Kifo cha Mhe. Chacha Wangwe na uchunguzi wake

Kifo cha Mhe. Chacha Wangwe na uchunguzi wake

Status
Not open for further replies.
Mtikila kuhojiwa na polisi

JESHI la Polisi limesema litamhoji Mchungaji Christopher Mtikila kutokana na madai yake kuwa kuna vigogo wamemuua aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Tarime, marehemu Chacha Zakayo Wangwe.

Akizungumza na mwandishi wetu jana Mkurugenzi wa Upelelezi na Makosa ya Jinai nchini, Robert Manumba alisema Mtikila atahojiwa kama atatoa ushirikiano kuhusu ushahidi alionao wa madai ya kuuawa kwa Wangwe.

"Ikiwa atathibitisha hayo madai ya kuuawa kwa Wangwe sisi kama jeshi la polisi tutashughulikia, tutamuomba tu aoneshe ushirikiano," alisema Manumba.

Juzi Jumapili Mchungaji Mtikila aliwaambia waandishi wa habari jijini Dare s Salaam kuwa, Wangwe aliuawa na watu kutoka Kenya kwa operesheni maalum iliyosukwa na vigogo (majina tunayahifadhi).

Alisema ana ushahidi wa kutosha wa jinsi vigogo hao walivyoshiriki kutekeleza mauaji hayo aliyoyaita ya kinyama.

Alimuomba Rais Jakaya Kikwete kukiajiri Kikosi Maalum cha Upelelezi cha Uingereza cha Scotland Yard kufanya uchunguzi wa kifo hicho kwa madai kuwa Wangwe alikuwa kiongozi wa kitaifa.
 
Huhitaji ushahidi kuona kwamba Mtikila ameingia katika kazi kama aliyoifanya mara kadhaa wakati wa uchaguzi wa mwaka 2000 na baadaye kabla na wakati wa uchaguzi wa mwaka 2005.

MUNGU anatupa mwanga kila kukicha na tuliweza kuona na kumfahamu Mtikila ni mtu wa aina gani kama ambayo sasa tunaona Mhariri Mkuu wa gazeti la Majira ni mtu wa aina gani.

We are giving Mtikila too much power ya kuwa anatumiwa kuwamaliza wapinzani. Sheria zipo, kwa nini wapinzani nao wasilale naye sambamba? After all kama Mtikila atakuwa anatumiwa basi yuko very cheap, maana baada ya miaka yote hiyo ya kutumiwa, say tokea 2000 and before, bado ni mchovu na anaganga njaa na kagari kake kale kabovu. Mtikila ni mtu wa kutafuta tu sifa na dawa yake ni kumminya kisheria mpaka asijaribu tena kukuchafua.
 
Mtikila siku zote ni kiongozi wa kutumiwa tu, halafu ni fisadi pia na ni tapeli mkubwa sana siku zote kazi kuomba omba hela na misaaada,

Binafsi siwezi kuamini hata neno moja toka mdomoni mwake, nimemuona kwa macho yangu akimtapeli mama mmoja pale ubalozini NY, dola $ 1,000 ambaye alijitolea kumsaidia baada ya Mtikila kukwama kama kawaida yake akiwa hana hata senti tano kwenye nchi za watu, mara ya mwisho hivi akribuni nilimuuliza yule mama akasema hajamlipa na amemsamehe!

Wakati mwingine tena nilimkuta London amekwama kama kawaida, mimi binafsi nikawapigia viongozi wa CCM, wakamtumia hela, huyu ni fisadi hana lolote siwezi kusikiliza anything from him, nashangaa sana kusikia hata anapewa majukwaa the man is just another tapeli period! Ila yeye ameamua kuufanyia kwenye siasa za Tanzania ambako wananchi wana desparation ya kusikia udaku kwamba they will take anything as the news of the day!
 
Kwa kweli nchi imefikia mahali pabaya sana. Kwa sasa nchi inayumba na wahusika wanahakikisha hakuna chama mbadala cha kuweza kuchukua madaraka na hayo yanafanyika kwa gharama kubwa na kwa kutumia kodi zetu.

Kuna kila sababu ya kila Mtanzania ukiwamo ndugu yangu Mtanzania wa hapa JF kulijua hilo na kwa kulijua hilo tutakua makini na kuangalia Tanzania Yetu iliyo njema kama alivyo ndugu yangu Tanzania Njema.

Tunahitaji mikakati mahususi ili angalau serikali iwe na woga wa kuwasaliti Watanzania kama si kuondolewa kabisa na kuingia wale wenye nia njema na nchi hii.

Kwa utangulizi huo, na kwa historia ya Mtikila ambayo si ngeni kwetu; na kwa mazingira na wakati (timing) ya taarifa ya Mtikila (akisema wazi anaweka mgombea Tarime), haihitaji mtaalamu kung'amua kinachoendelea.

Hawa jamaa wameingia gharama kubwa kufanya kila wawezalo kutimiza malengo yao na kuhakikisha wanafikishwa wanakokusudia. Kwa bahati mbaya sana tuna ombwe (vacum) kubwa la utawala na ombwe hilo tusipoangalia litazibwa na kafara ambayo niliwahi kuizungumzia. Kwa kawaida nchi nyingi zimeweza kuendelea baada ya kutoa kafara (umwagaji damu) kwa 'mizimu inayokalia' mali zilizopo ardhini na baharini. Kwa wanaoelewa nchi sasa imekidhi sehemu kubwa kama si kupitiliza vigezo vinavyoweza kusababisha nchi iingie katika machafuko.

Huhitaji ushahidi kuona kwamba Mtikila ameingia katika kazi kama aliyoifanya mara kadhaa wakati wa uchaguzi wa mwaka 2000 na baadaye kabla na wakati wa uchaguzi wa mwaka 2005.

MUNGU anatupa mwanga kila kukicha na tuliweza kuona na kumfahamu Mtikila ni mtu wa aina gani kama ambayo sasa tunaona Mhariri Mkuu wa gazeti la Majira ni mtu wa aina gani.


Mkuu Halisi,

Japo nakubaliana na karibu yote unayoyasema lakini pia kuamini upinzani wanaweza kulelewa kama mayai na kisha wakiingia madarakani na kuwa viongozi bora ni wishiful thinking or naivety at its best.

Kiongozi yeyote anayetaka kuingia madarakani lazima awe tested na ndio hicho ambacho watu mbalimbali wanafanya sasa kwa viongozi wa CHADEMA na vyama vingine.

Watu wengi wameandika umuhimu wa vyama kuungana na kushirikiana ili kuweza kupambana na CCM, matokeo yake tunaona CHADEMA inaona wengine wote ni vibaraka wa CCM isipokuwa wao.

Watu wamehoji umuhimu wa vyama kuwa na sera mbali ya mapambano na ufisadi, lakini hakuna kinachofanyika na badala yake sera pekee ninayoiona mimi ni vita vya ufisadi. Hata kama hakuna mtu hata mmoja atakayekula rushwa Tanzania bado tutaendelea kuwa maskini. Tunahitaji mikakati ya maana mbali ya hayo mapambano na ufisadi.

CHADEMA waliambiwa wakati ule wanagombana na Wangwe kwamba walichokuwa wanafanya kilikuwa ni makosa. Wangwe amekufa wanajifanya wao ndio walikuwa waumini wa Wangwe, unafiki mkubwa. Walikuwa wa kwanza kuingiza siasa kwenye msiba kwa lile tamko bovu la yule kijana wao. Bila kujua wakawa wamefungulia mkondo wa lawama na tuhuma kwenye kifo cha Wangwe. Kinachotokea sasa its like the chickens are coming home to roast.

Siamini na wala sina lengo la kutumia JF kulea au kukipendelea chama chochote. Hapa ni kumkoma nyani giladi. Kama ni suala la CCM tutaandika kwa nguvu zote lakini pia kama ni suala la CHADEMA tutaandika kwa nguvu hizo hizo.

Kila mtu anamjua Mtikila miaka na miaka, lakini hao hao wanaomtuhumu sasa ndio hao hao waliokuwa wanamshangilia aliposema CCM wamemua Kolimba, au aliposema Mkapa ni mtu wa Msumbiji nk. Kama Mtikila anaropoka ovyo, kitu ambacho mimi naamini ni kweli, je na hao wengine wanaoropoka hovyo nao wanatumiwa na nani? Kama analipwa mamilioni hayo ya kutumiwa mbona tunamwona kila siku anasota pale pale? Mbona anaenda hata kujidhalilisha kwa RA kwenda kukopa milioni tatu?

Challenge kubwa ya upinzani kwasasa ni kuunda umoja wa vyama vya upinzani, hicho ndicho Watanzania wengi tunataka. Kuungana sio kwa watu unaokubaliana nao tu, muungano wa maana ni ule unaoleta mawazo mapya na challenges mpaya ndani ya umoja. Sababu zinazotolewa sasa kuhusu kushindwa kutokea kwa huo muungano zinatokana na ubinafsi zaidi kuliko maslahi ya taifa.
 
Na wewe una ushahidi gani kuwa sina ushahidi kuhusu Dr Slaa au kwa vile una uhuru wa kuuliza kutoka kwenye nyuma ya screen yako ya kompyuta?

Kwa sababu umeuliza kama ana ushahidi halafu hapo hapo ukasema asifanye mambo ya kuokoteza udaku. Hujui jibu halafu ukatoa hukumu. Mimi nimeuliza tu. Notice the difference. Wewe umehitimisha, kwamba aache kuokota udaku baada ya kuuliza. Umetoa hukumu. Mimi nimeuliza tu. Hakuna hitimisho hapo kwamba wewe huna ushahidi.

Nafikiri ilibidi upate jibu la whether ana ushahidi kabla ya kumwambia aache kuokota udaku, maana umesema unamuheshimu. Lakini hapo hapo umemkung'uta dongo bila sababu, mtu unae muheshimu. Ilinisikitisha.
 
Mkuu Halisi,

Japo nakubaliana na karibu yote unayoyasema lakini pia kuamini upinzani wanaweza kulelewa kama mayai na kisha wakiingia madarakani na kuwa viongozi bora ni wishiful thinking or naivety at its best.

Kiongozi yeyote anayetaka kuingia madarakani lazima awe tested na ndio hicho ambacho watu mbalimbali wanafanya sasa kwa viongozi wa CHADEMA na vyama vingine.

Watu wengi wameandika umuhimu wa vyama kuungana na kushirikiana ili kuweza kupambana na CCM, matokeo yake tunaona CHADEMA inaona wengine wote ni vibaraka wa CCM isipokuwa wao.

Watu wamehoji umuhimu wa vyama kuwa na sera mbali ya mapambano na ufisadi, lakini hakuna kinachofanyika na badala yake sera pekee ninayoiona mimi ni vita vya ufisadi. Hata kama hakuna mtu hata mmoja atakayekula rushwa Tanzania bado tutaendelea kuwa maskini. Tunahitaji mikakati ya maana mbali ya hayo mapambano na ufisadi.

CHADEMA waliambiwa wakati ule wanagombana na Wangwe kwamba walichokuwa wanafanya kilikuwa ni makosa. Wangwe amekufa wanajifanya wao ndio walikuwa waumini wa Wangwe, unafiki mkubwa. Walikuwa wa kwanza kuingiza siasa kwenye msiba kwa lile tamko bovu la yule kijana wao. Bila kujua wakawa wamefungulia mkondo wa lawama na tuhuma kwenye kifo cha Wangwe. Kinachotokea sasa its like the chickens are coming home to roast.

Siamini na wala sina lengo la kutumia JF kulea au kukipendelea chama chochote. Hapa ni kumkoma nyani giladi. Kama ni suala la CCM tutaandika kwa nguvu zote lakini pia kama ni suala la CHADEMA tutaandika kwa nguvu hizo hizo.

Kila mtu anamjua Mtikila miaka na miaka, lakini hao hao wanaomtuhumu sasa ndio hao hao waliokuwa wanamshangilia aliposema CCM wamemua Kolimba, au aliposema Mkapa ni mtu wa Msumbiji nk. Kama Mtikila anaropoka ovyo, kitu ambacho mimi naamini ni kweli, je na hao wengine wanaoropoka hovyo nao wanatumiwa na nani? Kama analipwa mamilioni hayo ya kutumiwa mbona tunamwona kila siku anasota pale pale? Mbona anaenda hata kujidhalilisha kwa RA kwenda kukopa milioni tatu?

Challenge kubwa ya upinzani kwasasa ni kuunda umoja wa vyama vya upinzani, hicho ndicho Watanzania wengi tunataka. Kuungana sio kwa watu unaokubaliana nao tu, muungano wa maana ni ule unaoleta mawazo mapya na challenges mpaya ndani ya umoja. Sababu zinazotolewa sasa kuhusu kushindwa kutokea kwa huo muungano zinatokana na ubinafsi zaidi kuliko maslahi ya taifa.

Mkuu Mtanzania, kwa maelezo yako naamini wewe ni mtu makini sana na mwenye uelewa. Sikuwa na maana ya kuulea upinzani kwa mambo ya kijinga kwani hata Mtikila ni mpinzani. Ninachoweza kusema ni kuangalia kwa undani sababu na wakati wa mambo yanayotokea sasa. Tujue fika kwamba fedha, madaraka na mapenzi ni mambo ambayo yanaweza kusababisha maafa makubwa katika jamii na kwa kuanzia hata katika familia.

Ni kweli kwamba umoja kwa wapinzani ni jambo la msingi, lakini kuna wakati mzee Ndesamburo aliwahi kuzungumzia umoja wa vyama na si lazima uwe umoja wa wapinzani. Alisema kama CCM na CUF ama CCM na Chadema watakubaliana mambo ya msingi wanaweza kushirikiana na hakuna ubaya kwa hilo.

Imani ya sasa ya Chadema kwa mujibu wa maelezo ya Dk. Slaa humu ndani ni kwamba sehemu kubwa ya viongozi wa sasa wa upinzani wananunulika na kwa siasa za Tanzania sina sababu hata chembe za kutilia shaka hisia za Chadema. Kuna ushahidi mwingi nilionao kuhusu CUF kutumiwa na RA mwaka 2000, NCCR Mageuzi kutumika na RA mwaka 2005 na Mtikila (DP) kutumika mwaka 2005. NAyasema hayo kwa uhakika mkubwa na wale ambao wananifahamu wakiwamo hao viongozi watakibaliana nami kuwa nina uhakika. NIna uhakika pia kuna wakati hata Chadema kuna walioingia huo mkenge kabla ya wao wenyewe ndani kuwabaini wahusika na baadhi ya wahusika kujisalimisha, baadhi wakiondoka na wengine kuendelea kuwapo chini ya uangalizi (Hilo nalo nina hakika nalo).

Kwa hali hiyo, sioni ajabu kwa Chadema kujitenga kutoka kwa wenzao baada ya kuzingatia matukio ya miaka ya nyuma na wakiona wale waliohusishwa mwaka 2000 na mwaka 2005 bado wapo tena baadhi katika nyadhifa nzito.

Kwa kuwa Tanzania ni yetu sote, tusubiri tuone kama KAFARA itatolewa kwa ajili ya ustawi wa taifa letu wa kudumu lakini kwa kifupi ni kwamba, SIASA ZA TANZANIA SASA ZIMECHAFUKA. HALI YA NCHI SASA IMECHAFUKA. HAkuna tena amani
 
Unaweza kuwa ndio unamwongezea sifa, mahakamani ndipo mahali Mtikila anakopatia ujiko
Endapo allegations zitakuwa sahihi otherwise ndipo pa kummaliza politically! Huyu jamaa si nasikia alikemea mapepo wanaosababisha asiandikweandikwe na vyombo vya habari? Then nimekubali kuwa 'ukemeaji' wake umefanya kazi...
 
Nilipokuwa mdogo niliambiwa na mama kwamba nisizungumze na mwendawazimu maana hakuna atakayeona tofauti yoyote kati yetu.

Ninawashauri waandishi wa habari na vyombo vyote vya habari ikiwemo jamiiforums kuzika na kusahau kabisa habari za watu kama hawa. Hawana lolote jipya katika jamii na yeyote mwenye kuthamini wakati, nafasi na mchango wake kwa jamii hawezi kuwa na nafasi kwa watu kama hawa ambao wanaishi, kula, kunywa na kupata umaarfu kwa kujifanya wanajua hili au lile, wanapinga hili au lile au wanapigania hiki au lile. Mbona huyu bwana hajamaliza kazi yake ya kupiga vita Mahakama ya Kadhi sasa tayari kaingilia jipya...... Heri ukose yote kuliko kukosa aibu, heshima na utu katika dunia hii!
 
Challenge kubwa ya upinzani kwasasa ni kuunda umoja wa vyama vya upinzani, hicho ndicho Watanzania wengi tunataka. Kuungana sio kwa watu unaokubaliana nao tu, muungano wa maana ni ule unaoleta mawazo mapya na challenges mpaya ndani ya umoja. Sababu zinazotolewa sasa kuhusu kushindwa kutokea kwa huo muungano zinatokana na ubinafsi zaidi kuliko maslahi ya taifa.

Hicho kitu ni vigumu kuwezekana.Walishajaribu lakini njaa za baadhi yao zimesababisha wasambaratike
 
Hicho kitu ni vigumu kuwezekana.Walishajaribu lakini njaa za baadhi yao zimesababisha wasambaratike

Mafisadi walipotuweza ndo hapo! hapo kwenye njaa! ndo maana kipindi cha uchaguzi wagombea + mafisadi wao wanagawa vitu na vijisenti then wanashinda kwa kishindo. Eti hata viongozi wa kitaifa wameshindwa kuvumilia njaa sasa wananchi wa kawaida si t-shirt na kitenge vinatosha kabisa.
 
Kwa sababu umeuliza kama ana ushahidi halafu hapo hapo ukasema asifanye mambo ya kuokoteza udaku. Hujui jibu halafu ukatoa hukumu. Mimi nimeuliza tu. Notice the difference. Wewe umehitimisha, kwamba aache kuokota udaku baada ya kuuliza. Umetoa hukumu. Mimi nimeuliza tu. Hakuna hitimisho hapo kwamba wewe huna ushahidi.

Nafikiri ilibidi upate jibu la whether ana ushahidi kabla ya kumwambia aache kuokota udaku, maana umesema unamuheshimu. Lakini hapo hapo umemkung'uta dongo bila sababu, mtu unae muheshimu. Ilinisikitisha.

Kuhani,

Ni udaku kwa sababu huo unauita "ushahidi" hana na kama angekuwa nao angeupeleka kwenye vyombo vya sheria. Na hii inatokana na precedence aliyoijenga yeye mwenyewe Dr Slaa awali alipodai Gavana Ballali kakimbilia Malta. Once a liar always a liar!
 
Nimesoma sana maelezo yote kuhusu Mtikila,na kama mtu wa kwanza kuhojiwa kuhusu hili naomba awe mzee mwanakijiji.Mwanakijiji alishabikia sana mwanzoni kwamba kifo cha wangwe hakikuwa cha kawaida na laiungwa mkono na vijana wa Mbowe kama MK na wengineo.

Mzee Mwanakijiji alihusisha na aling'ang'ania kuwa kulikuwa na Mbinu za kimafia kuhsu kifo cha wangwe.Kipindi kile Mzee Mwanakijiji hakusema wazi ni nani alipanga mipango ya kumuuza marehemu wangwe.Inawezekana kabisa Mzee Mwanakijiji alimwambia maneno haya Mtikila.aliongelea hoja za muda wa tukio na kila kitu

Tatizo la JF ni kwamba linapokuaja suala linalohusu CHADEMA ,wanasema ni la Uongo na has alikimhusu Mhe. Mbowe.Inawezekana kabisa malya alitumiwa na kina Slaa..who know,Tuache Polisi waende kwa Mtikil akawape Full Details kushus anachokijua.

Suala lingine ambalo linaonesha ni kusihiwa hoja,ni jambo la Dr. slaa kuja ahapa na kusema amseikia Makamba kampa Mtikila pesa.Hizi zsiasa za kusikia bila kuwa na uhakika wa jambo lenyewe inaonesha ni upotoshaji wa khali ya juu sana.

Wana JF kama mtakumbuka kuna wakati nilisema maneno haya..Ole Wenu CHADEMA..nilirudia mara saba kutamka maneno haya baada ya kifo cha wangwe.CHADEMA walionesha kuwa kifo hiki si cha kawada na Mnyika alimwandikia IGP achunguze suala hili.Mtikila katumia haki yake kusema ukweli anaoujua.

Mnyika,Mwanakijiji haya mambo mliyaanzisha wenyewe na mkayang'ngania kwa dhati kwa kukipatamatope chama cha Mapinduzi ndicho kinachohusika ila kumbe ni vigogo hao hao.

Mie namuunga mkono Mtikila,na sasa kuna haja ya Mwanakijiji kutuambia habari za kifo hciho yeye anazozijua.

mpaka sasa Mzee MWanakijiji ahojiwe na Mbowe ahojiwe na Polisi kuhsu tuhuma hizi.Na mpaka sasa mie naamini kina Mnowe ,Dr. slaa wao ndio wanahosuika na mauaji ya chacha Wangwe.
 
Kweli isije ikawa wamemuua halafu mwili ukakalishwa kwenye gari, gari ikawashwa accelerator jiwe ikajibamiza huku na kule hadi likawa nyang'a nyang'a. Yule kijana Deus Malya anastori za kutusimulia.

Dr Slaa huyu Mtikila hajapata info zozote bali kasoma hapa JF
Ukisoma link hii
https://www.jamiiforums.com/newreply.php?do=newreply&p=257701 utaona ukweli wake hana jipya zaidi ya kuyafanya mambo haya ni ya kisiasa zaidi.
 
Nimesoma sana maelezo yote kuhusu Mtikila,na kama mtu wa kwanza kuhojiwa kuhusu hili naomba awe mzee mwanakijiji.Mwanakijiji alishabikia sana mwanzoni kwamba kifo cha wangwe hakikuwa cha kawaida na laiungwa mkono na vijana wa Mbowe kama MK na wengineo.

Mzee Mwanakijiji alihusisha na aling'ang'ania kuwa kulikuwa na Mbinu za kimafia kuhsu kifo cha wangwe.Kipindi kile Mzee Mwanakijiji hakusema wazi ni nani alipanga mipango ya kumuuza marehemu wangwe.Inawezekana kabisa Mzee Mwanakijiji alimwambia maneno haya Mtikila.aliongelea hoja za muda wa tukio na kila kitu

Tatizo la JF ni kwamba linapokuaja suala linalohusu CHADEMA ,wanasema ni la Uongo na has alikimhusu Mhe. Mbowe.Inawezekana kabisa malya alitumiwa na kina Slaa..who know,Tuache Polisi waende kwa Mtikil akawape Full Details kushus anachokijua.

Suala lingine ambalo linaonesha ni kusihiwa hoja,ni jambo la Dr. slaa kuja ahapa na kusema amseikia Makamba kampa Mtikila pesa.Hizi zsiasa za kusikia bila kuwa na uhakika wa jambo lenyewe inaonesha ni upotoshaji wa khali ya juu sana.

Wana JF kama mtakumbuka kuna wakati nilisema maneno haya..Ole Wenu CHADEMA..nilirudia mara saba kutamka maneno haya baada ya kifo cha wangwe.CHADEMA walionesha kuwa kifo hiki si cha kawada na Mnyika alimwandikia IGP achunguze suala hili.Mtikila katumia haki yake kusema ukweli anaoujua.

Mnyika,Mwanakijiji haya mambo mliyaanzisha wenyewe na mkayang'ngania kwa dhati kwa kukipatamatope chama cha Mapinduzi ndicho kinachohusika ila kumbe ni vigogo hao hao.

Mie namuunga mkono Mtikila,na sasa kuna haja ya Mwanakijiji kutuambia habari za kifo hciho yeye anazozijua.

mpaka sasa Mzee MWanakijiji ahojiwe na Mbowe ahojiwe na Polisi kuhsu tuhuma hizi.Na mpaka sasa mie naamini kina Mnowe ,Dr. slaa wao ndio wanahosuika na mauaji ya chacha Wangwe.

Karata tatu. Chekundu, Cheusi? ukiweka hapa umepata, chagua
 
Unaweza kuwa ndio unamwongezea sifa, mahakamani ndipo mahali Mtikila anakopatia ujiko

Endapo allegations zitakuwa sahihi otherwise ndipo pa kummaliza politically! Huyu jamaa si nasikia alikemea mapepo wanaosababisha asiandikweandikwe na vyombo vya habari? Then nimekubali kuwa 'ukemeaji' wake umefanya kazi...


Nakubaliana kabisaa na Invisible,
Dawa ya Mtikila ni kumpeleka mahakamani ambako kuna mwisho wa kila jambo kuliko kumuacha aendelee kumwaga sumu yake. Hao wanaosema eti waandishi waachane naye tu ndio dawa, wanaota ndoto za mchana maana sio kila gazeti/redio/TV wenye nia ya kuibeba Chadema. Kama akina Dr. Slaa wanataka Mtikila asiendelee kuwachongea kwa wananchi, basi watumie taratibu zinazoeleweka, ambayo sidhani kuna zaidi ya mahakama.
 
Kweli isije ikawa wamemuua halafu mwili ukakalishwa kwenye gari, gari ikawashwa accelerator jiwe ikajibamiza huku na kule hadi likawa nyang'a nyang'a. Yule kijana Deus Malya anastori za kutusimulia.
teh teh..CHADEMA kazi mnayo..
 
Nakubaliana kabisaa na Invisible,
Dawa ya Mtikila ni kumpeleka mahakamani ambako kuna mwisho wa kila jambo kuliko kumuacha aendelee kumwaga sumu yake. Hao wanaosema eti waandishi waachane naye tu ndio dawa, wanaota ndoto za mchana maana sio kila gazeti/redio/TV wenye nia ya kuibeba Chadema. Kama akina Dr. Slaa wanataka Mtikila asiendelee kuwachongea kwa wananchi, basi watumie taratibu zinazoeleweka, ambayo sidhani kuna zaidi ya mahakama.

unataka wampele mahakamani huku ushahidi anao,hadi waliompigia simu malya anawajua...


Period..
 
Kwa kuwa Tanzania ni yetu sote, tusubiri tuone kama KAFARA itatolewa kwa ajili ya ustawi wa taifa letu wa kudumu lakini kwa kifupi ni kwamba, SIASA ZA TANZANIA SASA ZIMECHAFUKA. HALI YA NCHI SASA IMECHAFUKA. HAkuna tena amani

Mkuu, imekuwa ukirejea sana hii habari ya KAFARA. Unajua ni neo linalowatisha baadhi ya watu, mimi nikiwa mmoja wao. Unataka tuchinjane?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom