Kama naanza kuichoka Azam TV vile

Kama naanza kuichoka Azam TV vile

kuna taarifa kwamba super sport imelazimika kufungua studio jijini dar kutokana na ushindani wanaopata toka kwa azam tv hususani ktk urushaji wa live wa ligi ya vodacom na ligi zingine.

hawa waswahili wenzetu hawajui kitu.wanabwabwaja tu.

Woga wa dstv ulikuwa ni kipindi azam wanaanza wakajua tumekwisha ila kwa kadri siku zinavyozidi songa hawoni ushindani wowote
 
Woga wa dstv ulikuwa ni kipindi azam wanaanza wakajua tumekwisha ila kwa kadri siku zinavyozidi songa hawoni ushindani wowote

hujui kinacho endelea kijana.I'm working in a broadcasting sector.
 
Mimi niko na Azam from begining.sijajuta na sitegrmei kujuta soon na hasa kwa hii package yao kubwa.
Nahisi wanaolalamika ni wale watu wasio na shughuli ya kufanya tv kwao ni 18/7 baba/mama anatafuta mama/dada anapakua mimi nakula.
Lakini kama mtu uko busy na issue za maisha ukiondoa mpira (yes i can watch 2 games in a row) siwezi kuangalia tv zaidi ya masaa matatu!hapo ina include one episode of ma fav tv series,taarifa ya habari(fully mpaka utabiri wa hali ya hewa)and if i real have time discovery channels.
 
Azam ukitoa mbc's hakuna kitu pale channel matangazo mia.binafsi ni mpenz wa movie but kwa azam sijaona channel za movie ukiachana na zile za kiarabu tena wanaonyesha movie za mwaka 47.nilijua watakuja na kitu kizuri kumbe ovyo tuuu
 
Azam ukitoa mbc's hakuna kitu pale channel matangazo mia.binafsi ni mpenz wa movie but kwa azam sijaona channel za movie ukiachana na zile za kiarabu tena wanaonyesha movie za mwaka 47.nilijua watakuja na kitu kizuri kumbe ovyo tuuu

hamjashikiwa bakora lazima mtazame azam TV,au lazime mnunue king'amuzi chao.

kama vp tazameni tbc1.
 
kama VP tazama tbc1,naambiwa Jana walikuwa wanarusha live harusi.hahaha

Ahahahaa kweli aisee..wamenishangaza sana channel ya taifa inakosa vipindi muhimu inaspend masaa mengi kuonesha watu wanacheza quaito....wanatakiwa wawe na chanel ya kuonesha mambo hayo na sio hiyo main chanel
 
Ni suala la muda tu. Kwa umri wao, naamini Azam Tv is the best in Tanzania.
 
Sinema zao nazo ni zile zile kila siku.. tena ni za zamani kishenzi...hiyo chaneli wangeitoaga tu..michaneli ya kiarabu kiiibaaaooo

........... Na za kihindi pia ni nyingi sana unadhani tuko Mumbai mkuu.
 
Kingne kinachoniuzi mm mvua ikianza tu kunyesha kinakata mawasiliano hata kama ni mvua ndogo,iwe na upepo au haina upepo hata kama ni ndogo aje lazima kizime,nauzika bas tu. Na wenzangu ni hivyo jamani? Au mm tu.

kwangu hata dstv! hii inatokana na nini?
 
Wewe utakuwa mfanyakazi wa azam tena mwambie boss wako ni jipu

sipo azam TV mkuu,lakini kwa kuwa mazingira ya shughuli zangu yanahusiana na secta ya habari na utangazi,nafahamu ueledi wa azam TV chini CEO tido mhando.
 
kinacho wabeba hawajamaa ni lingi ya vodacom lakini kwa channel zao hakuna kitu wamejaza michannel ya kiarabu yaani kwa ujumla hawana jipya dstv ndy mpango mzima
 
Kwa masuala ya teknolojia wapeni time kudogo wataimudu tu,na kuhusu haya mapungufu mengine watu wao wapo humu watayasoma na kuyafanyia kazi
 
Kuna jamaa yangu alikinunua na alianza kujuta from day one... Kizuri ni gharama. DSTV ina gharama but it remains the best...
 
Azam wapo vizuri kama kuna mapungufu tuwape muda; sijaona mbadala wa kisimbusi kingine local labda DSTV
 
Azam TV wao wanajua faida ya media wanaipata kwenye VPL. Na ndiyo huko waliko invest. Mleta mada kama Azam hawako vizuri kwenye live coverage naomba uniambie.

Pili, taarifa ya habari. Muundo wa taarifa yao ya habari bado haujazoeleka lakini wapo vizuri.

Kuhusu qaality hill nadhani labda uwe na lingine. Quality ya matangazo yao ni nzuri ukitoa kasoro mbili ambazo kwangu ipo moja ya mvua ikinyesha matangazo yanasumbua. Wengine wameongeza na jua Kali.

Tatu, ukilinganisha gharama za Azam na DSTV ni umbali wa magharibi na mashariki. Gharama za Azam zipo fair kuliko DSTV kwa mtanzania wa kawaida. Azam wakianza kuonyesha EPL nadhani ndiyo utakuwa mwisho wa DSTV EA. Sijaona cha ziada DSTV zaidi ya vipindi ambavyo wananunua kutoka channel nyingine.

Kuhusu uchanganyaji inawezekana standard ndiyo hiyo inayotakiwa kimataifa ila we we inapenda mbwembwe za local Tvs ambazo Hazina viwango.

Mbona haulaumu ITV saizi wamebadili tangazo lao la taarifa ya habari limekaa kishamba zaidi ya lile la awali?
 
Back
Top Bottom