Kati ya Samaki hawa wapi watamu zaidi?

Kati ya Samaki hawa wapi watamu zaidi?

Binafsi napenda samaki wanaoteleza km kamongo, kambale, hongwe nk
 
utamu wa samaki unategemea aina ya mapishi yake..

kuna samaki ukimkaanga ni mtamu zaidi ya kumchemsha au mwingine ukimpika mchuzi ni mtamu zaidi ya kumchoma..

take this
 
Kwa hiyo sangara anapikwaje ili awe mtamu zaidi ?
 
Hakuna
1. Sato
2. Sangara
3. Vibua nalia shida vikipikwa nyumbani au ugenini. ila kwangu hapana.
4. Kambale hata ugenini mkipika nitakataa kula bila wasiwasi. Samaki gani sasa yule 😒
Samaki watamu sana type ile, I mean kambale, mumi, ningu, nembe, na samaki flani hivi hua natafuta sana
 
Sangara
Sato
Jodari
Kitoga ni watamu sana
Ila kiboko yao ni CHANGU huyo ni mwisho wa matatizo.
 
Umekulia wap wewe? Kwa SISI TULIO kujaga dar es salaam Tanzania ukubwani nikimaanisha university ndio ilituleta dar.

First time dagaa, samakii maji chumbii na maji ya dar es salaam yalinishindaga now Nina miongo kadhaa hapa dar hivyo nime adapt ila mwanzo nilisumbukaga sanaa now nakula mpaka uduviiii
Ushawahi kula jodari au kingfish kaka?
Hao ndo samaki pekee Unakula Huku minofu yake unafunua Kama page za kitabu....hao samaki ni Hatari aisee
 
Watu wa bara mko wengi ila ukweli hao samaki wa huko kwenu ni kama vyura ,hamna mtamu

UKweli hao wa maji baridi sio watamu ,nimenunua sana hao Sangara na sato pale mwanza kama nakula sufi ,wamepooza sana.
 
Vinyama bahari...😂😂
Watu wa pwani kusifia sasa hayo mavitu yao.
Siku moja nimeenda ferry kigamboni nikaonja pweza wao.
Mmh! Overrated, hamna chochote.
Yaani wanakulakula ovyo tu mkuu,🤣🤣🤣🤣🤣
 
Back
Top Bottom