Kifo cha Mhe. Chacha Wangwe na uchunguzi wake

Kifo cha Mhe. Chacha Wangwe na uchunguzi wake

Status
Not open for further replies.
Wewe ni laghai na mzushi sana, na uzushi wako unatisha mno! Ni mtu gani wa chadema alisema Chacha apigwe risasi? Hivi huu uzushi unamtumikia nani na kwa manufaa gani, au una-abuse anonymity yako hapa?

Unafikiri kwa kuwa unatumia jina bandia basi una uhuru wa kuropoka na kupayuka unavyotaka?


Kitila kwa kukusaidia bonyeza CTRL+F harafu kwenye kasanduku andika CHACHA ana faa kupigwa risasi., utaona ni nani.
 
this brings me to this question:

Kama baada ya ajali vitu vyote walivyokuwa navyo laptop, masanduku n.k viliibwa na hatujaambiwa kama vimepatikana TBC1 wamepata wapi nyaraka zinazoonesha kuwa katika safari hiyo alikuwa anaenda kufungua kesi na kuzungumza na vyombo vya habari isipokuwa kama na wao TBC walikuwa na taarifa hiyo kabla? au mtu mwingine zaidi ya Chadema alikuwa na taarifa hiyo ya safari?

Shimo hilo hawatatoka salama.
 
Inawezekana sio JMUSHI ila mhusika mkuu aliposoma ushauri wa JMUSHI akaamua kuufanyia kazi. JMUSHI anaweza kuwa shahidi kwenye kesi hii na akajikuta anafungwa kwa kuuua bila kukusudia(Manslaughter).
na kauli zote kama vile SIWEZI KUFANYA KAZI NA WANGWE ukitizama sana zinaweza kuwaweka watu pabaya,kama Mwanakijiji alivyoishauri Polisi hivyo hivyo na MKAMAP anajaribu kuweka mawazo yake kama Mwanakijiji na baya zaidi pale Mwenyekiti aliposema kuwa Wangwe anashiriki kukihujumu chama kwa kutoa siri za chama nje. walimwita kwenye vikao vingi kumuonya asitoe siri,hakusikia na wakampa muda ajirekebishe, wanasema hakujirekebisha,hatuleti siasa ila kama sheria inafuatwa Chadema wana kubwa la kujibu.
Kwa hiyo Mgagagigikoko unatakakusema jmushi ndiye Deus Mallya?
 
Mazishi ya Mh. Chacha Wangwe, aliyekuwa Mbunge wa Tarime aliyefariki dunia kwa ajali ya gari majuzi huko Dodoma, yameshindwa kufanyika leo kijijini kwake Kamokorere baada ya kufumuka kwa vurugu kubwa ambapo wabunge na viongozi wa serikali na vyama vya siasa walohudhurian ilibidi watoke bomba kusalimisha maisha yao.

Vurugu hiyo ilianza dakika chache baada ya kuwasili kilioni hapo kwa Mwenyekiti wa Taifa wa CHADEMA, Mh. Freeman Mbowe, katika kijiji cha Kemokorere kiasi cha kilomita 20 hivi toka mjini Tarime.

Hali ilipokuwa mbaya, ilibidi Mh. Mbowe na viongozi wote waliohudhuria mazishini waondolewe kilioni chini ya ulinzi mkali wa FFU ukiongozwa na Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Mara Afande Leberatus Barlow ambao walifanya kazi ya ziada kuepusha balaa.

Viongozi wengine waliohudhuria walikuwa ni pamoja na wenyeviti wa vyama vya upinzani Profesa Ibrahim Lipumba (CUF), Augustino Lyatonga Mrema (TLP), John Cheyo (UDP) James Mbatia (NCCR-Mageuzi) na Mbunge wa Karatu Mh. Wilbroad Slaa pamoja na kiongozi wa upinzani bungeni, Mh. Hamad Rashid.

Wote hao walisindikizwa chini ya ulinzi mkali wa FFU kuondoka mahali hapo na kuelekea Musoma. Waziri wa Kilimo na Umwagiliaji, Mh. Steven Wassira, na Manaibu Mawaziri ambao ni wabunge wa Kanda ya Ziwa, Dr. James Wanyacha na Gaudensia Kabaka nao ilibidi waondoke.

Ujumbe toka Kenya ulioongozwa na Dr Wilfred Machage ambaye ni mbunge wa jimbo la Kurya na pia Naibu Waziri katika serikali ya mseto ya Kenya pamoja na wakuu wa wilaya wawili nao walikuwepo na ilibidi waondoke kwa kuruka ukuta.

Tofauti na walivyoingia, itifaki haikuweza kufuata kama walipowasili wabunge 20 wakiongozwa na mbunge wa Bumburi Mh. William Lukindo vurugu hilo lilipoanza na ilibidi kila mmoja aondoke chini ya ulinzi mkali.

Maelfu ya waombolezaji, wengi wao wakiwa vijana waliobeba mabango yenye ujumbe mbalimbali unaohoji kifo cha Mh. Wangwe, walitawala hapo kilioni. Juhudi za Mkuu wa mkoa wa Mara Mh. Issa Machibya kuwatuliza hazikuzaa matunda.

Hata juhudi za kututuliza ghasia hizo za Wah. Zitto Kabwe na mmoja wa wanafamilia waandamizi kama vile Profesa Samwel Wangwe na Mkuu wa zamani wa Halmashauri ya Tarime Mh. Peter Wangwe pia hazikuambulia kitu.

Prof Wangwe aliwaambia waombolezaji hao wenye hasira kwamba familia ya Wangwe imeamua kumtafuta mtaalamu huru kuifanyia upya uchunguzi maiti ya hayati Chacha Wangwe ili kubaini alifariki kwa njia ipi.

Wengi ya waombolezaji wanatuhumu kwamba Mh. Wangwe hakufa kwa ajali ya gari. Mtu moja aliyekuwa na marehemu wakati wa ajali, Bw. Mallya, anahojiwa na polisi na uchunguzi wa kina unaendelea.

IMETOKA: michuzi blog
 
mwili Wa Marehemu Ulipotolewa Dodoma Uliongopzana Na Ndugu Wa Marehemu Tuu Na Mtu Aliyepata Nafasi Ambaye Sio Ndugu Wa Marehemu Ni Mwenyekiti Wa Halimashauri Ya Wilaya Ya Tarime.

Ndege Hiyo Ilipangwa Ratiba Na Bunge Sasa Waulize Bunge Ni Kwanini Ujumbe Wa Wabunge Ulipangwa Kuwa Wanaenda Kwenye Msiba Leo?

Pili Wakati Msiba Unatokea Unajua Kuwa Mbowe Alikuwa Afrika Ya Kusini Akiongoza Ujumbe Wa Tcd Ambao Ni Muunganiko Wa Vyama Vya Ccm,cuf,chadema,na Tlp, Ulitaka Aweze Vipi Kuongozana Na Mwili Wakati Aliweza Kuingia Nchini Jana Mchana Baada Ya Kuahirisha Safari?

Fanya Kazi Nyingine Hii Unayofanya Inahitaji Watu Au Mtu Mwenye Iq Kubwa Sana ,sio Kama Ya Kwako,ashakumu Sio Matusi....

Kwani Chama Ni Cha Mtu Mmoja? Imekuwa Kama Masau Wa Taasisi Ya Moyo Kila Kitu Ni Yeye,adminstrator,daktari,mkurugenzi,pr,mwanasheria N.k
Nimesema Sio Mbowe,slaaa,zitto,mnyika ,halima Mdeee,suzan Lyimo,anna Komu,ndesamburo, Muhonga,chiku Abwao Au Tundu Lisu Aliyeongozana Na Maiti,jee Maiti Ingejipeleka? Tuseme Afe Pius Msekwa Hakuna Mwanaccm Atakayeongoza Msafara Wa Maiti? Jamani Mlitenga Akiwa Hai Na Hadi Akiwa Maiti Mmemtenga. Mnaitenga Hadi Maiti?

Kama Mbowe Yuko South Africa Aliwezaje Kumtuma Mnyika Aandike Barua Kwa Igp Lakini Ashindwe Kuagiza Mtu Wa Kuongoza Maiti Ya Wangwe?
 
smart attempt... "watu wa chadema" waliodai "apigwe risasi" ni kina nani na wapi walifanya hivyo? Hii ni new information, kwa sababu ukiweza kuwaonesha hao "watu wa chadema" na mimi nitakuunga mkono.


Ma fans wa CHADEMA ,kwani WWanachadema lazima wawe mwenyekiti ,au katibu mkuu ninyi mwaja kweli.

Unaposema CCM ni viongozi pamoja na wanachama ndio wanakamrisha taasisi ya ccm.

ama CHADEMA ni taasisi ya mwenyekiti na katibu mkuu tu,wanachama wenu hamuwatambui??
 
na kama jmushi hajakoma kuvurumisha maneno ............hakomi tena!!
 
VURUGU ZAZUSHWA NA WANAFAMILIA MSIBANI BAADA YA MBOWE KUWASILI
VIONGOZI wa vyama vya NCCR Mageuzi, CUF na TLP wametoa tamko kuhusu msimamo wa familia ya Marehemu Chacha Wangwe, wakisema uchunguzi ni haki ya marehemu na kuipongeza kwa kuweka shinikizo hilo.

Viongozi hao, Augustine Mrema (TLP), Prof Ibrahim Lipumba (CUF), na James Mbatia (NCCR Mageuzi) ndiyo pekee waliosalia kutokana na viongozi wengi kukimbia vurugu nyumbani hapo kwa marehemu zilizozuka baada ya mwenyekiti wa Taifa wa Chadema, Freeman Mbowe kuwasili.

Wa kwanza kuzungumza alikuwa Prof. Lipumba ambaye alisema marehemu Wangwe katika siasa alipata umaarufu kutokana na kuwa mpambanaji na mpiganaji kutetea haki za wanyonge.

Lipumba alisema hakuna njia nzuri ya kumuenzi marehemu zaidi ya kuhakikisha wananchi wa Tarime wanaendeleza mapambano dhidi ya uporaji wa raslimali ya nchi na wananchi kuendelea kunyanyasika.

''Marehemu alikuwa mpambanaji na mpiganaji, sasa njia pekee ya kumuenzi ni kuendeleza mapambano ya wanyonge dhidi ya uporaji wa raslimali,'' alisema na akaongeza kwamba wananchi wanapaswa kuwa na subira kuhusu uchunguzi wa familia.

Akizungumza kwa niaba ya chama chake, Mbatia alisema kuwa alivyomtambua na kumfahamu marehemu Wangwe alikuwa jasiri na hivyo kuwaomba wananchi nao kuendelea na ujasiri huo kudai haki hata ya marehemu.

''Huwezi kumnyang'anya mtu haki yake ya kuzaliwa wala kuishi, uhai ukitoweka huwezi kuulipa kwa kitu chochote, kuweni na subira, msiwe na itikadi katika msiba, hakuna itikadi, sasa msikubali kuteganishwa, tunangoja uchunguzi ufanyike watueleze nini kilimtokea na kama kuna watu walimuua tudai haki yetu na kwa aliyehusika basi sheria ifuatwe,? alisema na kushangiliwa na watu.

Mbatia alisema wakazi wa Tarime wamekuwa wakichukuliwa kama ni watu wenye vurugu, jambo ambalo ni kinyume kutokana na kuwa na msimamo wao unaopenda haki na kujali maslai ya wanyonge.

''Jamani Tarime siyo watu wa fujo, wamekuwa wakielewa hivyo, na kusema hivyo, lakini mimi najua Tarime ni haki na kuchukia kunyanyaswa kwa wanyonge, teteeni haki yenu,'' alieleza.

Naye Mrema ambaye alishangiliwa zaidi kuliko wote, alianza kwa kuwapongeza wananchi wa Tarime kwa kumchagua marehemu Wangwe.

