mangikule
JF-Expert Member
- Jun 11, 2012
- 6,054
- 5,432
Kumbe ukiona haya mamtu yenye sura mbaya yamekimbilia upolisi yameenda kutimiza azma yao ya ubaya na ujambazi bwana eeh!!. Muwe makini ndugu zangu kila kitu kimeshaharibika, ukikutana na haya majambazi pasipo na mtu porini kimbia kama una usafiri. Nimeshashuhudia uporaji unaofanywa usiku wakiwa wenyewe au wakiazima silaha majambazi.Last I checked, Kamuhanda kasema anakaribia kustaafu na pia amepokea maagizo toka ngazi fulani za juu kuwathibiti CHADEMA (read at all costs).
Elimu sifuri, maadili sifuri hao ndio polisi wa Tanzania. Hasara wanazosababisha tunaziona na kupata machungu sana. Kikwete akitaka kujua anavyodharaulika si tu na wananchi abali hata na watendaji wake athubutu kuangalia mtiririko wa matukio ya hivi karibuni. Tokea mwezi wa sita lile tukio la Dk Ulimboka hadi jana hili la Mwangosi, ni unyama, uhuni na kutotii sheria. Nchi ilishamshinda ila kwa vile hakuwa na exit plan basi ana hang-around!
Tuna hitaji dunia ijue kuwa hatuna serikali wala vyombo vya dola tena!!