Kifo cha Mhe. Chacha Wangwe na uchunguzi wake

Kifo cha Mhe. Chacha Wangwe na uchunguzi wake

Status
Not open for further replies.
Siku zote watu wamesema media zetu haziko balanced... wengine wakasema hapana... kipindi hiki at least zimekiminya CHADEMA... ndio mara ya kwanza na wao wakajua kwamba vyombo vyetu vya habari vinauwezo mkubwa hata wa kufanya machafuko kwenye taifa...

Naomba watu wajifunze hili vizuri...
 
Kitila,

Msimamo wangu mimi ni kuwatumia wabunge kuendesha mambo ya CHADEMA. Kuwapa ukurugenzi watu ambao wako nje ya bunge nafikiri ni makosa labda kwa vyama ambavyo havina wabunge wa kutosha.

Kwenye hili wangeanza na Dr. Slaa toka mwanzoni, au Zitto na mpaka mwisho.

Ukisoma kule kwenye ile thread nyingi ya Mnyika akutana na Bille na Rostam, utaelewa nina maana gani.

Hivi Mnyika alitumwa na chama hata kutuma sms kwa RA? Inabidi chama au kampuni kuwe na protocol ya aina fulani hivi inavyokuja kwenye mawasiliano na mtu/vyombo vya nje ya chama/shirika.

Swali lingine ninalojiuliza, kwanini Mbowe alikubali ushauri wa polisi kwamba asihudhurie mazishi ya Wangwe? Ile ilikuwa sio amri, ulikuwa ushauri, kama hakukuwa na hatari kabisa hata kwake, kwanini akubaliane na ushauri wa namna hiyo? Tumeona mara chungu nzima wanasiasa wakikataa ushauri kuhusu maisha yao kuwa hatarini, wengine wanakubali wengine wanakataa. Hata Bhutto alishauriwa asirudi Pakistan shauri ya usalama wake, lakini akaenda na kufa. Mbowe angweza kwenda kwenye mazishi na kumaliza kilimilimi cha waliosema kafukuzwa. Lakini pia angeweza kwenda na kufukuzwa na ingelikuwa mbaya zaidi kwake.


Mtanzania una point, lakini kumbuka hata katika uandishi wa habari, wanasema, "hakuna story yenye thamani ya maisha yako" na katika siasa, hakuna siasa yenye thamani ya maisha ya kiongozi, na umejijibu kwa Bhutto kukataa ushauri na kufa, sasa siasa atazifanyia kaburini na hakuna alichofanikisha kwa maana ya malengo ya kuwakomboa aliowakusudia kuwakomboa. Kwa Mbowe ina maana zaidi kwani siasa za Tanzania haziko Tarime pekee na hata za Tarime haziko katika msiba pekee na katika msiba si lazima Mbowe pekee anayeweza kufanya siasa kwa niaba ya Chadema. Alikuwapo Zitto hadi ktika posmoterm na wapo viongozi wa wilaya na mkoa ambao wanaendelea na kampeni. TLP na NCCR Mageuzi walifika na kumrubuni kaka yake Wangwe ajiunge nao agombee ubunge, lakini hakuna dalili na sasa siasa zinapamba moto huko Tarime, bila ya kuwapo Mbowe
 
Mtanzania una point, lakini kumbuka hata katika uandishi wa habari, wanasema, "hakuna story yenye thamani ya maisha yako" na katika siasa, hakuna siasa yenye thamani ya maisha ya kiongozi, na umejijibu kwa Bhutto kukataa ushauri na kufa, sasa siasa atazifanyia kaburini na hakuna alichofanikisha kwa maana ya malengo ya kuwakomboa aliowakusudia kuwakomboa. Kwa Mbowe ina maana zaidi kwani siasa za Tanzania haziko Tarime pekee na hata za Tarime haziko katika msiba pekee na katika msiba si lazima Mbowe pekee anayeweza kufanya siasa kwa niaba ya Chadema. Alikuwapo Zitto hadi ktika posmoterm na wapo viongozi wa wilaya na mkoa ambao wanaendelea na kampeni. TLP na NCCR Mageuzi walifika na kumrubuni kaka yake Wangwe ajiunge nao agombee ubunge, lakini hakuna dalili na sasa siasa zinapamba moto huko Tarime, bila ya kuwapo Mbowe

Halisi,

Mwanasiasa ukiogopa kifo kwenye kutetea ukweli, hutakiwi kuwa mwanasiasa.

Wewe utasema Bhutto yuko wapi? Huenda yale aliyokuwa anayaamini yanatekelezeka zaidi baada ya kufa kuliko alivyokuwa hai.

Huoni Nyerere amakuwa mungu mtu kwa TZ baada ya kufa?

Pia kama hakukuwa na umuhimu wa yeye kuwepo Tarime, kwanini akatishe ziara yake yote mpaka akafike Tarime? Naona hapo kuna kujichanganya kidogo.

Naona sasa lawama zimeanza kuhamia TLP/NCCR? Si walisema wanaungana na kuweka mgombea mmoja?

Tanzania kuna mafisi ya siasa, yakiona mnofu, yale makubaliano ya kufaidi nyama pamoja yanapotea na kila mtu anataka ashibe peke yake.

Hili ni lipicha lile lile tulilolizoea ila wachezaji ndio wamebadilika, ubinafsi badala ya maslahi ya taifa.
 
Mkuu hapa the ishu ni kwamba serikali ambayo wewe unaamini kuwa haikusema ukweli kwenye kifo cha Balali na EPA, Na sisi wengine tunaishangaa kuweza kusema ukweli kwenye kifo cha Wangwe na wengine, au?

Gari la Wangwe limepindukia kwenye eneo maarufu kwa kilimo cha karanga, huwezi lima karanga kwenye ardhi yenye miamba ya mawe chini ambayo inatakiwa kuwepo kwenye ardhi ili gari la Wangwe liumie kama lilivyoumia, au?
 
Jamani Hiyo Discussion ya Mnyika, Marehemu Wangwe naombeni tuiache....Haijengi nchi bali inabomoa Inabomoa Upinzania kwasbabu Comment zenu zinatumiaka kama wipon ya kutengeneza maangamizi mapya kwa wapinzani
 
inapokuwa ni kwa ajili ya usalama na ustawi wa taifa letu, kamwe hatutakaa kimya, hata kama ni kwa madhara ya chama chochote cha siasa

namshangaa sana jk, yeye kimyaa wakati huyu muajemi alitaka kulitumbukiza taifa kwenye vita
 
sasa kinachogomba hapa ni nini? kwamba wangwe aliuuwa halafu akaweka kwenye gari lilipata ajali before? au wangwe aliuuwa halafu mallya akaendesha gari kwenda kugonga miamba?

tusaidiane

lakini for sure hii ni ajali kama zingine
 
Mkuu, nadhani ungejitahidi kuwa unafuatilia mambo. Hakuna makosa kwani Msemaji wa Chadema ni Katibu Mkuu wa chama hicho kwa maana ya taasisi ya UKATIBU MKUU kutoka ofisi za chama hicho zilizopo Dar es Salaam na si kokote na si Dk. Slaa, Zitto, Mnyika au yeyote. Kwa mantiki hiyo kama utakumbuka wakati wote Dk. Slaa akiwa Dodoma ama nje ya Dar es Salaam, kunakua na msemaji ama Zitto, Mnyika, Antony Komu, Erasto Tumbo au yeyote seniour aliyeko ofisi za Dar es Salaam. Chama hicho hakijalishi umri wala umaarufu wa mtu na kwa mara ya mwisho, Mnyika ndiye aliyeandika barua kwenda kwa IGP na ndiye aliyekwenda TBC kutoa taarifa, sasa hapa sioni jambo la kushangaza. CCM pia kuna wakati wanafanya hivyo kwa wakati nakumbuka Makamba akiwa hayupo alikua akizungumza aliyekua Naibu Katibu Mkuu, Kapteni Jaka MWambi (Amekuwa balozi) na wakati mwingine KAtibu Mwenezi na kuna wakati hata Salum Msabaha Mbaruku na hivi karibuni tumemsikia Tambwe Hiza

Wewe na huyo mwenzako partisan kamende, acheni kukariri....ati nifuatilie mambo! mambo gani?? huu upuuuzi wenu unataka mtu nae awe "rocket scientist" kuuelewa!?? hallo?

Bila maelezo mingi ni kuwa, midomo mingi inaongeza chances za kuongea utumbo na hapo ndipo mnazidi kukaua ka-chama kenu!! kama unabisha endeleni, maana hata marehemu tuliwashauri msidili nae kivile kama mlivyofanya, mkabisha....ndivyo mlivyo, hamshauriki, hamsikii la muadhini msikitini wala la mgonga kengele kanisani! Masikio mmeweka pamba...Ujuaji wenu bila kujua ndio unakimaliza hicho chama....kalaghabao.
 
Gari la Wangwe limepindukia kwenye eneo maarufu kwa kilimo cha karanga, huwezi lima karanga kwenye ardhi yenye miamba ya mawe chini ambayo inatakiwa kuwepo kwenye ardhi ili gari la Wangwe liumie kama lilivyoumia, au?

Kupondeka kwa gari hakutegemei ardhi peke yake...Huko majangwani kwenye mchanga gari hupondeka pale zinapopinduka. The factor here is speed! Hivi hujajiuliza kama ile rolling haikuanzia kwenye tarmac na kuishia pembeni? Au conspiracy theories zina cloud your reasoning?

Wangwe alikuwa nyuma na wengi wanapokaa nyuma hawafungi mkanda. Mallya na mtu mwingine (aliyetoka baruti baada ya ajali) walikuwa mbele na wengi wa mbele hufunga mikanda.

Usipofunga mkanda unarushwa huku na kule gari linapobingirika na kichwa ni sehemu mojawapo itakayojigonga.

OUTSIDE THE BOX...

Mallya tried to save his skin by telling a lie on who was behind the steering. He knew, dead men don't talk.

The key is the third person as, why would Wangwe sit behind if there was no third person? Unless he was very sick and decided to sleep in the back seat in that case the issue of him not having put on seat belt is self explanatory.
 
Halisi,

Mwanasiasa ukiogopa kifo kwenye kutetea ukweli, hutakiwi kuwa mwanasiasa.

Hapana bwana; inategemea na wakati. Kama ni wakati wa vita sawa, huogopi kifo. Kama ni wakati wa mapinduzi, sawa huogopi kifo. Lakini katika hali ya kawaida, ya amani ambapo tunatarajia kuendesha mapambano haya kwa njia ya demokrasia na nguvu ya wananchi, mwanasiasa, kama binadamu mwingine yeyote, lazima aliweka swala la usalama wa maisha yake juu kabisa. Yeye ni binadamu kama binadamu mwingine, ana familia, watoto na wengi wa kumtegemea. Kama kuwa mwanasiasa ni kutokujali maisha yako, hapo wengi siasa itawashinda!

Lakini kuna kitu kikubwa zaidi hasa kwa mtu kama wewe ambaye ni mtetezi wa sheria na utaratibu, kwa kadri ninavyokuelewa katika post zako hapa. Mwenyekiti Mbowe, kiongozi mwenye dhamana ya chama na nchi yake, ameshauriwa na usalama wa taifa na vyombo vya usalama kwamba asibaki kwenye msiba kwa sababu usalama wake utakuwa hatarini, halafu akatae kufuata huo ushauri, huyu atakuwa ni kiongozi kweli? Akibaki halafu lolote likatokea, hata kama litafanywa na vyombo hivyohivyo, atakayelaumiwa hapo ni nani?
 
Mallya na mtu mwingine (aliyetoka baruti baada ya ajali) walikuwa mbele na wengi wa mbele hufunga mikanda.

And then Mallya akatoka akiwa mzima salimini..... na huyo mtu mwingine......., isipokuwa Wangwe tu,

ulikuwa umeanza maneno yako vizuri sana mpaka ulipofikia hapa tu mkuu!
 
Huyu Mallya hana hata vumbi!....

Insurgent,
Mkuu hiyo yako haiwezekani kuwa ni dhana isipokuwa ya upande huu!..Hivi maelezo yako hayawezi kuwa conspiracy theory isipokuwa ile inayosema kulikuwa na criminal act. Iweje ukisema vibaya serikali iwe ndio Conspirancy lakini yale yanayoikinga serikali kutohusika ndio yenye Ukweli wakati ktk maelezo yenu hamjui kwa uhakika kama kuna mtu wa tatu aliyekimbia.. Maswali yenu yasiwe kwa nini alikimbia, why huyu kijana hana hata vumbi na mengine mengi tu ambayo sisi tumejaribu kuyatazama. Kuna ubaya gani kwenda hatua moja zaidi kutafuta ukweli.

Mkuu hapa sote tunajenga hoja tu hakuna mwenye ukweli hata O J alishinda kesi kutona ana glove ambayo haikutosha!.. speculation from both sides zitaendelea kuwepo hata kama haziwezi kukubalika mahakamani, ndio starehe ya Mijadala mkuu!
Duh, mikanda ina serve kishenzi.. Na lini Bongo watu wameanza kufunga mikanda safari ndefu..
 
Huyu Mallya hana hata vumbi!....

Na kesi iliyofunguliwa atashinda maana hakuna ushahidi utakaothibitisha pasipo shaka yoyote kwamba yeye ndiye aliyekuwa anaendesha gari wakati ajali inatokea. very sad, wamefanikiwa.
 
Jamani kwa wenzetu mlio Musoma tafadhali tunaomba kujua ripoti ya mtaalamu wa familia inasemaje kuhusu kifo cha Chacha Wangwe?.
 
Nziku,
hadi sasa hivi ni waandishi wa habari wanaozungusha statement zao kukinga kitu kisichofahamika.. Mallya alisema yeye hakuwa dereva isipokuwa marehemu, Ilipochunguzwa na kukutwa damu nyingi kiti cha nyuma wakabadilisha statement na kuwa Chacha Wangwe marehemu alikuwa kiti cha nyuma na huyu kijana ndiye aliyeendesha. Mara ikajulikana hana liseni wakadai kulikuwepo mtu wa tatu yaani dereva.. Yuko wapi?... statement ikabadilika tena kuwa Mallya ndiye alikuwa dereva na kafunguliwa mashtaka.

Ajabu ni kwamba haya yote ni majibu yanayotolewa na vyombo vya habari na serikali vyombo ambavyo havikuwepo ktk ajali na wala hakuna uhakika isipokuwa speculations ambazo ajabu zinatumika kuandikwa ktk magazeti yetu kabla ukweli haujajulikana.

Mimi bado kabisa nahitaji maelezo ya kisawasawa kukubaliana na hizi habari za utunzi wa waandishi wetu. Hadi sasa hivi kazi kubwa wanayoifanya ni kutafuta mchawi wakati hakuna habari inayotupa hata kwa uchache kilitokea kitu gani hasa gari likaacha njia kwenda machakani. Kitu gani kichomuua Wangwe ama pigo la sehemu gani ya kichwa lililosababishwa na blaa blaa ndilo lilikuwa sababu ya kifo.
Statement ya Mallya ndio muhimu iwe ile ya kwanza ama sasa hivi amesema kitu gani na ameyazungumza haya chini ya wakili gani!.. Huyu kijana anaweza kabisa kulazimishwa kutunga ama kukubali maenezo yaliyokwisha andaliwa.
 
Wakuu,
Nimeangalia taarifa ya habari ya Chaneel Ten ya saa moja jioni hii, umoja wa vyama vinne vya upinzani wametoa tamko kuwa bado hawaamini kuwa Marehemu Wangwe alikufa kwa ajali kutokana na taarifa walizonazo kuhusu Deus Mallya, wamesisitiza kuwa uchunguzi wa kina ufanyike kuhusu kijana Deus, maana taarifa walizonazo zinaonesha kuwa aliwahi kuchukua mafunzo ya kijasusi.

Aidha, wamesisitiza kuwa wakati wa msiba Tarime kulikuwa na vurugu na kama polisi wasingefanya kazi yao wakurya wangechinja watu kwa sime, marungu na mapanga waliyokuja nayo msibani. Mrema na Mbatia wamelalamika sana na kusema kuwa wanawashangaa watu wanaokataa kuwa hakukuwa na vurugu wakati walikaribishwa na mabango yaliyoandikwa "hakuna Wangwe, Hakuna Amani", au walitaka mpaka waone watu wamechinjwa ndio waamini kuwa kulikuwa hakuna amani.

Naomba kuwasilisha, Mungu aturehemu.
 
Mkandara,

Serikali ya Tanzania na hasa CCM wanafikiri Watanzania ni wajinga na wapumbavu.

Wanafikiri hatuna uwezo au upeo wa kufikiri kwa kuwa wao ni Viongozi na Dola.

Ukiangalia majadiliano yaliyopo hapa kuhusu hii ajali ya Wangwe, matukio mengine ya Viongozi au Wanasiasa kupoteza maisha kiajabu ajabu, utagundua kuwa Wengi wetu tuliopo hapa, pamoja na ushabiki wa siasa au chumvi, tunafahamu tunachozungumza na tuna upeo mkubwa sana wa kuunganisha nukta au kutoa vigezo ambavyo vinadhihirisha kuwa kuna uzembe au hujuma.

Hata ukija katika mambo ya kawaida ya jamii, siasa na hasa sasa hivi suala la Uhujumu, Ufisadi na Mikataba mibovu, wengi wa Serikali na CCM na hata Watanzania wenzetu walioko nyumbani, wanatguona sisi tunaoishi nje ya nchi kuwa ni punguani fulani ambao hatujui tunachokisema au hatuelewi hali halisi.

Ukweli kwenu nyote mnaotushangaa uwezo wetu wa kufikiri na kutoa mifano kedekede kuwa ni nini kilitokea kwenye ajali hii ni kutokana na upeo wetu na kujifunza kwetu kwa kukaa katika nchi za wenzetu ambao sayansi na maarifa na hasa kufikiri kwa umakini vimepewa kipaumbele.

Msifikiri kazi yetu ni kubeba maboksi tu, au tukienda kusomea Uchumi, hatujifunzi sheria, sayansi au ujenzi. NI mfumo wa kielimu na kijamii ambao umezifanya nchi zilizoendelea kuwepo hapo zlipo ni kutokana na kuchochea fikra na upeo kwa watu wao.

Hawa jamaa wanaona kuwa tunawategemea sana, na hili ndilo kosa tunalolifanya kila miaka mitano, kukubali Ubwabwa, Ulabu, Kikoi na Gagulo.

Soma makala ya Mwanakijiji leo Tanzania Daima, anawafundisha Polisi kazi zao.

Soma tulichoandika humu ndani, tunafundisha Polisi kazi zao kutokana na ujuzi wa kuishi kwenye mazingira yanayotufundisha ni vipi hii ajali inawezekana haikuwa ajali ya bahati mbaya bali ni ajali iliyokusudiwa.

Hata hawa waandishi wa habari na mfadhili wao mkuu Rostam, bado wanafikiri Watanzania ni wajinga na punguani. Ole wao, tutawaumbua!
 
Kwamba wewe unataka kuwaambia watu kuwa Mbowe hakuwa kwenye wakati mgumu, na wala hakuondolewa pale akisindikizwa na askali. Mimi nilikuwepo jana na hivi niko Mwanza yaliyoandikwa ni kweli ndivyo ilivyo kuwa na kama hamuamini muone kama siku ya mazishi Mbowe atakuwepo. Halafu kuhusu habari kufanana hiyo siyo ajabu inategemeana na chanzo cha habari

Kufanana kwa habari ni jambo la ajabu, kwa vile hata katika biblia injili ziko nne hazifanani kama habari hii
 
Hawa jamaa kiboko, walipoona gumzo limenoga la ufisadi wakaona tuwapoteze,
SAWA ILA TUKO PALEPALE
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom