Kalonzo: Tunachunguza kwa umakini mauzo ya hivi karibuni ya hisa za Nation Media Group

Kalonzo: Tunachunguza kwa umakini mauzo ya hivi karibuni ya hisa za Nation Media Group

Mawele

JF-Expert Member
Joined
Jul 25, 2023
Posts
354
Reaction score
1,042
Kalonzo Musyoka ambaye ni kiongozi wa chama cha upinzani cha Wiper Democratic Movement na aliyewahi kuwa Makamu wa Rais wakati wa uongozi wa Mwai Kibaki, amesema wanafanya uchunguzi juu ya mauzo ya hisa yaliyofanyika hivi karibuni kwenye taasisi ya Nation Media Group kwa bwana Rostam Aziz, akisisitiza kuwa taasisi hiyo iliyoanzishwa na Aga Khan ilikuwa ni sehemu ya harakati na kupigania uhuru na kwamba uhuru wa vyombo vya habari haupaswi kuingiliwa

Pia soma
=====

"Tunachunguza kwa umakini uuzaji wa hivi karibuni wa hisa nyingi za shirika la Nation Media Group. Hii ni kwa sababu ni moja ya taasisi zilizoanzishwa na marehemu Aga Khan, na Nation Media Group ilikuwa sehemu ya harakati za kupigania uhuru wa nchi hii.

Kwa hivyo, uhuru wa vyombo vya habari hauwezi kuingiliwa kamwe. Tutachunguza mambo haya ili kuona nini hasa kimetokea, kwani nimeambiwa kuwa kwa siri, shilingi milioni 866 zimewekwa kwenye bajeti ya ziada kupitia Idara ya Serikali ya Utangazaji ili pesa hizo zilipwe haraka sana.

Jiulizeni, ni nani anayepokea pesa hizi? Tunataka kumuuliza mmiliki huyo mpya, au mwanahisa mkuu, jinsi atakavyohakikisha uhuru wa shirika la Nation Media. Hiki ni chombo muhimu sana cha mawasiliano katika nchi hii na ni lazima ahakikishe uhuru huo unakuwepo.

La sivyo, kumbukeni rafiki yangu Raila Odinga aliwahi kusema kuwa punda amechoka. Punda alilia hapa kwa sababu ya taarifa zilizotolewa na Rigathi Gachagua. Wakenya wamechoka!" - alisema Kalonzo


 
Mtanzania mwenye asili ya India/Arabuni
Mwizi
Fisadi
Tapeli
Acha ubaguzi wa rangi, haukusaidii kitu kwenye karne ya 21. Aweza kuwa mtu mwenye asili ya Iran kutoka jimbo la Baluchestan lakini kama amekidhi matakwa ya kikatiba ya uRaia anabaki ni Mtanzania. Hata wewe Mshana Jr tukirudi nyuma miaka 500, unaweza kuta asili yako ni Sudan

Umaskini wenu, kukosa maarifa ya biashara, mindset zenu mbovu, kupenda maisha ya anasa ndiyo kunawarudisha nyuma kimaendeleo kisha kuzaa chuki kama hii.

Mwaka 1990s-2000 Rostam alikuwa na raslimali za kurithi kutoka kwa Baba yake aliyekowa exporter wa hides and skins, akazi transform kupitia fursa alizozipata wakati washirika wake wengine waliishia kuponda starehe na kuwekeza hovyo.

Nilitegemea tumuunge mkono Rostam kwa kuweza kuingia Kenya, nchi ambayo imeifanya Tanzania kuwa soko la bidhaa la viwanda vyake kwa miaka.

Nilitegemea tutembee kifua mbele kumuunga mkono Rostam Mtanzania mwenzetu na kuanza kuingia Kenya na biashara zetu zingine. Ni aibu kwa watu kama Mshana Jr kuingiza chuki za kisiasa za ndani na kumpiga vita Rostam
 
Wakenya hawataki kuamini mTanzania anaweza kuwekeza uwekezaji mkubwa kwao
Ni kweli hawawmini, wangetaka tuendelee siku zote kuwauzia machungwa ya muheza, halafu na sisi kununu Delmonte juice kutoka viwanda vyao.

Tumuunge mkono Rostam Aziz kwa hatua aliyopiga. Na watanzania wengine wenye mitaji waendelee kuingiza Kenya
 
Acha ubaguzi wa rangi, haukusaidii kitu kwenye karne ya 21. Aweza kuwa mtu mwenye asili ya Iran kutoka jimbo la Baluchestan lakini kama amekidhi matakwa ya kikatiba ya uRaia anabaki ni Mtanzania. Hata wewe Mshana Jr tukirudi nyuma miaka 500, unaweza kuta asili yako ni Sudan

Umaskini wenu, kukosa maarifa ya biashara, mindset zenu mbovu, kupenda maisha ya anasa ndiyo kunawarudisha nyuma kimaendeleo kisha kuzaa chuki kama hii.

Mwaka 1990s-2000 Rostam alikuwa na raslimali za kurithi kutoka kwa Baba yake aliyekowa exporter wa hides and skins, akazi transform kupitia fursa alizozipata wakati washirika wake wengine waliishia kuponda starehe na kuwekeza hovyo.

Nilitegemea tumuunge mkono Rostam kwa kuweza kuingia Kenya, nchi ambayo imeifanya Tanzania kuwa soko la bidhaa la viwanda vyake kwa miakaNilitgemeaegemea tutembee kifua mbele kumuunga mkono Rostam Mtanzania mwenzetu na kuanza kuingia Kenya na biashara zetu zingine. Ni aibu kwa watu kama Mshana Jr kuingiza chuki za kisiasa za ndani na kumpiga vita Rostam
Mkuu nisaidie kunijuza maana ya kuwekeza hovyo nifahamu
 
Acha ubaguzi wa rangi, haukusaidii kitu kwenye karne ya 21. Aweza kuwa mtu mwenye asili ya Iran kutoka jimbo la Baluchestan lakini kama amekidhi matakwa ya kikatiba ya uRaia anabaki ni Mtanzania. Hata wewe Mshana Jr tukirudi nyuma miaka 500, unaweza kuta asili yako ni Sudan

Umaskini wenu, kukosa maarifa ya biashara, mindset zenu mbovu, kupenda maisha ya anasa ndiyo kunawarudisha nyuma kimaendeleo kisha kuzaa chuki kama hii.

Mwaka 1990s-2000 Rostam alikuwa na raslimali za kurithi kutoka kwa Baba yake aliyekowa exporter wa hides and skins, akazi transform kupitia fursa alizozipata wakati washirika wake wengine waliishia kuponda starehe na kuwekeza hovyo.

Nilitegemea tumuunge mkono Rostam kwa kuweza kuingia Kenya, nchi ambayo imeifanya Tanzania kuwa soko la bidhaa la viwanda vyake kwa miakaNilitgemeaegemea tutembee kifua mbele kumuunga mkono Rostam Mtanzania mwenzetu na kuanza kuingia Kenya na biashara zetu zingine. Ni aibu kwa watu kama Mshana Jr kuingiza chuki za kisiasa za ndani na kumpiga vita Rostam
Upo sahihi na Mshana Jr yupo wrong maana tunapokwenda nje ya mipaka, masuala madogo madogo tunayaweka kando. Musyoka anachukia kuona mtu kutoka Tiseti (TZ kwa Kikenya) ananunua kampuni. Huo ni ushindi kwetu wa TZ
 
Kalonzo: Tunachunguza kwa umakini mauzo ya hivi karibuni ya hisa za Nation Media Group.
View attachment 3558466
Ni jambo la kusikitisha, na pengine la kuchekesha, kumuona mwanasiasa mkongwe kama Kalonzo Musyoka akipagawa na kupatwa na kiwewe baada ya kusikia kuwa Mtanzania, Rostam Aziz, amechukua udhibiti wa Nation Media Group (NMG). Badala ya kupongeza ukuaji wa mtaji wa ndani ya Afrika Mashariki, Kalonzo ameamua kuvaa miwani ya mbao na kuanza kueneza hofu, akidhani kuwa milki za kiuchumi ni haki ya kuzaliwa ya tabaka fulani la Kenya pekee.

Huu hapa ni ukweli mchungu ambao Kalonzo na wenzake wanapaswa kuumeza:

Dunia ya kibiashara haiongozwi na itifaki za kidiplomasia au "vibe" za kisiasa za Wiper. Katika soko huria, bidhaa humfuata mwenye fedha. Ikiwa Aga Khan ameamua kuuza hisa zake asilimia 54, na Rostam Aziz ana ukwasi wa kutosha kuzinunua, huo ndio mwisho wa mjadala.

Kalonzo anapaswa kuelewa kuwa NMG ni kampuni ya umma inayotafuta faida, siyo idara ya serikali ya Kenya. Kulalamika kuwa Mtanzania amenunua kampuni ya Kenya ni dalili ya "uhafidhina" uliopitwa na wakati. Biashara haina pasipoti; ina namba pekee.

Lugha ya Biashara ni Faida, Wakati Kalonzo akihubiri hofu na hisia za kutaifishwa kwa fikra, Rostam Aziz anazungumza lugha ya Return on Investment (ROI). Wawekezaji hawanunui hisa ili "kuishawishi" siasa za Kenya—wananunua hisa ili kukuza mitaji yao.​


Zama za kufikiri kuwa vyombo vya habari ni dhana za propaganda za wanasiasa waliofeli zimepitwa na wakati. Rostam ni mfanyabiashara wa kimataifa; hawezi kuweka mabilioni yake kwenye hatari kwa ajili ya mashindano ya kijinga ya kisiasa ya Nairobi.

Kwa miaka mingi, baadhi ya wasomi na wanasiasa nchini Kenya wamekuwa na mtazamo wa "kaka mkubwa," wakidhani Tanzania ni shamba la bibi au soko la kuuzia bidhaa zao tu. Amkeni! Tanzania ya sasa ina mabilionea wenye uwezo wa kununua taasisi kubwa popote barani Afrika.

Kama Rostam Aziz anaweza kupeleka Taifa Gas nchini Kenya na sasa kumiliki chombo kikubwa cha habari, ni ishara kuwa mizani ya nguvu za kiuchumi imehama. Tanzania si nchi ya kusubiri misaada au bidhaa kutoka Nairobi; ni nchi inayozalisha wawekezaji wenye njaa ya kutawala ukanda huu.
 
Ni jambo la kusikitisha, na pengine la kuchekesha, kumuona mwanasiasa mkongwe kama Kalonzo Musyoka akipagawa na kupatwa na kiwewe baada ya kusikia kuwa Mtanzania, Rostam Aziz, amechukua udhibiti wa Nation Media Group (NMG). Badala ya kupongeza ukuaji wa mtaji wa ndani ya Afrika Mashariki, Kalonzo ameamua kuvaa miwani ya mbao na kuanza kueneza hofu, akidhani kuwa milki za kiuchumi ni haki ya kuzaliwa ya tabaka fulani la Kenya pekee.

Huu hapa ni ukweli mchungu ambao Kalonzo na wenzake wanapaswa kuumeza:

Dunia ya kibiashara haiongozwi na itifaki za kidiplomasia au "vibe" za kisiasa za Wiper. Katika soko huria, bidhaa humfuata mwenye fedha. Ikiwa Aga Khan ameamua kuuza hisa zake asilimia 54, na Rostam Aziz ana ukwasi wa kutosha kuzinunua, huo ndio mwisho wa mjadala.

Kalonzo anapaswa kuelewa kuwa NMG ni kampuni ya umma inayotafuta faida, siyo idara ya serikali ya Kenya. Kulalamika kuwa Mtanzania amenunua kampuni ya Kenya ni dalili ya "uhafidhina" uliopitwa na wakati. Biashara haina pasipoti; ina namba pekee.

Lugha ya Biashara ni Faida, Wakati Kalonzo akihubiri hofu na hisia za kutaifishwa kwa fikra, Rostam Aziz anazungumza lugha ya Return on Investment (ROI). Wawekezaji hawanunui hisa ili "kuishawishi" siasa za Kenya—wananunua hisa ili kukuza mitaji yao.​


Zama za kufikiri kuwa vyombo vya habari ni dhana za propaganda za wanasiasa waliofeli zimepitwa na wakati. Rostam ni mfanyabiashara wa kimataifa; hawezi kuweka mabilioni yake kwenye hatari kwa ajili ya mashindano ya kijinga ya kisiasa ya Nairobi.

Kwa miaka mingi, baadhi ya wasomi na wanasiasa nchini Kenya wamekuwa na mtazamo wa "kaka mkubwa," wakidhani Tanzania ni shamba la bibi au soko la kuuzia bidhaa zao tu. Amkeni! Tanzania ya sasa ina mabilionea wenye uwezo wa kununua taasisi kubwa popote barani Afrika.

Kama Rostam Aziz anaweza kupeleka Taifa Gas nchini Kenya na sasa kumiliki chombo kikubwa cha habari, ni ishara kuwa mizani ya nguvu za kiuchumi imehama. Tanzania si nchi ya kusubiri misaada au bidhaa kutoka Nairobi; ni nchi inayozalisha wawekezaji wenye njaa ya kutawala ukanda huu.
Muda ni mwalimu mzuri.
 
Mkuu nisaidie kunijuza maana ya kuwekeza hovyo nifahamu
Mifano hii hapa michache:-
1. Kununua magari ya kifahari yanayoshuka thamani haraka badala ya mali inayozalisha faida.

2. Kuingiza fedha kwenye biashara usizozielewa kisa tu umeona wengine wanapata faida.

3. Kuweka mtaji kwenye miradi ya upatu (Pyramid schemes) inayoahidi utajiri wa haraka bila kazi.

4. Kutumia mtaji wa biashara kulipia anasa na sherehe badala ya kuuzungusha ili ukue.

5. Kununua ardhi yenye migogoro ya kisheria bila kufanya utafiti wa kina wa umiliki.
 
Upo sahihi na Mshana Jr yupo wrong maana tunapokwenda nje ya mipaka, masuala madogo madogo tunayaweka kando. Musyoka anachukia kuona mtu kutoka Tiseti (TZ kwa Kikenya) ananunua kampuni. Huo ni ushindi kwetu wa TZ
Wakenya watuburuza sana kiuchumi, nitamuunga mkono Mtanzania wa itikadi yeyote, kabila yeyote, dini yeyote na rangi yeyote as long as anachuma fedha Kenya. Tutofautiane tukiwa hapa Tanzania, tukitoka nje tuwe wamoja
 
Wakenya watuburuza sana kiuchumi, nitamuunga mkono Mtanzania wa itikadi yeyote, kabila yeyote, dini yeyote na rangi yeyote as long as anachuma fedha Kenya. Tutofautiane tukiwa hapa Tanzania, tukitoka nje tuwe wamoja
Hii filosofia inawashinda watu wengi hapa JF. Tutofautiane tukiwa ndani, tukitoka nje tuwe wamoja hata wakiwa ni Wazanzibari
 
Is not about mtanzania ila huyo bwana hana track record nzuri tz kwenye sias ana biashara . Anahusishwa na matukio mengi
Track nzuri ndiyo zipi? Wewe hujawahi kufanya biashara na hujui lugha ya biashara. Wachukue matajiri hata 10 Afrika kama akina Motsepe, Mo Ibrahim, Dangote etc halafu nenda kawachunguze.

Kwenye biashara siyo seminary school ambako kunatakiwa maadili mema ili uje kuwa Padre. Biashara inahitaji mtu jasiri ambaye anaweza kumeza nyuki mwenye hasira au msumari wa kutu. Aggressiveness
 
Track nzuri ndiyo zipi? Wewe hujawahi kufanya biashara na hujui lugha ya biashara. Wachukue matajiri hata 10 Afrika kama akina Motsepe, Mo Ibrahim, Dangote etc halafu nenda kawachunguze.

Kwenye biashara siyo seminary school ambako kunatakiwa maadili mema ili uje kuwa Padre. Biashara inahitaji mtu jasiri ambaye anaweza kumeza nyuki mwenye hasira au msumari wa kutu. Aggressiveness
Well huku duniani kwenye ulimwengu wa sasa a dirt kwenye profile yako inaweza kukuathiri.
Hii sio biashara ya mchicha au maharage where no body cares

In US and europe, even south africa some places if una bad reputatiion katika maeneo fulani good luck getting chance over there
 
Back
Top Bottom