Kifo cha Mhe. Chacha Wangwe na uchunguzi wake

Kifo cha Mhe. Chacha Wangwe na uchunguzi wake

Status
Not open for further replies.
Mtikila anaweza kusema kitendo cha wangwe kufukuzwa chamani kilimuathiri kisaikolojia akawa disorganize.

Kidogo sounds interesting.

Huyu jamaa wakati baba wa Taifa alipofariki alisema kafariki kwa UKIMWI na walipomkamata akasema Rais Mkapa alitutangazia kuwa baba wa taifa anaumwa Mkanda wa Jeshi ambao husababishwa na kinga ya mwili kuwa chini. Sasa Ukimwi ni nini? ni Upungufu wa kinga mwilini. Jamaa wakamwachia. Tungoje tuone
 
Nani amekwambia kuwa mimi ni mwakilishi au msemaji wa CHADEMA hapa? Umeona chochote kwenye maandishi yangu kilichoonyesha kuwa ninaiwakilisha CHADEMA hapa?

Usiingize siasa kwenye mambo makubwa kama hili la kifo cha Wangwe. Maisha ya watu yako kwenye very high stake hapa na wanatarime wamezungukwa sasa hivi na mamia ya askari ambao wamekuja "kutuliza fujo" ambazo no body so far amezithibitisha.

Ukitaka kuongelea siasa za CHADEMA na vyama vingine, unaweza kuanzisha thread nyingine hapa na ukaanza kuleta sera za CCM kabla ya kuwauliza wengine walete za vyama vyao.

Kuwa serious kidogo poti, maisha ya watu wengi wa Tarime yako kwenye line hapa na hizi propaganda zako hazimsaidii yeyote yule.

Da kumbe poti nawewe ni mtaalamu wakuruka vihunzi teh teh teh teh.

Tuliwaambia Akina DR Slaa,Zitto na wezanke SIASA zakupandiana migongoni sio siasa ,maana ukipandiria mgongo wa mwenzako ipo siku na wewe mgongo wako lazima upandiriwe.

Mfano Suala la UFISADI sio suala la KISIASA kabisa ni suala la KISHERIA lakini wao wakaona kutumia migongo ya MIFISADI kuchuma matunda ya kisiasa wakaona ni jambo la maana haya sasa .Ukiliazisha jua lazima ulimalize.

Nilitoa mfano hapo kabla ya kua ninaweza kua na MSICHANA tumuite XX lakini nikawa nakengine pembeni tukaite YY basi kumbe nawewe ukawa unamtaka XX na njia uliyotumia ni kuvumbua uovu wangu kua mimi ni mhuni kwani ninaye mwingine yy kwa kumwambia XX huo uovu wangu na kwa kutumia mgongongo huo ukajitwalia XX .nimakosa makubwa.

Nikweli ninaye mwingine ambaye ni YY na nikweli ni uhuni lakini kupandiria mgongo wangu kujitwalia XX nimakosa makubwa sana.
Hili CHADEMA nitawaambia wasipotaka kusikia sawa . Mbinu ya kutumia migongo ya Mifisadi kujijengea umaarufu ni mbinu CHAFU .
 
Ahsante Dr. Slaa kwa juhudi zako za kutuokoa watanzania, katika sentensi yako hapo juu nilivofahamu mimi ni kwamba hivi sasa una ushahidi wa Makamba kumpa rushwa Mtikila, kama hii na sahihi basi naomba umfungulie mashtaka ya rushwa bw. Makamba kwani utakuwa unasaidia taifa kuondoa uchafu toka kwa viongozi wabovu, najua siasa ni mchezo wa karata na wewe unasubiri wakati mwafaka wa kutupa hii Ace uliyonayo lakini kusubiri huku ni kutowatendea haki watanzania, kutokana na nafasi yako nasema weka wazi na fungua kesi dhidi ya makamba kwa manufaa ya Umma, Ahsante.

True...Nilijuwa kifo hiki kitatumika kisiasa.
Kama uchunguzi ulikuwa HURU NA HAKI...Basi ni wazi kuwa SI HAKI kutumia kifo hiki kama turufu ya kisiasa maana mnatarisha hali ya usalama.
Kama hakuna uchunguzi huru uliokubalika kwa pamoja baina ya serikali ya ccm na chadema pamoja na wanafamilia...Then kwanini Mtikila ama ccm waruhusiwe kutumia kifo hiki kama nguzo ya kisiasa?
 
Da kumbe poti nawewe ni mtaalamu wakuruka vihunzi teh teh teh teh.

Tuliwaambia Akina DR Slaa,Zitto na wezanke SIASA zakupandiana migongoni sio siasa ,maana ukipandiria mgongo wa mwenzako ipo siku na wewe mgongo wako lazima upandiriwe.

Mfano Suala la UFISADI sio suala la KISIASA kabisa ni suala la KISHERIA lakini wao wakaona kutumia migongo ya MIFISADI kuchuma matunda ya kisiasa wakaona ni jambo la maana haya sasa .Ukiliazisha jua lazima ulimalize.

Nilitoa mfano hapo kabla ya kua ninaweza kua na MSICHANA tumuite XX lakini nikawa nakengine pembeni tukaite YY basi kumbe nawewe ukawa unamtaka XX na njia uliyotumia ni kuvumbua uovu wangu kua mimi ni mhuni kwani ninaye mwingine XX kwa kumwambia YY huo uovu wangu na kwa kutumia mgongongo huo ukajitwalia XX .nimakosa makubwa.

Nikweli ninaye mwingine ambaye ni YY na nikweli ni uhuni lakini kupandiria mgongo wangu kutitwalia XX nimakosa makubwa sana.
Hili CHADEMA nitawaambia wasipotaka kusikia mimi simo. Mbinu ya kutumia migongo ya Mifisadi kujijengea umaarufu ni mbinu CHAFU .

Poti maneno yako lakini! Count to ten kabla ya ku-submit
 
Kifo cha Wangwe si uamuzi ulishatolewa kuwa ilikuwa ni ajali, hakukuwa na risasi, na haikuwa mauaji. Na kijana Mallya anashtakiwa kwa kuendesha gari kwa mwendo wa kasi na kusababisha kifo cha Mbunge huyo? Wengine tulipozua maswali ambayo ukiangalia utaona kuwa haiitaji uchunguzi kuweza kuibuka na hoja alizotoa Mtikila (tafuta makala yangu niliyouliza maswali kuhusu kifo cha Wangwe). Leo hii anasimama kutaka Scotland Yard waje, wakati wengine tulifanya hivyo kabla hata mwili haujazikwa?

Serikali imesema and that settles it, ama?

Profesa Wangwe yuko wapi?
Si ni yeye alisema tuiachie familia?
Sasa Mtikila ni familia?
Ama Mtukila anaiwakilisha familia na serikali?
Wabongo kweli michosho...Sasa wavumilie tu.....Maana hata Mh Rais yeye yuko busy kujenga ngome yake na wabongo wakija kushtukia kuwa nani wamulize...Lango kuu la geti litakuwa limefungwa na solution itakuwa kuendelea kuomba Mungu tu...Either Msikitini ama kanisani...Huku mkisubiri kufa...Maana wabongo wanaishi ili wale.
 
Profesa Wangwe yuko wapi?
Si ni yeye alisema tuiachie familia?
Sasa Mtikila ni familia?
Ama Mtukila anaiwakilisha familia na serikali?
Wabongo kweli michosho...Sasa wavumilie tu.....Maana hata Mh Rais yeye yuko busy kujenga ngome yake.


Raia mwema teh teh teh teh teh
 
Raia mwema teh teh teh teh teh
Si haki kabisa kwa kifo hiki kutumika kisiasa.
Kwasababu ni wazi kuwa madhara ya Wangwe yalikuwa ni bungeni na si mtaani.
Mtaani kungebadilika kama hoja yake ingepita.
Wanatarime mkitaka kujuwa mtu wa kweli basi ni yule atakeiiwakilisha hoja ya Wangwe bungeni.
Zaidi ya hapo huu upinzani na ufilie mbali!
Tunapoteza maisha ya watanzania wenzetu na pesa zao za kodi bila sababu zaidi ya siasa na tamaa za madaraka.
Wanasiasa hawafai kabisa...NI MBWA MWITU!
Bajeti wapitishe halafu wasubiri siasa...Siasa na zife.
Siasa hizi zisipokufa basi Mungu na awashughulikie wanafiki wote wasiokuwa na huruma hata chembe kwa watanzania wajinga!
 
Hivi Mtikila ni Mchungaji wa kanisa gani na waumimni wake ni wanamna gani??? Jamaa nashindwa kabisa kumuelewa, yaani hata ndugu na jamaa wa Chacha walienda kumsikiliza huyu jamaa. Napenda kumuunga mkono bwana mmoja huko nyuma aliyesema Mtikila sasa awe declared INSANE!!!!!!
 
Wakuu,

Hivi Mtikila hawezi kusema jambo bila kuambiwa anatumiwa na mtu?

Hivi Tanzania mtu hawezi kufa bila kuwepo mkono wa mtu?

Hivi JF mtu hawezi kuwa na mawazo yake pekee bila kuambiwa kibaraka wa mafisadi?

Hivi Mtikila anawezaje kuja na madai makubwa namna hiyo bila hata kutoa ushahidi wowote wa maana?

Inakuwaje waandishi wanamsikiliza na kuandika habari nzito kama hiyo bila kumbana atoe ushahidi?

Dr. Slaa anawezaje kuandika hapa kwamba Mtikila kapewa 50m za makamba bila ushahidi wowote?

Hivi sisi Watanzania tunaenda wapi? Tunawezaje kupakana matope kiasi hicho bila kudirika angalau hata kidogo kutoa ushahidi (data)?

Ninachokiona kwenye huu mjadala hakitii tumaini juu ya viongozi wetu wa sasa na baadaye. Watu kama mnataka kuwa wapiga ramli nendeni huko, ila kuanza kuja na tuhuma kubwa kubwa bila data sio dalili nzuri kabisa.
 
Hivi Mtikila ni Mchungaji wa kanisa gani na waumimni wake ni wanamna gani??? Jamaa nashindwa kabisa kumuelewa, yaani hata ndugu na jamaa wa Chacha walienda kumsikiliza huyu jamaa. Napenda kumuunga mkono bwana mmoja huko nyuma aliyesema Mtikila sasa awe decleared INSANE!!!!!!

Na hao ndugu za Chacha walioenda kumsikiliza ni INSANE?
Ni bora ungeenda kuwauliza wao kuwa kama ni kweli jamaa waliyeenda kumsikiliza ni insane.
Pia labda mngewauliza kuwa ni nani aliwatuma kwenda kumsikiliza Mtikila badala ya kudai haki yao ya uchunguzi wa kifo chake serikalini....Hilo likiwa tofauti na aliyoyasema msemaji mkuu wa familia yao...Professa Wangwe mwenyewe ambaye hata brother wake zilikuwa haziivi.
Mbona Deus na ujasusi wake amesahaulika sasa?
Deus alitumwa na chadema kweli?
Ama serikali itamtumia Deus kuwageuka chadema?
Deus mwenyewe si yuko kwenye payroll za ccm na chadema?
 
Si haki kabisa kwa kifo hiki kutumika kisiasa.
Kwasababu ni wazi kuwa madhara ya Wangwe yalikuwa ni bungeni na si mtaani.
Mtaani kungebadilika kama hoja yake ingepita.
Wanatarime mkitaka kujuwa mtu wa kweli basi ni yule atakeiiwakilisha hoja ya Wangwe bungeni.
Zaidi ya hapo huu upinzani na ufilie mbali!
Tunapoteza maisha ya watanzania wenzetu na pesa zao za kodi bila sababu zaidi ya siasa na tamaa za madaraka.
Wanasiasa hawafai kabisa...NI MBWA MWITU!
Bajeti wapitishe halafu wasubiri siasa...Siasa na zife.
Siasa hizi zisipokufa basi Mungu na awashughulikie wanafiki wote wasiokuwa na huruma hata chembe kwa watanzania wajinga!

Wanasiasa wetu wote malengo yao ni yaleyale.Ndio maana kwa kutegemea hivi vyama ulivyoviita MBWA MWITU kusubiri maendeleo tutasubiri wee miaka nenda miaka rudi.
 
Hivi katika maneno yake Mtikila alisema hao waliomuua Wangwe walifanya hivyo kwa sababu gani? Yaani motive yao ya kumuua Wangwe ilikuwa nini?
 
Wakuu,

Hivi Mtikila hawezi kusema jambo bila kuambiwa anatumiwa na mtu?

Hivi Tanzania mtu hawezi kufa bila kuwepo mkono wa mtu?

Hivi JF mtu hawezi kuwa na mawazo yake pekee bila kuambiwa kibaraka wa mafisadi?

Hivi Mtikila anawezaje kuja na madai makubwa namna hiyo bila hata kutoa ushahidi wowote wa maana?

Inakuwaje waandishi wanamsikiliza na kuandika habari nzito kama hiyo bila kumbana atoe ushahidi?

Dr. Slaa anawezaje kuandika hapa kwamba Mtikila kapewa 50m za makamba bila ushahidi wowote?

Hivi sisi Watanzania tunaenda wapi? Tunawezaje kupakana matope kiasi hicho bila kudirika angalau hata kidogo kutoa ushahidi (data)?

Ninachokiona kwenye huu mjadala hakitii tumaini juu ya viongozi wetu wa sasa na baadaye. Watu kama mnataka kuwa wapiga ramli nendeni huko, ila kuanza kuja na tuhuma kubwa kubwa bila data sio dalili nzuri kabisa.

Mtanzania
umekosea
Mtu yeyote anaekinyoshea kidole chadema ama baadhi ya viongozi wake lazima awe AMETUMWA.Maana yeyote anayekisema chadema kwa vyovyote vile si mtu mwenye fikra za kibinadamu ni lazima awe mwendawazimu ama ROBOT.

Huyuhuyu mtikila alipomtolea uvuvi RA kule KKT hakuonekana katumwa na mtu wala mwendawazimu.
 
Hivi katika maneno yake Mtikila alisema hao waliomuua Wangwe walifanya hivyo kwa sababu gani? Yaani motive yao ya kumuua Wangwe ilikuwa nini?

Mtikila kama kweli kanunuliwa na anatumika na ccm...Basi tunaweza kutabiri wazi kabisa kuwa huu utakuwa mwisho wake.
Wangwe haku uwawa kwasababu ya matatizo ya chadema.
Aliuwawa kwasababu ya hoja yake ambayo mafisadi wanaogopa isifikishwe bungeni.
Tatizo la chadema ni kuwa hata wao waliona kuwa hoja yake ina ukali zaidi na wao walitaka irekebishwe kidogo....Hapo
 
Hivi Mtikila ni wa kumuamini tena? Wanaomuamini nadhani wamesahau kuwa huyu jamaa ameishiwa sera na anarukia vijihabari ili kujipatia legitimacy. mie simuamini! Kesi ya mauaji ya Wangwe iko mahakamani na mtuhumiwa namba moja yuko mashtakani. Tusubiri tujue yataishaje.

Kwahili la huyu hawa jamaa ni mbinu za kutumiwa tu ili wananchi wa lile jimbo waone kuwa chadema ni chama cha wauaji. nasikia kuna bilioni moja imetengwa na chama tawala ili kunyakua jimbo hili kwa nguvu yeyote. may be hii ni moja ya nguvu hiyo.

hakika simuamini Mtikila kutokana na historia yake!!
 
Hivi Mtikila ni wa kumuamini tena? Wanaomuamini nadhani wamesahau kuwa huyu jamaa ameishiwa sera na anarukia vijihabari ili kujipatia legitimacy. mie simuamini! Kesi ya mauaji ya Wangwe iko mahakamani na mtuhumiwa namba moja yuko mashtakani. Tusubiri tujue yataishaje.

Kwahili la huyu hawa jamaa ni mbinu za kutumiwa tu ili wananchi wa lile jimbo waone kuwa chadema ni chama cha wauaji. nasikia kuna bilioni moja imetengwa na chama tawala ili kunyakua jimbo hili kwa nguvu yeyote. may be hii ni moja ya nguvu hiyo.

hakika simuamini Mtikila kutokana na historia yake!!

Cha kusikitisha na kujiuliza ni kwanini hao ndugu za Wangwe walikuwa hapo kama ni kweli hakuna anayemwamini Mtikila.
 
Hivi jamani mnasahau kuwa huyu nndo yule yule aliyemshukia kwa maneno makali sana Rostam? Na baadaye akaja kuwa mpole kama amemwagiwa maji baada ya Rostam kusema hadharani kuwa alimpatia milioni kadhaa huyu mchungaji feki?
Huyu jamaa kama tungekuwa tunaruhusiwa kutukana hapa JF basi mimi ningekuwa wa kwanza kumtukana huyu mtu maana anaonekana dhahiri kuwa anaupungufu wa vitu fulani fulani kichwani mwake maana haiwezekani mtu wa kawaida maisha yako yote yakawa ni mahakamani kila kukicha must be something is not right kwenye kichwa chake na nafikiri hata hao wanachama wake wanaweza kuwa ni wale wale tu kama wale ndugu zetu wanafukuzwa kila siku pale airport eti wanataka kwenda ulaya bila passport wala viza.


SHAME ON YOU MTIKILA....... UNATIA AIBU NI BORA UKAPIGANIA UPATE RUZUKU YA CHAMA CHAKO KULIKO KUTUMIWA NA WATU AMBAO WANAIMALIZA HII NCHI KWA ULAFI WA MATUMBO YAO, TUMECHOKA NA WEWE SIJUI NI MTU WA AINA GANI AMBAYE UPO KAMA KINYONGA HUTULII NA RANGI MOJA... NI BORA UENDE KIJIJINI KWENU UKAANZISHE MASHAMBA TU MAANA SIASA ZIMEKUSHINDA SASA UMEBAKIA KUWA KIBARAKA... UNATIA AIBU
 
Habari ukiisoma kwa mtiririko wake kama haijatiwa chumvi na mwandishi, basi hakuna shaka kuwa Mtikila alikuwepo katika tukio hilo la kuuwawa Wangwe. Au amekutana na Deus Malya, na kupata maelezo ya yote yaliyotukia siku ya kifo cha Wangwe. Lakini cha ajabu, haya yangeelweka na polisi ambao ndio waliopeleleza tukio hili. Inatia shaka pale ambapo Mtikila anadai kuwa hana hata imani ni jeshi la polisi, na anachokihitaji ni tume!!???

Kabla ya kifo cha Wangwe, nadhani ni mtikila huyu huyu alieanzisha shutuma kwa MBOWE kuhusiana na suala la NSSF, ambapo mbowe alimjibu kuwa asingependa kuingia kwenye malumbano na yeye. HAPA KUNA NINI? KWELI HUYU MTIKILA NI MCHUNGAJI WA KANISA AU NI WA MBUZI NA NG'OMBE?

Ni habari ya kusikitisha mtu unapodai kuwa na taarifa kama hizi kuzitumia kisiasa! Hapa Mtikila anasema anamsimamisha mgombea wa ubenge huko tarime ili apate mahali pa kusemea!!!?? Je kweli, huu ndio utaifa na ndio utawala wa sheria? Mimi nashawishika kabisa kwamba kwa hili MTIKILA AMENUNULIWA, KWAMBA IONEKANE KUWA CHADEMA NDIO WANAHUSIKA NA KIFO CHA WANGWE, ILI WAKATALIWE NA CCM WAJISHINDIE JIMBO HILI KIRAHISI.

Kweli, Mtikila hii sasa ndio tafsiri yako mpya ya SAA YA UKOMBOZI? AU UMEJIRIDHISHA KUWA kwa siasa za pupa hutafika mbali??

Sote tutakufa lakini sio kabla ya ukweli wa hili jambo kudhihirika, na hakika hili ikiwa kinyume na shutuma zako, hutainuka tena.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom