lugha ya kigeni bila aibu, si wa kubezwa.

Sasa wewe unayejua na kukerwa na makosa hayo uliwaelekeza?
 
Last edited by a moderator:
mkuu Kiranga, tatizo wanakosea sana hiyo lugha. Mfano last week nilikuwa nimepumzika namsubiri mwanangu achorwe usoni

kwenye bench wamekaa mabinti wawili, mmoja anasema "am listening to Diamond musics, they are delicious"

Hahahahaa nimecheka sana, ze music is so delicious....lugha ya watu hii ilisafiri miles nyingi kwa meli😀
 
Last edited by a moderator:
Kama englishi ndio lugha ya taifa la mlimani city...inabidi wakina sie tuishie nje na tuagizie wakalimani wakatununulie bidhaa huko ndani....
​Ina maana kama kienglish hakipandi sidhani hata bidhaa za huko utaziweza kaka..LOL
 
​Ina maana kama kienglish hakipandi sidhani hata bidhaa za huko utaziweza kaka..LOL

Kwa wakina sisi tuliozoea kizaramo hapo hapatufai...unaweza ukaanguka kwa presha kwa mshangao...utakapoambiwa sambusa elfu tano..wakati hiyo ni bajeti yako ya siku mbili....
 
Kwa wakina sisi tuliozoea kizaramo hapo hapatufai...unaweza ukaanguka kwa presha kwa mshangao...utakapoambiwa sambusa elfu tano..wakati hiyo ni bajeti yako ya siku mbili....
Wapii kaka, hao waongeaji english wanaosemwa hapo wala sio wanunuzi ni watembezi tu..Hata sisi wa kisambaa hapo mwake tu .
 
Wabongo bwana 😂😂😂
Mtu unamsemesha kiswahili anakuchanganyia lugha, ukiongea kingereza anaanza kuchanganya R na L humo humo kingerezani, past tense zinakuwa future na future zinakuwa present, present tense zinakuwa mixed grill😂😂😂

Hahahahahaha
 
Hahaaa kiongozi, kuna sarcasm hapo.

Ila kuna watu waonavyo hivyo, kwamba Kiingereza ni ishara au alama ya ustaarabu.

Hujawahi kukutana na Wabongo ambao hawajawahi hata kuishi Uingereza au popote pale nje ya Tanzania lakini wanajifanya kama hawakijui Kiswahili?

Binafsi nimeona. Hata mimi mwenyewe hua nikiingia ofisi ambazo najua watendaji ni wazembe huwa ni English tu. Na wakisikia unaongea basi unahudumiwa haraka. Nilijifunza hilo kwa rafiki yangu mmoja na nilipo apply hiyo style kwakweli unahudumiwa haraka.
 
Kuna mtu anayejifunza lugha ya kigeni bila kukosea?

Wasipojifunza mnawasema kwamba wabongo kiingereza kituo cha polisi, wakijifunza mnawasema wanakosea.

Mimi mtu anayejifunza lugha ya kigeni nategemea akosee, si lugha yake ati.

Hao ni wa kupongezwa kwa kujitahidi kujifunza lugha ya kigeni bila aibu, si wa kubezwa.

Sasa wewe unayejua na kukerwa na makosa hayo uliwaelekeza?

Hapo sawa. Masuala ya lugha sahihi ni wakati wa kujibu mtihani. Kiukweli mkuu hata mimi huwa nakerwa sana na mtu ambaye mnapo ongea English yeye kazi yake ni kutafuta makosa. Na hili huwa linafanywa na sisi wabongo. Lengo la lugha ni kuelewana kwa wanayoitumia na ndio maana ukiongea na mtu ambaye si mtanzania (nasisitiza si mtanzaniaa) hutapata shida hata kidogo na kama hujui vizuri hapo ndio utakuwa unajifunza.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom