Kati ya Samaki hawa wapi watamu zaidi?

Kati ya Samaki hawa wapi watamu zaidi?

I had this same argument with my wife yesterday samaki wapi ni wazuri zaidi?

Waswahili wanapenda samaki na shombo lao - ukikutana na mzanzibar ukimpa sangara samaki ambao hawama shombo kali hawezi kuwaelewa

Raha ya samaki wa baharini ni lile shombo kali

Samaki wa maji baridi wamepoa sana, sangara na sato naona wamepoa kulingana na changu - changu hata umoaange vipi anateleza teleza tu

Napenda samaki ukimkausha anakauka kama tasi - Tasi anakauka vizuri sana

Samaki wa baharini ukanda wetu watamu zaidi coz wako kwenye chumvi mda mwingi - my opinion
 
Sio maji Moto, ni maji chumvi.

Samaki wa maji chumvi yaani wa baharini ndio wazuri na wanamadini na virutubisho vingi zaidi kuwashinda wa maji baridi (mtoni,ziwani na bwawani).

Hata ukija eneo la ladha,samaki wa baharini hawanaga mpinzani.

Hata ukitazama bei zao wa baharini katika soko la dunia wanakimbiza zaidi.
 
Wasalamu.Tumsifu Yesu Kristo.Wapo samaki wa maji moto yani Bahari na hawa maji baridi yani ziwani.
Ila kwa leo naomba kujua Kati ya Sangara,Sato na vibua na kambale ni kundi gani ni watamu zaidi?
Sato ni hbr nyingine acha kumfananisha na hizo shombo zingine, kwa mbaaaali sangara anafuatia
 
Wasalamu.Tumsifu Yesu Kristo.Wapo samaki wa maji moto yani Bahari na hawa maji baridi yani ziwani.
Ila kwa leo naomba kujua Kati ya Sangara,Sato na vibua na kambale ni kundi gani ni watamu zaidi?
Huyu kiumbe wa maji baridi hana mpinzani kwa UTAMU aisee........ Wakuitwa KAMONGO
1755694246441.jpg
 
Back
Top Bottom