Kiingereza cha Mlimani City

Kiingereza cha Mlimani City

Jamani kwa nini kila mtu akikanyaga tu lango la kuingilia Mlimani City anaanza kuongea kiingereza? Utasikia cha kuungaunga mara IS na WAS kibao. Kwani mkiongea Kiswahili chenu mtakuwaje? Acheni uzuzu, ubitozi na usister duu!

Imesimama kama Islamic State!
 
Hiyo sehemu ukifika kila mtu yupo busy kama mzungu.eti na wao waonekana wazungu.
 
Wabongo bwana 
Mtu unamsemesha kiswahili anakuchanganyia lugha, ukiongea kingereza anaanza kuchanganya R na L humo humo kingerezani, past tense zinakuwa future na future zinakuwa present, present tense zinakuwa mixed grill

Hahahahahaha,we Clues ni Sheeeeda.
Blessed you have made my day(he namie kizungu pori kimekuja kwa kuona mtoto mzuri tu,sijui nikiendanae mlimani City itakuwaje)
 
Hahaaa kiongozi, kuna sarcasm hapo.

Ila kuna watu waonavyo hivyo, kwamba Kiingereza ni ishara au alama ya ustaarabu.

Hujawahi kukutana na Wabongo ambao hawajawahi hata kuishi Uingereza au popote pale nje ya Tanzania lakini wanajifanya kama hawakijui Kiswahili?


teh teh..nilijuwa kuna ka sarcasm hapo! Tena sie ambao hatujawahi kwenda huko uingereza ndo tunapenda kiswanglish balaa.
 
Naona wote wenye app ya dictionary kwenye sm zao wameamua kuepuka uzito wa kitabu
 
Hahahahahaha,we Clues ni Sheeeeda.
Blessed you have made my day(he namie kizungu pori kimekuja kwa kuona mtoto mzuri tu,sijui nikiendanae mlimani City itakuwaje)


Mwenzio diamond kang'ang'ana, koma mtoto mzuri akufundishe .. akikuzingua mrudishie kingereza chake
 
Hawafanyi makusudi bali ...

Lile jengo limekuwa equiped with Special gravity ambayo iko standby kuchezesha lips za midomo mara tu unapoingia mjengoni ili uweze kuzungumza kimombo hata bila ya ridhaa yako.......... ...!

Endapo ukifanikiwa kukaa mule kwa zaidi ya saa mbili.. basi utakuwa tayari umekidhi vigezo vya mtu anayestahili kuwa interviewed kwa ajili ya nafasi ya kazi............!
Hahahaha dah kuna watu mko talented jaman...umenifurahisha sana rafiki
 
ila si kama chako ambacho kinamfanya mwenzio atembee na dictionary!!

ha ha ha ha ha ....teh teh jf ni mzuuuka kwa kweli. Kiinglish cha mliman city ni cha Is na Was...ila wanaelewana. Kumbe kuna kiinglisha cha kwingne ambacho hakina Is na Was ambacho ukimsikia muongeaji ni shurti uwe na dictionary!

Jf...., Burudani!!!!!!!!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom