BARD AI
JF-Expert Member
- Jul 24, 2018
- 3,376
- 8,120
ZANZIBAR: Mwanachama zamani wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mohamed Shamte amedai kuwa suala la kujiuzulu kwa aliyekuwa Waziri wa Utalii na Mambo ya Kale, Simai Mohamed Said lina kitu ambacho hakiwekwi wazi juu ya uamuzi huo.
Shamte ambaye alifukuzwa uanachama wa CCM mwaka 2022 kwa kilichoelezwa kuwa ni kutomheshimu Rais wa Zanzibar, Dkt. Hussein Mwinyi, amesema kama kitu hicho kitaendelea kufichwa, kuna Mawaziri wengine watajiuzulu.
Mwanasiasa huyo ambaye amekuwa akitajwa kuwa na misimamo inayopingana waziwazi na kilichokuwa chama chake (CCM) ameongeza kuwa kujiuzulu kwa Simai ni sehemu ya Demokrasia ya Vyama vingi.
Ikumbukwe, Januari 24, 2024 Simai aliilalamikia Bodi ya Vileo kubadilisha Mawakala wa kuingiza Vinywaji Zanzibar. Januari 26, 2024, Simai aliamua kuachia nafasi yake katika Serikali ya Zanzibar akidai mazingira yake ya kikazi si rafki kwake.