Juu ya OIC na Mahakama ya Kadhi

Juu ya OIC na Mahakama ya Kadhi

.......kwi kwi kwi kwi kwi.......very interesting.........


for real, I had four questions and the one you are asking is among them. Mswahili utamjua tu... he he he heeeeeee. So hakuna ubaya hata wakijiunga na jumuiya yeyote ile as long as sio kila mmoja anaridhishwa na katiba ya nji hii mbee.
 
Kaka hili ndio tatizo. Kwa kuwa napishana mawazo nawe haina maana kuwa nimsaliti. Kwa kuwa nasema kuwa alichokifanya Membe ni kutekeleza wajibu wake kama Waziri wa Mambo ya Nje haina maana kuwa mimi ni mmoja wa wanamtandao walio- MGARAGAZA Mzee wetu kule CHIMWAGA. Na ukweli ni kuwa Chimwaga hakukuwa na wizi wa kura. Kilichotokea ni wafuasi wa Mzee Malecela walipoona ulaji wao unaondoka wakakubali yaishe na kufanya deal na JK wakiogopa kutengwa kimaslahi. Ndio hasara ya kufanya siasa katika KUNDI FISADI chini ya MFUMO FISADI

Mzee wa PHD kama ninavyosema kila wakati, ukitaka mjadala wa ksitaarabu nitakupa na ukitaka hizi nyepesi nyepesi pia sina noma, kutokubaliana kwangu na mgombea wako wa UV-CCM, hakuna uhusiano wowote na hii ishu, ya Dodoma hayana anything to do na haya ya ndugu zako mafisadi kutaka kutuingiza kwenye mashirika ya kiisialmu, uongozi waliouiba umewashinda sasa wanajaribu kutugawa a nation na ishu za kidini kama alivyofanya Idd Amini aliposhindwa kuongoza, kwanza aliwaingiza Wa-Ganda OIC halafu akakimbilia Saudia na nidvyo mnavyotaka kutupeleka sasa ndio maana kuna watu kama mimi hatukubali huu upuuzi, Malecela baba yako ame-retire anakula pension hahusiki na haya yenu mafisadi, wananchi wamechoka ndio maana mmekula kipigo Tarime, na ndio mwanzo huo sasa mmeshidnwa Tarime mnataka kutudanganya na OIC, nevr ndugu yangu!Malecela hayumo infact anajitayarisha kwa ziara ndefu ya mwezi mmoja na nusu Europe na USA, ambako pamoja na mengine atashirki sana kutoa speech katika midahalo mbali mbali kwenye vyuo vikuu huko, na pia kushirki kwenye sherehe za kusimiwka kwa rais mpya huko USA.

Na hili suala la kumhusisha dogo Beno na kina Lowassa just t because anaonekana kikwazo kwa kijana wa Mzee Malecela and other disgruntled old and young guards katika chama "CHENU" sio uana-demokrasia wala uanasiasa bora tunaojidai kuupigia kelele hapa. I stand to be corrected kaka...hakuna mkono wa MAFISADI MAARUFU nyuma ya ugombea wa BENO MALISA...

Bwa! ha! ha! ha! ah! ha! mbona una hasira na mimi ndugu yangu toka niseme wazi kua mgombea wako ni mgombea wa Lowassa? Malecela alisha-retire hahusiki nyinyi mafisadi nchi imewashinda huko OIC hatuendi mtaenda wenyewe, this time hakuna kusingizia Malecela ngoma imewashinda wenyewe, milifikiri utawala ni mchezo, sasa dawa ni kujitoa tu kwenye uongozi mle vizuri mali zenu za ufisadi, uongozi hamuwezi lakini kuna wa-Tanzania wenmgi wenye uwezo bro! hizo dinari za mafisadi huko Iran zitawatokea puani mwaka huu!

Mwenzio ndugu yangu naangalia siasa kama proffesion yangu na sio maslahi yangu wala emotions...i wish nawe ungejitahidi kufanya hivyo ukizingatia unajianda kwenda kupambana na bingwa wa longolongo LUSINDE mdogo (najua hana undugu na JOB) ambaye Mzee Malecela alimkatia kidogo pamoja na kumuahidi kumwachia ufalme wa ijijini MTERA....Nipo maeneo yako kaka nitakutafuta siku za karibuni tuendelee na mijadala...

sijakuuliza mahali ulipo maana ninapajua, pukipsi sio Dodoma mzee wa PHD, hakuna watu wenye PHD huko unakosema jaribu kua mtu mzima, sio nia yangu kuharibu kitumbua cha brother wetu Beno, ila ilikuwa kuwafahamisha wananchi tu ukweli na naona imefanya kazi maana since then kilio kikubwa sana, Lusinde alinyimwa hela za kugombea na chama chake, Mazengo aliyetumwa na Kusila na mafisadi wenzako aliishia kuwa kichekesho, sasa na wewe utagomeba wapi ndugu yangu huko kwenu Moshi watu wote wana akili huwezi danganya mtu ndio maana mnakimbilia Vijana maana mnajua kua kule kwa Ndesamburo hakuna kitu, pole sana bro lakini ukweli lazima usemwe hata kama mnatumwa na mafisadi kuja kutuvuruga hapa JF hatuwaogopi!

na OIC hatuingii never, toka majuzi Membe anahangaika ndio matatizo ya kukurupuka, mmepigwa Tarime na huku kwenye OIC nako tutawapiga tena kama watoto, mafisadi wakubwa wa taifa hili.
 
