Kifo cha Mhe. Chacha Wangwe na uchunguzi wake

Kifo cha Mhe. Chacha Wangwe na uchunguzi wake

Status
Not open for further replies.
Mkuu, nadhani ungejitahidi kuwa unafuatilia mambo. Hakuna makosa kwani Msemaji wa Chadema ni Katibu Mkuu wa chama hicho kwa maana ya taasisi ya UKATIBU MKUU kutoka ofisi za chama hicho zilizopo Dar es Salaam na si kokote na si Dk. Slaa, Zitto, Mnyika au yeyote. Kwa mantiki hiyo kama utakumbuka wakati wote Dk. Slaa akiwa Dodoma ama nje ya Dar es Salaam, kunakua na msemaji ama Zitto, Mnyika, Antony Komu, Erasto Tumbo au yeyote seniour aliyeko ofisi za Dar es Salaam. Chama hicho hakijalishi umri wala umaarufu wa mtu na kwa mara ya mwisho, Mnyika ndiye aliyeandika barua kwenda kwa IGP na ndiye aliyekwenda TBC kutoa taarifa, sasa hapa sioni jambo la kushangaza. CCM pia kuna wakati wanafanya hivyo kwa wakati nakumbuka Makamba akiwa hayupo alikua akizungumza aliyekua Naibu Katibu Mkuu, Kapteni Jaka MWambi (Amekuwa balozi) na wakati mwingine KAtibu Mwenezi na kuna wakati hata Salum Msabaha Mbaruku na hivi karibuni tumemsikia Tambwe Hiza

Halisi,

Nakubaliana na Yournameismine, kwenye jambo moja hilo hilo hakuna haja ya kuwa na wasemaji watatu. Ni rahisi mno kujichanganya.

Pia hata kama Dr. Slaa yupo Dodoma sioni kwanini ashindwe kuwa msemaji wa chama, maana anaweza kupatikana kwa simu na njia zingine.

Nitaelewa kama atakuwa nje ya nchi.

Labda wana uwezo mkubwa wa kufanya cordination miongoni mwao, ila kwa mwanadamu ambaye wengine tunamjua, ni rahisi mno kuvurunda pale jambo moja linapoongelewa na watu zaidi ya mmoja. Kwa kutambua ukweli huo ndio maana kwenye vyama vya siasa mpaka kwenye kampuni ni kawaida kuwa na msemaji mmoja tu. Huyo msemaji anakuwa briefed mambo yote ili asijichanganye.

Kwa hili jambo CHADEMA wangeweza kumwachia Mnyika ambaye ndiye alianza nalo na badala yake wakampa briefings za kutosha ili awe na nondo zote.

Uzuri wa siasa hakuna jibu moja kwahiyo hatuwezi kuwa 100% sure kama njia waliyotumia CHADEMA ni mbaya au nzuri. Ila historia inatufundisha kwamba kuwa na mtu zaidi ya mmoja ni rahisi mno kujichanganya.
 
mkamap,

Nianvyofahamu mimi humu ndani kuna makundi mawili makubwa yanayotofautiana kimawazo - jambo ambalo si baya kwa chombo huru kama JF.

Kuna wale wanaoona uchungu kwa yanayototendeka nchini chini ya uongozi uliopewa mamlaka na wananchi. Hawa hawako tayari kumtafuta mchawi nje ya hii serikali kwa sababu waliipigia kura CCM na serikali yale kwa ahadi zilizotolewa za kuleta matumaini ambazo sasa ni wazi hata kwa kipofu kuwa hazikuwa za kweli. Serikali isiyo na ubia na mtu, haiwezi kuwa held at ransom na kikundi cha watu na ikashindwa kufurukute hata kidogo.

Kuna wale ambao kwa sababu ambazo haziko wazi wanatetea hiyo hiyo system iliyokosa mwelekeo wa maendeleo katika karibu kila nyanja. Wao kila mara watatafuta mchawi nje ya hiyo serikali na kama kuna tukio lolote lile linaloweza kuipa ahueni serikali hawasiti kulishupalia. Vyama shindani kama CHADEMA ambayo imeonyesha kwa kiwango kikubwa kukabiliana na uovu katika jamii, kinakuwa target ya watu hawa kukizuulia kila aina ya vituko.

Mimi siijui CHADEMA na wala simjui Mbowe apart from the fact kwamba ni chama shindani na mwenyekiti wake ni Mbowe. Naweza kudiriki kusema kuwa watu wanaoniimpress CHADEMA, Mbowe si mmoja wao. Lakini matendo ya serikali chini ya CCM has driven me to a point ya kutokuiamini tena na niko tayari kuungana na mtu ama kundi lolote lile litakaloonyesha upinzani wa kweli dhidi yao.

Mkamap, nakushangaa kwa jitihada zako za kuwakatisha tamaa hawa watu ambao kwa akili yangu kidogo nawaita mashujaa. Kupambana na zimwi la CCM na taasisi zake kunahitaji ushupavu ambao watu wengi yawezekana ama hawana au wanalinda maslahi ya kibinafsi na si ya Taifa. Hawa watu ambao wamejitolea mhanga - kumbuka msururu wa waliojaribu na hatima zao - ndio tegemeo tu hai lililobaki kwa nchi yetu ya Tanzania.

Hebu fikiria kwamba sasa Mkapa anaweja kuzomewa na vijana mtaani bila kujali aliwahi kuwa Raisi, watoto wa shule wanaweza kuwataja hadharani mafisadi bila kujali huyu ni mwenyekiti wa maadili wa CCM, wananchi wanaweza kulala barabarani kumzuia Kikwete asipite bila kuwasikiliza bila kujali ni Raisi wa nchi, JF wanaweza kumkoma nyani giledi bila kujai ni CEO wa multinational conglomerate - jamani hii ni achievement dhidi ya UFISADI.

Mkamap, wewe pamoja na wote unaokubaliana nao ukianza kupima haya kwa mtizamo wa CCM na CHADEMA, huitendei mema nchi yako ya Tanzania. Sisi wengine hata kuwa mwanachama tu wa chama chochote hatujafikiria na mimi nimejiunga na JF mwaka huu baada ya kufuatilia mada mbalimbali kwa miaka karibu miwili. Niliridhika na maoni ya wachangiaji na hata pale wanapotofautiana, lengo kubwa ni kuisaidia nchi yetu.

Mwisho naomba katika hili msitukatishe tamaa na kama mnayo imani ya kweli kweli kuwa JF si huru, MKAE PEMBENI. Nimeshuhudia kejeli, majigambo, uwongo na mengine mengi tu, lakini hili la JF kuwa CHADEMA imetia fora na kama ikithibitika hivyo na mimi nitakaa pembeni.

I can feel your pain brother/sister. Ninaposoma maandiko yako haya ni kama nakuona, na naona machozi yakikutiririka, kama sio machoni basi moyoni.

Katika mapambano haya hawatakosekana wa kuweka vizingiti na kwa hakika sio wote watakaofurahia, lakini ni wazi kwamba wananchi walio wengi wanatuunga mkono, na ndio muhimu. Kwa hiyo wakatisha tamaa watakuwepo lakini the good news ni kwamba tutawashinda, kwa sababu haya mapambano siyo ya chadema tena, bali ni ya wananchi wenyewe, chadema ni chombo tu au tungeweza kusema ni silaha. Hata wakituponya silaha zitanunuliwa zingine maana waliiua NCCR wakidhani ndio mwisho wa mageuzi Tanzania, lakini, kwa majuto yao makubwa, leo wameibuka wengine.

Keep the spirit burning, this war must won. And, yes there will be hurdles and bumps and muds, here and there, but the wind of change is unstoppable!
 
Mag3

Leo hii mnajichanganya zaidi pale mnapotaka vyombo vya habari viandike habari mnavyotaka ninyi. You are asolutely Wrong! sasa hivi siyo kipindi cha nyie kutegemea kuandikwa vizuri. Mlitegemea nini, Mbowe ahudhurie msiba wa mtu ambaye kila mtu anajua ni adui yake na kila mtu ali pay attention kuona kinachotokea, na kesho yake wauze magazeti. Matokea yake hayatakiwi kushangaza. Nashauri CHADEMA wakae chini watulie kivuli kipite wajipange upya, tuendeleze libeneke.
Tutafakari sequence ya matukio haya ndani ya CHADEMA (kwa kutokuzingatia tukio la kifo cha Wangwe pekee yake) tutafute chanzo chake Objectively kuanzia uchanguzi wa Desemba 2007, tuzipime hoja za marehemu Wangwe (Ukabila, ruzuku kwa wananchi), tuzingatie kwa nini watanzania wanamlilia Wangwe na nini kinaandikwa zaidi (alichotuachia Wangwe ili tumkumbuke) halafu ndo tutafute mchawi.

Unachanganya mambo makubwa mawili:

I. Hakuna mtu katika chadema au hapa JF anayetaka "vyombo vya habari viandike habari [tunavyotaka sisi]", na sijui unaposema ninyi hao ninyi ni akina nani. Tunachosema hapa ni kwamba vyombo vya habari viandike ukweli. So far hakuna ukweli kwamba wananchi wa Tarime walibeba mishale na mapanga, na wala hakuna ukweli kwamba Mbowe alifukuzwa kwa mapanga na mishale huko Tarime kama walivyoandika waandishi wa habari. Ni kwa sababu ya uwalakini wa habari hizi ndio maana wahariri wameunda kamati kuchunguza nia hasa ya habari zilizoandikwa kwenye msiba huu. Sasa tell me, wewe unashabikia vyombo vya habari kuandika habari za uongo, na kusema ndivyo siasa ilivyo, unaishi nchi gani hiyo mwenzetu?

II. Hakuna mtu ambaye alikuwa anamkosoa Wangwe kuhusu uongozi wake ndani ya chadema ambaye sasa amebadili msimamo baada ya kifo chake. No, far from it. Na haina maana kwamba kupingana na Wangwe ndio sasa imekuwa kwamba waliouwa wanamkosoa walikuwa hawatambui potential yake. Again, wrong, and far from it. Na haina maana kwamba kwa kuwa ulikuwa hukubaliana naye basi akifariki hutasikitika, again you are just grossly and awfully wrong and, and to suggest this, you are just displaying your ignorance about human nature. Unachojaribu kufanya wewe kwa kuwaona wale waliokuwa wanampinga Wangwe wanafiki kwa kusikitikia kifo chake ni kujaribu kuwavua ubinadamu, jambo ambalo huwezi, na ninaanza kuwa hata na wasiwasi kama kweli unajua sawasawa maana ya unafiki. Ukijifunza vizuri maana ya neno mnafiki utagundua kwamba kujaribu kuwazomea na kuwazuia wale waliokuwa hawakubaliana naye wasisikitikie kifo chake ndio unafiki wenyewe huo!!
 
Halisi,

Nakubaliana na Yournameismine, kwenye jambo moja hilo hilo hakuna haja ya kuwa na wasemaji watatu. Ni rahisi mno kujichanganya.

Pia hata kama Dr. Slaa yupo Dodoma sioni kwanini ashindwe kuwa msemaji wa chama, maana anaweza kupatikana kwa simu na njia zingine.

Nitaelewa kama atakuwa nje ya nchi.

Labda wana uwezo mkubwa wa kufanya cordination miongoni mwao, ila kwa mwanadamu ambaye wengine tunamjua, ni rahisi mno kuvurunda pale jambo moja linapoongelewa na watu zaidi ya mmoja. Kwa kutambua ukweli huo ndio maana kwenye vyama vya siasa mpaka kwenye kampuni ni kawaida kuwa na msemaji mmoja tu. Huyo msemaji anakuwa briefed mambo yote ili asijichanganye.

Kwa hili jambo CHADEMA wangeweza kumwachia Mnyika ambaye ndiye alianza nalo na badala yake wakampa briefings za kutosha ili awe na nondo zote.

Uzuri wa siasa hakuna jibu moja kwahiyo hatuwezi kuwa 100% sure kama njia waliyotumia CHADEMA ni mbaya au nzuri. Ila historia inatufundisha kwamba kuwa na mtu zaidi ya mmoja ni rahisi mno kujichanganya.

Inabidi kwanza kuelewa context ya hili jambo. Zitto alienda kwenye kikao cha wahariri (yeye sio mhariri) kwa ajili ya kuwakilisha malalamiko ya chadema juu ya taarifa za vyombo vya habari kuhusu msiba ule. Na ilikuwa ni muhimu aende yeye, badala ya Mnyika au Slaa au mtu mwingine yeyote katika chadema, kwa kuwa yeye ndiye alikuwa mwakilishi rasmi wa CHADEMA huko Tarime na yeye nidye aliyeshuhudia matukio ya msiba huu mwanzo hadi mwisho. Sasa ningeshangaa sana kama ingetokea kwamba Mnyika, ambaye hakuwepo kule Tarime, ndiye ajibu maswali ya waandishi wa habari kuhusu ukweli au uwongo wa kufanyka fujo kule.

Lakini hili la uongo wa Mbowe kufanyiwa fujo sio tu kwamba linaelezwa na CHADEMA. Hata familia ya marehemu, kupitia Profesa Samwel Wangwe, wamekanusha vikali madai haya.
 
gari limeharibika sana. Mbona huyo Mallya yeye hajaumia???????.Ajali ya Diana aliyepona alikuwa koma kwa mwaka. Jamani tujiulize kilakitu .
 
Inabidi kwanza kuelewa context ya hili jambo. Zitto alienda kwenye kikao cha wahariri (yeye sio mhariri) kwa ajili ya kuwakilisha malalamiko ya chadema juu ya taarifa za vyombo vya habari kuhusu msiba ule. Na ilikuwa ni muhimu aende yeye, badala ya Mnyika au Slaa au mtu mwingine yeyote katika chadema, kwa kuwa yeye ndiye alikuwa mwakilishi rasmi wa CHADEMA huko Tarime na yeye nidye aliyeshuhudia matukio ya msiba huu mwanzo hadi mwisho. Sasa ningeshangaa sana kama ingetokea kwamba Mnyika, ambaye hakuwepo kule Tarime, ndiye ajibu maswali ya waandishi wa habari kuhusu ukweli au uwongo wa kufanyka fujo kule.

Lakini hili la uongo wa Mbowe kufanyiwa fujo sio tu kwamba linaelezwa na CHADEMA. Hata familia ya marehemu, kupitia Profesa Samwel Wangwe, wamekanusha vikali madai haya.

Sioni tatizo kwa Chadema kumtuma Zitto kama Naibu Katibu Mkuu na mtu aliyekuwapo Tarime hadi mwisho. Hata kama Zitto asingekuwapo Tarime, kama Naibu Katibu Mkuu, alikua na haki ya kuzungumza. Siwezi kuwasemea Chadema, ila ninavyoona na kwa mtiririko wa matukio, wanaaminiana na hakuna mwenye kuhodhi mamlaka ya kuzungumza, mradi tu mawasiliano yanakuwapo na kupata baraka za uongozi wote wa juu. Mtanzania unapohoji uwezo wa kuwasiliana, nadhani huwatendei haki Chadema kwa kuwa wana simu za mkononi, kuna mitandao na kadhalika. Sidhani kama Dk.Slaa alitakiwa aje toka Dodoma kukutana na Wahariri, lakini pia kwa ninavyomfahamu ZItto, Chadema wanamuamini zaidi kuwa anamudu vyema kuongea na waandishi wa habari na walio wengi wanamheshimu. Mbona hujasema Tambwe, alipozungumzia suala nyeti la "Zanzibar si nchi?"
 
MWL KITILA

MNAFIKI hujinafikisha mwenyewe wala hamna haja yakutupa defination ktk hilo .

Mfano RIP alipotimuliwa uenyekiti Chadema na wengi humu JF walisema chacha ni mzigo .anakihujumu chama na anatoa siri za chama kwa RA na CCM ,Anaeneza uongo kwa kukigawa kwa staili ya ukabila na ruzuku ya kwamba CHACHA alibomoa UDSM akijaribu kuiba fedha na akakibilia kenya na ya kwamba CHACHA amemzalisha mkewe watoto 12 na kumkimbia na sasa yupo ktk kimada chake DAR.

LEO Marehemu hatunaye hao hao waja na stori mpya ya kwamba RIP Chacha alikua mpigania haki na demokrasia. Mtu aliyeelezewa hapo juu anaweza kua mpigania haki na demokrasia??

Huyu Mbatia naye hivyo hivyo CHADEMA mtimueni chacha uanachama maana tunamjua alikua NCCR alikivuruga chama na kukiangusha .Juzi kwenye mazishi anasema chacha alikua mpigania haki na mwanamapinduzi ktk demokrasia na tumuenzi.

Huu unafiki huu yani hata MTOTO GENDERE mwituni naye atautambua ,HAWA jamaa ni manafiki sana ndio maana hawawezi kuungana kutengeneza chama chenye nguvu maana malengo yao si kuikomboa nchi ila malengo yao ni kuongeza RUZUKU.
 
Opinion

Monday, August 20, 2001

Making a Killing from Politics Can be Deadly By MICHEAL OKEMA

In a span of eight months, six members of the Tanzania National Assembly have died. Apart from the late vice president Omar Ali Juma, there was Ernest Nyanda, MP for Busega. Then came Mohammed Bhiku of Solwa, to be followed by Crispin Hauli of Ludewa and Abbas Gulamali of Kilombero. Now Sebastian Kinyondo, MP for Bukoba Rural, has gone to his eternal rest (August 14).

The late Nyanda was Minister for Home Affairs during President Mkapa's first term. He was re-elected in October 2000 but failed to make it back to the Cabinet. Within two months, he was dead.

In the run-up to the 1995 general election, Dr Alex Khalid, a businessman tipped to become one of the new Tanzanian millionnaires, lost in the primaries for Mtama constituency. Then Alhaji Namkua, who won in the primaries, died before the general election. This cleared the way for Dr Khalid to contest and become Mtama MP. Dr Khalid in turn died three years later.

Ludewa is another constituency notorious for "killing" its MPs. First was Horace Kolimba, who died in 1997. Kolimba was once CCM secretary general before falling out with the late Mwalimu Nyerere in 1993.

In 1995, Kolimba made an unsuccessful bid for the presidency. He then turned on CCM, accusing the party of losing sense of direction. Kolimba was summoned to defend himself before the party's top brass. He died the same evening of a heart attack.
 
MWL KITILA

MNAFIKI hujinafikisha mwenyewe wala hamna haja yakutupa defination ktk hilo .

Mfano RIP alipotimuliwa uenyekiti Chadema na wengi humu JF walisema chacha ni mzigo .anakihujumu chama na anatoa siri za chama kwa RA na CCM ,Anaeneza uongo kwa kukigawa kwa staili ya ukabila na ruzuku ya kwamba CHACHA alibomoa UDSM akijaribu kuiba fedha na akakibilia kenya na ya kwamba CHACHA amemzalisha mkewe watoto 12 na kumkimbia na sasa yupo ktk kimada chake DAR.

LEO Marehemu hatunaye hao hao waja na stori mpya ya kwamba RIP Chacha alikua mpigania haki na demokrasia. Mtu aliyeelezewa hapo juu anaweza kua mpigania haki na demokrasia??

Huyu Mbatia naye hivyo hivyo CHADEMA mtimueni chacha uanachama maana tunamjua alikua NCCR alikivuruga chama na kukiangusha .Juzi kwenye mazishi anasema chacha alikua mpigania haki na mwanamapinduzi ktk demokrasia na tumuenzi.

Huu unafiki huu yani hata MTOTO GENDERE mwituni naye atautambua ,HAWA jamaa ni manafiki sana ndio maana hawawezi kuungana kutengeneza chama chenye nguvu maana malengo yao si kuikomboa nchi ila malengo yao ni kuongeza RUZUKU.

Kaka unachanganya madawa. Huhitaji utaalamu wa aina yoyote kujua kwamba unafanya usichoamini. Siamini kwamba hujui ulisemalo. Nadhani unaweza kuwa unafanya kama walivyofanya Ze Comedy katika mchezo wao mmoja wakionyesha mazishi. Pengine na wewe unafanya "Ze Comedy" humu JF kama si uko kwa "kazi maalumu"
 
Kaka unachanganya madawa. Huhitaji utaalamu wa aina yoyote kujua kwamba unafanya usichoamini. Siamini kwamba hujui ulisemalo. Nadhani unaweza kuwa unafanya kama walivyofanya Ze Comedy katika mchezo wao mmoja wakionyesha mazishi. Pengine na wewe unafanya "Ze Comedy" humu JF kama si uko kwa "kazi maalumu"

Currently Active Users Viewing This Thread: 17 (4 members and 13 guests)
Halisi, Augustoons, mfwatiliaji, mkamap
 
kwa sababu kila siku ya Mungu, alikuwa akifuatana na mtoto wake aliyekuwa akimshikia dawa zake maalum za moyo,

Uchunguzi wa mwili wa marehemu ulisema hivyo hivyo kwamba kafa kwa heart attack ambayo ilikuwa ni matokeo ya intensive pressure aliyokuwa nayo kabla na kwenye hicho kikao.

Uchunguzi wa mwili wa marehemu ulisema hivyo hivyo kwamba kafa kwa heart attack ambayo ilikuwa ni matokeo ya intensive pressure aliyokuwa nayo kabla na kwenye hicho kikao. Kama una report inayosema tofauti, tuletee. Wakati anafariki 1997 wengine tulikuwa kwenye hivi vijiwe na suala lake lilijadiliwa vizuri sana kule Tanzanet.

Suala la kuzunguka kila sehemu na mtoto wake ni hearsay, hakuna ukweli kabisa. Ni mtoto gani huyo aliyekuwa anazunguka naye ili kumbebea dawa?
Kolimba alikuwa anaumwa, laiti hata angemwona daktari yoyote wa magonjwa ya moyo angemshauri kabisa asiende kwenye kile kikao akiwa katika hali ile. Au angechukua tahadhari muhimu kabla ya kwenda.

Wacha tuendelee na mambo mengine maana hili la mtoto kuwepo au kuto kuwepo haliongezi tija yoyote. Hata kifo cha Mwaikambo kilikuwa ni ajali tu. Inasikitisha kwamba lazima tuweke mkono wa mtu kwenye kila kifo. Tabia hii inatufanya tusiwe waangalifu maana tunaondoa uzembe kutoka kwetu na kuuhamishia kwa wengine. Badala ya watu kujifunza hapa kuwa na madereva wazuri, watu wanaamua kuwa vilaza bungeni na kutokukosoa mambo wakifikiri hapo hakutakuwa na mkono wa mtu. Hata watu wanaokufa kwa ngoma, tunasema kuna mkono wa mtu, hivi kweli tuko serious?


Mkuu Mtanzania,

Naona unajichanganya mwenyewe, niliposema ugonjwa wa moyo ulikata baadaye tena unasema kuwa alikufa kwa ugonjwa wa moyo, anyways siwezi kuamini maneno ya zaidi ya watoto wa marehemu, kwamba na wao wanadanganya hapana, kwamba eti wake za marehemu wanadanganya? hapana, a day kabla Kibona hajafariki nilikuwa naye nyumbani kwa balozi wetu DC wakati huo akiwa Nyirabu, sio siri kuwa hakuwa sawa sawa kwa sababu dalili zilikuwa wazi,

Mwaikambo, ile ajali walisoema imetokea mbele ya jengo la ubalozi wa Rwanda, nayo pia ilikuwa ni Ze-Comedy of all times, hakuna anayeweka mkono wa mtu, lakini watu wanaowajali marehemu wanapouliza serious questions with evidence, huwezi kuwa-dismiss kuwa ni hearsay, mke wa Rutihinda hawezi kuwa anasema uongo kuhusu kifo cha mumewe, kwa sababu waliomuua then waka-plant story kuwa alikuwa na ngoma, that is unfair kwa familia za marehemu,

Kushindwa kupata ukweli wa vifo vya viongozi wetu kwa sababu ya mazingara yanayokuwa under control ya waliohusika, haina maana kukata tamaa kabisa kwa sababu kuna siku zoezi linaweza kubadilika tukashika power watu wenye uchungu na taifa, tutazifufua kesi zote hizi bro na kuwafikisha kwenye mikono ya sheria wahusika wote watakaokuwepo, maana wote wanafahamika na ushahidi upo, mkuu nimepoteza a relative na huu mchezo tayari na ninajua deatils zote za kifo chake, ambazo hazikusemwa na serikali, sasa kama wewe unaamini kuwa hawa viongozi wote wanaokufa kwa kutaka mabadiliko hawakuuliwa good for you, ila tu huwezi kuwa dismiss wanaofikiri tofauti eti kuwa ni uzembe wa kutaka kuhamishia kwa wengine mkuu that is very irresponsible statement kwa wenye ndugu waliwahi kufa kwa utata na wanaoujua ukweli, wake wa rutihinda na Kibona hawawezi kuwa wanasema uongo kuhusu vifo vya waume zao,

Waliokufa kwa ngoma wanafahamika haijawahi kuwa siri, Nyanda RIP alikufa kwa ngoma sio siri na kuna walioko kwenye power sasa hivi wana ngoma sio siri kabisa mkuu, kuwepo kwenye hizi forum wakati wa vifo vyao haibadli ukweli kuwa vifo vyao vina utata, halafu hizi precautions measures mnazozisema ingekuwa ni rahisi kujua kuwa leo unaenda kufa hivi ni nani asingezichukua mapema? Unafikiri Kolimba angekubali kwenda kwenye kile kikao? Au Wangwe juzi angekubali kusafiri?

I mean kutokukubali kwako na mijadala yaina fulani haina maana wengine wote tuache kujadili, in fact hiyo ndio hasa sababu tuko hapa JF ni kujadili ishus bila kuziogopa na kuelimishana kutokana na yal tunayoyajua, na tutaendelea kufanya hivyo bila wasi wasi wowote, kama vile tulivyojadili kifo cha Balali wewe ulisema hajafa ambayo ni haki yako na kuna tuliosema amekufa ambayo ni haki yetu pia, the ishu ni uzito wa hoja tu!

Ahsante Mkuu, na week end njema na kwako mkuu!.
 
Kaka unachanganya madawa. Huhitaji utaalamu wa aina yoyote kujua kwamba unafanya usichoamini. Siamini kwamba hujui ulisemalo. Nadhani unaweza kuwa unafanya kama walivyofanya Ze Comedy katika mchezo wao mmoja wakionyesha mazishi. Pengine na wewe unafanya "Ze Comedy" humu JF kama si uko kwa "kazi maalumu"

Kaka
Huo unafiki utawamaliza.
Ubinadamu unataburika na unafiki nao pia unataburika wala hakuna haja ya madawa.
mfano mara nyingi hata ukikuta jambazi/mwizi kaua wa ubinadamu unakuingia unapata huzuni,unasikitika lakini kama wewe mwenyewe awali ulitamka mbele ya kadamnasi kua yule jamaa ni jambazi na mwizi harafu baada ya kuuawa ukasema yule jamaa hakua mwizi wala jambazi na alikua mtu wa haki basi wewe utakua mnafiki mkubwa .

Naamini sana ninayosema maana yamo humuhumu ndani ya forum hii wala haina haja ya kwenda mahala kuyapata na uzuri wengi wameyasoma.Comedy ni kama hizo zako mkuu tena zinatisha.

Unajua mnakimbilia mno kua tunafanya kazi maalumu wewe nithibitishie kama hayo maneno hayakusemwa na chadema,jf na Mbatia ukithibitisha ni ya uongo hapo 100% nitakua nimetumwa na mimi ni mnafiki lakini ukishindwa wewe ndiyo umetumwa na mnafiki mkuu hata shetani atawaogopa maana hata digrii ya unafiki itakua imempita .
 
Zamani tulikuwa tunaambiwa Kenya ni mabingwa wa hii tekero, lakini katika miaka 20 iliyopita Tanzania tumekuwa mstari mbele na kuwa nambari wani.


Mkuu Kishoka,

You got this one right, halafu kama kweli bongo hatuna hili tatizo sasa inakuwaje viongozi wetu hawakubali kula dinner za kualikwa kama zamani? I mean bongo sasa tumefikia pabaya sana mkuu, hili ninakuabli lakini dawa ni mabadiliko tu ya uongozi na yanakuja ingawa sio leo,

Hata serikali yetu sasa hivi inaelewa sana hili kuwa sasa hali sio nzuri sana mkuu, na sio suala la kujigamba ila ni jana tu niliiitwa kwenye special kikao ili ni-explain jinsi JF tunavyoiona hii nchi inakokwenda for almost 5 hours, I had to explain misimamo mingi sana tuliyonayo hapa kuhusiana na jinsi tunavyo ona uongozi wa taifa letu, kwa sababu hata serikali pia sasa inaona the change kwenye tone zetu hapa, kuwa wengi hapa ambao zamani tulikwua na hope, sasa tumeanza kukata tamaa kabisaa na hilo linawasumbua sana baadhi ya watendaji wakuu wa taifa letu kwa sababu wananiambia in private kuwa hapa wanapata maoni muhimu sana on our nation kuliko mahali popote pale bongo,

I wish in the future ningeweza kuwa-include members wengine hapa ninapoitwa kwenye hivi special vikao, lakini pia ninaishukuru serikali kwamba hatuko hapa kupoteza muda kama wengi mnavyofikiri, kwamba kila linalosemwa hapa, ukweli ndugu zangu ni kwamba linaangaliwa sana na watendaji wetu, ndio matatizo yanaweza kuwepo kwenye ufuatiliaji, lakini haina maana kama nilivyojifunza sana jana kuwa hakuna follow up kabisa, hapana!

Ahsante mkuu na samahani kwa kutoka nje ya mada kidogo!
 
Kaka
Huo unafiki utawamaliza.
Ubinadamu unataburika na unafiki nao pia unataburika wala hakuna haja ya madawa.
mfano mara nyingi hata ukikuta jambazi/mwizi kaua wa ubinadamu unakuingia unapata huzuni,unasikitika lakini kama wewe mwenyewe awali ulitamka mbele ya kadamnasi kua yule jamaa ni jambazi na mwizi harafu baada ya kuuawa ukasema yule jamaa hakua mwizi wala jambazi na alikua mtu wa haki basi wewe utakua mnafiki mkubwa .

Ni kweli ndio maana leo, Adamu Kighoma Ali Malima, ni Naibu Waziri na alimwagiwa kila aina ya sifa. Ndio maana Spika wa Bunge na wabunge wa CCM waliokua wakimuona Chacha kama "mwehu" walilia na kumwagia sifa kem kem. Chacha hakufukuzwa uanachama na hata uongozi alisimamishwa tu na kulikua na uwezekano wa kuwa angeweza hata kushinda katika vikao vya juu. Chacha aliendelea kuwa na mahusiani mazuri na viongozi wenzake wa Chadema na ni mbunge pekee aliyefika kwanza kumuona Zitto hospitali na alikaa kwa muda mrefu pale Muhimbili, na hakua mnafiki, alikwenda kwa dhati. Sasa leo unataka watu waende msibani kwa mila zetu, wasema Chacha hafai na mengineyo!!!!!?? Na kwa nini wewe unaona hiyo ndio HOJA? na si HOJA ya CCM kutaka kutumia msiba kufanya kampeni za Taarime kabla ya kutimuliwa? Sasa Tarime watu wanakamatwa kwa kusema serikali inahusika na kifo cha Chacha na hasa baada ya kubomoa nyumba iliyokua inajengwa na Mbunge wa CCM, ambaye ni Naibu Waziri, G.Kabaka na kubeba mabati wakimtuhumu kuwa anaandaliwa kuwa mbunge wa Tarime. mbona hiyo hulioni na huoni unafiki?
 
Ukweli ni ukweli, kama umeonwa na wengi hakuna haja ya kuingiza siasa, ukweli usemwe wazi, hakuna sababu ya kuingiza siasa kwenye ukweli hata kama utasemwa na viongozi wote wa chama, haibadili anything ukweli ni ukweli na uongo ni uongo tu!

Kama viongozi wengi wa Chadema, wameuona ukweli, basi waseme ukweli sisi tuuchambue, FULL STOPP! So far wanaonekana kuwa na ukweli zaidi kwenye hii ishu kuliko viongozi wa vyama vingine that is not even a brainer ku-figure out!
 
Mkuu FMES,

Wapi nimekataa kwamba Kolimba hakufa kwa ugonjwa wa moyo? Tafadhali naomba highlight hiyo sehemu.

Ugonjwa wa moyo ni neno pana ambalo linaongelea magonjwa chungu nzima ya moyo. Mtu akisema heart attack, stroke, BP nk. yote kwa ujumla kwa kiswahili yanajulikana kama mtu kafa kwa ugonjwa wa moyo.

Hao wengine mimi sitaandika tena maana naamini walikufa kawaida ila simzuii mtu mwingine kuamini tofauti.
 
Opinion

Monday, August 20, 2001

Making a Killing from Politics Can be Deadly By MICHEAL OKEMA

Mkuu FMES,

Duh, umenikumbusha huyo mshua Okema, unajua naye alifariki miaka nadhani miwili iliyopita? Sorry kutoka nje ya mada, lakini jamaa alikuwa Mtabiri, Mwanamuziki (amewahi kuimba na Dr Remmy zamani) na pia mwalimu? Sauti yake ya chini sana na upole kwenye mwili mkubwa...well, kila mtu atapitia njia ile. RIP Okema.
 
gari limeharibika sana. Mbona huyo Mallya yeye hajaumia???????.Ajali ya Diana aliyepona alikuwa koma kwa mwaka. Jamani tujiulize kilakitu .

Wajinga,

Kuna ajali nyingi tu gari zimepondeka vibaya na watu wametoka salama. Ukiangalia gari la Wangwe, mtu kama alikuwa upande wa kulia na alifunga mkanda, kuna chance kubwa sana angeweza kutoka salama.

Vifo vinatokea sana pale gari linapogonga kitu kingine, kama vile mti, mwamba au vyuma kama gari la Diana. Ukiangalia gari la Wangwe sidhani kama aligonga kitu kwa mbele, labda aligonga kwa ukutani kushoto.

Kwa jeraha la Wangwe, huenda hakufunga mkanda. Mkanda ni mlinzi mkubwa sana kwenye gari ndio maana muda wote nashangaa kwanini TZ watu hawapendi kufunga mikanda?

Kama umewahi kuhusika kwenye ajali, ile gari likianza kuporomoka tu, mkanda unakubana, haukupi nafasi kabisa hata ya kusogea hatua mbele au nyuma. Labda kitu ncha kikuchome kwa ndani, au ugonge kitu, vinginevyo utaumia kwa vioo lakini una nafasi ya kutoka salama.
 
Ni kweli ndio maana leo, Adamu Kighoma Ali Malima, ni Naibu Waziri na alimwagiwa kila aina ya sifa. Ndio maana Spika wa Bunge na wabunge wa CCM waliokua wakimuona Chacha kama "mwehu" walilia na kumwagia sifa kem kem. Chacha hakufukuzwa uanachama na hata uongozi alisimamishwa tu na kulikua na uwezekano wa kuwa angeweza hata kushinda katika vikao vya juu. Chacha aliendelea kuwa na mahusiani mazuri na viongozi wenzake wa Chadema na ni mbunge pekee aliyefika kwanza kumuona Zitto hospitali na alikaa kwa muda mrefu pale Muhimbili, na hakua mnafiki, alikwenda kwa dhati. Sasa leo unataka watu waende msibani kwa mila zetu, wasema Chacha hafai na mengineyo!!!!!?? Na kwa nini wewe unaona hiyo ndio HOJA? na si HOJA ya CCM kutaka kutumia msiba kufanya kampeni za Taarime kabla ya kutimuliwa? Sasa Tarime watu wanakamatwa kwa kusema serikali inahusika na kifo cha Chacha na hasa baada ya kubomoa nyumba iliyokua inajengwa na Mbunge wa CCM, ambaye ni Naibu Waziri, G.Kabaka na kubeba mabati wakimtuhumu kuwa anaandaliwa kuwa mbunge wa Tarime. mbona hiyo hulioni na huoni unafiki?

Tatizo lako unazungusha gurudumu wakati ukweli upo wazi,Mimi msimamo wangu ni uleule CCM ni wanafiki kama CHADEMA walivyo wanafiki na mbaya wote kwa pamoja na ndio tukasema jogoo ni lile lile (watu wa ccm) ila limepakwa rangi kichwani(watu wa chadema)

Hapo kwenda msibani nakua na huzuni huo ni ubinadamu nikakupa mfano hata jambazi likuawa watu hua wanapatwa huzuni lakini huzuni huo na kifo hicho cha jambazi si guaratee ya kubadili msimamo wa kua jamaa alikua si jambazi.ukifanya hivyo unakua mnafiki mkubwa hata shetani hatoufanya.

Chadema walisema chacha alikua na mkakati na RA kuvuruga chadema,Mbatia naye alisema CHACHA ni wakutimuliwa maana ameshavuruga demokrasia NCCR wana JF nao wamesema japo si wote chacha alibomoa udsm akijaribu kuiba fedha na amemtelekeza mkewe wa watoto 12,huyo mke anamlilia TUNDU LISU kwa kumpeleka chacha DAR,leo hii Marehemu hatunaye hao hao wanasema Chacha alikua mpigania demokrasia na haki huo ndio unafiki wenu .
Na lazima nitausema tu
Mimi naamini Marehemu Chacha alikua mpigania haki,mzalendo na mpagania demokrasia lakini Minafiki ndiyo ilimnafiki na kumvua uenyekiti.
 
Sioni tatizo kwa Chadema kumtuma Zitto kama Naibu Katibu Mkuu na mtu aliyekuwapo Tarime hadi mwisho. Hata kama Zitto asingekuwapo Tarime, kama Naibu Katibu Mkuu, alikua na haki ya kuzungumza. Siwezi kuwasemea Chadema, ila ninavyoona na kwa mtiririko wa matukio, wanaaminiana na hakuna mwenye kuhodhi mamlaka ya kuzungumza, mradi tu mawasiliano yanakuwapo na kupata baraka za uongozi wote wa juu. Mtanzania unapohoji uwezo wa kuwasiliana, nadhani huwatendei haki Chadema kwa kuwa wana simu za mkononi, kuna mitandao na kadhalika. Sidhani kama Dk.Slaa alitakiwa aje toka Dodoma kukutana na Wahariri, lakini pia kwa ninavyomfahamu ZItto, Chadema wanamuamini zaidi kuwa anamudu vyema kuongea na waandishi wa habari na walio wengi wanamheshimu. Mbona hujasema Tambwe, alipozungumzia suala nyeti la "Zanzibar si nchi?"

Kitila,

Msimamo wangu mimi ni kuwatumia wabunge kuendesha mambo ya CHADEMA. Kuwapa ukurugenzi watu ambao wako nje ya bunge nafikiri ni makosa labda kwa vyama ambavyo havina wabunge wa kutosha.

Kwenye hili wangeanza na Dr. Slaa toka mwanzoni, au Zitto na mpaka mwisho.

Ukisoma kule kwenye ile thread nyingi ya Mnyika akutana na Bille na Rostam, utaelewa nina maana gani.

Hivi Mnyika alitumwa na chama hata kutuma sms kwa RA? Inabidi chama au kampuni kuwe na protocol ya aina fulani hivi inavyokuja kwenye mawasiliano na mtu/vyombo vya nje ya chama/shirika.

Swali lingine ninalojiuliza, kwanini Mbowe alikubali ushauri wa polisi kwamba asihudhurie mazishi ya Wangwe? Ile ilikuwa sio amri, ulikuwa ushauri, kama hakukuwa na hatari kabisa hata kwake, kwanini akubaliane na ushauri wa namna hiyo? Tumeona mara chungu nzima wanasiasa wakikataa ushauri kuhusu maisha yao kuwa hatarini, wengine wanakubali wengine wanakataa. Hata Bhutto alishauriwa asirudi Pakistan shauri ya usalama wake, lakini akaenda na kufa. Mbowe angweza kwenda kwenye mazishi na kumaliza kilimilimi cha waliosema kafukuzwa. Lakini pia angeweza kwenda na kufukuzwa na ingelikuwa mbaya zaidi kwake.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom