Habari za ndani kabisa zinasema kuwa maamuzi ya familia yanaelekea kwenye kuzika mwili ili yaishe. Keba na Samuel (Prof) Wangwe wanajulikana Tarime kwa kutopenda maneno mengi na mwelekeo hapa ni kuwaambia wana Tarime kuwa yamekwisha na watu wazike, walie, waomboleze, na kisha kuendelea na kazi zao za maendeleo.
Katika hili, inaonekana chochote kile kitakachoonekana kwenda kinyume na yale yanayotakiwa kufanyika kitakumbana na vikwazo na usumbufu mwingi huku pia watu wa Tarime tukiwekwa hostage na kuamshwa emotions zetu kiaina kwa propaganda bab kubwa inayoendeshwa na TBC1 na magazeti yote ya Rostam Azizi na wapambe wake.
Katika hili, ukweli utajulikana mioyoni mwetu no matter what they do. Sisi sio wajinga na watu wa Tarime sio wanyama kama wengine wanavyotuonyesha hapa. Thanks GOD hakuna ugomvi au mapigano yaliyotokea kama wengine wenye nia mbaya na Tarime walivyotaka. MUNGU ashukuriwe kwa kuwalinda na kuwatunza watu wote wa Tarime.
Chacha Wangwe, umepigania mengi sana kwa maisha ya wana Tarime. Kwa miaka zaidi ya 15 umekuwa mstari wa mbele kutusaidia watu wa Tarime kwa kila kitu - kuanzia sheria batili za ulinzi wa sungusungu hadi kwenye sheria onevu za watoza kodi wa halmashauri ya Tarime. Umekuwa mstari wa mbele kwa sana kuwaunganisha wamiliki wadogowadogo wa machimbo ya madini kupambana na makampuni makubwa ya kifisadi ambayo sasa yatafurahia kuondoka kwako.
Chacha umekuwa mstari wa mbele kujaribu kusuluhisha migogoro ya ardhi Tarime hata pale ambapo serikali ilionekana kupuuzia. Nakumbuka nilipokuwa shule ya upili ulianzisha kampeni ya kuondoa adhabu zisizo na maana kwa watoto wa shule, kampeni ambayo ilikuchukua karibu miaka kumi kufanikiwa. Chacha Wangwe - rastafarian, nakumbuka ulinifundisha maneno halisi ya nyimbo za Bob Marley na Dube na kuniambia tafsiri yake nikiwa kinda tu.
Chacha Wangwe, watu wa Tarime tutakukumbuka milele kwa yote mema uliyofanya na tutasahau milele zile tofauti za kawaida za kibinadamu ambazo zimeweza kuwa zimetokea.
MUNGU wa mbinguni ailinde familia yako na ndugu zako. Kuna watakaodhani kuwa wameshinda kwa yaliyotokea lakini MUNGU wa mbinguni ataleta Chacha mwingine kutoka kwa jamii ya wakurya wa Tarime ambaye atafanya yote yale uliyotaka yafanyike na kuendeleza mazuri zaidi. Kuna wanaodhani kuwa huu msiba wako ndio utamaliza upinzani Tanzania. Hata kama Chadema na NCCR - vyama ambavyo ulivihamasisha sana Tarime vitakufa, bado ari na nia ya kuwa na serikali bora Tarime na Tanzania itaendelea kuwa mioyoni mwa wana Tarime forever and ever.
Kwaheri Wangwe, kwa heri rasta man, kwa heri mpambanaji, kwa heri murra, kwa .....inhi inhi inhi hiiiiiiiiiiiiiiiii inhi .... uwiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii
ENOKWE ikuhituke naghukuha ahasi ha kumunya hano YESO aricha.
Amen
I dedicated this song for u RASTA CHACHA
Verse 1
I love to see my people living in love
I hate to see them fighting and swimming in blood
Nuff neglect the farming, scourning the mud
Yet they wanna be the first to reap the food as it bud
Oh, dem fill the earth wid prison, church, and whorehouse
Love the rum-bar, yet dem hate the pure-house
Dem tek di micro-chip, and now a wrath go pour out
Less food, more drought and more mouth
Chorus
Oy, rasta tell dem all di while
Stop war and go till di soil
Stop fighting for land and oil
Fi di coil, so many go defile
Slavemaster spit inna dem face, dem tek dat wid a smile
The banks of the Nile, so mild and so fertile
Acres mores than a zillion mile
People acting vile, pick up cannibal style
Waan devour mama, papa, and child
Verse 2
Oh, sew thy seed and let it buss earth
Dem say dem ting deh tek too long fi grow and start to cuss earth
I couldnt trust none a those as how I trust earth
Such is life, dem say a just earth
High Tikasha Heights, weh dem call this spot a land
Some say fi government, some say fi Mattaland
Still no waan share although dem got a lot a land
Dem waan fi turn inna gun range and shotta land
Chorus
Verse 3
Politician a talk, certain ting dem nah mention
Say a drugs and gun di people tax money spend pon
Come wid plastic smile and dem wicked intention
Inna yuh hand, a weh dem put dem evil invention
Turn gun model, seeking attention
See it deh now yuh dead and death is no redemption
Parents a wonder where to get the first cent from
To bury di dead, dem not even got pension
RIP RASTA CHACHA