Kifo cha Mhe. Chacha Wangwe na uchunguzi wake

Kifo cha Mhe. Chacha Wangwe na uchunguzi wake

Status
Not open for further replies.
Jamani hivi polisi wako wapi mpaka muda huu hawajamsweka lupango huyu mtikila?jamani na hao ndugu za wengwe wakiohudhuria huo mkutano si wangeanza nae hapo hapo kwenye mkutano awape ushahidi wa kutosha?Jamani napata mashaka kama wangwe aliuliwa mtikila atakuwa anajua kila kitu .
 
JF,
Siyo fedha za Rostam tu. Taarifa zinazotufikia ni kuwa ana 50 za Makamba pia. Amepewa kwa jukumu pekee la kuimaliza Chadema kama prelude ya Kampeni za Tarime. Amechelewa tu kwenda kule baada ya kuona kuna mvua ya mawe kwa wanaoichafua Chadema. Logic ya kuomba Scotland Yard ieleweke kwa msingi huo. Haitaitwa,na ataendelea kwa kisingizio hicho kukataa kutoa ushahidi. Hata hivyo, sina sababu ya kujibizana na Mtikila, mwisho umma hautajua kichaa ni nani.

Dr Slaa sitashangaa kuwa Mtikila anatumiwa na yeyote.Nimeandika kabla kuwa Mtikila kwa muda mrefu amekuwa akiendesha siasa za gizani sana na kwa mujibu wa taratibu za uanzushwaji na uendeshaji wa vyama vya siasa siasa za UDP siyo rasmi.Hiki ni chama ambacho kiutaratibu kilitakiwa kuchunguzwa.

Lakini haitatokea DP ikachunguzwa pamoja na kufanya siasa za gizani.Huu ni uthibitisho kuwa Mtikila na DP yake yupo pale kama an affiliation party of the rulling party.Uhai wa kisiasa wa Mtikila unategemea michezo michafu ya watawala.Hainishangazi kuwa hata Makamba amemlipa 50 millions.

Kampeni za CCM hazifanyiki Tarime peke yake.Magazeti uchwara na wanasiasa uchwara nao wapo kazini.Kisa Kuiua Chadema kisiasa na kudhoofisha upinzani bungeni.
Kama wanatarime wakihadaiwa kwa porojo za CCM na vibaraka wake ni wazi kuwa wantarime watapoteza haki yao ya kikatiba na kujikabidhi mikononi mwa CCM.NI sawa na kuyarudia mataapishi ukayala.Haiyumkiniki jamani.

Hata hivyo naamini wana Tarime hawatahadaiwa kamwe
 
MTIKILA, mchungaji ujivikaye ngozi ya kondoo huku matendo yako na tabia yako ikiwa ni ya mbwa mwitu alaye kondoo! Shame on you! Shame on your beliefs! Shame on your conscienceness!!

Why would you be this cheap! And you think that principled people will accept your propaganda after having snatched a few coins from corrupt CCM officials!
 
JF,
Siyo fedha za Rostam tu. Taarifa zinazotufikia ni kuwa ana 50 za Makamba pia. Amepewa kwa jukumu pekee la kuimaliza Chadema kama prelude ya Kampeni za Tarime. Amechelewa tu kwenda kule baada ya kuona kuna mvua ya mawe kwa wanaoichafua Chadema. Logic ya kuomba Scotland Yard ieleweke kwa msingi huo. Haitaitwa,na ataendelea kwa kisingizio hicho kukataa kutoa ushahidi. Hata hivyo, sina sababu ya kujibizana na Mtikila, mwisho umma hautajua kichaa ni nani.

Mheshimiwa Dr. Slaa,

Binafsi siamini kuna mkono wa mtu kwenye kifo cha Wangwe na niliandika hivyo toka siku ya kwanza.

Ila nina wasiwasi na madai yako ya leo kwamba Mtikila anasema hivyo kwasababu kapewa 50m ya Makamba. Je una ushahidi gani juu ya hilo? Kama huna, kuna tofauti gani na huyo Mtikila ambaye unamwita kichaa?

Kama nilivyoandika mwanzoni pia ilikuwa ni makosa makubwa mno kuingiza siasa kwenye msiba wa Wangwe. Lile tamko la Mnyika lilikuwa linafungua njia ya siasa kuingia kwenye msiba wa Wangwe na sasa hata akina Mtikila nao wameamua kuendeleza siasa hizo hizo.

Siasa zetu zinaelekea kubaya kweli kweli.
 
JF,
Siyo fedha za Rostam tu. Taarifa zinazotufikia ni kuwa ana 50 za Makamba pia. Amepewa kwa jukumu pekee la kuimaliza Chadema kama prelude ya Kampeni za Tarime. Amechelewa tu kwenda kule baada ya kuona kuna mvua ya mawe kwa wanaoichafua Chadema. Logic ya kuomba Scotland Yard ieleweke kwa msingi huo. Haitaitwa,na ataendelea kwa kisingizio hicho kukataa kutoa ushahidi. Hata hivyo, sina sababu ya kujibizana na Mtikila, mwisho umma hautajua kichaa ni nani.

Mh. Daktari Slaa,
Nadhani ulichotakiwa kutufahamisha ni juu ya hatua mtakazochukua kutokana na matamshi ya Mtikila then ndio uongezee hizo allegations za 50-Makamba. Ninavyoelewa hadi hivi sasa ni kuwa hujakanusha aliyosema Mtikila bali umongezea tu spin na kuelezea tu tabia mpya ya Chadema ya Go Alone . Wengi wetu tulitegemea mfungue kesi ya defermation au nyie hamuoni kuwa Mtikila anawachafua?
 
Mh. Daktari Slaa,
Nadhani ulichotakiwa kutufahamisha ni juu ya hatua mtakazochukua kutokana na matamshi ya Mtikila then ndio uongezee hizo allegations za 50-Makamba. Ninavyoelewa hadi hivi sasa ni kuwa hujakanusha aliyosema Mtikila bali umongezea tu spin na kuelezea tu tabia mpya ya Chadema ya Go Alone . Wengi wetu tulitegemea mfungue kesi ya defermation au nyie hamuoni kuwa Mtikila anawachafua?

Nina wasi wasi kwa hili Mtikila huenda anajichafua mwenyewe pia! Soon and very soon ataonekana hafai mbele ya macho ya jamii. Nimekuwa mtaani leo nikisikia gumzo kwa watu wa vijiweni kabisa na kwa haraka imeonyesha wengi wao kumstukia na kumuona hafai kabisa! By the way mimi ni mmoja wao ambaye nilikuwa nikimshabikia sana Rev. tangu enzi za gabachori, am sorry to say that as from now I count him off...
 
JF,
Nashukuru kuwa angalau sasa somo linaanza kueleweka. Tuliposema, Chadema tuko tayari kwenda peke yetu wengi walitulaumu wakadhani tumefanya makosa makubwa kukataa ushirikiano. Tuliweka wazi kuwa hatuhitaji kufanya siasa ya unafiki, na wala kushirikiana na watu ambao mchana tunacheka usiku wanatuhujumu. Nadhani somo linaanza kueleweka, na tunakaribia wakati ambapo Watanzania sasa tunaweza kuwaambia, kuwa viko ni vyama vichache sana vilivyo serious ambavyo mtu anaweza kushirikiana navyo.Watanzania nadhani sasa mnaanza kutuelewa.


Daktari Slaa,
Naona kwa huu mtazamo wenu wa holier than thou, nafikiri mko hatarini kuanguka kwa kishindo kibaya. Vyama vikubwa na vya kugeresha vitakuwepo nchini TZ hata kama kutatungwa sheria ya kuvibana.

Lakini hiki kiburi cha CHADEMA cha kujiona kuwa wao ni bora kuliko vyama vingine, including NCCR, CUF, UDP n.k., na kujaribu kutumia maneno ya Mtikila kama kielelezo cha ubovu wa wanamageuzi wengine, ni jambo la kusikitisha sana na sidhani kama litavifikisha vyama vya upinzani mbali. Sitashangaa Chadema ikipoteza Tarime, kama vyama vingine navyo vikiamua kupingana nao huko. Mh. Daktari, mmekosea sana kuacha ushirikiano na wapinzani wengine, na kiburi chenu nafikiri kinawaingia vichwani hivi sasa na nafikiri unaelewa matokeo yake. Mungu ibariki Tanzania.
 
Daktari Slaa,
Naona kwa huu mtazamo wenu wa holier than thou, nafikiri mko hatarini kuanguka kwa kishindo kibaya. Vyama vikubwa na vya kugeresha vitakuwepo nchini TZ hata kama kutatungwa sheria ya kuvibana.

Lakini hiki kiburi cha CHADEMA cha kujiona kuwa wao ni bora kuliko vyama vingine, including NCCR, CUF, UDP n.k., na kujaribu kutumia maneno ya Mtikila kama kielelezo cha ubovu wa wanamageuzi wengine, ni jambo la kusikitisha sana na sidhani kama litavifikisha vyama vya upinzani mbali. Sitashangaa Chadema ikipoteza Tarime, kama vyama vingine navyo vikiamua kupingana nao huko. Mh. Daktari, mmekosea sana kuacha ushirikiano na wapinzani wengine, na kiburi chenu nafikiri kinawaingia vichwani hivi sasa na nafikiri unaelewa matokeo yake. Mungu ibariki Tanzania.
Kubwajinga,

Niliposoma maneno ya Dr. Slaa kwenye hili la vyama vingine, nimetikisa kichwa kwa masikitiko. Hayo maneno niliyasikia 1995 yakitoka kwa akina Marando. Leo hii CHADEMA wanaongea hivyo hivyo, kweli TZ hatujifunzi. CCM wataendelea kupeta kwa muda mrefu sana kama siasa zetu ni hizi za kutengana na kuambiana wengine wako kwenye payroll ya CCM, tusahau muungano wa vyama. Labda tuombee tu kuwe na wagombea huru.
 
Nina wasi wasi kwa hili Mtikila huenda anajichafua mwenyewe pia! Soon and very soon ataonekana hafai mbele ya macho ya jamii. Nimekuwa mtaani leo nikisikia gumzo kwa watu wa vijiweni kabisa na kwa haraka imeonyesha wengi wao kumstukia na kumuona hafai kabisa! By the way mimi ni mmoja wao ambaye nilikuwa nikimshabikia sana Rev. tangu enzi za gabachori, am sorry to say that as from now I count him off...

Mkuu Rwabugiri,
Allegations ni allegations mpaka zitakapokuwa proven otherwise. Kifo cha Wangwe kilikuja katika mazingira ya kutatanisha, kwa hiyo kwa Mtikila kuja na semi alizotoa bila ya CHADEMA au waliotajwa kumchukulia hatua, ina maana na wao wana wanayoogopa kuyaweka wazi kupitia mahakama au watueleze sababu za kumwacha Mtikila awapake matope. Otherwize kwa nini wasimchukuie Mtikila hatua za kisheria? Mtikila might be corrupt, but we need not to push aside his statements without thorough review.
 
Kuna umhimu wa kujua IQ ya Mchungaji C.Mtikila kwa sasa kutokana na mfululizo wa matukio ya ajabu ajabu anayo yadhusha.........tukisha jua tunaomba report ipelekwe MAELEZO ili litolewe onyo kwa vyombo vya habari visireport habari za Mtikila.......... huyu akili zake hazipo sawa sawa amewehuka si bure........
Na kile chama chake DP hivi kipo kweli???au wafuasi wake ni kondoo wake anao wahubilia neno la Mungu...
Naomba kujua na kanisa la Mtikila lipo wapi??
 
Kazi kubwa ya muhimili wa mahakama ni kuhakikisha kuwa haki ya kila mmoja inalindwa na hakuna yeyote, mmoja mmoja ama taasisis anaharibu na kuingilia haki ya mtu, kikundi ama taasisi. Hapa ni mahali ambapo mtu ama kikundi hakisafishwi bali hapa haki inatolewa na hii ni bila shinikizo(katika nchi zile zinazojali mgawanyo wa madaraka)

Mtikila anachofanya ni kile tunachoweza kuita, 'kufanya watu wa HABARI wamtafute na kumtangaza kwa sana. Uchunguzi umeshafanyika tena mara mbili kuhusu kifo cha Wangwe, sasa anaposema ushahidi atatoa hadi waje Scotland yard ni kauli yenye utata.


Wakati mwingine ni vizuri kukaa kimya kuliko kuongea na kuonesha kutoelewa kwako
 
Kubwajinga,

Niliposoma maneno ya Dr. Slaa kwenye hili la vyama vingine, nimetikisa kichwa kwa masikitiko. Hayo maneno niliyasikia 1995 yakitoka kwa akina Marando. Leo hii CHADEMA wanaongea hivyo hivyo, kweli TZ hatujifunzi. CCM wataendelea kupeta kwa muda mrefu sana kama siasa zetu ni hizi za kutengana na kuambiana wengine wako kwenye payroll ya CCM, tusahau muungano wa vyama. Labda tuombee tu kuwe na wagombea huru.

Mtanzania,
Nakubaliana kabisa na wewe kuwa hii picha tulishaiona hapo awali lakini inaelekea Chadema wao hawaikumbuki. Ndio shida ya hvi vyama vyetu, wanapoona wamepata umaarufu kidogo, badala ya kuutumia kupanua nguvu za wanamageuzi wengineo kwa ujumla, wanawageuka wenzao wakitegemea kuwa umaarufu wao pengine utawarusha mbele sana ya wengine. This is day dreaming kwani kila chama cha upinzani TZ kina maeneo yake, na muungano wao ndio tu silaha walionayo.
 
Kubwajinga,

Niliposoma maneno ya Dr. Slaa kwenye hili la vyama vingine, nimetikisa kichwa kwa masikitiko. Hayo maneno niliyasikia 1995 yakitoka kwa akina Marando. Leo hii CHADEMA wanaongea hivyo hivyo, kweli TZ hatujifunzi. CCM wataendelea kupeta kwa muda mrefu sana kama siasa zetu ni hizi za kutengana na kuambiana wengine wako kwenye payroll ya CCM, tusahau muungano wa vyama. Labda tuombee tu kuwe na wagombea huru.



Unajua tatizo la siasa za Hapa Tanzania ni NJAA wewe fikiria mtu ananunuliwa kwa milioni 3 duh!!!! si mchezo nafikiri anaweza kununuliwa hata kwa mafuta ya kujazia gari lake ile.........Benz ya long....
 
Mkuu Rwabugiri,
Allegations ni allegations mpaka zitakapokuwa proven otherwise. Kifo cha Wangwe kilikuja katika mazingira ya kutatanisha, kwa hiyo kwa Mtikila kuja na semi alizotoa bila ya CHADEMA au waliotajwa kumchukulia hatua, ina maana na wao wana wanayoogopa kuyaweka wazi kupitia mahakama au watueleze sababu za kumwacha Mtikila awapake matope. Otherwize kwa nini wasimchukuie Mtikila hatua za kisheria? Mtikila might be corrupt, but we need not to push aside his statements without thorough review.

Mkuu Kubwa.. nimekupata, ila naomba nikuulize swali kupitia mfano huu,

Hivi ukiwa upo bwawani unaogelea umeweka nguo zako pembeni akaja chizi mmoja akazikwapua akaanza kimbia nazo utafanya nini? je utatoka uchi uanze mfukuza ukiita chizi chizi? na je umati utakao kutana nao kati yako wewe na yule chizi nani ataonekana chizi?

Wakati mwingine ni busara zaidi kutofukuzana na kichaa kwani waweza onekana wewe ndo kichaa kwa kumfukuza kichaa!

Just count Rev. off!
 
Kifo cha Wangwe si uamuzi ulishatolewa kuwa ilikuwa ni ajali, hakukuwa na risasi, na haikuwa mauaji. Na kijana Mallya anashtakiwa kwa kuendesha gari kwa mwendo wa kasi na kusababisha kifo cha Mbunge huyo? Wengine tulipozua maswali ambayo ukiangalia utaona kuwa haiitaji uchunguzi kuweza kuibuka na hoja alizotoa Mtikila (tafuta makala yangu niliyouliza maswali kuhusu kifo cha Wangwe). Leo hii anasimama kutaka Scotland Yard waje, wakati wengine tulifanya hivyo kabla hata mwili haujazikwa?

Serikali imesema and that settles it, ama?
 
Kifo cha Wangwe si uamuzi ulishatolewa kuwa ilikuwa ni ajali, hakukuwa na risasi, na haikuwa mauaji. Na kijana Mallya anashtakiwa kwa kuendesha gari kwa mwendo wa kasi na kusababisha kifo cha Mbunge huyo? Wengine tulipozua maswali ambayo ukiangalia utaona kuwa haiitaji uchunguzi kuweza kuibuka na hoja alizotoa Mtikila (tafuta makala yangu niliyouliza maswali kuhusu kifo cha Wangwe). Leo hii anasimama kutaka Scotland Yard waje, wakati wengine tulifanya hivyo kabla hata mwili haujazikwa?

Serikali imesema and that settles it, ama?

I was the first one to call for an independent investigation by the Scotland Yard......call it a fluke or whatever, but I did it first........yeeeepaaaaaa.....
 
Mkuu Kubwa.. nimekupata, ila naomba nikuulize swali kupitia mfano huu,

Hivi ukiwa upo bwawani unaogelea umeweka nguo zako pembeni akaja chizi mmoja akazikwapua akaanza kimbia nazo utafanya nini? je utatoka uchi uanze mfukuza ukiita chizi chizi? na je umati utakao kutana nao kati yako wewe na yule chizi nani ataonekana chizi?

Wakati mwingine ni busara zaidi kutofukuzana na kichaa kwani waweza onekana wewe ndo kichaa kwa kumfukuza kichaa!

Just count Rev. off!

Mkuu Rwabu,
Mfano wako ni mzuri ila ungeufanya kuwa yule aanayeogelea awe amevaa angalau bukta, maana sidhani kuwa Chadema wana lolote wanalotaka kuficha kuhusiana na kifo cha Wangwe (yaani hawako uchi). Kwa hiyo kama wamevaa bukta, hawawezi kushindwa kutoka majini na kumkimbiza au hata kumpa kipigo yule chizi.

Kulingana na Mtikila, Dr. Slaa ni mmoja wa watuhumiwa, kwa hiyo kuja kwake mtandaoni na ku-spin hoja ya Mtikila bila kupinga aliyosema ni sawa na kukubaliana na mashambulizi ya Mtikila. Alitakiwa atuambie hatua atakazochukua kumuadhibu Mtikila na sio kuzua lingine la Makamba-50 bila kutupa ushahidi.
 
Mkuu Rwabu,
Mfano wako ni mzuri ila ungeufanya kuwa yule aanayeogelea awe amevaa angalau bukta, maana sidhani kuwa Chadema wana lolote wanalotaka kuficha kuhusiana na kifo cha Wangwe (yaani hawako uchi). Kwa hiyo kama wamevaa bukta, hawawezi kushindwa kutoka majini na kumkimbiza au hata kumpa kipigo yule chizi.

Kulingana na Mtikila, Dr. Slaa ni mmoja wa watuhumiwa, kwa hiyo kuja kwake mtandaoni na ku-spin hoja ya Mtikila bila kupinga aliyosema ni sawa na kukubaliana na mashambulizi ya Mtikila. Alitakiwa atuambie hatua atakazochukua kumuadhibu Mtikila na sio kuzua lingine la Makamba-50 bila kutupa ushahidi.

Perhaps unahitaji kumpa muda zaidi hawezi kukulupuka na kusema tutakwenda mahakamani bila kuwasiliana na wenzake, inawezekana pampja na kuongea hapa vilevile watachukua hatua za kisheria maana kama amewataja ana ushaidi wa kutosha maana anajua nini kitaendelea juu yake na wao wanajua kuwa hawausiki na hawaogopi kwenda mahakamani, otherwise watu wanataka kujua ukweli kama kweli mtikila anahitaji scotland yard basi waitwe waje watafute ukweli badala ya kutumia kifo cha mwenzetu kwa kujinufaisha kisiasa.

Mimi binafsi simwamini mch. Mtikila kwa kuwa siku zote najua kuwa kichwa chake hakiko sawa na anatumiwa na CCM sana. lakini kwa hili nafikiri ni wakati mzuri wa kutafuta ukweli huko wapi, kwani ninachokiona mimi kuna dalili sio CHADEMA tu bali kuna mkono wa watu wengine na ndo maana police hawataki kumbana mallya aseme ukweli.
 
Mchungaji wa Bwana.
huyu ni mwongo sana kama ni kweli alipaswa kuleta ushaidi wake . hata hivyo polisi washatamka kwamba kama kuna mtu yeyote mwenye ushaidi apoleke yeye alikuwa wapi! au kwa sababu kesi yake dhidi ya rais imefutwa!!!

NADHANI JINAMIZI LA ROSTAM BADO LINAMWANDAMA
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom