Rais Mwinyi apangua Baraza la Mawaziri

BARD AI

JF-Expert Member
Jul 24, 2018
3,376
8,118
Screenshot_2024-01-27-10-06-26-139_com.instagram.android-edit.jpg

Siku chache tangu aliyekuwa Waziri wa Utalii na Mambo ya kale wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Simai Mohammed Saidi kujiuzulu nafasi hiyo leo, Jumamosi Januari 27.2024 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Hussein Ali Mwinyi amefanya mabadiliko ya Baraza la Mapinduzi kwa kuteua Mawaziri wapya wawili (2) na kumbadilisha Wizara Waziri mmoja (1), pia ameteua Naibu Mawaziri wapya wawili (2) na kumbadilisha Wizara Naibu Waziri mmoja (1)

Taarifa iliyotolewa Ikulu Zanzibar ambayo imesainiwa na Katibu Mkuu Kiongozi na Katibu wa Baraza la Mapinduzi SMZ Mhandisi Zena Ahmad Saidi imeeleza kuwa Rais Mwinyi amemteua Mudriky Ramadhan Soraga kuwa Waziri wa Utalii na Mambo ya kale ambapo kabla ya hapo alikuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Kazi, Uchumi na Uwekezaji, wakati Ali Suleiman Ameir (Mrembo) akiteuliwa kuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais -Ikulu ambapo kabla ya hapo alikuwa Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango

Aidha, Shaaban Ali Othman ameteuliwa kuwa Waziri wa Uchumi wa Buluu na Uvuvi akitokea kuwa Naibu Waziri wa Nishati, Maji na Madini, naye Juma Makungu Juma aliyekuwa Naibu Waziri wa Ardhi na Maendeleo ya Makaazi sasa anakuwa Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango

Mwakilishi wa Viti maalum kutoka kundi la Vijana Kusini Unguja Salha Mohammed Mwinjuma ameteuliwa kuwa Naibu Waziri wa Ardhi na Maendeleo ya Makaazi, wakati Mwakilishi wa Jimbo la Konde, mkoa wa Kaskazini Pemba Zawadi Amour Nassor yeye anakuwa Naibu Waziri wa Maji, Nishati na Madini,

Taarifa hiyo imeeleza kuwa wateule hao wataapishwa kwa Tarehe itakayotangazwa hapo baadaye
 
Zanzibar isingepaswa kuwa na hata hiyo baraza la mawaziri.

Sisi Tanganyika mbona hatuna baraza letu??
 
Mean while bibi kiremba hata aelewi nini ana fanya .. wizara za nishati na kilimo ni utoporo
 
View attachment 2884393
Siku chache tangu aliyekuwa Waziri wa Utalii na Mambo ya kale wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Simai Mohammed Saidi kujiuzulu nafasi hiyo leo, Jumamosi Januari 27.2024 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Hussein Ali Mwinyi amefanya mabadiliko ya Baraza la Mapinduzi kwa kuteua Mawaziri wapya wawili (2) na kumbadilisha Wizara Waziri mmoja (1), pia ameteua Naibu Mawaziri wapya wawili (2) na kumbadilisha Wizara Naibu Waziri mmoja (1)

Taarifa iliyotolewa Ikulu Zanzibar ambayo imesainiwa na Katibu Mkuu Kiongozi na Katibu wa Baraza la Mapinduzi SMZ Mhandisi Zena Ahmad Saidi imeeleza kuwa Rais Mwinyi amemteua Mudriky Ramadhan Soraga kuwa Waziri wa Utalii na Mambo ya kale ambapo kabla ya hapo alikuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Kazi, Uchumi na Uwekezaji, wakati Ali Suleiman Ameir (Mrembo) akiteuliwa kuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais -Ikulu ambapo kabla ya hapo alikuwa Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango

Aidha, Shaaban Ali Othman ameteuliwa kuwa Waziri wa Uchumi wa Buluu na Uvuvi akitokea kuwa Naibu Waziri wa Nishati, Maji na Madini, naye Juma Makungu Juma aliyekuwa Naibu Waziri wa Ardhi na Maendeleo ya Makaazi sasa anakuwa Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango

Mwakilishi wa Viti maalum kutoka kundi la Vijana Kusini Unguja Salha Mohammed Mwinjuma ameteuliwa kuwa Naibu Waziri wa Ardhi na Maendeleo ya Makaazi, wakati Mwakilishi wa Jimbo la Konde, mkoa wa Kaskazini Pemba Zawadi Amour Nassor yeye anakuwa Naibu Waziri wa Maji, Nishati na Madini,

Taarifa hiyo imeeleza kuwa wateule hao wataapishwa kwa Tarehe itakayotangazwa hapo baadaye
Hivi huko hakuna wakristo/wapagani maana naona wote ni waislamu!
 
Mean while bibi kiremba hata aelewi nini ana fanya .. wizara za nishati na kilimo ni utoporo
Ivi wana wizara ya nishati wakati umeme tunawapa bure? Kwa awamu hii wangeachana na baraza la mawaziri huko, lile la muungano linamaliza kila kitu
 
Back
Top Bottom