Kwanza,Nampongeza Waziri Wa Mambo ya Nje Bernard Membe kwa kukubali kuwa kuna haja ya kuwa na wataalamu wa uchumi kwenye Balozi zetu nje ambao wamebobea katika Diplomasia ya Uchumi .Hili suala nimeshaandika hapa mara kadhaa,nimeaandika JF na Pia makala kwenye magazeti.Ni hatua nzuri sasa kama Wizara imetambua umuhimu wa kutumia Balozi Zetu kuvutia watalii ,kuhamasisha Biashara kati ya Watanzania na watu au makampuni ya Nje na pia kuvutia wawekezaji (Foreign Direct Investment).Sasa tumeanza kwenda na wakati ingawa tunahitahi Sera yenye strategic focus kwa EAC,SADCC,AU,ARAB LEAGUE,ASIA,CHINA ,US n.k kama Potential Partners. Uingereza,Kenya,SA,China na US ni strategic partners katika Uwekezaji.Hapa ni lazima tufanye formulation ya Unique Policy ili hata wanadiplomasia wetu waongozwe na Framework Specific
Pia Economic Intelligence Unit au Think Tank iundwe na iwe na Coordination ya Moja kwa Moja na Department ya Economic Diplomacy.kwa bahati mbaya Wabunge hawakumbana katika Eneo hili.Diplomasia ya sasa ni ya Uchumi na sio Diplomasia ya Kisiasa tena. Leo tunatuma wanasiasa wakatuwakilishe kule Doha kwenye Mikutano ya WTO wakati Wenzetu wanapeleka mabingwa mbinu za majadiliano ya kibiashara na Uchumi kutoka kwenye Economic Intelligence Unit zao
Pili,jana nilitahadharisha juu ya matamshi ya Mbunge Kessy kuhusu yeye kuituhumu Rwanda na nikasema alikosa weledi unaohitajika katika majadiliano ya mijadala ya kidiplomasia ndani ya bunge na nikaonyesha masikitiko yangu kwa Mhe.Bernard Membe kushangilia kauli ya Mhe.Kessy kuwa Rwanda inaiba Raslimali za Congo-DRC na pia inafadhili M-23.
Well,Nilisema Kessy ametuhumu (Hata kama ni Kweli) bila kufanya Rejea .Nikasema labda Membe aje afanye Rejea ya Ripoti ya UN lakini nikatahadharisha kuwa hata akifanya hivyo lakini Rwanda hajaadhibiwa.
Kweli Mhe.Membe alikuja kumsaidia Kessy kwa kufanya Rejea ya Ripoti ya UN na kutumia flirting Skills akidhani kuwa anamshambulia msemaji wa kambi ya upinzani.
Membe alichofanya ni makosa makubwa kidiplomasia na hili litachochea mgogoro mkubwa na Rwanda.
Je,Kauli alizotoa Kessy au Membe kuwa Rwanda ni Wezi na M-23 ni kundi la Serikali ya Rwanda,Rais Kikwete anaweza kuzitamka kwenye Mkutano wa EAC,SADCC,ICGLR,AU Au Kule UN General Assembly? Waziri mkuu Pinda aliyelitangazia Bunge Mwaka jana kuwa Serikali imemuomba Rais Museveni wa Uganda awapatanishe Kikwete na Kagame alimaanisha nini?Kwamba Rais angefuta kauli yake ya kumshauri Kagame kuongea na FDLR?Vipi mbona Ripoti aliyoinukuu Membe Bungeni pia imeituhumu Uganda kuwa wanashirikiana na Rwanda kulifadhili Kundi la March-23 Movement(M-23)? Siis wengine tulipinga tangu Mwanzo Uganda kuhusishwa maana kama ni confidence ya Mediator sidhani kama Tanzania ingekua nayo kwa Museveni na tena ningeshangaa sana.
Tanzania tumeonyesha kutokua na ajenda kimataifa na nimeshasema mara nyingi tunafuata sera ya fuata mkumbo (Bandwagoning Diplomacy).Tupo tupo tu na tunadandia kila kitu halafu tunasema tunaheshimika sana kimataifa?
Hiyo nguvu ya usuluhishi unaitoa wapi wakati huu wa sera ya Diplomasia ya Uchumi ambako nguvu ya uchumi na kijeshi ndiyo inayokupa nguvu katika medani za kimataifa ikiwepo usuluhishi? Marekani wakisema Usalama wanamaanisha nguvu ya kiuchumi. Nigeria baada ya Rebasing ya uchumi wao imekua taifa lenye uchumi mkubwa Afrika na hivyo nguvu ya taifa na sauti yao itaheshimika
Kenya wanatupita katika nguvu na sauti kimataifa katika ukanda huu kwa sababu ya nguvu ya kiuchumi na sisi tunaendelea kutumia ile akiba ya Diplomasia ya siasa za Frontline aliyoacha Mwalimu Nyerere
Sasa Ripoti ya Mhe.Membe iliyoandikwa na UN Expert Group ilipingwa na Rwanda,pia Ripoti hiyo ilipingwa na Uganda maana hata Uganda walituhumiwa lakini Membe kwa upotoshaji Mkubwa hakuitaja.
Ni jambo la ajabu kuwa Top Diplomat wa Nchi anashindwa kuzingatia kuwa Tayari Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa lilishaidhinisha Vikwazo kupitia Azimio namba 2136 (2014) ambalo liliungwa mkono na Rwanda kwa mtazamo wa kuwa Azimio namba 1533(2004) lilotanguliwa na Azimio 1494(2003) linaheshimiwa
Azimio namba 2136 liliweka Vikwazo kwa M-23(Bila kuitaja Rwanda katika Adhabu hiyo) na pia Congo -DRC waliadhibiwa kwa kuifadhili UFDLR ambayo pia ilitajwa na UN report aliyoitumia Membe
FDLR wana extrime Ideology iliyohusika na Mauaji ya Kimbari ya Rwanda na ilithibitishwa na UN Security Council.
Haya Membe hakuyajadili wakati Bunge lilihitaji mjadala ili nchi yetu iangalie namna ya kuwasaidia majirani zetu,pia tudumishe amani,mahusiano ya kidiplomasia hasa ya kiuchumi na pia kulinda mtazamo mpana wa umajumui wa Afrika
Membe alichagua Kufanya siasa kiduchu(Petty Politics) kumshambulia Wenje binafsi(Personal Attack) kinyume na weledi wa Diplomasia na pia kutoa matamshi yatakayochochea mgogoro zaidi baina ya Tanzania na Rwanda kwa kuituhumu Rwanda kuifadhili M-23 huku akijua kwa sasa kulingana na azimio 2136 Nchi wanachama wa ICGLR(Nchi za Ukanda Maziwa Makuu) zina jukumu la jumla na binafsi katika kusaidia kutekeleza maazimio hayo ikiwa ni pamoja na kushirikiana na UN Expert Group iliyopewa Mandate ya kurefusha Sanction Regime hadi February 1,2015 ili kuleta amani ya Kudumu
Waziri wa Mambo ya Nje kupotosha mjadala na kutuhumu kuwa Msemaji wa Kambi ya Upinzani anatumiwa na Mataifa ya Nje (Pengine Rwanda) ni udhaifu mkubwa katika kukwepa hoja .Kama kuhoji kuhusu tuhuma za Rais Kukutana na Kiongozi wa Waasi(Tena Sio Upinzani) basi inamfanya Wenje kuwa Mamluki anayelipwa na Rwanda kuisemea ndani ya bunge ,Je ni wapi Duniani tuliwahi kuona Rais Wa Nchi kulisemea na kulionea huruma kundi la Waasi? Membe hakupima Kauli zake
Ni mwaka jana tu Membe alitoa matamshi tata kuhusu kutengwa kwetu kwenye Jumuiya ya Afrika Mashariki na kudai "tunasubiri Talaka".Tuliipinga kauli hii na kwa bahati nzuri Rais Kikwete aliliona hilo na akatoa hotuba nzito Bungeni kuwa hatuendi Popote.
Mimi ni mzalendo ninayelipenda Taifa langu na nitalipigania popote duniani.Sipendi Blind Patriotism.
Kagame ana matatizo yake ndani ya Rwanda lakini hatuwezi kuruhusu kauli aliyoitoa JK kuwa Rwanda Iongee na Waasi(Kauli ambayo niliiunga mkono na niliendelea kuiunga mkono hadi azimio 2136 lilipopita ingawa yeye JK hatekelezi hayo) itumike kuhatarisha mahusiano yetu na watu wa Rwanda au Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa kauli za Mawaziri ambazo wanazitoa bila kipimo
Pia suala la Majeshi yetu kule Congo DRC lipo na ni sehemu ya Tanzania katika kutimiza majukumu yake ya kimataifa(International Obligation) kupitia Azimio no.2098 la kuunda MONUSCO.
Hata hivyo halizuii mijadala bungeni maana hata Obama aliposema "Dumb War" ilikua ni matokeo ya mjadala ndani ya Congress kule US kuhusu Rais Bush kulidanganya Taifa kuwa Iraq ina silaha za Kemikali kumbe ni Uongo.Marekani ilipata hasara.
Ni lazima kuwe na mjadala bungeni kwa kukosoana na kurekebishana ili tuunde mwafaka wa kisera kama nchi tusonge mbele.Waziri alikosa weledi juu ya matumizi ya Code Words and Politeness
Unachagua kujadili millitary adventure huko DRC halafu unashindwa kutoa majibu ya kushindwa kwa Serikali kutuma Millitary Plane kufanya Evacuation hata ya Raia wetu kule Sudan Kusini wakati wa Vita? Kwanza nampongeza Membe kwa kukubaliana na ile Hoja yangu ya jana kuwa Tanzania imezubaa na wizara haina takwimu ya idadi ya Raia wa Tanzania nje hivyo hata mikakati ya kunufaika na Diaspora ni lazima tutatue changamoto hii kwanza
Tatu,Membe Alishangaza kwa kutetea ziara za Rais nje .Rais amefanya ziara zaidi ya 365 nje ya nchi kushinda Mwalimu Nyerere ambaye hakufikisha ziara 70 kwa kipindi chake cha miaka 24 madarakani.Rais anataka kuwa Member wa Diaspora?Maana ameshinda angani na nje ya nchi kwa sababu dhaifu kabisa kabisa.
Membe anatoa sababu dhaifu kuwa Rais anapendwa na kuheahimika,Je kati ya Rais Kikwete na Mwl.Nyerere ni nani alikua akiheshimika zaidi kimataifa?
Rais anashindwa kubaki nyumbani na kudhibiti wizi wa mali za umma kama bilioni 200 za ESCROW kwenye sakata la IPTL badala yake anaenda kuomba bilioni 40 au 100 nje ya nchi tena sehemu nyingine kama Singapore anapokelewa na mkurugenzi wa Idara kinyume na Itifaki kabisa?
You can't defend the trip maniac president in that way
Ifike Mahali sasa kwenye Katiba tudhibiti ziara hizi kama Mexico ambako Rais Vicente Fox alionja fedheha hii kwa kuzuiwa na Bunge lake la Senate mara Mbili Kusafiri ikiwepo ziara yake US na Canada.Safari za Rais ilikua ni lazima zipate approval ya Bunge. Chama cha Upinzani cha PRI kilizuia safari zisizokua na Tija.
Mexico walipata dawa ya kudhibiti Marais ambao ni wazururaji utadhani wamelelewa kwa supu za usafiri(Makanyagio) ya kuku wa kienyeji. Balozi za nje na hata wizara zinaweza kufanya baadhi ya safari na kupunguza gharama.
Hatuwezi kuegemea kwenye ziara za Rais katika Diplomasia ya Kuomba na Kushukuru badala ya kuweka Diplomasia ya Uchumi.Tunahitaji kudhibiti ziara za Rais kikatiba kabisa na safari zipate Approval ya Bunge kama Mexico. How can we justifty global trotting to seek aid and loans while we cant manage our Cash reserves?