Unajua Lenny Kravits ni MYAHUDI na MJAMAICA? Ingawa kwa kimila, hatakiwi kuwa Myahudi kwa sababu Mama ni Mjamaica ila alikuwa akienda kwa Baba basi anavaa Kibalaghashia na kushuka kwenye Masinagogi yao.
Mnyarwanda pia anaweza kuwa Myahudi. Hujawahi kusikia zile ndege za jeshi zilikuwa zimetengenezwa kwa msaada wa Wageruman na zikawa zimeshawekwa Egypt uwanja wa ndege tayari kwenda kuisambaza Israel? Kuna Mdada ambaye Mama yake alikuwa Myahudi na Baba M-Misri. Alipoona zile ndege na zipo pale kwa nini, basi akachukua simu na kupiga kwenye hiyo namba aliyopewa na MAMA yake na dakika kadhaa baadaye, Ndege kadhaa zilishuka na kuzisambaza ndege zote za wa Egypt na ngoma ikalala. Inasemekana na Watusi wako hivyohivyo.
Sasa hivi Silaha ni pesa yako. Nilishawahi kuishi sehemu ambapo kama kilomita mbili kutoka ninapoishi, kulikuwa na Soko ambalo watu walisema pale ukitaka hata kifaru au ndege ya kivita utanunua. Na kweli, Guinea Conacry pamoja na kuwa walikuwa na kizuizi cha kununua Silaha, walikuja na kununua silaha za kutosha. Usafirishaji wake hapa analaumiwa sana kampuni ya MAERSK kuwa na yeye huwa anacheza rafu. Mzigo utachukuliwa hadi sijui Canada, huko unabailidhwa na kuwa mbao na kuletwa tuseme Spain, na Spain ukifika unakuwa ni msaada wa nguo na madawa kwenda Guinea, kumbe ndani ni SILAHA.
Kama sisi tunaweza, na wao wanaweza kununua. Hapa ni mwenye silaha kali na askari wazuri anashinda vita.
Lugha kali? Mungu bariki nilipitia JKT.