Salam wakuu.
Naomba kwanza kupandisha clip ya January Makamba akiwa Waziri wa Nishati na pia kuweka barua ya Ikulu ya teuzi.
Baada ya kumsikiliza January Makamba na kurejea barua ya Ikulu, je ni nani haswa alihusika na anahusika na hizi teuzi zinazotangazwa kutoka Ikulu?
Kwa sasa tumeona Maharage Chande kapelekwa TTCL, je huko amefanyiwa usaili na?
Alichoongea January, ni kudhihirisha kuwa mengi ya Tanesco Rais Samia hahusiki na wapo wanaohusika ama ndio kuwa huko kwenye teuzi mambo ni zigzag kila mtu na don wake na barua zinazotoka ni ceremonial tu za kiitifaki?
Updates:
Tarehe 25 September (siku 2 baada ya kuteuliwa) Maharage Chande amehamishiwa posta na kua PostaMasta.
NB- kuruka ruka kwa Maharage ndio kuiva kwake,Maharage yanaruka ruka mpaka yaive,mpishi wa maharagwe ndio anajua umuhimu wake baadala ya samaki ama nyama!!!