Kifo cha Mhe. Chacha Wangwe na uchunguzi wake

Kifo cha Mhe. Chacha Wangwe na uchunguzi wake

Status
Not open for further replies.
Msomaji wa taarifa ya habari jana usiku amekiri wanayo hayo makabrasha!

na wayaweke wazi tuyaone basi
wayachapishe kwenye magazeti...hizo barua. .....mwaka wa unafiki umeisha.
 
Vipi kama ni CHADEMA ndiyo wahusika umeshajiuliza hilo?...., yawezekana wao ndiyo wahusika wakumtoa huyu jamaa duniani ukizingatia mambo hayakuwa swari baina yake na uongozi wa CHADEMA, Sirikali inaweza ikawa inaujua mchezo wote wa CHADEMA na kwa kujua kwao wanaweza wakawa wanataka kuitumia kama silaha yao(remember wht rostam did to mtikila), wanajua fika sasa CHADEMA watakaa kimya na endapo watasema kitu chochote kuikosoa sirikali, basi sirikali itamwaga habari yote hadharani kitu ambacho kitakuwa kibaya kwa CHADEMA, wataitumia kuiua CHADEMA kwa guilty concious.....sirikalini kuna watu wenye akili zaidi ya tunavyo fikiri, lakini akili zao huzitumia kwenye mambo kama hayo...
Ni mtazamo tu.
.

CCM,hawa Political Prostitutes?Wajue jambo wakuache hivi hivi!Labda siyo wenyewe.When they want you down they will manipulate and do anything in their power to make you go down.They would never accept the fact of being junior they think and believe that they belong up there and they will always maintain that seniority status!
 
Hii inanikumbusha Mgogoro wa Patrice Lumumba na makamu wake ambao ulipelekea Mobutu kama mkuu wa jeshi ku-take advantage na kupanga mpango na wabelgiji na US wakamu-eliminate Lumumba.Sasa hapo nafikiria kuna kitu zaidi maanake hata CCM na Mafisadi wanaweza kusimama side aliyosimamia Mobutu Sese Seko.Maanake wanashabihiana kwa umafia

What's your point?

What is shocking- Miafrika ndivyo tulivyo!!
sorry kama nimekuudhi I guess I was thinking aloud bro.
 
Taarifa za uhakika ni kuwa wamempata Daktari na tayari wameshafanya Postmotum na hakukugundulika jeraha la Risasi, ila taarifa za ndani ni kuwa kutokana na ajali ubongo ulimwagika ndani.
 
kama kawa!
Inasikitisha saana.....nikifikiria serikali ya Tanzania naumwa kichwa tena siasa ndio kabisa nasikia kupasuka kichwa......I hate politics sasa Wangwe mafisadi wamemtenganisha na familia yake.SI MAPENZI YA MUNGU KIFO CHA WANGWE
 
Taarifa za uhakika ni kuwa wamempata Daktari na tayari wameshafanya Postmotum na hakukugundulika jeraha la Risasi, ila taarifa za ndani ni kuwa kutokana na ajali ubongo ulimwagika ndani.


Shauri yako mzee mwanakijiji akikusikia!!!
 
Mambo Jambo,
Kama kuna upepelezi wa POLISI basi wewe hufai hata chembe. Kuna faida gani ya kumuuwa Wangwe kwa CHADEMA? Kwanza walishamuondoa madarakani kama mwenyekiti. Sanasana wangelimfanyia mizengwe ili aondolewe kwenye chama. Hii kwao hailipi kabisa. Wangelikuwa wamekwama kumuondoa na jamaa bado ana nguvu ndani ya chama, hapo tungelijua kweli. Itakuwa jambo la kuchekesha sana CHADEMA kukata tawi upande wa kuanguka. Sasa hivi nashangaa MTU akisema ni CHADEMA au CCM au MAFISADI. Inabidi kwanza kupata uhakika amekufa kwa sababu ipi. Uchunguzi ufanyike. Ila nashinjwa jua eti Dr wa Kenya hana kibali. Wangelikuwa ni CCM wanataka Dr, basi angelipewa kibali within minutes. Walitaka kununua ndege wakanunua huku wakitamba eti IKIBIDI KULA NYASI basi tutakula ila chombo kinakuja. Ndege yenyewe nasikia iko hoi inapiga unyende tu.
Ipo siku CCM haya mambo kama (Kama ni nyie) basi yatakuja watokea puani. Dunia ilishawaona akina Pharao, Kaisaria, Napoleon, Hitler, na sasa USA ambao au walianguka ama wanaanguka kidogokidogo. Hata siku moja CHINA itaja anguka na kitawaangusha kiburi chao wenyewe. Kama hawa walienda itakuwa CCM? Heri mjiandae maana mwisho wenu utakuwa mbaya sana kama ikija gundulika kuwa MIKONO YENU INA DAMU.

Wangwe alikuwa na nguvu sana na alisema hatima yake iko kwa wanachama.ina maana anakubalika.
na MBowe alisema kuwa Wangwe anauza siri zao na walimkataza hasikii, kwa kauli hiyo wanaweza kumdhuru kama wale KGB walivyomfanya yule Mrusia aliyekwenda Uingereza kiasi ya kuwa UK na russia hawana mahusiano mazuri.IT MORE LIKELY CHADEMA WAMEMBOWESHA WANGWE ili siri zao zisivuje.
 
Taarifa za uhakika ni kuwa wamempata Daktari na tayari wameshafanya Postmotum na hakukugundulika jeraha la Risasi, ila taarifa za ndani ni kuwa kutokana na ajali ubongo ulimwagika ndani.
Elezea kinaga ubaga huyo Dktari ndio yule serikali ilimpendekeza? kama ndie basi majibu nilitegema yatakuwa hayo......
 
Taarifa za uhakika ni kuwa wamempata Daktari na tayari wameshafanya Postmotum na hakukugundulika jeraha la Risasi, ila taarifa za ndani ni kuwa kutokana na ajali ubongo ulimwagika ndani.
possibly ni Sangoma kwani Mbowe alikwenda south Africa.
 
Wangwe alikuwa na nguvu sana na alisema hatima yake iko kwa wanachama.ina maana anakubalika.
na MBowe alisema kuwa Wangwe anauza siri zao na walimkataza hasikii, kwa kauli hiyo wanaweza kumdhuru kama wale KGB walivyomfanya yule Mrusia aliyekwenda Uingereza kiasi ya kuwa UK na russia hawana mahusiano mazuri.IT MORE LIKELY CHADEMA WAMEMBOWESHA WANGWE ili siri zao zisivuje.
Unataka kusema kuwa Wangwe kauliwa na CHADEMA? nani ni Muhusika mkuu CHADEMA kwa mauaji hayo(kama kweli)?
 
na wayaweke wazi tuyaone basi
wayachapishe kwenye magazeti...hizo barua. .....mwaka wa unafiki umeisha.

Wanaubavu huo?They are damn cowards and they are there to serve the interests of the rulling party which is the owner na siyo Televisheni ya Taifa maana siku hizi ukisema Taifa una maanisha CCM!
Bloody Power Mongers!
 
Taarifa za uhakika ni kuwa wamempata Daktari na tayari wameshafanya Postmotum na hakukugundulika jeraha la Risasi, ila taarifa za ndani ni kuwa kutokana na ajali ubongo ulimwagika ndani.

Imekwisha!!!!!!!!!!!!!
 
Swali la kujiuliza ni kwa nini wananchi hawana tena imani na vyombo vyetu kuanzia polisi na sasa hadi madaktari? Kuna precedence hapa. Sokoine alikufa katika mazingira ya kutatanisha yakapita hivihivi hadi leo umebaki uvumi, na hatutaki kufanya uchunguzi.

Kifo cha Amina, Mbatia vyote vilikuwa na maswali mengi na hadi leo tumebaki na maswali yetu. Sasa na hiki ni hivyohivyo, utata upo wazi, tumebaki tunafanya siasa na itaisha hivihivi.

Inawezekana kabisa wenye malengo yao wakafanikiwa kutumia msiba huu kuidhoofisha chadema, lakini kwa vyovyote vile haitatusaidia katika kujibu maswali tuliyo nayo, zaidi ya kuzidisha hofu miongoni mwa wananchi, na wala kuidhoofisha chadema kwa njia chafu za kutumia msiba huu haisaidii kutatua matatizo ya wananchi yaliyosababisha wawe na chuki na serikali yao. Chacha amefariki, na inawezekana wakafanikiwa kuizima chadema kama walivyopania, lakini kwa hakika hawatazima msisimko wa mabadiliko ambao unachemka nchini. Ataibuka Chacha mwingine na itazaliwa chadema ingine.

Kinachonipa shida kuliko vyote mimi ni imekuwaje vyombo vyote muhimu kama polisi na sasa madaktari vimefika mahala vinakubali kutumikia wanasiasa badala ya kutumikia utaalamu wao? Tumefikaje hapa na tutajitoaje?

Mkuu,
Bila spin wala nini, lakini Amina aliondoka kwa ngoma...hivyo hayupo kwenye orodha ya "waliouawa."!! Kama huamini, basi ulizia contacts zako za kitabibu pale dar! Crypto ile, hands down.
 
ssa hao TBC wanategemewa waaminiwe kwa kuwa wamesema tu!! bila ushahidi?

watawapata hao hao wana ccm ...........wakitaka waaminiwe na wote na watowe ushahidi kwenye magazeti wachapishe ..........

hatutaki fitna
 
Haijakwisha!

Kama hawajaona uhusiano wowote wa kuhujumiwa kwa risasi, sasa tunataka kujua nani alikuwa anaendesha gari? Isije ikawa hii gari iligongwa na Gari nyingine kubwa ambayo ilitoweka unnoticed au hata dereva kuichepusha gari pembeni ya barabara na yeye kuruka? Nini kilitokea hasa? Nawasifu wannchi wa tarime (hasa Vijana waliofika na mabango ktk msiba) kwa kudai uchunguzi wa wazi na kweli mwanzo mzuri wa wananchi kujua haki zao
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom