Wakati Marehemu Chacha Wangwe alipotofautiana na Mwenyekiti wake na hadi kufikia kusimamishwa umakamu Mwenyekiti, wengi wa wachangiaji katika Thread hii tuliyomo mli-mlima sana Wangwe na kufikia hadi kumtakia afe, ikibidi kwa kupigwa risasi.
Leo hii bado mnajitahidi ku-speculate na hata kubadilisha taarifa halisi ya tukio zima lililotokea kule Tarime, kwamba Mwenyekiti wa CHADEMA alitaka kuvamiwa na watu wenye hasira kali ambao wanamtuhumu juu ya kifo cha Wangwe. Kuna ambao wanajitahidi ku-twist zaidi mtiririko wa thread hii kwa ajili ya manufaa ya mtu binafsi au kundi fulani, si vibaya kwani mnalolifanya mnalielewa vizuri. Lakini mwisho ya yote ni kuwa mnasherehekea ushindi mlioupata wa kuona kuwa sasa Wangwe mlilokuwa mnamtakia limekwishamfika, Sioni sababu ya kutaka KUMSAFISHA MTU ambaye hata kutuhumiwa bado hajatuhumiwa, au kushinikiza yale mnayoyataka ninyi dhidi ya Deus bila ya kujali haki zake za kimsingi na sheria zinazomlinda hadi sasa.
Endeleeni ku-speculate kama mnadhani hiyo ndiyo njia sahihi ya kubadilisha matokeo halisi