Kiingereza cha Mlimani City

Kiingereza cha Mlimani City

Mkuu, bbwaoy, Iko Mwanza mitaa gani hii kitu?.

Iko mitaa ya Ghana karibu na maeneo Ya CCM kirumba.. mzigo ulisha isha huu... Ni watu tu ndio wana uchelewesha hawa taki kujifunza English course!! Tume pewa mwezi 1 wa kijifunza English mzigo ufunguliwe... Manake itakua vurugu hapa!
 

Attachments

  • 1430077594699.jpg
    1430077594699.jpg
    65.5 KB · Views: 352
  • 1430077614248.jpg
    1430077614248.jpg
    38.1 KB · Views: 337
  • 1430077626862.jpg
    1430077626862.jpg
    40.9 KB · Views: 325
Last edited by a moderator:
Kiingereza kinaongeza hadhi bana. Kinakufanya uonekane msomi, wa kileo, na mstaarabu.

Acha Hizoo, Rais wa China, Korea, Urusi, German, Italy nk hawajui kingereza na hawana mda na kutaka kukijua, huku Wananchi wao Wengi hawajui hiyo Lugha, hawa hawana Hadhi? Waarabu wengi hawajui Lugha hiyo mbona pesa ya Oman ndiyo yenye thamani kuliko pesa zote Duniani?
 
Jamani kwa nini kila mtu akikanyaga tu lango la kuingilia mlimani city anaanza kuongea kingereza? Utasikia cha kuungaunga mara IS na WAS kibao. Kwani mkiongea Kiswahili chenu mtakuwaje? Acheni uzuzu ubitozi na usister duu!

Huu ni Ulimbukeni wa kijinga jinga, kwani Lugha na Taaluma ni Vitu viwili tofauti, Taaluma ( Elimu) hupatikani kwa Lugha mbalimbali ndiyo maana wapo wasomi maprofesa wenye utaalamu mkubwa hawajui kingereza wamepata taaluma kwa Lugha zao mama.
 
Acha Hizoo, Rais wa China, Korea, Urusi, German, Italy nk hawajui kingereza na hawana mda na kutaka kukijua, huku Wananchi wao Wengi hawajui hiyo Lugha, hawa hawana Hadhi? Waarabu wengi hawajui Lugha hiyo mbona pesa ya Oman ndiyo yenye thamani kuliko pesa zote Duniani?

Hoja yako imekaa kutetea umaimuna
 
Wabongo bwana 😂😂😂
Mtu unamsemesha kiswahili anakuchanganyia lugha, ukiongea kingereza anaanza kuchanganya R na L humo humo kingerezani, past tense zinakuwa future na future zinakuwa present, present tense zinakuwa mixed grill😂😂😂

Ona sasa umeshanichanganya...mara kiswahili mara kidhungu
 
Ni utumwa kuongea lugha za wanaume wenzako au mataifa mengine wakati tuna lugha yetu jameni tujivunie
 
Niko njiani naelekea mlimani city. Dah! Nimesahau kamusi ya kiingereza na daftari la inglishi kozi nimemuazima jirani! Majangs
 
'...like seriously?'' hili neno nililisikia kwa wadada zaidi ya 7 tofauti tofauti, nkadhani ni kamsemo ka kuulizia bei mule mlimani city, basi namimi bila kuvunga ndani ya duka la airtel nanunua zangu modem,kheee kuambiwa bei si ndo nikalitamka.like seriously? hahahahahaha!!!! napenda sana kingereza cha mlimani city yaan kila neno lazima lianze na ''like...''
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom