Kampeni ya kuikataa Vodacom

Kampeni ya kuikataa Vodacom

moja kati ya makampuni yaliokuwa na jeuri sana na masoko yao ni HUAWEI, ona sasa kilichotokea, Consumers ni consumers chembe moja tu ya mchanga inaweza kuleta madhara makubwa katika uhalisia wa biashara, Makampuni yanahitaji sana wateja kuliko wateja wananavyohitaji makampuni. Mgomo huu ni mzuri kwa upande mmoja maana yatayafanya makampuni yasibweteke na sasa wataamua kufanya biashara na wananchi ama kujikita kwenye kuvujisha taarifa zao. Tunataka kampuni za simu zilizo strong zenye kulinda faragha ya wateja wake. Ni sawa na gesti ama hoteli, fumanizi zikizidi wateja wanakimbia, Law of motion. Nasema wananchi wamechelewa sana kuanzisha mgomo huu. Marekani ukihitaji kudukua kwanza unaenda mahakamani kutafuta kibali na si jambo la rahisi hata kidogo. Na sisi tufike huko maana tunawatengenezea hawa jamaa faida kubwa sana kwa nini wasitulinde
 
Kuna umuhimu wa kutoa elimu juu ya somo la udukuzi hapa JF..
Siyo Kila Mtu Anadukuliwa, Jambo Hilo Hufanyika Maalum Pia Watu Hawajui Nini Maana Ya Kuyaweka Makampuni Sambamba.
Yaani Airtel, Vodacom, Halotel, Tigo
 
Bakini na milaini yenu ya voda ila wenye akili timamu kama sisi hatuwezi kuendelea kuvumilia upuuzi wa wapuuzi.. Kwanza wamewahi kunizima 30000 kwenye mpesa mpaka leo kimya.
malisa_gj-20190731-0001.jpeg
 
Watanzania tusiwe na akili nyepesi kiasi hichi, Vodacom wamejipambanua jinsi wanavyolazimishwa kutoa siri za wateja wao, kosa lao kubwa sana ni kukubali kutoa mawasiliano kinyume na sheria ya nchi. Lakini je, mnajua mitandao ambayo haijatoa taarifa kama vile TIGO,ZANTEL,HALOTEL na AIRTEL ambao serikali ina hisa nyingi ina matatizo kiasi gani?

Tunapoulaumu mtandao ambao umekua huru kueleza masahibu unayopitia, kumbukeni kua kuna mitandao ambayo haijasema kitu. Kwa ujumla kupitia mazingira haya ya Vodacom ni lazima tuwe na hofu mitandao yote iliyopo nchini.
halafu mpaka wasomi kabisa na akili zao, eti....wanaacha kutumia VODA!!! wakati ni mitambo ya TCRA na makampuni yote wanafanya hivyo
 
Kama una mambo ya hovyo lazima utadukuliwa hata tutumie mtandao gani!Sihami Voda ng'o...
 
Habari zenu wana wa nchi na poleni kwa majukumu mbali mbali ya ujenzi wa taifa.
Baada ya tafakuli ya kina juu ya tukio la kukamatwa Mwandishi Erick Kabendera jana na Kufungiwa huduma ya mawasiliano ya simu yake na Vodacom nimeoma kuna mambo kadhaa yana tia simanzi sana juu ya Usalama wa raia yeyote kwa sasa hapa nchini.

Mwandishi Erick Kabendera anasema alipoona Mawasiliano yake yamefungwa aliwapigia vodacom na kuwauliza kulikoni? Vodacom wakamjibu kuwa wameagizwa na TCRA wafunge mawasiliano yake. Lakini baadae TCRA ambao ndio wenye jukumu la usimamizi wa Mawasiliano wakakanusha kuwa hawahusiki na tukio hilo na wala sio kazi yao kufungia watu mawasiliano.

Majibu ya TCRA yanatupa maswali magumu juu ya Mtandao wa Vodacom kama ifuatavyo.

1. Kwa nini Vodacom wanawaficha wahusika halisi waliotoa amri ambayo kama waliona ni halali?
2. Lengo halisi la kufunga mawasiliano ya mwandishi ni nini? Ili akitekwa asipatikane hewani na kuwasiliana na ndugu zake?

3. Kama mtuhumiwa anatafutwa na chombo cha usalama SIMU yake ikiwa hewani husaidia chombo cha usalama kujua mahali alipo na kumkamata kirahisi. Sasa Hawa Vodacom kumzimia Simu mtuhumiwa anaye tafutwa wana LENGO gani?

4.Makosa anayotuhumiwa Kabendera hayahusiani na mambo ya Mawasiliano kwa nini Vodacom wamfungie huduma mteja wao ambaye amelipia huduma?

Maswali haya yanatuonesha Vodacom sio Mtandao salama tena kwetu watanzania. Unashirikiana na wahalifu, watekaji, wauaji, na watesaji hapa mchini.

Pili Vodacom wameonesha dharau kubwa sana kwetu watanzania. Kama wanaweza kukufungia Mawasiliano mtu ambaye huna hatia ili udhurike na watekaji watashindwa kuvujisha habari zako?

Je, Pesa zetu tunazo ziweka huko M.PE.SA ni salama tena? Huwezi amka ukaambiwa akaunti yako imefungwa na pesa zako zimechukuliwa kwa maagizo toka juu?

Kitendo hiki hakipaswi kufurahiwa. Vodacom wanapaswa kuchukuliwa hatua na sisi wenyewe wananchi ili kulinda usalama wetu na kuwaonesha kuwa tumefedheheshwa sana na tukio hili.

Hatua za kuchukua ni hizi wana bodi.
1. Kuacha kutumia mtandao wa Vodacom na mitandao mingine kama hiyo inayo shirikiana na waharifu kutesa raia wema.

Vodacom wamejidhihirisha pasi na shaka kuwa ni hatari kwa usalama wetu hima hima tuchukue hatua haraka.
Asanteni.


unawaonea voda

wamepewa amrri na TCRA, na mkataba wao na leseni yao ilisema kabisa serikali ikihitaji chochote kutoka kwao watatoa

HII SIO KWA VODA TU NI MAKAMPUNI YOTE YA SIMU, kuna wakati tumieni akili zenu ngau kidogo tu
 
Siku wakitoa siri zangu nitaacha kuitumia ila kwa sasa sina sababu ya kuacha.
 
Ni wazi kampuni ya simu ya VODACOM inapitia kipindi kigumu na hii ni kutokana na tuhuma za kuruhusu mamlaka za nchi kudukua mawasiliano ya wateja wake.... Hili ni jambo baya na itawachukua muda kidogo mpaka kuja kukaa sawa tena.... Si kwamba watatetereka sana la hasha ila watu wengi watahoji umahiri na weledi wao kwenye kuhifadhi taarifa za wateja wao!

Kuna outrage kubwa kutoka kwa watu mbali mbali hasa viongozi wa kisiasa na watu wengine wa kaliba mbali mbali wakihamasisha watu waususie huu mtandao... Baadhi ya watu ni prominent figures ambao wana wafuasi wengi hivyo wanaisulubu VODACOM watakavyo....

Swali la kujiuliza.. Kwanini kadukuliwa Voda na si mitandao mingine....
Jibu ni kwamba si kwamba mitandao mingine ina kikubwa cha ziada na haiwezi kudukuliwa...
Kilichowaponza VODACOM ni uimara wa mtandao wake, huduma bora (mapungufu yapo) na kuweza kuhimili soko muda mrefu bila kuyumba wala kubadilibadili jina la biashara zaidi ya kubadili rangi na logo zake
Uimara wa vodacome na uhakika wa huduma zake.. Umevutia watu wengi prominent wakiwamo viongozi wa kaliba zote, watu maarufu na watu wa kawaida pia
Sinema za udukuzi zinazoendelea wateja wake wengi ni wa vodacome lakini si kwamba mitandao mingine haidukuliwi wala haidukuliki....
Tunaweza kufuata panic ya wanasiasa na kuususia mtandao wa vodacome... Lakini ni vema kumakinika ili usije ukajikuta unaruka mkojo na kukanyaga kinyesi.... Si vema kufuata mkumbo.. Hakuna mtandao ambao haidukuliki Tanzania....! Tusidanganyane kabisa... Maadui wa Voda na wenye chuki binafsi na huu mtandao wasikubebe kwenye mkumbo usiojua.... Ukitaka usidukuliwe tumia satellite mobile phones kama thuraya nk

Nitabaki VODACOM bado sijaona mbadala wake.... Huu ni upepo mchafu tu utapita... Mawasiliano yetu bado yataendelea kulindwa kwa kadiri inavyowezekana... Tunailaumu VODACOM lakini kamwe hatujariribu kujiuliza kama tungekuwa sisi kwenye nafasi yao tungefanyaje...

VODACOM client since 2000
tunahama kama huwezi hama wewe baki ili kuonyesha nguvu ya uma tunahama voda
 
Mi nawaomba kwa umoja kabisa tuanze kampeni hii ya kukataa kutumia vodacom labda akili itawarejea, haiwezekani sisi kama wateja siri zetu zinatolewa pasipo ruhusa ya mteja na kama haitoshi unafungiwa kupiga simu pasipo kutaarifiwa na kubwa zaidi tabia yao ya kupunguza vifurushi. Tuseme sasa inatosha voda wameota mapembe wakati sisi ndo tumewafikisha hapo.
# TuikataeVoda
# HawatufaiVoda
hashtag boycottvodacom
 
Kwa kuwa vodacom wameamua kutumia tabaka dhalimu la watawala badala ya kufanya biashara...

Na kwa kuwa vodacom wameamua kuwa sehemu ya mhimili huo wa uovu...

Na kwa kuwa sasa ni dhahiri wanashiriki kusaidia raia wema kufuatiliwa mawasiliano yao na kufanyiwa uhalifu na vyombo dhalimu vya dola...

Nimeamua kuungana na watanzania wazalendo walioamua kususia bidhaa za vodacom na hivi natangaza rasmi kuivunja vipande na kuichoma moto line yangu ya Vodacom ambayo nimekuwa nikiitumia tangu mwaka 2002.

Nimewaachia salio la Shilingi 0.56 kwenye akaunti yangu ya m'pesa...wale wafaidi.

May the unscrupulous and evil dogs of Vodacom go to hell and burn among the rocks!

Shubaaamit!

umefanya hayo kwa sababu ya ujinga

kampuni gani hawatoi mawasiliano wakiamriwa na TCRA, wakiamriwa na serikali??

umejipa hasara na umefuata mkumbo

makampuni yote wanafanya hivyo na sio kosa lao Voda

hivi wasomi mnawaza nini siku hizi??
 
Siyo siri kua serikali karibia zote zinamonitor mawasiliano ya watu wake.

Wakati mwingine hata serikali ya nchi C humonitor mawasiliano ya nchi A.

AU ilikua ikiibwa taarifa zake na serikali ya China. Sijawahi kusikia nchi yeyote imeishtaki China. Na China wamefuatilia hizo taarifa illegally.

Vifaa vya Huawei inasemekana vinakusanya data mbalimbali bila wewe kujua na kuzipeleka kwa serikali ya China. USA imezuia maofisa wake wa serikali kutotumia bidhaa za Huawei. Hapa Tz sijaona katazo.

Vitu serious kama hivyo ambavyo vimefanywa illegally siyo Halima wala mtu yeyote Tz ambaye amevisemea. Voda imetenda kwa kufuata matakwa ya serikali, JF ilipishana na serikali na tunajua ilikua off air kwa muda gani.

Same shit happening to Voda ingekua na hasara kuliko watu wachache kuhimizana kuiacha Voda.

Mtu mwingine atanipa mfano wa Apple kugoma kutoa password ya Iphone 5 ya yule gaidi. Lakini naomba ajiulize Apple wanaoperate nchi ya namna gani na Voda wako nchi ya namna gani.
 
Back
Top Bottom