Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,884
- 6,885
Tukio la kuuawa kwa mwandishi huyo bado limevuta hisia za wananchi wengi ambapo shinikizo linaelekezwa kwa Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Iringa, Michael Kamuhanda, likimtaka ajiuzulu kama sehemu ya uwajibikaji.
Akihutubia wananchi hao, Mchungaji Msigwa, alilaani kitendo cha kuuawa kwa Mwangosi na kusema kuwa hatatoa kauli yoyote isipokuwa atafanya kazi kwa vitendo na kuhakikisha Kamanda Kamuhanda anaondoka. "Hatuwezi kulinda ujinga huu uendelee, mimi sitatoa tamko ila nitaanza kwa vitendo. Hatuwezi kuuacha uozo huu. Kamuhanda lazima aondoke," alisema.
Alilitaka jeshi la polisi kumuogopa Mungu na kutenda haki badala ya kutii amri zinazohatarisha usalama wa raia na kuwakatisha uhai. "Nalaani vitendo vyote vya jeshi la polisi vinavyohatarisha usalama wa raia. Na wale wote wanaotoa amri kwa askari kwa ajili ya kuwapiga na kuwaua wananchi washindwe na walegee kwa jina la aliyehai Yesu Kristo, Iringa hatukuzoea matukio haya, sasa basi Kamuhanda lazima aondoke," alisema Msigwa.
Aliwataka wananchi wa Iringa kushiriki katika maandamano ya amani yatakayofanyika leo kuanzia ofisi yake kuelekea katika ofisi ya Kamanda Kamuhanda kushinikiza aondoke Iringa.
"Nyumbani kwetu kuna nyoka, huyu nyoka lazima aondoke. Kila Ijumaa tutakuwa na maandamano ya amani kumng'oa huyu nyoka na lazima polisi walinde maandamano hayo. Kamuhanda ni nyoka lazima aondoke," aliongeza.
Polisi chupuchupu kupigwa na wananchi mkutanoni Iringa Mjini
MAUAJI ya mwandishi wa kituo cha runinga cha Channel Ten, marehemu Daud Mwangosi, aliyeuawa kwa kufyatuliwa bomu na polisi kijijini Nyololo mkoani Iringa, yameendelea kuliandama jeshi hilo, ambapo wananchi mjini hapa nusura wampige askari aliyevamia mkutano wa mbunge juzi.
Katika mkutano huo wa mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa (CHADEMA), uliofanyika katika eneo la Soko Kuu mkabala na kituo cha polisi, askari mmoja alijitokeza na kutaka kuwapiga wananchi kwa virungu bila sababu. Wakati Mchungaji Msigwa akiendelea kuhutubia, askari huyo alitokea kituoni hapo na kwenda kutembeza virungu kwa watu, lakini kabla ya kuanza kazi yake, sauti za wananchi zilipazwa zikisema, "Muacheni huyo ndiye atakayetuonyesha Mwangosi leo hii."
Wakati zogo hilo likiendelea, kundi la vijana lilianza kumsogelea huku likisema: "Hatuogopi mabomu wala bunduki za polisi." Purukushani hizo, ziliwafanya askari wenzake kufika na kumvuta huku wakimkimbizia kituoni kumnusuru na uamuzi waliotaka kuuchukua wananchi dhidi yake.
na Gustav Chahe, Iringa
imechapishwa: Tanzania Daima
Iringa - Maandamano kushinikiza Kamuhanda ajiuzuru yapigwa stop
Polisi wakizunguka mji wa Iringa kuzuia maandamano yaliyoandaliwa na Mbuge Msigwa kushinikiza Kamanda Kamuhanda ajiuzuru.
Msigwa amesema kutokana na barua aliyoipata toka kwa zikitaka kusitisha maandamano hayo, aneleza barua inawataka kusitisha na kueleza kuwa sababu kubwa ni kwamba maandamano hayo hayataweza kuwa na polisi wa kusimamia na kukataza kufikia katika ofisi ya RPC ambayo ni ofisi ya kiserikali.
Hata hivyo Msigwa ameeleza kuwa msimamo wao uko pale pale ila anajiandaa kujibu hoja za barua hiyo na kuwataka wananchi wawe na subira mpaka atakapowatangazia tena kuwepo kwa maandamano hayo ya amani. Wakati huo huo wameonekana askari wakiwa katika magari yao kudhibiti wananchi kuandamana. Hali hiyo ilitokana na wananchi hao kumiminika kwenye ofisi za Chadema mjini hapa kwa ajili ya kujiandaa maandamano.
Katika mkutano huo wa mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa (CHADEMA), uliofanyika katika eneo la Soko Kuu mkabala na kituo cha polisi, askari mmoja alijitokeza na kutaka kuwapiga wananchi kwa virungu bila sababu. Wakati Mchungaji Msigwa akiendelea kuhutubia, askari huyo alitokea kituoni hapo na kwenda kutembeza virungu kwa watu, lakini kabla ya kuanza kazi yake, sauti za wananchi zilipazwa zikisema, "Muacheni huyo ndiye atakayetuonyesha Mwangosi leo hii."
Wakati zogo hilo likiendelea, kundi la vijana lilianza kumsogelea huku likisema: "Hatuogopi mabomu wala bunduki za polisi." Purukushani hizo, ziliwafanya askari wenzake kufika na kumvuta huku wakimkimbizia kituoni kumnusuru na uamuzi waliotaka kuuchukua wananchi dhidi yake.
na Gustav Chahe, Iringa
imechapishwa: Tanzania Daima
Iringa - Maandamano kushinikiza Kamuhanda ajiuzuru yapigwa stop
Polisi wakizunguka mji wa Iringa kuzuia maandamano yaliyoandaliwa na Mbuge Msigwa kushinikiza Kamanda Kamuhanda ajiuzuru.
Mbunge wa Iringa mjini Msigwa akitoka eneo la ofisi akielekea hospitali kwa matibabu ya mguu wake baada ya kusitishwa kwa maandamano
Mbunge wa Iringa mjini kupitia tiketi ya chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Peter Msigwa, akizungumza na wanachama na wapenzi wa chama hicho katika ofisi za Wilaya za chama hicho kuhusu kuahirishwa kwa maandamano ya amani yaliyokuwa yafanyike siku ya leo kushinikiza kamanda wa polisi mkoa wa Iringa Michael Kamuhanda kujiuzulu kutokana na kifo cha mwandishi wa habari wa channel ten Daudi mwangosi kilichotokea tarehe 2 septemba mwaka huu.
Msigwa amesema kutokana na barua aliyoipata toka kwa zikitaka kusitisha maandamano hayo, aneleza barua inawataka kusitisha na kueleza kuwa sababu kubwa ni kwamba maandamano hayo hayataweza kuwa na polisi wa kusimamia na kukataza kufikia katika ofisi ya RPC ambayo ni ofisi ya kiserikali.
Hata hivyo Msigwa ameeleza kuwa msimamo wao uko pale pale ila anajiandaa kujibu hoja za barua hiyo na kuwataka wananchi wawe na subira mpaka atakapowatangazia tena kuwepo kwa maandamano hayo ya amani. Wakati huo huo wameonekana askari wakiwa katika magari yao kudhibiti wananchi kuandamana. Hali hiyo ilitokana na wananchi hao kumiminika kwenye ofisi za Chadema mjini hapa kwa ajili ya kujiandaa maandamano.