Kifo cha Mhe. Chacha Wangwe na uchunguzi wake

Kifo cha Mhe. Chacha Wangwe na uchunguzi wake

Status
Not open for further replies.
mrema kasema mapanga yalikuwepo ......ila kasisistiza kuwa mbowe hakutaka kupigwa mapanga.

sasa hapo chambua mwenyewe .......what is what and which is which
 
..well, yawezekana akawa Jasusi au Prof. Killer, hili halitegemei sana nchi za nje kujifunza hata Tz nadhani haya mafunzo yapo kwa wahusika fulani ktk idara nyeti za serikali.
..Binafsi niliposikia juu ya ajali na kifo cha Wangwe nilikumbuka kifo cha Gibons Mwaikambo, yawezekana ni jamii ile ile ya wahusika. Ndani ya vyama kuna watu wanaoweza kuondesha vikundi vichafu kama kilichowahi kusikika huko miaka ya nyuma.
 
Sasa tumegundua, kumbe hivi vya upinzani havikuwa vya kweli! Da !!!! yaana sasa wanajitahidi ili wakisambaratishe CHADEMA? Sisi watanzania hatulala tuko macho, wameitisha comfrence wenyewe, wanataka kuonekana mashujaa wa taifa hili, haya tuone kama nini kitajili,
 
hivi mtu akisema "nilipokuwa mjini, mvua ilinyesha" ina maana mvua imemnyeshea? Wale wanaotoka maeneo ya Mbulu watatambua kwamba ukiitisha watu wa Mbulu kuwatangazia mpango wa maendeleo ya ujensi wa shule karibu wanaume wote watakuja na fimbo zao ndefu tu. Mgeni kama ukisema "walikuwa na fimbo nyingi" utakuwa sahihi.

Nina uhakika kulikuwa na watu wengi waliokuwa na kamera kule, basi tuonesheni angalau picha ya moja ya mtu aliyebeba panga.

Huu ni mfano wa picha ambayo inaweza kuletwa toka Tarime. Hii ilipigwa Kenya baada ya vurugu za uchaguzi. HIvyo wale waandishi waliokuwa kule Tarime walete picha ambayo inaonesha Mbowe angalau anafukuzwa na mapanga na mikuki hadi kwenye gari; hiyo itathibitisha maneno yao na mjadala utafungwa. Mwenye picha aiweke hapa JF anakomwa nyani giledi! NI picha tu ndiyo itakata ngebe za Chadema.

r214082_828024.jpg
 
Kwa hiyo ina maana Mufti Simba na Wabunge wa CCM walikwenda na Mallya kujifunza ujasusi? Nina habari za uhakika kabisa kuwa katika safari hiyo ya siku chache Mallya alikwenda na wabunge. Na Juma Kilimba Mbunge wa Iramba amesema mahali kuwa alikuwa naye huko.

Habari zaidi zinanieleza kwamba Profesa Lipumba ana ukaribu wa kikazi na Profesa Wangwe na hii hoja ya Libya ilijadiliwa kwa kina mara baada ya maziko, huko mke mdogo wa marehemu anayeitwa Mariam akisisitiza kwamba Mallya ni jasusi.

Naona Mbatia ameongezea na kusema kwamba ana uhakika kuwa ana mafunzo ya kupindua magari. Sasa ni wakati wa IGP kwenda kukutana na Mbatia ili amweleze kile anachojua. Inaelekea anajua mengi sana ambayo polisi hawayajui.

PM
 
Yaani wanaenda kwa IGP.. wakitaka uchunguzi huru na kweli wanataka kupata ukweli; waitishe Scotland Yard. Mbona inakuwa ngumu hivyo?
 
mimi nadhani tunajifunza kitu kimoja. kosa la chadema kumfukuza chacha, lilikuwa kosa kubwa ambalo tulilipinga tukaonekana wendawazimu ikabidi tunyamaze. tulichokiona ni serikali kutumia mwanya huo kueneza propaganda zao. sisemi he was assassinated, ila bado serikali inaweza kufanya vile, au kutumia loophole hiyo kueneza izo hisia, hata kama kifo kimefanywa na mtu mwingine, au kimetokea kama incidence.

tujifunze kuangalia mambo kwa upana zaidi, maana nieli kuendelea na mtu kuwa mzigo kama unadhani kuweka chini utaleta madhara. reasonability sio degree au PhD, bali ni namna unavyojichuni kumsikiliza kila mtu anachokiongea hata kama ni mlalahoi. tuliooa hata familia zetu sio pure 200%, Makanisani Bishops wanapata pressure kwa sababu ya offences za wachungaji/mapadre wao, Bush amepingwa sana na jamaa zake wa karibu, hata mawaziri wa Blair kujiuzuru.

tungesikilizana yasingetukuta haya. baada ya kujadili ufisadi, tunaanza kujadili mapanga na hatima ya vyama vya upinzani!

