Kifo cha Mhe. Chacha Wangwe na uchunguzi wake

Kifo cha Mhe. Chacha Wangwe na uchunguzi wake

Status
Not open for further replies.
Aisee BongoTZ ambae kashikilia suala la mapanga kuwepo au kutokuwepo ni Zito Kabwe. Yaani safari hii wanaogopa na wameona kifo cha Chacha Wangwe kimewaharibia kisiasa. Angalia hata Dr Slaa hasikiki ilhali alikuwa huko na alionekana kwenye TV amejaa hofu na woga wa kucharazwa mapnga na waombolezaji. Lakini kwa kuwa yeye ni bingwa wa kuhonga waandishi wa magazeti hakuna ambacho wamekiandika juu yake. Sisi tuliohudhuria tunajua Slaa na Mbowe mzimu wa Chacha Wangwe utaendelea kuwasuta. Hamkuuona unafiki wao baada ya kifo chake. Ni kama wiki 3 zilizopita walimfukuza umakamu wenyekiti. Leo yule dogo Mnyika ambaye Slaa kuijanja kaona eti awe Kaimu Katibu Mkuu, ndiyo anasema Chacha alikuwa Vice Chairman wao na blah blah. Kweli unafiki huo ulinitia kichefuchefu. Hawana lolote. Wanafiki wakubwa. Wakae wakijua by election ijayo hicho kiti wamekipoteza. Ndiyo maana kama umesoma gazeti la Tanzania Daima jana utaona jitihada ya kumsafisha Mbowe. Naye huyo Datoo eti kaunda tume ya kuchunguza. Nothing but cheap propaganda.

Kabla ya kuendelea nilikuwa nahitaji kuhoji kitu kimoja maana kwa upande wangu naona kwamba tunajitahidi kupotosha habari tofauti na ukweli wenyewe ulivyo. Na inawezekana kwamba ikawa ndio what we were set to do.

Je Marehemu Chacha Wangwe alifukuzwa Umakamu Mwenyekiti ama alisimamishwa? Maana kwa sasa nashindwa kufahamu lipi lipo sawa? Na mtu unaposimamishwa ina maana umefukuzwa?
 
deus mallya................ you have a case to answer here.

Kwa nini mara ya kwanza ufiche kuwa sie ulokuwa unaendesha?
Kwa nini usiwe na leseni kama kweli wewe ni dereva mzuri tu?
Ulitokea wapi hata ukawa karibu na marehemu namna ile?
 
Nina maswali mengi ambayo ninashindwa kupata majibu. Mengi yanasemwa ambayo hayana majibu na ni magumu kuyatolea ushahidi.

Je kuna haja ya kufanya uchunguzi juu ya kifo cha Mheshimiwa Chacha Wangwe? Mimi binafsi sioni haja kwa sababu ushahidi ambao ungethibitisaha ukweli ni riport kutoka kwa Daktari lakini Daktari aliyefanya uchunguzi wa mwili pale Dodoma alikiri kifo cha Wangwe kilitokana na ajali, vivyo hivyo kwa daktari aliyeteuliwa na familia.

Vyama vya upinzani vimeshikilia jambo hilo kidedea kwamba Mallya ni jasusi. Sikatai ila ninchoweza kusema ni kwamba vyama hivyo vitapoteza muda na rasilimali nyingi kufuatilia jambo hilo. After all Chacha Wangwe will not come back.

So what is to be done.
 
Naona wakuu hapa walikuwa wanajiburudisha vinywa vyao baada ya shughuli nzito ya msiba.Ameniacha hoi Mbatia hapo....angalia Mrema anateremshia kabisa.
View attachment 1928
 
deus mallya................ you have a case to answer here.

Kwa nini mara ya kwanza ufiche kuwa sie ulokuwa unaendesha?
Kwa nini usiwe na leseni kama kweli wewe ni dereva mzuri tu?
Ulitokea wapi hata ukawa karibu na marehemu namna ile?

Does this amount to ujasusi?
 
mjadala huu umekaa kushoto.

Mwanakijiji na wengine wanaochangia msifanye watu mazezeta.

1 kama hawataonyesha hizo picha za rungu na sime; mtadai ziko wapi.

2. kama itaonekana picha yenye marungu sime na mapanga, mmetangulia na defence kuwa na utamaduni wao na wala sio kwa nia ya vurugu.

unapoanza na defence kabla ya utetezi, then there is no case to answer.



basi mchague moja kuwa,

picha ikipatikana, defence ya hiyo ni tamaduni yao haitakuwa pleaded; vinginevyo hamna haja ya kuendelea kudai picha hizo hali mnajua admissibility yake ni ndogo.
 
Mzee wa Gumzo naungana na maelezo yako,

Mzee wa Gumzo uliyosema si ya kudharau. Siwezi kusema kwa uwazi na kwa uhakika kwamba Deus Mally ni Jasusi kwani sijui sifa za jasusi. Na je vyama hivyo vya upinzani vitamshitaki mallya kama muuaji au jasusi?
 
Mzee wa Gumzo naungana na maelezo yako,

Mzee wa Gumzo uliyosema si ya kudharau. Siwezi kusema kwa uwazi na kwa uhakika kwamba Deus Mally ni Jasusi kwani sijui sifa za jasusi. Na je vyama hivyo vya upinzani vitamshitaki mallya kama muuaji au jasusi?
 
Polisi wanayo passport ya Bwana Mallya, kwa hiyo ninachoeleza ni kwa mujibu wa habari toka vyanzo vyao. Ni vyema Mbatia akahojiwa kwa kina aseme anachokifahamu cha ziada ili aisaidie polisi katika uchunguzi

PM

hata vile wamesema watakutana na IGP. acha upelelezi ufanyika, mnaopiga kelele mnaogopa nini? au mnajua mengi na uenda kwenye huu msafara mkaitwa kama mashaidi.

sasa kama police hawatafanya hiyo kazi unataka wafanye nini. walale tu ofisini. au wapinzani unataka wafanye nini, wakae ofisini. hata kama haikuumi, acha upelelezi ufanyike, haujui hii inaweza ikampata mtu umpendaye, au wewe pia.

USHABIKI WA VYAMA TUUWEKE CHINI KWANZA, HII SIO AGENDA YA CHAMA BALI YA TAIFA ZIMA
 
Aisee BongoTZ ambae kashikilia suala la mapanga kuwepo au kutokuwepo ni Zito Kabwe. Yaani safari hii wanaogopa na wameona kifo cha Chacha Wangwe kimewaharibia kisiasa. Angalia hata Dr Slaa hasikiki ilhali alikuwa huko na alionekana kwenye TV amejaa hofu na woga wa kucharazwa mapnga na waombolezaji. Lakini kwa kuwa yeye ni bingwa wa kuhonga waandishi wa magazeti hakuna ambacho wamekiandika juu yake. Sisi tuliohudhuria tunajua Slaa na Mbowe mzimu wa Chacha Wangwe utaendelea kuwasuta. Hamkuuona unafiki wao baada ya kifo chake. Ni kama wiki 3 zilizopita walimfukuza umakamu wenyekiti. Leo yule dogo Mnyika ambaye Slaa kuijanja kaona eti awe Kaimu Katibu Mkuu, ndiyo anasema Chacha alikuwa Vice Chairman wao na blah blah. Kweli unafiki huo ulinitia kichefuchefu. Hawana lolote. Wanafiki wakubwa. Wakae wakijua by election ijayo hicho kiti wamekipoteza. Ndiyo maana kama umesoma gazeti la Tanzania Daima jana utaona jitihada ya kumsafisha Mbowe. Naye huyo Datoo eti kaunda tume ya kuchunguza. Nothing but cheap propaganda.

Pole bwana mkubwa, unatiwa kichefuchefu na unafiki ambao haupo! Hivi ni wapi ambako wangwe ALIFUKUZWA Umakamu uenyekiti wa Chadema? Aidha wewe unaishi sayari nyingine, au mimi sipo duniani
 
Uchunguzi wa kina unahitajika. niliposikia kifo cha wangwe na kwamba kijana huyu amenusurika, nikajua lazima kuna mkono wa mtu. suala la ajali ni la kawaida, na hakuna mtu anayeweza kukwepa, hata kama dereva hana leseni. hizo ni traffick case ambazo zimejaa kila mahali. iweje yeye adai kwamba hajawahi kuendesha gari tangu avunjike mkono wakati akijifunza jijini nairobi 2004 wakati mtoto wa marehemu anashuhudia kwamba ndiye aliyekuwa akiendesha muda wote na akamuonya kwa mwendo kasi? alikuwa anajaribu kuficha nini? na iweje achomoe memory card ya simu yake na kuitupa? ilikuwa na nini? nadhani vyombo vya usalama vijaribu kutrace kwenye mitandao yote ya simu mawasiliano yote yaliyofanywa kwa simu za marehemu na huyo mallya. assumption sometimes leads to truth. alikutwa na vitambulisho vya ajabu ajabu, akakutwa na bastola, ndivyo tunavyoambiwa, ichunguzwe hiyo bastola pia ilikuwa ya nani au kama anaimiliki kihalali, kama ni kweli alikutwa nayo. kauli zake nazo zichunguzwe kwa makini, kwamba alikuwa nyuma, amelala, amesikia kishindo akajua magurudumu yamepasuka, alijuaye na alikuwa amelala hata kama amezinduka usingizini? anasema alipoteza fahamu, lakini anasema yeye ndiye aliyesaidia kuchukua simu za marehemu na pesa, na ndiye aliyepiga simu kwa spika, inawezekanaje kama alikuwa amepoteza fahamu? huyu jamaa kama ni jasusi, basi ni yule anayejifunza, maana hajui hata kudanganya.
 
pole Bwana Mkubwa, Unatiwa Kichefuchefu Na Unafiki Ambao Haupo! Hivi Ni Wapi Ambako Wangwe alifukuzwa Umakamu Uenyekiti Wa Chadema? Aidha Wewe Unaishi Sayari Nyingine, Au Mimi Sipo Duniani

Naomba Tofauti Ya kufukuzwa Na Kusimamishwa katika Siasa Bwaba Mkubwa


na kama unafiki anaokutia ahupo, kwanini unatiwa na kichefuchefu?
 
Lakini mbona watu wanaegemea zaidi kwenye hujuma za kisiasa kuliko kutafuta ukweli? hivi kwanini wasiangalie na upande wa pili wa shilingi; kwamba, C Wangwe kama binadamu alikuwa akifanya shughuli nyingine kwa manufaa yake, familia yake na jamii yake. I mean, alikuwa na shughuli za kipato. kwa nini huko nako kusitazamwe kwamapana na marefu kujua kama kulikuwa shwari ama la? haya mambo haya ya kuingiza siasa katika suala nyeti kama hili hayafai. ni sawa na wale wanaokwenda kwa waganga na kuambiwa aliyekuroga mama yako mzazi. ukitoka huko unamchukia kila mtu na hata unaweza kucommit mauaji. tuangalie uhusiano wa Mallya na marehemu kwa upande wa pili pia, kwa sababu tunaambiwa kwamba eti ni mfanyabiashara wa dar es Salaam. kuna ukweli gani?
 
Mapanga shahshahsha ni wana ngangari wenye ujumbe huo n ndio WaTanzania tunavyotakiwa tuwe tayari kama WaKenya mambo ya kuiba matokeo ya kura kwa manufaa ya mafisadi na walio karibu yao inabidi ,yafikishwe mwisho,hakuna cha kulaziana damu ,wagombea ubunge ni lazima watayarishe wapiga kura wao kama kule Pemba ,mtu siku ya uchaguzi anamsimami polisi na kumwambia fulani hawezi wala hana haki ya kupiga kura hapa na kama unarisasi zimalize kwenye kifua changu ,mtu wako apige kura wakati mimi nimekufa lakini nipo hai basi mamluki hapigi kura hapa.Huku mtu kamtolea mijicho polisi aliebeba SMG ambae anaona kweli imedhihiri na wapemba hao wakaondoka na viti vyao vya Ubunge na Uwakilishi.
Sasa kama mapanga yalikuwepo au hayakukuwepo ni ishara kwamba dalili za watu kusimama kidete kwa upande wa Tanganyika zimewasili ,hivi kama ni mkoa ni Pemba peke yake ndio wameweza kustand na kuiangusha CCM kwa nini na huku bara ambako mambo ya ufisadi yameshamiri mnashindwa kuiangusha CCM japo mkoa mmoja ? Inaonyesha kampeni za vyama vya Upinzani bado ni ndogo ,na ni ndogo sio kwa sababu vyama havina watu ,ni ndogo kuwashawishi watu kuweza kusimama kidete kwenye kulinda haki yao,ni kushindwa kuwashawishi watu nini na vipi wawe wakakamavu kupinga uonevu.
Mambo ya kunadi mafisadi bila ya kuwaelimisha watu ni vipi wawakatae mafisadi hayatasaidia kitu ,ni lazima mkakati wa kuwajenga wafuasi kuwa na ushujaa kuwatia ari na kuwapandisha mori wa kuwepo tayari kwa lolote kwani haki yao hawatiliwa ndani ya sahani au Mrema ,mbowe ,Lipumba wataweza kuilinda ni wao wananchi ndio waathirika wakubwa ni wao ambao ndio wataweza kulinda haki yao na si kiongozi anaepanda jukwaani kisha akahamia mkoa mwingine kwenda kufanya siasa.
Mapanga yalikuwepo haiwezekani watu wazunguluke mikono mitupu mji mzima huku wakiimba nyimbo za jadi....si ajaaali ni lisaaasi !
 
Wakurywa hata kwenye sherehe za kutahiri wanabeba mapanga bana..tena wanacheza wanayarusharusha....
Mbura tataa nakutema kirungu!!
Nimemiss lithungu! Sorry nime-divert ila mi mgonjwa wa lithungu lao, utafikiri nafuata mdundiko 🙂
 
you Know, Kitu Ambacho Watu Wanashindwa Kuelewa Ni Kwamba: Kwa Wakurya (esp. In Rural Areas) Kutembea Na Silaha Za Jadi Kama Rugu, Panga, Sime, Bakora Ni Kitu Cha Kawaida Kabisa. Ni Kitu Cha Kawaida Kwasababu Ya Nature Ya Maisha Yao (ufugaji/uwindaji/ukulima) Inayo Demand Wao Kutembea Na Silaha Hizo Za Jadi At Any Time. Kama Ilivyo Kwa Wazaramo Kushindia Vijiweni Na Vikombe Vya Kahawa Na Kashata (most Of The Time), Wakurya Nao Kutembea Na Paga/sime/rugu/bakora Muda Wote (walioko Vijijini Hususani) Is A Part Of Who They Are. So, Hata Kama Hayo Mapanga Yalikuwepo Msibani (na Hukuna Aliyeripotiwa Kujeruhiwa), Then Sioni Point Ya Kulishikia Bango Suala Hili. Besides, Wangwe Alikuwa Anapendwa Sana! So You Can See Kwanini Damu Za Watu/wakurya Zilikuwa Zina Boil-up Siku Ya Mazishi.
Ninawauliza Wakuu, Sokoine Alipokufa Kwa Ajali Wamasai Walikuwa Na Mapanga,mikuki Na Mawe?

Tusiogope Ukweli Pale Unapokabiliana Nao ,dawa Si Kuukwepa Nali Ni Kuukubali Na Kukabiliana Nao Kiustarabu Tu.
 
Wakurywa hata kwenye sherehe za kutahiri wanabeba mapanga bana..tena wanacheza wanayarusharusha....
Mbura tataa nakutema kirungu!!
Nimemiss lithungu! Sorry nime-divert ila mi mgonjwa wa lithungu lao, utafikiri nafuata mdundiko 🙂
Ndio hapo sasa ,halafu watu wanasema kama kulionekana upanga ,si mnataka kuwasaidia mafisadi tu .
 
Kama huyu kijana ndiye alikuwa anaendesha gari, hana leseni, na kwa mwendo kasi; kwanini ameshtakiwa kwa makosa ya kutokuwa na leseni na kuendesha gari kasi bila kushtakiwa kwa kosa la kusababisha kifo? Akili mukichwa. Tukubali tu ilikuwa ni ajali ya kawaida (kwamba mtu asiye ne leseni, anaenda kasi, anamuendesha Mbunge wa Bunge la Muungano - ni kawaida tu)?
 
Tatizo ni kutotaka kupokea ukweli, Zitto kasema hapakuwa na uvunjifu wa amani, kambi ya upinzani kama inavyojiita imekaa na wana wana habari na kusema kuwa hali ilikuwa mbaya hata wasira alikimbia sasa Mbowe kukimbizwa haiwezekani kwa lipi? kibaya zaidi wanaobishana, they all come from the same port! UPINZANI nadhani acha wabishane then watatupa majibu maana hata Zitto alipokuwa akiongea na waandishi ile kauli yake kuwa NCCR ilikufa miaka 10 iliyopita sidhani kama ni ya kisiasa zaidi kwa maana ya upinzani, maana hata bwana Mbatia sijui amepokea ujumbe ule kuwa NCCR ilikufa 10 ilopita kwa maana halisi hata yeye Mbatia hayupo Duniani kisiasa miaka 10 iliopita! binafisi nakubali kuwa hali ya mazishi haikuwa nzuri kwa maana ya usalama ukizingatia utamaduni wa wakulya ni kutembea na mapanga n.k kuwa kawaida yao kama msemaji alipita yawezekana Mbowe alikimbia kwa sababu si mazoea yake kwa mazingira kama hayo.
 
Moja ya maswali magumu ambayo sijapata kupambana nayo katika maisha ni pamoja na hili ambalo ndugu ameuliza nadhani tusubiri kidogo tutapata jibu muda si mrefu kwa kuwa kuna wanaosema kuwa wana ushadi kuwa Deus ni Jasusi !
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom