Kifo cha Mhe. Chacha Wangwe na uchunguzi wake

Kifo cha Mhe. Chacha Wangwe na uchunguzi wake

Status
Not open for further replies.
Mnachekesha sana, sijui mnajadili nini....., kwanza ninyi si wapiga kura, mnajipendekeza tu, mnadhani sisi wana Tarime ni wajinga? nadhani hamna kazi za kufanya.

Ni kipindi sasa na ninyi wanaJF mtoke huko mjini mrudi vijijini mwenu mkawaelimishe baba zenu, mama zenu, watoto wenu jinsi ya kupambanua mambo.

Fikra za wanaTarime ni chanya na si kama mnavyodhani, mnakumbuka pale TBC walivyojaribu kutuchonganisha na ndugu zetu wachaga? tuliwatuuza na tukaendelea na msiba wa ndugu yetu CHACHA.

Tunapenda kuwajulisha kuwa, mwambieni huyo MTIKILA AJE HATA KESHO, Kama itawezekana, yeye anajua na ndiyo maana anasuasua kuja hapa nyumbani.

WanaJF mimi nawauliza mbona kule mikoani mwenu mnakotoka hamjawa na uamuzi wa kimageuzi kama tunavyofanya hapa Tarime?

Laiti mngekuwepo jana ktk maandamano ya CCM mngecheka hadi meno yawatoke,
 
chadema wala wasihangaike na mtikila, kwani lengo lake linajulikana ni kuwapotezea focus ya uchaguzi wa Tarime, wala wasiifanye kabisa ajenda ya kushughulikia! assume kwamba mwehu kalipuka!
 
Kama ana ushahidi kuwa ni hao waliotajwa ndio waliohusika basi ashitaki mahakamani. Kama hatafanya hivyo, hatakuwa tofauti na waganga wa kienyeji wanaochochea vitina miongoni mwa ndugu na jamaa.

Na kama kwa hili hatathibitisha vizuri, atakuwa amejisusha kwa kiwango cha hali ya juu sana, hasa kwa kuzingatia kuwa yeye ni mchungaji na mchungaji hawezi kuwa na sifa ya kuleta mafarakano kwenye kundi analolichunga. Nadhani inabidi aseme vizuri kwa hili la sivyo hatakuwa ametenda haki kwa ndugu na jamaa na Watanzania wote.

uchungaji wa mtikila mie siuoni ila ninachojua mimi ni tapeli anayeganga njaa. maana hakuna mchungaji asiye na msimamo,huyu kwa sasa hana tofauti na changu doa yeyote wa mtaani
 
Mkuu Rwabu,
Mfano wako ni mzuri ila ungeufanya kuwa yule aanayeogelea awe amevaa angalau bukta, maana sidhani kuwa Chadema wana lolote wanalotaka kuficha kuhusiana na kifo cha Wangwe (yaani hawako uchi). Kwa hiyo kama wamevaa bukta, hawawezi kushindwa kutoka majini na kumkimbiza au hata kumpa kipigo yule chizi.

Kulingana na Mtikila, Dr. Slaa ni mmoja wa watuhumiwa, kwa hiyo kuja kwake mtandaoni na ku-spin hoja ya Mtikila bila kupinga aliyosema ni sawa na kukubaliana na mashambulizi ya Mtikila. Alitakiwa atuambie hatua atakazochukua kumuadhibu Mtikila na sio kuzua lingine la Makamba-50 bila kutupa ushahidi.

Kubwa,
Rev. kama angekuwa wa maana kesi ya Malya iko mahakamani ushahidi wake angeupeleka huko tena ukaharakisha kesi hiyo kwisha. Lakini yeye anadai kwamba ushahidi hautoi mpaka ije scotyard?? Na ku organise nduguze Rip Wangwe waje kwenye Press conf. yake? so what? sidhani kama unahitaji zaidi ya hii kujua kwamba kufukuzana na mtu wa hivi utaishia wewe kuonekana hamnazo pia badala ya kuendeleza mpambano dhidi ya mafisadi!

Njaa ya Rev. ina maliza mvuto wake!

Kwa kweli hapo ukimfukuza utakuwa wewe ndo chizi.. (ni mtazamo wangu tu ) and I stand on my point as from to day Icount Rev. off...
 
Perhaps unahitaji kumpa muda zaidi hawezi kukulupuka na kusema tutakwenda mahakamani bila kuwasiliana na wenzake, inawezekana pampja na kuongea hapa vilevile watachukua hatua za kisheria maana kama amewataja ana ushaidi wa kutosha maana anajua nini kitaendelea juu yake na wao wanajua kuwa hawausiki na hawaogopi kwenda mahakamani, otherwise watu wanataka kujua ukweli kama kweli mtikila anahitaji scotland yard basi waitwe waje watafute ukweli badala ya kutumia kifo cha mwenzetu kwa kujinufaisha kisiasa.

Mimi binafsi simwamini mch. Mtikila kwa kuwa siku zote najua kuwa kichwa chake hakiko sawa na anatumiwa na CCM sana. lakini kwa hili nafikiri ni wakati mzuri wa kutafuta ukweli huko wapi, kwani ninachokiona mimi kuna dalili sio CHADEMA tu bali kuna mkono wa watu wengine na ndo maana police hawataki kumbana mallya aseme ukweli.

Mkuu jamco,
Nkubaliana na wewe kuwa labda Dr. Slaa na wenzie, watachukua hatua za kisheria na itakuwa jambo la busara sana. Kifo cha Wangwe kina sura ya faulu, kwa hiyo yeyote yule, hasa wa mChadema, anayeunganishwa nacho anatakiwa kwa nguvu na spidi ya hali ya juu kujisafisha. Hebu fikiria leo hii, Mungu aepushie mbali, Nape Mnauye apate ajali na kufariki, halafu awe alikuwa na msaidizi anayetokea kijijini kwa Lowassa na asiwe hata amechubuka, kweli kitaeleweka? Ni vema Dr. Slaa na wenzake wakatumia nafasi hii ya kuropoka kwa Mtikila kujisafisha badala ya kuitumia kuongelea walivyoamua kujitenga na wanamageuzi wengine.
 
Mkuu Rwabu,
Mfano wako ni mzuri ila ungeufanya kuwa yule aanayeogelea awe amevaa angalau bukta, maana sidhani kuwa Chadema wana lolote wanalotaka kuficha kuhusiana na kifo cha Wangwe (yaani hawako uchi). Kwa hiyo kama wamevaa bukta, hawawezi kushindwa kutoka majini na kumkimbiza au hata kumpa kipigo yule chizi.

Kulingana na Mtikila, Dr. Slaa ni mmoja wa watuhumiwa, kwa hiyo kuja kwake mtandaoni na ku-spin hoja ya Mtikila bila kupinga aliyosema ni sawa na kukubaliana na mashambulizi ya Mtikila. Alitakiwa atuambie hatua atakazochukua kumuadhibu Mtikila na sio kuzua lingine la Makamba-50 bila kutupa ushahidi.

Kubwa jinga,

Hili jina lako si jema hata kidogo, hata kama ukitoa hoja mtu anazihukumu moja kwa moja kuwa ni za (mtu mkubwa na pia mjinga) sasa nataka ujinga ukutoke ili uwe mwerevu na si mjinga tena.

Kubwa jinga, naona kama maisha yako yanategemea ujinga wako ndipo uishi, haiwezekani kabisa kweli kama wewe si mjinga ushindwe kuelewa kuwa uwepo wa vyama vya upinzani pale bungeni ni msaada kwa watanzania.

Unajua mtu waweza kudharaulika kwa yale yakutokayo kinywani mwako,
 
Laiti mngekuwepo jana ktk maandamano ya CCM mngecheka hadi meno yawatoke,

Mkuu Mwita naona una Data sana tupe basi sisi ambao hatujui kinacho jili huko Tarime...
 
Kubwa,
Rev. kama angekuwa wa maana kesi ya Malya iko mahakamani ushahidi wake angeupeleka huko tena ukaharakisha kesi hiyo kwisha. Lakini yeye anadai kwamba ushahidi hautoi mpaka ije scotyard?? Na ku organise nduguze Rip Wangwe waje kwenye Press conf. yake? so what? sidhani kama unahitaji zaidi ya hii kujua kwamba kufukuzana na mtu wa hivi utaishia wewe kuonekana hamnazo pia badala ya kuendeleza mpambano dhidi ya mafisadi!

Njaa ya Rev. ina maliza mvuto wake!

Kwa kweli hapo ukimfukuza utakuwa wewe ndo chizi.. (ni mtazamo wangu tu ) and I stand on my point as from to day Icount Rev. off...

Mkuu Rwabu,
Kumuacha Rev. aendelee kutoa sumu ni njia mojawapo ya kukwepa hoja zake, kama hakuna watakaomsikiliza Rev. Kama atapata audience, basi inaweza ikawa shida kwa Chadema hasa wakati huu wa uchaguzi. Ndio maana nikasema, kama Dr. Slaa na wenzake hawana wanalotaka kuficha, basi wampe Mtikila kipigo mahakamani kitakachomfanya asirudie tena kuwashambulia. Unaweza kuachana tu na Mtikila kama hatapata wanaomsikiliza, otherwise leaving him is at your own peril, you need to hit him the hardest.
 
uchungaji wa mtikila mie siuoni ila ninachojua mimi ni tapeli anayeganga njaa. maana hakuna mchungaji asiye na msimamo,huyu kwa sasa hana tofauti na changu doa yeyote wa mtaani

kwi kwi kwi kwi!
Siasa ya Mtikila sawa na Machinga mitaani anabuni mwezi huu sijatoa au sijaonekana kwenye media ngoja niibue hiki basi anaonekana kisha kimyaaa na anasaulika baadae tena anaibuka na uzushi mwingine ili apate za kula.........ana njaa sana Mtikila ni bora aachane na uzushi kisha awe anachangisha harambee kanisani kwake...awe anafanya mikutano mingi ili awe anajiongezea kipato....kuliko kuja na uzushi kila mara.
 
I was the first one to call for an independent investigation by the Scotland Yard......call it a fluke or whatever, but I did it first........yeeeepaaaaaa.....


Hata hili nalo ni la kushindania nani alisema wa kwanza?
Inawezekana kabisa Mchungaji kayasema haya kwa kuwa kapewa ujira fulani.... lakini kwa nini tusimpe nafasi naye kutudhihirishia yale anayofahamu kwanza kabla ya kumpa hukumu? Busara kidogo ichukue mkondo wake na kisha ndipo tutafute upande wa kuegemea.Milioni tatu za Rostam zisimfanye Mtikila kuwa hawezi sema chochote hata kama ana evidences(kama anazo)
 
Chama chenye kiburi kuliko vyote Tz ni CCM.

Na chama cha ubishi kuliko vyote ni CHADEMA .

Chama kisicho na SERA kuliko vyote ni CHADEMA eti kwenye kampeni za kuuza SERA wao wanauza SERA zao hivi MSICHAGUE chama cha mafisadi.hii ni hatari na nusu

Hivyo ndg zangu huko Tarime akili ni nywere.
 
Chama chenye kiburi kuliko vyote Tz ni CCM.

Na chama cha ubishi kuliko vyote ni CHADEMA .

Chama kisicho na SERA kuliko vyote ni CHADEMA eti kwenye kampeni za kuuza SERA wao wanauza SERA zao hivi MSICHAGUE chama cha mafisadi.hii ni hatari na nusu

Hivyo ndg zangu huko Tarime akili ni nywere.

Mkuu hapa ulimaanisha akili ni nywele...... au sio?
 
Hata hili nalo ni la kushindania nani alisema wa kwanza?
Inawezekana kabisa Mchungaji kayasema haya kwa kuwa kapewa ujira fulani.... lakini kwa nini tusimpe nafasi naye kutudhihirishia yale anayofahamu kwanza kabla ya kumpa hukumu? Busara kidogo ichukue mkondo wake na kisha ndipo tutafute upande wa kuegemea.Milioni tatu za Rostam zisimfanye Mtikila kuwa hawezi sema chochote hata kama ana evidences(kama anazo)

Nah...hakuna anayeshindana (kwa upande wangu)....I'm just having more fun than you should be allowed to have....that's all.....
 
Wale wanaotaka kuleta machafuko na migogoro Tarime naona hawajachoka na sasa hivi wanataka kufanya haya yote kwa nia, ari na kasi ya ajabu wakimtumia anayejiita mtumishi wa MUNGU - Mtikila.

Naomba tena niwaambie nyie waandishi wa habari kuwa Tarime haitageuka kuwa Congo au Rwanda. Wanatarime wana akili zao na wanajua kutofautisha ujinga na upumbavu. Katika hili, likiwemo la kuleta askari mamia ili "kutuliza fujo" Tarime ambazo hazipo, ni mfano mbaya sana kwa uongozi wa serikali yetu.

Watu hapa waliitisha uchunguzi huru wa kifo hiki na serikali ikakaa kimya, vyama karibu vyote vya siasa vilitaka serikali ichunguze kifo hiki ili kuondoa maneno ya wapumbavu na wapenda damu kumwagika kama Mtikila, lakini wengi wakakataa, sasa haya ya kuleta mamia ya askari Tarime na huu upuuzi wa vyombo vya habari yana nia gani kwetu wana Tarime?

MUNGU yuko na tutashinda tu jaribu hili..... nawahakikishia nyie wenye kiu ya damu ya wana Tarime kuwa hakuna mapigano yoyote yatakayotokea Tarime hata mkimwaga sumu mbaya kiasi gani kwenye vyombo vya habari.
 
Hivi mbona polisi hawajaenda kuwakata waliotajwa kuhusika na kifo cha Wangwe, pamoja na Mtikila mwenyewe kwa mahojiano ya kipolisi zaidi?

Mtikila anatakiwa achukuliwe na polisi aende akatoe maelezo ya kutosha, kisha ndipo hao watuhumiwa wanaweza kuhojiwa pia. Ni nani anaweza kukurupuka kwenda kubishana kwenye vyombo vya habari?

Lengo la Mtikila ni kuwafanya CHADEMA wawe na mambo mawili kwa wakati mmoja, kesi mahakamani, na uchaguzi Tarime. Dawa ni kumwacha tu, kama polisi wanamwamwini, waende wakawakamate watuhumiwa.
 
Hivi mbona polisi hawajaenda kuwakata waliotajwa kuhusika na kifo cha Wangwe, pamoja na Mtikila mwenyewe kwa mahojiano ya kipolisi zaidi?

Mtikila anatakiwa achukuliwe na polisi aende akatoe maelezo ya kutosha, kisha ndipo hao watuhumiwa wanaweza kuhojiwa pia. Ni nani anaweza kukurupuka kwenda kubishana kwenye vyombo vya habari?

Lengo la Mtikila ni kuwafanya CHADEMA wawe na mambo mawili kwa wakati mmoja, kesi mahakamani, na uchaguzi Tarime. Dawa ni kumwacha tu, kama polisi wanamwamwini, waende wakawakamate watuhumiwa.

Mkuu Masaki,

Lengo la Mtikila na wapenda umwagaji wa damu wenzake sio kuibwaga CHADEMA bali ni kuiingiza Tarime kwenye mapigano. Kuna watu wanataka kuona Tarime ikiingia kwenye mapigano ili wapate sababu ya kufanya mambo yao ya ajabu ambayo wamekuwa wanapanga kwa miaka mingi.

Coverage ya TBC1 na magazeti ya Rostam Azizi wakati wa msiba wa Wangwe ni uthibitisho tosha wa kile wasiopenda amani wanachopanga kufanya Tarime na kwingine kokote kama wakipewa nafasi.

Kwa hili tutawapinga kwa nguvu zote hapa na kila sehemu tutakakowaona.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom