Juu ya OIC na Mahakama ya Kadhi

Juu ya OIC na Mahakama ya Kadhi

WALIOPITIA Charter ya OIC kiudini wameangalia vipengee vilivyogusa tu maslahi ya Waislamu na kuikosoa Charter kwa kile walichokielewa wao kutokana na hili. Lakini kuna mengi yamo katika 'charter' ambayo yamelenga pamoja na mengine:

. Kumpunguzia umasikini Mtanzania wa kawaida.
. Kuwaondolea wanawake ugumu wa maisha,
. Kuwalea watoto na vijana wetu ili waapukane na madawa ya kulevya, ngono na ukimwi,
. kusaidia biashara ndogondogo na kubwakubwa,
. kuisaidia Tanzania kupata masoko nchi za nje bila kujali mfanyabiashara ni mkiristo au Muislamu kama walivyo wafanyabiashara wengi wa Tanzania (asilimia 76%) ya wanaokwenda Dubai na UAE.
. kutusaidia kujenga miundo mbinu ikiwemo daraja la Kifgamboni ambalo NSSF imejiondoa baada ya kuona Viiongozi wa Kikiristo hawataki Maendeleo ila dini,
. kuhakikisha kuwa hatuingiliwi kimabavu na nchi za nje, uhuru na mipaka yetu vinaheshimika daima dawamu.

Kwa hiyo ninachokiona mimi hapa ni kuwa kwa kila zuri OIC inalotaka kulifanya Wakatoliki, Mapentakoste na Waludherani hawayataki na hawataki wananchi wa nchi hii wafaidike nayo:

1.

In the name of Allah, the most Compassionate, the most Merciful

Wakiristo wanachosema hapa ni kuwa haifai kutaja jina la Mungu katika nia njema, na wala Mungu sio mwenye Rehema wala Huruma!


2.
to be guided by the noble Islamic values of unity and fraternity, and affirming

Wanachosema wenzetu ni kwamba hawataki maadili, umoja wala udugu na Waislamu.

3.
the essentiality of promoting and consolidating the unity and solidarity among
the Member States in securing their common interests at the international
arena;

Hawataki pia kujiunga na taasisi yoyote ile itakayowapa nguvu na uwezo wa kupambana na mataifa makubwa.... Yaani, wakiristo, wabnaamini kuwa sisi kama nchi tuna uwezo wa kutoshirikiana na mashirika yoyote ya kimataifa na tukafanikiwa mambo yetu.....

4.
to adhere our commitment to the principles of the United Nations Charter, the
present Charter and International Law;


Na pia hawatambui kwamba IOC ina baraka za Umoja wa Mataifa.


5.
to preserve and promote the lofty Islamic values of peace, compassion,
tolerance, equality, justice and human dignity;

Na zaidi ya hayo nia njema ya OIC kuchangia katika maadili mema. amani, huruma, uvumilivu, usawa, haki na utu wa mwanadamu vyote hivi havina maana kwa wenzetu.


6.
to endeavour to work for revitalizing Islam’s pioneering role in the world
while ensuring sustainable development, progress and prosperity for the
peoples of Member States;

Misaada na kujitolea kwa OIC kuhakikisha nchi wanachama wanafanikiwa katika masuala ya kiuchumi na kijamii pia ni nongwa kwao. Kote huku wanaona harufu mbaya ya maneno mawili tu: UISLAMU NA WAISLAMU!

7.
to enhance and strengthen the bond of unity and solidarity among the Muslim
peoples and Member States;
to respect, safeguard and defend the national sovereignty, independence and
territorial integrity of all Member States;

Hawataki IOC kusaidia kujenga daraja kati ya nchi za Kiislamu na nchi kama Tanzania kwa sababu za hofu ya Wakiristo kumezwa na Waislamu?


8.
to contribute to international peace and security, understanding and dialogue
among civilizations, cultures and religions and promote and encourage
friendly relations and good neighbourliness, mutual respect and cooperation;

Je, kuna nchi yoyote au mtu yeyote anayepata hasara kwa kuzungumza, kujadili au kuingia katika midahalo na watu wengine. Hivi hatujui kuwa mazungumzo ndio mwanzo wa maendeleo yote?


9.
to promote human rights and fundamental freedoms, good governance, rule of
law, democracy and accountability in Member States in accordance with their
constitutional and legal systems;

Wakiristo hawataki hili pia, yaani, haki za binadamu (kama wao wanavyotaka kuwanyima Waislamu haki zao), uhuru wa kila mtu,utawala bora,utawala wa kisheria,demokrasia na uwajibikaji.....halafu hapo hapo wanaicharura serikali kwa kushinda eti majukumu yake ya msingi. Kuna majukumu makubwa zaidi ya haya.



10.
to promote confidence and encourage friendly relations, mutual respect and
cooperation between Member States and other States;


Hawataki pia kupromoti kuaminiana na urafiki kati yetu. Hivi wakiristo hawa wa miaka hii wana nia njema na sisi kweli?


11.
to foster noble Islamic values concerning moderation, tolerance, respect for
diversity, preservation of Islamic symbols and common heritage and to defend
the universality of Islamic religion;

Kinachosemwa hapa kina ubaya gani. Huku waislamu wanalumiwa kwa Ugaidi na sheria ya ugaidi imeptishwa kwa shinikizo la manasara na Marekani. Hapa IOC inatuambia kuunga mkono Waislamu wasio na siasa kali; wavumilivu; kuheshimu tofauti baina yetu; na kulinda mali na urithi wa Waislamu nini hapa Tatizo? Au wao hawataki kulinda mali na urithi wao?


12.
to advance the acquisition and popularization of knowledge in consonance
with the lofty ideals of Islam to achieve intellectual excellence;

Elimu na maarifa nayo imekuwa nongwa kwa Wakiristo pia siku hizi? Angelifuka Mtakatifu Mtarajiwa wenu Mwalimu Nyerere angeliwaelewa kweli katika hili?


13.
to promote cooperation among Member States to achieve sustained socioeconomic
development for effective integration in the global economy, in
conformity with the principles of partnership and equality;

Hapa tunapewa pia silaha ya kupambana na utandawazi, ajira kwa machinga wetu na kunyanyuliwa biashara ndogo ndogo kwa masoko ya uhakika kwenye nchi za Kiislamu tunakaataa au Wakiristo wanatulazimisha kukataa na sisi tunakubali. Ni viziwi? Ni vipofu? Kwanini?


14.
to preserve and promote all aspects related to environment for present and
future generations;

Wakiristo hawana shida pia ya IOC kutusaidia kulinda mazingira yetu ya bahari yanayoharibiwa (labda kwa sababu waathirika wakubwa ni waislamu?)


15.
to respect the right of self-determination and non-interference in the domestic
affairs and to respect sovereignty, independence and territorial integrity of
each Member State;

Wakiristo wanasema hapana kuhusu suala la kutoingiliwa na mataifa makubwa. Kwa hiyo Marekani ikipenda kwa mujibu wa wenzetu au Waingereza au Wafaransa au wachina basi ruksa kwao wao kutuvamia tu. Mlipinga tusipewe uhuru sasa mnaomba tuvamiwe na mataifa ya nej?


16.
to support the struggle of the Palestinian people, who are presently under
foreign occupation, and to empower them to attain their inalienable rights,
including the right to self-determination, and to establish their sovereign state
with Al-Quds Al-Sharif as its capital, while safeguarding its historic and
Islamic character, and the holy places therein;

Bila shaka kwa kuwa jamaa zetu hapa wanakula sahani moja na Vatican na Mayahudi hili linawaumwa wanaona miji hiyo ni yao na sio yetu. Lakini Haqq itafichika hadi lini?


17.
to safeguard and promote the rights of women and their participation in all
spheres of life, in accordance with the laws and legislation of Member States;

Tunalaumiwa tunakandamiza wanawake wetu. OIC inakuja kutushikisha adabu wakiristo wanakataa sasa mnalaumu nini na mnamlaumu nani ndugu zetu katika Kitabu?


18.
to create conducive conditions for sound upbringing of Muslim children and
youth, and to inculcate in them Islamic values through education for
strengthening their cultural, social, moral and ethical ideals;

Mnadai vijana wetu ndio wezi wakubwa, wavuta bangi, ndio walevi wakubwa, ndio malaya wakubwa, watumiaji madawa ya kulevya, wamejaza magereza yote nchini. Halafu hamuitaki IOC inayokuja kusaidia serikali kupunguza baa hili hivi tuwaelewaje jamaa hawa?
 
Iga,
Kujitangaza tu kuwa ni Taasisi ya Kidini inatosha ku-disqualify Tanzania kujiunga na Jumuiya hiyo maana Katiba yetu iko wazi kuwa Serikali yetu haina dini sasa inatupeleka kwenye Jumuiya za Kidini tukafanye nini? Honi kama ni controvesy? Hapo ndipo mtafaruku ulipo.
 
Kithuku. Mbona UN wanavitengo vyake vingi ambavyo vinafanyakazi zake? Haujasikia UNIDO, Habitat, FAO, WFP n.k ? Mbona kazi zote hawaiachii serikali? Mbona wanashirikiana na serikali, NGO's n.k? Hawa nao wanavitengo vyake ambavyo vitafanya kazi ama kwa kushirikiana na serikali, NGOs au taasisi nyingine. Tatizo liko wapi?

Elewa hili suala Fundi Mchundo, OIC siyo UN. Kumbuka UN haina itikadi ya kidini wala malengo ya kidini ya kulinda na kutetea dini moja. Na kazi zinazofanywa na UN zina baraka za nchi wanachama ambao ndio wachangiaji wake kwa utaratibu wa rasilimali mbalimbali kuanzia fedha hadi watu. Lakini hiyo OIC ni kitu tofauti, ni ya kidini, malengo ya kidini na hayana nafasi sawa kwa watu wa dini nyingine. Huwezi kuajiriwa OIC kama siyo muislamu, bisha nikupe ushahidi sasa hivi! Lakini UN inao utaratibu hadi wa quota, wa kuhakikisha wanachama wake wote wanafaidika kwa namna mbalimbali ikiwamo ya ajira.

Bado nasubiri majibu kutoka kwako kuhusu jinsi malengo ya OIC yanavyoshabihiana na yasivyopingana na malengo ya Tanzania kama taifa.
 
Sina la ziada nadhani umetuelimisha vya kutosha, nachoweza kusema ni kwamba: Idadi ya Waislamu nchini inazidi kila siku na itafika stage ambapo Tanzania itabidi ijiunge na OIC kwani nguvu ya Waislamu itazidi upinzani juu ya hoja hii.....ndugu zangu waislam tuwe na subira na tuepushe shari kwani iko siku Inshallah tutajiunga na OIC na hawa wenzetu wataona manufaa yanayopatikana kutokana na kujiunga na organisation hii.
 
Elewa hili suala Fundi Mchundo, OIC siyo UN. Kumbuka UN haina itikadi ya kidini wala malengo ya kidini ya kulinda na kutetea dini moja. Na kazi zinazofanywa na UN zina baraka za nchi wanachama ambao ndio wachangiaji wake kwa utaratibu wa rasilimali mbalimbali kuanzia fedha hadi watu. Lakini hiyo OIC ni kitu tofauti, ni ya kidini, malengo ya kidini na hayana nafasi sawa kwa watu wa dini nyingine. Huwezi kuajiriwa OIC kama siyo muislamu, bisha nikupe ushahidi sasa hivi! Lakini UN inao utaratibu hadi wa quota, wa kuhakikisha wanachama wake wote wanafaidika kwa namna mbalimbali ikiwamo ya ajira.

Bado nasubiri majibu kutoka kwako kuhusu jinsi malengo ya OIC yanavyoshabihiana na yasivyopingana na malengo ya Tanzania kama taifa.

Mbona nimeishakujibu? Sasa wewe unayejua sera za taifa tubandikie humu hizo sera zinasemaje na sio kujificha nyuma ya kivuli. O.I.C. kama ilivyo UN, EU, Jumuia ya Madola, AU n.k. ni chombo kinachounganisha mataifa yaliyo huru. Kazi zinazofanywa na OIC nazo zina baraka za wanachama wake.

Si tu kuwa hauwezi kuajiriwa katika OIC kama sio muislamu basi hata kama umeoa au kuolewa na asiye muislamu. Mimi hili toka mwanzo nililiweka wazi lakini kwa sababu umekaa kiubishi basi hausomi yanaoyoandikwa bali unachagua vijisehemu vinavyokupendeza.

Umeuliza maswali nimekujibu. Langu mbona hautaki kujibu. Ni vipi wale wasio waislamu watakavyodhulumika kwa sisi kujiunga na chombo hiki? Toa migfano halisi na sio blah blah za kuwa ati dini moja itakuwa inapendelewa. Kama unaona itakuwa inapendelewa tuambie basi watapendelewa vipi?

Naona unanipotezea muda.
 
Sina la ziada nadhani umetuelimisha vya kutosha, nachoweza kusema ni kwamba: Idadi ya Waislamu nchini inazidi kila siku na itafika stage ambapo Tanzania itabidi ijiunge na OIC kwani nguvu ya Waislamu itazidi upinzani juu ya hoja hii..... subira na tuepushe shari kwani iko siku Inshallah tutajiunga na OIC na hawa wenzetu wataona manufaa yanayopatikana kutokana na kujiunga na organisation hii.

Tanzania haijiungi na OIC kwa nguvu ya Waislamu.Bali tu kama Katiba ya nchi inayotuongoza na ndio mhimili mkuu wa nchi ikiandikwa upya na kuingiza humo majukwaa ya Uislamu,Ukristo,ubhuda,ubahahi,usayuni,upagani,urastafariani n.k.
 
Sina la ziada nadhani umetuelimisha vya kutosha, nachoweza kusema ni kwamba: Idadi ya Waislamu nchini inazidi kila siku na itafika stage ambapo Tanzania itabidi ijiunge na OIC kwani nguvu ya Waislamu itazidi upinzani juu ya hoja hii.....ndugu zangu waislam tuwe na subira na tuepushe shari kwani iko siku Inshallah tutajiunga na OIC na hawa wenzetu wataona manufaa yanayopatikana kutokana na kujiunga na organisation hii.

Eti nini????
ina maana sasahivi wakristo, wabudha, wapagani na wengine wameacha kuzaa??au rate ya kuzaa kwa waislamu ni kubwa compared to others?
halafu hapa inaonekana wazi kabisa katika kila bandiko la muislamu, hata mazungumzo ya waislamu kuanzia kwenye vyombo vya habari mpaka vijiweni, ni dhahiri kuwa wanatetea kujiunga OIC si kwa faida yoyote kitaifa isipokuwa ni kwa maslahi yao binafsi.hivi somalia,djibout na sudan kwa uchache ni wanachama wa OIC, mbona hayo manufaa mnayotaka kutuaminisha kuwa tutayapata tukijiunga OIC tutayapata mbona hatuyaoni??OIC itatuleteaje amani wakati somalia,djibout,eritrea,sudan(kusini na darfur),uganda kaskazini watu wanuana kila kukicha.OIC wako wapo ku-promote peace & harmony???
hapa kuna agenda ya siri, kati ya waislamu, serikali na OIC.
kwahiyo basi maadam nchi ni yetu sote tuna haki ya kutoa maoni yrtu na kuchagua jumuia/mataifa ya kushirikiana nayo.
namalizia kwa kuwataka wale mnaotaka tujiunge na OIC, muwaeleze OIC wasaidie kuleta amani na maendeleo somali,djibout,eritrea,afghanistan,sudan na uganda kisha waje kutushawishi kujiunga nao.
 
Nakubali kwamba katiba ndio inaendesha nchi lakini narejea kauli yangu na kusema kwamba Waislamu wanazidi kwa kasi mno na itafika stage ambapo hata katiba yetu itakuwa ammended ili kutupa fursa ya kujiunga na umoja huu....kujiunga na OIC ni "maendeleo"(rejea post ya iga) na nasikitika kutambua kwamba kuna watanzania wenzangu wanapinga maendeleo ya nchi?! Inabidi mfahamu kwamba kujiunga na OIC ni tendo ambacho hakiwezi kufanya nchi hii iwe ya kiislamu bali itatambulika kwamba ni mmoja kati ya nchi yenye waislamu walio na msimamo....na sisi tunataka msimamo wetu uonekane!!! Nadhani tunahitaji kufanya referendum juu ya swala hili....kwani ni zito na linahitaji uamuzi wa wananchi wote!
 
Nakubali kwamba katiba ndio inaendesha nchi lakini narejea kauli yangu na kusema kwamba Waislamu wanazidi kwa kasi mno na itafika stage ambapo hata katiba yetu itakuwa ammended ili kutupa fursa ya kujiunga na umoja huu....kujiunga na OIC ni "maendeleo"(rejea post ya iga) na nasikitika kutambua kwamba kuna watanzania wenzangu wanapinga maendeleo ya nchi?! Inabidi mfahamu kwamba kujiunga na OIC ni tendo ambacho hakiwezi kufanya nchi hii iwe ya kiislamu bali itatambulika kwamba ni mmoja kati ya nchi yenye waislamu walio na msimamo....na sisi tunataka msimamo wetu uonekane!!! Nadhani tunahitaji kufanya referendum juu ya swala hili....kwani ni zito na linahitaji uamuzi wa wananchi wote!

Kwa hiyo waislamu wakizidi kuwa wengi ndio wawaburuze raia wengine? Buasara wapi ndg?

Hapa kutachimbika ndg usione simba kalala ukazani ni pakamwitu...Ohooo..
 
Nakubali kwamba katiba ndio inaendesha nchi lakini narejea kauli yangu na kusema kwamba Waislamu wanazidi kwa kasi mno na itafika stage ambapo hata katiba yetu itakuwa ammended ili kutupa fursa ya kujiunga na umoja huu....kujiunga na OIC ni "maendeleo"(rejea post ya iga) na nasikitika kutambua kwamba kuna watanzania wenzangu wanapinga maendeleo ya nchi?! Inabidi mfahamu kwamba kujiunga na OIC ni tendo ambacho hakiwezi kufanya nchi hii iwe ya kiislamu bali itatambulika kwamba ni mmoja kati ya nchi yenye waislamu walio na msimamo....na sisi tunataka msimamo wetu uonekane!!! Nadhani tunahitaji kufanya referendum juu ya swala hili....kwani ni zito na linahitaji uamuzi wa wananchi wote!

my friend you got it very very wrong!!!!
hebu niambie with evidence kuwa rate ya kuzaana waislamu ni kubwa kuliko wengine.
pili uniambie hayo maendeleo unayoyazungumzia ni yapi??hivi ni nchi ngapi wanachama wa oic ni maskini wa kutupwa???na oic imechukua hatua gani kuwasaidia wanachama wake?hivi kwa ulinganifu mdogo tu kati ya wanachama wa oic na wasio wanachama ni nchi zipi zenye mauaji na vita visivyoisha?ni nchi zipi zenye maendeleo??
 
Maendeleo gani yatapatikana? Kama OIC wana mahela, ruhusa tu kuyaleta wayamwage Bongo kama Serikali ya Japan inavyomwaga mamisaada, na si lazima iwe kwamba kwanza tujiunge nayo (OIC). Kama masharti ya misaada ni kujiunga kwanza, basi hatutaki kabisa, na hakika patachimbika hapa nchi ikijiunga OIC!
 
Kithuku,Fundi Mchundo,Mkandara,FMES,Mwanakijiji,Game-Theory,AbdulK,Opaque,Mwita,..

..nadhani tumeshajadiliana kiasi cha kutosha suala la OIC.

..nadhani kila upande umetoa hoja nzito na zenye ushawishi wa hali ya juu kabisa.

..itafika wakati serikali itachukua uamuzi ambao inawezekana usiupendezeshe upande mmoja wapo.

..i would want you to step back, halafu mfikirie lugha ya kuwatuliza wale ambao wako-against au pro OIC, wakati serikali itakapotoa uamuzi.

..say, Kithuku umekuwa ukipinga Tanzania kujiunga na OIC. nipe kauli/sababu/nasaha ambazzo utaitumia kuwatuliza wale wanaokuunga mkono.

..hivyo hivyo Fundi Mchundo umekuwa ukiunga mkono Tanzania kujiunga na OIC. nipe kauli/nasaha utakazotumia kuwatuliza wale wanaokuunga mkono ikiwa serikali itachukua uamuzi tofauti na matakwa yao.

..huu mjadala umekuwepo kwa zaidi ya miaka 10 sasa. nadhani umefika wakati wa kuangalia jinsi ya kuvuka dharuba hii, huku nchi ikiendelea kuwa na amani na mashirikiano baina ya dini mbili za Waislamu na Wakristo.
 
Nakubali kwamba katiba ndio inaendesha nchi lakini narejea kauli yangu na kusema kwamba Waislamu wanazidi kwa kasi mno na itafika stage ambapo hata katiba yetu itakuwa ammended ili kutupa fursa ya kujiunga na umoja huu....kujiunga na OIC ni "maendeleo"(rejea post ya iga) na nasikitika kutambua kwamba kuna watanzania wenzangu wanapinga maendeleo ya nchi?! Inabidi mfahamu kwamba kujiunga na OIC ni tendo ambacho hakiwezi kufanya nchi hii iwe ya kiislamu bali itatambulika kwamba ni mmoja kati ya nchi yenye waislamu walio na msimamo....na sisi tunataka msimamo wetu uonekane!!! Nadhani tunahitaji kufanya referendum juu ya swala hili....kwani ni zito na linahitaji uamuzi wa wananchi wote!

Inawezekana ndio mkakati waislamu wamejiwekea .....Lakini ku-outnumber wakristo kwa idadi tu haitoshi, inabidi muhakikishe vile vile watoto wanaozaliwa wanapata elimu nzuri, familia zinajishughulisha kuinua kipato chao n.k....
 
Eti nini????
ina maana sasahivi wakristo, wabudha, wapagani na wengine wameacha kuzaa??au rate ya kuzaa kwa waislamu ni kubwa compared to others?
halafu hapa inaonekana wazi kabisa katika kila bandiko la muislamu, hata mazungumzo ya waislamu kuanzia kwenye vyombo vya habari mpaka vijiweni, ni dhahiri kuwa wanatetea kujiunga OIC si kwa faida yoyote kitaifa isipokuwa ni kwa maslahi yao binafsi.hivi somalia,djibout na sudan kwa uchache ni wanachama wa OIC, mbona hayo manufaa mnayotaka kutuaminisha kuwa tutayapata tukijiunga OIC tutayapata mbona hatuyaoni??OIC itatuleteaje amani wakati somalia,djibout,eritrea,sudan(kusini na darfur),uganda kaskazini watu wanuana kila kukicha.OIC wako wapo ku-promote peace & harmony???
hapa kuna agenda ya siri, kati ya waislamu, serikali na OIC.
kwahiyo basi maadam nchi ni yetu sote tuna haki ya kutoa maoni yrtu na kuchagua jumuia/mataifa ya kushirikiana nayo.
namalizia kwa kuwataka wale mnaotaka tujiunge na OIC, muwaeleze OIC wasaidie kuleta amani na maendeleo somali,djibout,eritrea,afghanistan,sudan na uganda kisha waje kutushawishi kujiunga nao.

Asilimia kubwa ya nchi hii ni Waislam, yani Tanzania Bara na Visiwani kwa hio obviously Birth Rate ya Waislam itakuwa higher ukiweka na factors zingine kama Uislamu unavyoruhusu kuoa mke zaidi ya mmoja....maximum ni wanne. Halafu pia hivi sasa tuna watu wengi ambao wanasilimu na kuukubali Uislamu kuliko wakati wowote kwenye historia yetu(Source: islamic propagation centre). Ni uwongo kwamba sisi tunataka kujiunga na OIC kwa ajili ya maslahi yetu, je ni maslahi gani hayo? yaweke wazi ili na sisi tujue! Nchi za Sudan, Somalia na Djibouti ziko kwenye vita kwa ajili ya ukabila na sio udini...kwa nini unahoji uwezo wa OIC kuzisaidia nchi hizi na uihoji Umoja wa Mataifa(UN), au nchi hizi haziko kwenye umoja huo? UN ina nguvu kuliko OIC, OIC ni bado changa na inahitaji mchango wa nchi kama Tanzania ili iweze kutimiza agenda zake. Uganda ina matatizo kwa ajili ya Rebel Force army ijulikanayo kama LRA(Lords Resistance Army) ambayo inaongozwa na wakristo na si waislamu, hapo pia ninaomba ungeihoji UN au hoji Umoja wa Africa Mashariki (EAC)! Afghanistan ilivamiwa na Marekani na Uingereza ambazo ni mmoja kati ya nchi zinazopiga vita Uislam, na Wa-afghani wanahaki ya kutetea ardhi yao na uhuru wao na pia OIC iko 'against' conflict katika nchi zote ulizotaja na inajitahidi kadri iwezayo kutatua matatizo yaliokumba nchi hizi. Ninawashauri watanzania wenzangu kujiunga na OIC ili wote tusimame na tutokomeze uonevu, umasikini, ufisadi na matatizo yote yanaetukumba sisi nchi masikini!
 
Kwa hiyo waislamu wakizidi kuwa wengi ndio wawaburuze raia wengine? Buasara wapi ndg?

Hapa kutachimbika ndg usione simba kalala ukazani ni pakamwitu...Ohooo..

Kuna Busara mbele ya Haki na Nguvu ya Umma? Hamuwezi kuiendesha nchi hii kama ni ya kikristo, enzi hizo zimeshapita! hii ni nchi ya wote na hata sisi waislamu tuna haki ya kutetea mapendekezo yetu.

Tutaona nani ndio Simba na nani ndio Paka Mwitu!
 
Kwa hiyo waislamu wakizidi kuwa wengi ndio wawaburuze raia wengine? Buasara wapi ndg?

Hapa kutachimbika ndg usione simba kalala ukazani ni pakamwitu...Ohooo..

Kuna Busara mbele ya Haki na Nguvu ya Umma? Hamuwezi kuiendesha nchi hii kama ni ya kikristo, enzi hizo zimeshapita! hii ni nchi ya wote na hata sisi waislamu tuna haki ya kutetea mapendekezo yetu.

Tutaona nani ndio Simba na nani ndio Paka Mwitu!
 
my friend you got it very very wrong!!!!
hebu niambie with evidence kuwa rate ya kuzaana waislamu ni kubwa kuliko wengine.
pili uniambie hayo maendeleo unayoyazungumzia ni yapi??hivi ni nchi ngapi wanachama wa oic ni maskini wa kutupwa???na oic imechukua hatua gani kuwasaidia wanachama wake?hivi kwa ulinganifu mdogo tu kati ya wanachama wa oic na wasio wanachama ni nchi zipi zenye mauaji na vita visivyoisha?ni nchi zipi zenye maendeleo??

Nooooo my friend...I am defending my ideal, so I am right!
Soma bandiko langu la juu utapata jibu lako.
Naona tusubiri mwafaka wa serikali juu ya hili jambo.....ama sivyo tutabishana milele hapa.
 
Sakata la OIC

Habari Zinazoshabihiana
• Ndugu wa marehemu Mgaya wajipanga kwenda mahakamani 31.03.2008 [Soma]
• Sakata la ujambazi MbeyaWanahabari wawekwa 'kikaangoni' 29.03.2007 [Soma]
• Tume ya Bomoabomoa Tabata Dampo yakabidhi taarifa 29.03.2008 [Soma]

Masheikh Dar:Msimamo wa maaskofu ni ugaidi

Na Gaudence Massati

BARAZA Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA) mkoa wa Dar es Salaam limewaonya maaskofu wa Jumuiya za Kikristo Tanzania (CCT) kutoitisha Serikali katika suala la kujiunga na Jumuiya ya Kiislamu (OIC) na kuanzisha Mahakama ya Kadhi nchini wakitishia kuwa kitendo hicho ni uhafidhina na ugaidi.

Tamko hilo limetolewa na Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam, Sheikh Mussa Salum kwa waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, mara baada ya kikao cha masheikh na maimamu wa mkoa huo kujadili pamoja na mambo mengine, kauli ya maaskofu hao.

"Waislamu tunasema suala la Tanzania kujiunga ama kutojiunga ni suala la Serikali ya Tanzania kwa maslahi ya wananchi wote," alisema Sheikh Salum.

Sheikh Salum aliongeza kuwa suala la Mahakama ya Kadhi ni haki ya Waislamu wa nchini na wala halina mjadala kwa kuwa haliwahusu watu wa dini nyingine na kwamba mifano mingi ipo katika nchi mbalimbali juu ya kuwepo kwa mahakama hizo.

"Mahakama hizi zilikuwepo tangu ukoloni, hivyo hili siyo suala la kuomba kuanzishwa kwake bali tunaiomba Serikali izirejeshe," alisema.

Pia masheikh na maimamu hao walihoji uhalali wa kuwepo kwa Balozi wa Vatican hapa nchini kuwa anawakilisha nchi gani na kuliita kuwa suala hilo limegubikwa na udini lakini Waislamu hawakuwa wakihoji.

"Tunawaonya maaskofu kuacha kuishinikiza Serikali mara kwa mara kuhusu masuala yanayohusu Waislamu na waache kupandikiza chuki kwa waumini wao juu ya suala la OIC na Mahakama ya Kadhi na waumini wa dini ya kiislamu kwa ujumla," alisema.

Mwishoni mwa wiki iliyopita maaskofu 64 wa makanisa mbalimbali nchini walisaini waraka wa kumpinga Waziri Membe aliyekaririwa awali akiwataka Watanzania kutoogopa kujiunga na OIC kwani ni jumuiya yenye maslahi mazuri ya kiuchumi kwa taifa, akikariri utafiti uliofanywa na Serikali.

Tayari BAKWATA makao makuu imeshatangaza kuitisha mkutano wa hadhara utakaofanyika kwenye viwanja vya Kidongo Chekundu kesho kueleza msimamo wake kuhusu suala hilo.
 
Back
Top Bottom