Kampeni ya kuikataa Vodacom

Kampeni ya kuikataa Vodacom

Unahis tigo ,airtel ,halotel hakuwez ingilika mkuu,..ni vile tuu watumiaj walikua voda...kokote kambi,wazeiya wanaingia kokote kule wakitaka....kama mnahatarisha usalama wa nchi wafanyeje sasa
sheria kwani inataka kuachiwa kwa clips za maongezi za watu waliodukuliwa?,Vipi kuna kesi mahakamani baada ya kudukua hao wanaohatarisha usalama wa nchi?
 
Kwa kampuni kubwa kama Vodacom haya ni mapito tu,,wabongo wengi akili za nyumbu,
 
Kwa kampuni kubwa kama Vodacom haya ni mapito tu,,wabongo wengi akili za nyumbu,
Nyumbu ni wale wanaotetea matendo ya kishetani ya mfalme kama vipofu na viziwi ila hali wana macho na masikio.
 
Wana siasa tuu ndio wanaweza kuhama.. ila mazungumzo yangu wanaruhusiwa kuyadukua kila siku.. sija kitu cha siri wala situkani mtu..

Tena wakidukua waniletee maana nataka nihifadhi mazungumzo yangu yote ya simu.
 
Ni wazi kampuni ya simu ya VODACOM inapitia kipindi kigumu na hii ni kutokana na tuhuma za kuruhusu mamlaka za nchi kudukua mawasiliano ya wateja wake.... Hili ni jambo baya na itawachukua muda kidogo mpaka kuja kukaa sawa tena.... Si kwamba watatetereka sana la hasha ila watu wengi watahoji umahiri na weledi wao kwenye kuhifadhi taarifa za wateja wao!

Kuna outrage kubwa kutoka kwa watu mbali mbali hasa viongozi wa kisiasa na watu wengine wa kaliba mbali mbali wakihamasisha watu waususie huu mtandao... Baadhi ya watu ni prominent figures ambao wana wafuasi wengi hivyo wanaisulubu VODACOM watakavyo....

Swali la kujiuliza.. Kwanini kadukuliwa Voda na si mitandao mingine....
Jibu ni kwamba si kwamba mitandao mingine ina kikubwa cha ziada na haiwezi kudukuliwa...
Kilichowaponza VODACOM ni uimara wa mtandao wake, huduma bora (mapungufu yapo) na kuweza kuhimili soko muda mrefu bila kuyumba wala kubadilibadili jina la biashara zaidi ya kubadili rangi na logo zake
Uimara wa vodacome na uhakika wa huduma zake.. Umevutia watu wengi prominent wakiwamo viongozi wa kaliba zote, watu maarufu na watu wa kawaida pia
Sinema za udukuzi zinazoendelea wateja wake wengi ni wa vodacome lakini si kwamba mitandao mingine haidukuliwi wala haidukuliki....
Tunaweza kufuata panic ya wanasiasa na kuususia mtandao wa vodacome... Lakini ni vema kumakinika ili usije ukajikuta unaruka mkojo na kukanyaga kinyesi.... Si vema kufuata mkumbo.. Hakuna mtandao ambao haidukuliki Tanzania....! Tusidanganyane kabisa... Maadui wa Voda na wenye chuki binafsi na huu mtandao wasikubebe kwenye mkumbo usiojua.... Ukitaka usidukuliwe tumia satellite mobile phones kama thuraya nk

Nitabaki VODACOM bado sijaona mbadala wake.... Huu ni upepo mchafu tu utapita... Mawasiliano yetu bado yataendelea kulindwa kwa kadiri inavyowezekana... Tunailaumu VODACOM lakini kamwe hatujariribu kujiuliza kama tungekuwa sisi kwenye nafasi yao tungefanyaje...

VODACOM client since 2000
 


Hii hapa chini ni tweet ya Mbunge Halima Mdee ikiwa ni miongoni mwa tweets nyingi za watu maarufu wanaokusudia kuacha kutumia mtandao wa Vodacom:

Nimekuwa Mteja wa VODACOM kwa MIAKA zaidi miaka 10!! Najua nitaathirika kimawasiliano pale nitakapo SITISHA matumizi ya NAMBA yangu!! Lakini kwa HAYA yanayoendelea, NIKO TAYARI KUJIONDOA VODACOM!!!Tususie BIDHAA za WAKANDAMIZAJI!!!
Kachero m-bobezi alisema hivi.....
Kwa haya yanayo ruhusiwa na mitandao ya simu kutowa faragha za mawasiliano ya wateja wake, hata asipo enda mahakamani lakini hili litawaathiri sana kibiashara.
 
kama ni utoto , akili yako imepitiliza. Huwezi kuikimbia sheria hata uende wapi, ukitaka kuikimbia sheria jitahidi uitii na kuiheshimu.

Mbona uzi uko wazi tu kuwa hataki kutumia voda kwa sababu voda wamekiuka maadali, sasa wewe ishu ya kukimbia sheria umeitoa wapi?
 
 
 
Watanzania tusiwe na akili nyepesi kiasi hichi, Vodacom wamejipambanua jinsi wanavyolazimishwa kutoa siri za wateja wao, kosa lao kubwa sana ni kukubali kutoa mawasiliano kinyume na sheria ya nchi. Lakini je, mnajua mitandao ambayo haijatoa taarifa kama vile TIGO,ZANTEL,HALOTEL na AIRTEL ambao serikali ina hisa nyingi ina matatizo kiasi gani?

Tunapoulaumu mtandao ambao umekua huru kueleza masahibu unayopitia, kumbukeni kua kuna mitandao ambayo haijasema kitu. Kwa ujumla kupitia mazingira haya ya Vodacom ni lazima tuwe na hofu mitandao yote iliyopo nchini.
 
Back
Top Bottom