''Nawapongeza kwa kumchangua Marehemu, lakini sasa ametutoka, hivi ukizaa mtoto akafa unaacha kuzaa tena? hapana unaendelea, Chacha amezaliwa Tarime na atazaliwa mwingine,'' alisema.

Alisema kifo cha marehemu kina utata kutoka Dodoma, lakini familia imesema 'no' (hapana) mpaka uchunguzi umefanyika jambo ambalo ameunga mkono.

''Kuna watu hawajui kama marehemu ana haki zake, na mimi siondoki hapa mpaka kieleweke, uchunguzi lazima ufanyike kisha naomba tumzike kwa heshima zote huyu ndugu yetu,'' alisema Mrema huku akishangiliwa.

Source: Mwananchi Communication Ltd
 
~Those who say it can't be done shouldn't interrupt those who are doing it~
 
mh! Niliposikiliza swali toka kwa mtangazaji kwenda kwa Manyika, hili swali limenijia akilini; Je, nini hasa interest ya TBC ktk migogoro ya vyama? Na kwani interest hy watake kuonyesha ktk kipindi cha msiba.

R. I. P Wangwe!
 
Taifa liko njia panda. Naanza kuogopa sasa kama chombo kinachotegemewa kama TBC kimefikia hapa, nimeogopa. kazi ni kubwa kuliko tunavyofikiri.
 
Tatizo lako katika line of your thinking unashindwa kuuliza nani atanufaika sana na kifo cha Wangwe hasa katika mazingira hayo? Obviously siyo Chadema. Kwa sababu kwa wao walikuwa na uwezo wa kumfukuza uanachama na kumuondoa kwenye picha. Kuna mtu ambaye atanufaika na Chacha kutokuwa mbunge wa Tarime; and believe me, siyo Chadema. Think about it. Na inawezekana siyo CCM. Ukiondoa mawazo ya vyama vya kisiasa you might get real close na ukweli wenyewe. Haya mawazo ya Chadema na CCM yatapoteza muda sana.

Mwanakijiji elewa jambo moja Chadema walikuwa wakitaka ruzuku za Wangwe kupitia jimbo la Tarime, kwa vile priority ya Chadema ni RUZUKU NA UKABILA wasingeweza kumnyanganya uanachama,angekuwa si mwanachama wa Chadema nao makao makuu wangepata Ruzuku, kwa hiyo kilichokuwa kinambakiza Wangwe chadema ni lile kundi la Tarime linalizalisha Ruzuku Makao makuu.

Wangwe alibaki kuwa Mwanachama kwa ajili ya ruzuku si vinginevyo.
 
Naanza kuamini sasa kuwa kale ka usemi ka kizungu ka 'politics is a dirty game' kalitungwa bongo, sehemu nyingine zote duniani wanatuiga tu!
 
Mwanakijiji elewa jambo moja Chadema walikuwa wakitaka ruzuku za Wangwe kupitia jimbo la Tarime, kwa vile priority ya Chadema ni RUZUKU NA UKABILA wasingeweza kumnyanganya uanachama,angekuwa si mwanachama wa Chadema nao makao makuu wangepata Ruzuku, kwa hiyo kilichokuwa kinambakiza Wangwe chadema ni lile kundi la Tarime linalizalisha Ruzuku Makao makuu.

Wangwe alibaki kuwa Mwanachama kwa ajili ya ruzuku si vinginevyo.
Kwa maneno yako ni kuwa CHADEMA sio waliomuua kwani sasa watakosa hiyo ruzuku.

maneno yako yana maana kubwa sana sasa nani kamuua?
 
Huyu mbati naye Mnafiki kama watu humu JF Leo CHACHA kawa jasili kwa mbatia na baadhi ya memba humu JF.

Mwezi uliopita tu walimwita mzigo.mfisadi,mtu asiyefaa leo wanajifanya kua na uchungu na na masikitiko eti kwa kumpoteza jasili.


Haya mambo ya kinafiki haya ndio yatumeng'enyua simameni mnapoamini ndipo s mahala sahihi na si kufanya unafiki.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom