Nyankurungu2020
JF-Expert Member
- Oct 2, 2020
- 4,086
- 6,568
Wananchi wa kila kada wamepiga kelele na kushauri mkuu wa nchi amfute kazi January Makamba maana tangu aingie Wizara ya Nishati kila kitu kimeenda mrama. Bwawa la Nyerere ambalo kama lingekamilika Juni 2022 lingekuwa msaada mkubwa kwa Watanzania na kuleta ahueni ya maisha maana gharama za maisha zingepungua.
Upo ushahidi wa wazi na kimazingira January Makamba amezembea na kuhujumu mradi wa JNHP maana alileta zengwe la krane mpaka kuchepusha maji kukakwama.
Sasa hivi amegeuza Tanesco kama mradi wake wa kupiga madili yeye na Maharage Chande kila kukicha ni matengenezo yasiyoisha na kuingia mikataba ya ajabuajabu na Mahindra Tech.
Huyu mwingine anaitwa Nape anatumia madaraka vibaya na kusababisha upotevu wa pesa za umma ambazo zingetumika kwa manufaa ya umma. Anazunguka nchi nzima na helikopta kwenda kupaka rangi vibao vya mitaani. Huu ni uhujumu uchumi wa wazi kabisa.
Mama sababu unapaswa kushaurika. Sikia kilio cha Watanzania na wafute kazi hawa mawaziri wawili ukiwa huko huko USA.
Upo ushahidi wa wazi na kimazingira January Makamba amezembea na kuhujumu mradi wa JNHP maana alileta zengwe la krane mpaka kuchepusha maji kukakwama.
Sasa hivi amegeuza Tanesco kama mradi wake wa kupiga madili yeye na Maharage Chande kila kukicha ni matengenezo yasiyoisha na kuingia mikataba ya ajabuajabu na Mahindra Tech.
Huyu mwingine anaitwa Nape anatumia madaraka vibaya na kusababisha upotevu wa pesa za umma ambazo zingetumika kwa manufaa ya umma. Anazunguka nchi nzima na helikopta kwenda kupaka rangi vibao vya mitaani. Huu ni uhujumu uchumi wa wazi kabisa.
Mama sababu unapaswa kushaurika. Sikia kilio cha Watanzania na wafute kazi hawa mawaziri wawili ukiwa huko huko USA.