Kama mwanaume: Jitahidi mazingira yako ya nyumbani yawe bora kuliko mazingira ya nyumbani kwa mke wako

Synthesizer

JF-Expert Member
Feb 15, 2010
11,143
18,774
Kuna hili suala la watu kusema hata ukioa mwanamke ambaye kwao wana uwezo kukuzidi sio tatizo. Huko ni kujidanganya. Inakuwa sio tatizo labda mwaka wa kwanza wa ndoa yenu, wakati wa honeymoon period.

Ndani ya moyo wake, mkeo ambae ataishi na wewe katika mazingira duni kuliko ya nyumbani kwao ataanza tu kuya-miss mazingira ya nyumbani kwao.

Utakuta kila mwaka anataka aende likizo kwao, na wewe siku zote utakuwa unasita kwenda nae kwao, kwa sababu kila wanachofanya utaona ni kama wanakuonyesha maisha bora ya mke wako akiwa kwao kuliko unayompa. Ukiwa na shemeji zako wakati huo ndio kabisa.

Na utambue kuwa kila mkeo akienda kwao baba yake au mama yake huwa atamwita chemba na kumuuliza vipi mwanangu, mnamudu maisha? Unahitaji msaada wowote?

Kaka zake watakuwa wanatoa ofa za ada za shule, au kumkatia pochi, au namna tu fulani ya kumsaidia, mara nyingine kwa makusudi tu kukuonyesha humtunzi vema dada yao. Mkizaa watoto ndio kabisa, kila wakifunga shule utasikia baba tunataka kwenda kuwasalimia babu na bibi!

Changamoto ni kubwa zaidi kama mazingira ya kwenu wewe ni duni, maana itakuumiza kwamba watoto wako na mkeo wanasita kwenda kwenu kwa wazazi wako wakati wa likizo, hata kama mkeo anaonyesha angependa kwenda. Ujue huwa anawaita watoto chemba anawakemea kusema hawataki kwenda kwenu! Kwa hiyo pia, unapofanikiwa kimaisha, tengeneza mazingira mazuri kwenu pia.

Kwa hiyo bwana, ukioa, kwa udi na uvumba jitahidi kwamba mazingira ya nyumbani kwako yawe ni bora kuliko yale ya nyumbani kwa mkeo. Ukishindwa basi omba mkweo akusaidia ili kumtengenezea mwanae mazingira kama ya kwao alikotoka!
 
Huo ndiyo ukweli... Maisha ya ndoa yana phases nyingi sana, vijana wanadanganyagwa na kale kapenzi ka mwanzo mwanzo, ila mbeleni wanaanza majuto.

Maisha ya ndoa mkiwa hamna mtoto, mkiwa na mmoja, mkiwa na watatu, mkiwa na wa tano nk ni tofauti sana.
 
Kweli Tanzania Upagani hautaisha, sasa Mke wako atakuwaje na kwao tofauti na Mume wake?

Mungu amewaunganisha kuwa kitu na mwili mmoja, hivyo hakuna kwao au kwako kuna kwenu, kama Mwanaume jenga Mji ili uishi na Mke na Familia yako yaani watoto wako, hiyo ndiyo maana ya Ndoa Kidini.

Ukishaingia kwenye ndoa unaondoka nyumbani kwa wazazi na kuanzisha mji wenu yaani mke, mume na mkijaaliwa watoto!
 
Kweli Tanzania Upagani hautaisha, sasa Mke wako atakuwaje na kwao tofauti na Mume wake?

Mungu amewaunganisha kuwa kitu na mwili mmoja, hivyo hakuna kwao au kwako kuna kwenu, kama Mwanaume jenga Mji ili uishi na Mke na Familia yako yaani watoto wako, hiyo ndiyo maana ya Ndoa Kidini.

Ukishaingia kwenye ndoa unaondoka nyumbani kwa wazazi na kuanzisha mji wenu yaani mke, mume na mkijaaliwa watoto!
Wewe endelea tu kuishi katika nchi ya kusadikika! Kuwa kitu kimoja na wewe haina maana inafuta kuwa na kwao! Kwani wewe ukioa kwenu kunaisha? Mbona unakubali urithi wa mashamba na vinginevyo vilivyo kwenu basi?
 
Huo ndiyo ukweli... Maisha ya ndoa yana phases nyingi sana, vijana wanadanganyagwa na kale kapenzi ka mwanzo mwanzo, ila mbeleni wanaanza majuto.

Maisha ya ndoa mkiwa hamna mtoto, mkiwa na mmoja, mkiwa na watatu, mkiwa na wa tano nk ni tofauti sana.
Na Ndio Mana wakiambiwa waoe kijijini kwao wanakuja kuoa town waliojaza hips wanaenda mcity shopping wakati uhalisia wa maisha yatataka ukaemee tandika sokoni jamani. Waoe watu wanaofahamu tokea mababu zao Mana na wewe unakuwa unajua asili ya mbegu ama dna zao.

Sema wakishasoma na kupata kadegree kamoja ama tuwili Basi they feel to be at the top of the others/world. They feel already to above shoulder and head of all the people. Hata Mama yake ama baba yake akimwambia mwanangu oa hapa hapa nyumbani kwetu. Akikaa na wenzake anaanza yaani ujue shida mno kuwa wazazi locally na ambao sio educated and civilized wanaleta ubaguzi wa kikabila.

Hata hawajifunzi hata ukitaka ubunge Ni lazima uende kwenu kule wanakokujua na wewe unawajua.kama hakuna hizi mambo nenda Moshi kagombee ubunge na uwe unatokea let say singida or kigoma. Wanapata kitu kinaitwa perceptual blind spot Kama kwenye design za roads Kuna icho kitu huwa kinaletaga ajali ukicheki Kama ajali inatokea frequently on the same spot Basi Engineer wakati anasimamia ama anadesign alikuwa na mbususu pembeni ama anachati ivyo hakuwa majini kabisa.

So baadaye wazazi bana wanakuwa kimya na kuwapa baraka. Ila kijana kila akipiga hatua Ni majuto, akifika uzeeni kabisa above 50/60/70 ndipo anaanza kuona Ile spot ambayo ule muda hakuiona. Kwanza miaka kuanzia mitano tu nadhani anaanza kuliona tantamtira la kutosha nadhani.kwanza mama yake aje hapo home kumsalimia na tope la bush jekundu Kama la Tarime kigoma karatu ndio aambiwe mbona mama yako Ni mchafu atatuchafulia nyumba mpeleke kwa rafiki yako alale naye anampelekea.mara mama yako Ni mchawi nimekuta nguo ya mtt ikiwa kwenye begi lake,miti itasagwa itawekwa kwa kichupa chumbani kwake baadaye utaitwa kuonyeshwa kuwa mama yako akaja na uchawi hapa anataka kuniua.

Mara mdogo wako ananitongoza,atamuita chumbani kumsadia kufunga neti anayo kanga moja atamkumbatia atafunga mpango ataanza kulia kuomba Msaada kwa majirani atapiga kelele ama yowe kuwa kweli Keisangora unanibaka jamani nabakwa niokoeni. Ukisaidia ndugu ananunaje Kama story ya jackal Daniel ,mama Kyle's hataki samsoni asomee boarding Mana anaona Kama atawafilisi na atafurahia yeye ukisaidia kwenu ama nbora hata rafiki kuliko ndugu ama hata mchepuko mke haumii Ila kusaidia ndugu Ni kero. Na Ile story samsoni atakuja kuwa mtu mkubwa kuliko wale mapacha. Mana anatengenezwa strong emotionally ndio Siri kubwa duniani.
 
Kuna ukweli.
Lakini mapenzi ndo yanaanza halafu familia,uwezo badae..... Sasa tumesha pendana katika hali zetu ..mengine ni kusaidiana tu na kupambana mfikie malengo yenu....

Kikubwa chunguza tabia za mwenzako kama mtaendana...usioe au kuolewa kwa tamaa ya kitu..mf mali na muonekano.
 
Kuna ukweli.
Lakini mapenzi ndo yanaanza halafu familia,uwezo badae..... Sasa tumesha pendana katika hali zetu ..mengine ni kusaidiana tu na kupambana mfikie malengo yenu....

Kikubwa chunguza tabia za mwenzako kama mtaendana...usioe au kuolewa kwa tamaa ya kitu..mf mali na muonekano.
Hayo mapenzi ama kupendana huwa Ni temporary emotions jamani kama hasira, furaha,maumivu moyoni ya kufiwa. People forget. Na ndio Mana hili suala huwa wanaongea na vijana wao mpaka wanalia ujue. Wao walipangiwa oa Koo/familia fulani ,Hawa digital generation wanajifanya wamesoma wamebadilika. Wakati since the universe dawn behavior za binadamu hazijawahi change hata ufanyeje.


Yaani nakuambia huo upendo wa mwanzo unaisha huwa Ni temporarily tu.

Ni sawa na kufaki mtu fulani first time ama lile la kwanza ,Ila kadri muda unavyoenda unaona kawaida so nothing special. Sasa subconscious ikishajua kuwa hakuna Cha special or peculiar ingawa kwa hii conscious mind yake atakuaminisha na maneno kuwa mnapenda Ila deep down tayari ameshachoka. Na mind zetu huwa zinanasa Mambo hasi,mabaya,yaani Ni mwendo wa kucheki mabaya ndio ubongo tulio nao jamani na sio kuwa Kuna anayeponea chupuchupu.
Wote tuko ivyo. Sasa bwana akishajaza mabaya yako yote uliyomkosea naakuambia utaanza kuziona kila rangi ambazo hujawahi kuziona.



Hebu cheki ukinunua gari yako first time,yaani kavumbi kidogo unaifuta car wash hukosi Kama chooni kwa style yako.


Lift hutoi hata kwa jirani Mana atakuchafulia gari ama ataharibu seat cover Ila asa time goes ,utaiazima mshkaji akalie mbususu,unakawia kuiosha, lile bashasha la ugeni halipo Tena.


Sasa kilio ama msiba unakuja kwanza utajaza wesee wewe e.
Iyo Ni kawaida hata utaenda kununua mhindi nalo na hushuki utaita muuzaji akuletee kwa gari.


Sasa finally utakapoanza kuiepeleka gereji unayo laki 2 mfukoni unashangaa inataka kukata laki tano inabidi uka draw nyingine. Ile kwenda vijana wanachomoa kifaa kizima waanakuwekea kibovu ,ama ukirudi unauziwa icho icho. Smt kile kipato kikate. Na Kama una akili mno utaanza kuona Kama inakula hela nyingi kuliko familia yako.yaani gari inakula laki tano na unakuta labda una mwezi kwako hamjala kuku choma ama samaki makange.


Taratibu unaanza kuiacha home unacheki hiace na unarudia kudandia bomba.

Later mind inakushauri kuwa iuze Mara unatafuta dalali na unakuja kupondea hapa gari kuwa Ni ubishoo tu. Unaiona haina umuhimu. Jamani hii mfano tu wa gari tu mojawapo wa vitu tunavyomiliki.
 
Wewe endelea tu kuishi katika nchi ya kusadikika! Kuwa kitu kimoja na wewe haina maana inafuta kuwa na kwao! Kwani wewe ukioa kwen kunaisha? Mbona unakubali urithi wa mashamba na vinginevyo vilivyo kwenu basi?

Kwetu ni kwangu nilipoanzisha Mji, nikioa Mke wangu anaondoka/hama kwao anakuja kwangu kunakuwa kwetu tunaungana pamoja kuwa mwili na kitu kimoja tunaanzisha Mji na Familia, ndivyo Dini ilivyonifundisha na siyo ya kusadikika.

Kwa Wazazi wako siyo kwenu pale unapoamua kufunga Ndoa, huo ndio ukubwa, kuita kwa Wazazi kwenu wakati umeshaoa na una Familia ni kuwa immature na kukataa kukuwa na majukumu!
 
Maoni yangu ktk hili swala kupitia ushuhuda wangu bjnafsi.

Mimi na mke wangu tulikutana chuoni miaka 11 iliyopita, mimi natokea familia ya kipato cha chini ila yeye kwao wanamaisha mazuri hasa, yaani unaweza sema familia yao yote wapo vyema kuanzia baba, baba wa dogo nk. Ni wafanyabiashara wa kubwa wa usafirishaji, real estate na sasa wameingia ktk mashule.

Binti alikubali nimuoe kwa mahari ya sawa na bure mpaka kwetu wakashangaa akaulizwa mara tatu tatu mwisho akaishia kuipunguza zaidi. Kwa ufupi alikubali nimuoe kwa hali yangu yoyote, tulianza maisha ktk chumba kimoja, tukahamia viwili na sasa tuna nyumba zetu 2 na viwanja kadhaa na tupo mid thirties.

Nalotaka kusema ni hivi, inategemea na mwanamke mwenyewe na hulka zake na familia yake, unaweza ukanyanyaswa kupita maelezo na pia unaweza kupewa confort kuliko unavyotegemea. La msingi kuwa mwanaume, sababu ushamuoa basi hakikisha unaishi kutokana na uwezo na mipango yako uwezo wake na familia yake usiwe sehemu ya maisha yenu.

Binafsi hupitia kipindi nafulia mpaka msosi ndani hakuna na watoto wanasimamishwa shule lakini napambana of which am sure akipiga simu kwa mzee wake just one call muamala wa kutosha tu unaingia.

Ninachoshukuru mzee wake ananipa sana ushauri wa maisha hasa ktk utafutaji na anapenda niwe karibu nae, may be kwa sababu ya prosperity ya mwanae na wajukuu zake.
 
Mi kwangu kama mke ni wangu kweli Kwa mpango wa Mungu, hili halina shida, mwanamke nikimpenda anasahau kama ana kwao au wazazi wake maana mimi naziba gape, ndiomana huwa sipendi hovyo walau siku hizi nafanya kumhitajia mwanamke tu kupenda nimepunguza
 
Back
Top Bottom