TUIOMBEE CHADEMA IONGOZWE KIBUSARA ZAIDI, TUWAOMBEE VIONGOZI WAKE WATAZAME MBELE KIMAWAZO, VINGINEVYO MAFISADI WANAANZA KUCHEKELEA.
 
Nimetoka benki sasa hivi. Pale, wapo askari na bunduki zao. Kama wanavyosema wengi hapa, silaha kama sime, rungu, kisu, mkuki ni sehemu ya VAZI la MWANAUME yeyote wa Kikurya iwe ni kwenye sherehe, msiba, mkutano na matembezi ya kawaida. Ndio maana walienda wengi sana Jeshini kwa kuwa kazi hiyo iko karibu mno na "hobby" yao hiyo ya kuwa karibu na SILAHA!
 
Kwa hiyo ina maana Mufti Simba na Wabunge wa CCM walikwenda na Mallya kujifunza ujasusi? Nina habari za uhakika kabisa kuwa katika safari hiyo ya siku chache Mallya alikwenda na wabunge. Na Juma Kilimba Mbunge wa Iramba amesema mahali kuwa alikuwa naye huko.

Habari zaidi zinanieleza kwamba Profesa Lipumba ana ukaribu wa kikazi na Profesa Wangwe na hii hoja ya Libya ilijadiliwa kwa kina mara baada ya maziko, huko mke mdogo wa marehemu anayeitwa Mariam akisisitiza kwamba Mallya ni jasusi.

Naona Mbatia ameongezea na kusema kwamba ana uhakika kuwa ana mafunzo ya kupindua magari. Sasa ni wakati wa IGP kwenda kukutana na Mbatia ili amweleze kile anachojua. Inaelekea anajua mengi sana ambayo polisi hawayajui.

PM


inakuwaje mnapinga any doubt isifanyiwe kazi? inakuwaje mnataka kudumaza uhuru wa kufikiria? au wewe unanjua vizuri Mallya? si utueleze? kifo hiki upinge usipinge kinahitaji uchunguzi wa kuondoa doubt yoyote ili kuweka sawa upinzani.

alafu kuwa Alienda Libya, haimaanishi wanaongelea siku hiyo walipoenda na SISEMU, uenda alirudi baadaye, uenda alikuwa alishaenda, uenda ni wakati huo na huo ndio mkakati!

pili kuwa wanataka kuusambaratisha CHADEMA, ni mapema mno maana kama Zitto alivyosema Wachagga kufukuzwa Tarime, inasikitisha na itasaidia kutuliza zaidi watu wa huko kutowatisha na itakuwa suluhu kama ukweli utabaki wazi; siku hizi watu wanareason tofauti na nyuma.
 
we cant rule out anything......
mallya anahitaji kufanyiwa uchunguzi wa kina mno. .....
historia yake ina utata na anaonyesha ni msemaji uongo.
Jamani hebu tuwekee hapa ka-Cv ka huyu Mallya tumjue vizuri yaelekea dogo ana viji-mambo fulani...
 
inakuwaje mnapinga any doubt isifanyiwe kazi? inakuwaje mnataka kudumaza uhuru wa kufikiria? au wewe unanjua vizuri Mallya? si utueleze? kifo hiki upinge usipinge kinahitaji uchunguzi wa kuondoa doubt yoyote ili kuweka sawa upinzani.

alafu kuwa Alienda Libya, haimaanishi wanaongelea siku hiyo walipoenda na SISEMU, uenda alirudi baadaye, uenda alikuwa alishaenda, uenda ni wakati huo na huo ndio mkakati!

pili kuwa wanataka kuusambaratisha CHADEMA, ni mapema mno maana kama Zitto alivyosema Wachagga kufukuzwa Tarime, inasikitisha na itasaidia kutuliza zaidi watu wa huko kutowatisha na itakuwa suluhu kama ukweli utabaki wazi; siku hizi watu wanareason tofauti na nyuma.

Polisi wanayo passport ya Bwana Mallya, kwa hiyo ninachoeleza ni kwa mujibu wa habari toka vyanzo vyao. Ni vyema Mbatia akahojiwa kwa kina aseme anachokifahamu cha ziada ili aisaidie polisi katika uchunguzi

PM
 
[QUOTE=Mushobozi;261100]mimi nadhani tunajifunza kitu kimoja. kosa la chadema kumfukuza chacha, lilikuwa kosa kubwa ambalo tulilipinga tukaonekana wendawazimu ikabidi tunyamaze. ........................[/QUOTE]


....sidhani kama kumsimamisha wangwe kulikuwa na ubaya wowote....kwani hakuna aliyeweza kuiona kesho..au kutabiri kuwa Mungu atamuita na ingezua mjadala...kwa kifupi ..kama walimsimamisha kwa nia njema ..hakuna ubaya ....

..unajua hata ukiwa mzazi mwanao anaweza kukosea ukamchapa akatoroka nyumbani.....akaenda akapotelea mitaani...ukabaki unajuta ..aaah nisingemchapa mwanangu asingetoweka!!!....lakini Mungu anajua kuwa ulikuwa ukimwadhibu kwa nia njema!!!..............tusianze kuogopa kuchukua hatua za kinidhamu nyumbani,maofisini,sehemu za kazi ets kwa kuogopa reppurcations..kwani ukubwa ni jalala.......!!!....serikalini ni watu wangapi tunaowakumbuka waliachishwa uwaziri...kufukuzwa kazi ...na wakafa kwa pressure..sasa tutasema aah ningejua nisingemfukuza kazi???...NO ...ni sehemu ya maisha....haya mambo yanatokea ....kila siku na yataendelea kutokea....unaweza pia kugombana na rafiki yako akaondoka kwa hasira akagonga akafa...thats ...sad ..reality.......

....tatizo kubwa la chacha au uzuri wake ni mkweli na muwazi!!!...lakini hili katika collective responsibility ni kuwa mara zote inakuwa ilikuwa vigumu kwake kukubali hoja...amabayo haitaki ...hata kama imeamuliwa na wote...kama haiamini ataendelea kuipinga tu....watu wenye misismamo ya aina hii isiypyumba wana sifa za uwanamapinduzi....!!!!
 
hivi mtu akisema "nilipokuwa mjini, mvua ilinyesha" ina maana mvua imemnyeshea? Wale wanaotoka maeneo ya Mbulu watatambua kwamba ukiitisha watu wa Mbulu kuwatangazia mpango wa maendeleo ya ujensi wa shule karibu wanaume wote watakuja na fimbo zao ndefu tu. Mgeni kama ukisema "walikuwa na fimbo nyingi" utakuwa sahihi.

Nina uhakika kulikuwa na watu wengi waliokuwa na kamera kule, basi tuonesheni angalau picha ya moja ya mtu aliyebeba panga.

Huu ni mfano wa picha ambayo inaweza kuletwa toka Tarime. Hii ilipigwa Kenya baada ya vurugu za uchaguzi. HIvyo wale waandishi waliokuwa kule Tarime walete picha ambayo inaonesha Mbowe angalau anafukuzwa na mapanga na mikuki hadi kwenye gari; hiyo itathibitisha maneno yao na mjadala utafungwa. Mwenye picha aiweke hapa JF anakomwa nyani giledi! NI picha tu ndiyo itakata ngebe za Chadema.

r214082_828024.jpg

Kuna watu watasema hiyo ni picha ya Kenya, huwezi kuwaridhisha binadamu pale wanapotaka kupindisha ukweli.
 
Mnamsifia hata kwa mambo asiyoyajua.Chadema wanataka kumtoa dogo kafara....kukinusuru chama chao..lakini ukweli utajulikana tu.....dogo ni innocent ...kama mna ushahidi upelekeni polisi sio mnasema magazetini mnarudi kukaa ofisini kwenu...
 
CHADEMA sijui watatokea wapi maana wamekaliwa kooni sasa fuatilia maswala yote kuanzia kusimamishwa kwa CHACHA,hawaja kaa sawa msiba mzito wa waliyemsimamisha CHACHA,maziko ya CHACHA propaganda za vyombo vya HABARI- MEDIA ,propaganda za ZITTO,kauli ya MREMA,tamko la vyama 3 vya upinzani.TUombe Mungu msikiiue CHAMA.
 
nafikiri vyama vya upinzani kwa kusema waliyosema ni hatua sahihi kwa wapelelezi kuwauliza kwa wale wanayoyajua.

kusema passport yake wanayo polisi, doesnt mean much. kuna watu wana passport za tanzania zaidi ya moja, zikiwa na majina tofauti.......seuze kuwa na passport ya tanzania na nchi nyengine!

afanywiwe uchunguzi wa kina.........sisemi kuwa ni mhalifu, ila tabia za kusema uongo anazo, na hakuonekana kushtuka sana baada ya ajali.
 
Too many questions arise. Kama ni kweli yeye ni jasusi;

1. Who is he working for? The party, outside the party, special(Classified) department in the party?

2. Any connections with the death of Late Hon. Wangwe, if there was any Project going on, is he part of it?

Please tell me more about this guy!.........
 
[QUOTE=Mushobozi;261100]mimi nadhani tunajifunza kitu kimoja. kosa la chadema kumfukuza chacha, lilikuwa kosa kubwa ambalo tulilipinga tukaonekana wendawazimu ikabidi tunyamaze. ........................



....sidhani kama kumsimamisha wangwe kulikuwa na ubaya wowote....kwani hakuna aliyeweza kuiona kesho..au kutabiri kuwa Mungu atamuita na ingezua mjadala...kwa kifupi ..kama walimsimamisha kwa nia njema ..hakuna ubaya ....

..unajua hata ukiwa mzazi mwanao anaweza kukosea ukamchapa akatoroka nyumbani.....akaenda akapotelea mitaani...ukabaki unajuta ..aaah nisingemchapa mwanangu asingetoweka!!!....lakini Mungu anajua kuwa ulikuwa ukimwadhibu kwa nia njema!!!..............tusianze kuogopa kuchukua hatua za kinidhamu nyumbani,maofisini,sehemu za kazi ets kwa kuogopa reppurcations..kwani ukubwa ni jalala.......!!!....serikalini ni watu wangapi tunaowakumbuka waliachishwa uwaziri...kufukuzwa kazi ...na wakafa kwa pressure..sasa tutasema aah ningejua nisingemfukuza kazi???...NO ...ni sehemu ya maisha....haya mambo yanatokea ....kila siku na yataendelea kutokea....unaweza pia kugombana na rafiki yako akaondoka kwa hasira akagonga akafa...thats ...sad ..reality.......

....tatizo kubwa la chacha au uzuri wake ni mkweli na muwazi!!!...lakini hili katika collective responsibility ni kuwa mara zote inakuwa ilikuwa vigumu kwake kukubali hoja...amabayo haitaki ...hata kama imeamuliwa na wote...kama haiamini ataendelea kuipinga tu....watu wenye misismamo ya aina hii isiypyumba wana sifa za uwanamapinduzi....!!!!
[/QUOTE]

ndio hapo nikasema, kama hakuna ubaya wowote sawa. lakini kama kuna procedural illigalities, ambavyo wengi tulisema wakati huo, unakuwa unatoa mwanya kwa adui wako kushinda. yeyote mwenye taadhari hukwepa neno " I wish I knew sababu wuwa inakuja baadaye'
 
Kuna watu watasema hiyo ni picha ya Kenya, huwezi kuwaridhisha binadamu pale wanapotaka kupindisha ukweli.

Kwangu mimi mwanakijiji hana haki yoyote ya kutafuta uthibitisho... kwa kuwa hao anawasema kila siku mafisadi hana uthibitisho wa namna yoyote... hili analisemea tu kwa kuwa ana maslahi binafsi ndani yake...

Kuna mambo mengi tu ambayo mwanakijiji ameyatunga akiwa marekani akalazimisha watu kuamini hapa...
 
Kuna watu watasema hiyo ni picha ya Kenya, huwezi kuwaridhisha binadamu pale wanapotaka kupindisha ukweli.

Yes, ni picha ya Kenya. Unataka kusema hiyo picha ni ya kutoka Tarime? Please mkuu, wakurya hawafanani na hao jamaa.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom