Kampeni ya kuikataa Vodacom

Kampeni ya kuikataa Vodacom

halafu mpaka wasomi kabisa na akili zao, eti....wanaacha kutumia VODA!!! wakati ni mitambo ya TCRA na makampuni yote wanafanya hivyo

Hapo kwenye mitambo ya TCRA sijakuelewa unamaanisha nini. Ujumbe upi ulitaka kuufikisha? TCRA wana mtambo upi huo?
 
Vodacom wamevimbiwa pesa zetu wanazo tulangua ktk huduma zao uchwara wameona haitoshi wanashirikiana Majini, mashetani na vibaraka wote wa uovu kumwaga Damu za wa Tanzania. Vodacom ikataliwe na kilapenda Haki, amani na umoja hapa nchini? Voda ni janga la kitaifa?
 
Mkuu hapo kwenye nyumbu namaanisha wabongo wengi wasahaulifu,
Vodacom wakitoa ofa mfululizo kama 2 au 3 hivi watarudi tu wapenda dezo,ila wachache watakomaa
 
Kweli hawawezi kukataa, fikiria sakala lile la vigogo wakuu wa Voda kuswekwa ndani kwa Uhujumu uchumi, je wangekataa vipi?
Ila mi binafsi nilishaachana nao mwaka 2014 baada ya kukaa nao miaka miaka saba. Walisepa na vijisenti vyangu nikaachana nao mpaka leo naona maisha yanaendelea kwingineko
 
Ona huu ujinga yani umeshabebwa na mazwazwa ya kisiasa tayari?

Wewe una siri gani Mpaka voda wahangaike kuliweka hadharani?

Pumbavu kabisa! Basi usitumie simu kabisa, maana kama una baya lolote utapatikana tu.

Mm siwezi kuhangaika eti nisuse mtandao kisa huo ujinga wenu wa siasa. Hivi kwa akili yako unafikiri kuna mtu anahangaika na kufuatilia kutongazana kwako kila siku na kina mwajuma.?
Chochote nisichokusudia kisikiwe na MTU asiyetarajiwa nami ni siri yangu bila kujali mtazamo wako ndugu
 
Mitandao yote ipo chini ya TCRA na sheria ya mawasiliano ,sasa mtahamia mtandao gani ambao TCRA na sheria hazifanyi kazi!?
 
Hadi sasa mzee anapata taabu sana kutawala analazimika kudukua kuteka kupiga risasi kuua kufanya chochote kwa hata anayetoa mawazo guru kikatiba lakini hola he akikaa miaka 10 ataua wangapi?
Kuhoji uraia, kupiga marufuku mikutano halali ya kisiasa.

Nchi inaendeshwa kwa uhuni wa kishamba sana.
 
Wanachofanya Voda sasa hivi ni ku Troll, wanapost mada nyingi za kujitetea kwa kutumia account za watu wao mbalimbali. Ishakula kwenu tayari Vodacom will never b the same again Kuajiri trolls kutetea ujinga wenu haitowaokoa. Solution mliyokuwa nayo ni moja tu, mshushe bei ya vifurushi vyenu kuwavutia wateja na hii inamaanisha mtapoteza faida na hapa tunarudi kulekule Vodacom will never b the same again
Wabongo wameamua kususia kweli? Au stories za Twitter tu?
 
Watanzania tusiwe na akili nyepesi kiasi hichi, Vodacom wamejipambanua jinsi wanavyolazimishwa kutoa siri za wateja wao, kosa lao kubwa sana ni kukubali kutoa mawasiliano kinyume na sheria ya nchi. Lakini je, mnajua mitandao ambayo haijatoa taarifa kama vile TIGO,ZANTEL,HALOTEL na AIRTEL ambao serikali ina hisa nyingi ina matatizo kiasi gani?

Tunapoulaumu mtandao ambao umekua huru kueleza masahibu unayopitia, kumbukeni kua kuna mitandao ambayo haijasema kitu. Kwa ujumla kupitia mazingira haya ya Vodacom ni lazima tuwe na hofu mitandao yote iliyopo nchini.
Kama wanajua sheria zinakataza kwa nini wakubali kutoa siri za watu,kwani wao hawawezi kutumia sheria zilizopo,huoni utetezi rahisi kabisa,kama kuna mitandao mingine itabainika nayo tutaipigia kelele kama Vodacom.
 
Kwa kuwa vodacom wameamua kutumia tabaka dhalimu la watawala badala ya kufanya biashara...

Na kwa kuwa vodacom wameamua kuwa sehemu ya mhimili huo wa uovu...

Na kwa kuwa sasa ni dhahiri wanashiriki kusaidia raia wema kufuatiliwa mawasiliano yao na kufanyiwa uhalifu na vyombo dhalimu vya dola...

Nimeamua kuungana na watanzania wazalendo walioamua kususia bidhaa za vodacom na hivi natangaza rasmi kuivunja vipande na kuichoma moto line yangu ya Vodacom ambayo nimekuwa nikiitumia tangu mwaka 2002.

Nimewaachia salio la Shilingi 0.56 kwenye akaunti yangu ya m'pesa...wale wafaidi.

May the unscrupulous and evil dogs of Vodacom go to hell and burn among the rocks!

Shubaaamit!
Safi sana..
 
Badala ya kuwachukia wabunge waliopitisha sheria, mnawachukia Voda wanaotii sheria zilizotungwa na bunge lenu ajabu...
 
Watanzania tusiwe na akili nyepesi kiasi hichi, Vodacom wamejipambanua jinsi wanavyolazimishwa kutoa siri za wateja wao, kosa lao kubwa sana ni kukubali kutoa mawasiliano kinyume na sheria ya nchi. Lakini je, mnajua mitandao ambayo haijatoa taarifa kama vile TIGO,ZANTEL,HALOTEL na AIRTEL ambao serikali ina hisa nyingi ina matatizo kiasi gani?

Tunapoulaumu mtandao ambao umekua huru kueleza masahibu unayopitia, kumbukeni kua kuna mitandao ambayo haijasema kitu. Kwa ujumla kupitia mazingira haya ya Vodacom ni lazima tuwe na hofu mitandao yote iliyopo nchini.
Voda wameshajipambanua tayari, hayo makampuni mengine wakifanya hivyo, tutajua namna ya kupambana nao.

Vv
 
Back
Top Bottom