Sasa kama tunataka kujiunga na OIC kwa maslahi ya kiuchumi naomba kujibiwa hapa.

1. Ni maslahi gani ambayo yapo OIC ambayo hatujayapata/au hayamo kwenye SADC, COMESA, EAC, COMMONWEALTH ambako sisi ni wanachama?

SASA HIVI KUNA JITIHADA ZA KUPUNGUZA MEMBERSHIP KWENYE HIZI REGIONAL BLOCKS NA NDO MAANA TUMEONDOKA COMESA.

Jamani tuache emotions hoja ijibiwe kwa hoja.

What do we want exactly as a country when we join OIC??? Kimsingi mimi napinga hizi hoja mfu! Tuambiwe ni kwa nini tunataka kuingia OIC...kama nchi tumepata nini kwa hizi organization ambazo tumo tayari? na OIC tutapata nini amabcho sasa hivi hatukipati!

Hao member wa OIC wenyewe wamechoka tuu kama sisi...ndo akina Sudan, Iran, Iraq et al! watatupa nini? zaidi ya migogoro? we have enough problems guys.

We should strive for strategic partnership..tuachane na hizi blah blah za kisiasa.

Saafi sana, maana sometimes inachosha kusoma pumba na hewa za mtu mmoja akibadili badili majina kama mtoto mdogo akidhani sisi wote hapa ni watoto kama yeye watu wengine bwana miaka 60 bado mtu ana behave kama ten years old, sijui ni ugonjwa wa aina gani huu, sijawahi kuona maishani mwangu!
 
Fundi mbona unasisitiza tu kujiunga na OIC bila kunijibu maswali yangu haya:
1. Je Tanzania kama taifa inayaamini na kuyakubali malengo ya OIC kama yalivyobainishwa kwenye charter yao?
2. Watanzania, pamoja na wewe, tuko tayari kushiriki kutekeleza malengo yote yaliyobainishwa humo?
3. Ni sahihi kwa Tanzania kama nchi yenye watu wenye dini mbalimbali kujiunga na kufungwa na maazimio na makubaliano yanayopendelea dini moja tu?

Na hebu tuambie, hiyo OIC charter umeisoma au unashabikia tu kwa sababu kama zile za Bernad Membe?



Kithuku.

Nimeisoma charter ya OIC (pengine kabla yako) na nilikuwa mmoja wa waliobandika link humu mapema tu. Muulize Mkandara.

Hayo ya Membe siyajui wala mimi si mshabiki wake.

Kuhusu maswali yako:

1. Nani anayeweza kuzungumzia utashi wa taifa la Tanzania? Kwani hao waislamu wanaokubaliana na malengo yote katika OIC hawamo katika taifa letu? Hatuwezi kujidai kuwa tu wazungumzaji wa taifa lilo diverse kama la kwetu. Ndiyo maana tumechagua wawakilishi kutuzungumzia. Lakini wao ni binadamu, na kunasema wanakosea. Hilo linaeleweka.

Ni lazima tuelewe kuwa kujiunga katika chombo chochote si lazima ukubaliane na YOTE yaliyomo katika katiba yake. As long as unakubaliana na mwelekeo wake in general basi kuna sehemu unaweza kuzimezea. Mimi ninavyoelewa ni kuwa lengo kuu la OIC ni kuleta maendeleo na mshikamano kwa waislamu na si ku proselytize wasio waislamu kujiunga na dini hiyo. Wenzangu mmeona hiyo ya pili zaidi wakati mimi nimeona ya kwanza. Sasa kwa nini nimpinge mtu anayetaka kuwainua ndugu zangu waislamu?

2. Kwani watanzania wote tunakubali kutekeleza malengo yote yaliyo kwenye FIFA? Hata sisi wapenzi wa kriketi! Kama hautaki hautalazimishwa. Ni haki yako kama mtanzania kukataa kupeleka watoto wako kusoma katika shule iliyojengwa na pesa kuto OIC:


3. Nani amesema kuwa wasio waislamu watafungwa na maazimio ya OIC? Kama nilivyosema hapo awali, mbona sisi wapenzi wa kriketi hatufungwi na maazimio ya FIFA?

Sasa wewe nijibu mimi:

Niambie kama usie muislamu utaathirika vipi kwa kujiunga kwetu na chombo hicho? Unipe mifano rahisi.

Amandla.................................
 
nami naungana na wote wanaomtaka waziri Membe ajiuzuru mara moja ili kulinda heshima ya nchi, Katiba na viapo vyote vya uwaziri na ubunge wake.

Namtaka aondoke kwani kwa makusudi ameamua kuivunja katiba ya nchi ambayo aliapa kuilinda, na kuitetea popote pale, ni mlevi wa madaraka wa wazi ambaye kwa masikio yangu nilikuwa namsikiliza akiongea na wanahabari juu ya hilo.

Huyo ni mvunjaji wa katiba wa waziwazi ambaye hana tofauti na mtoa rushwa au mpokea rushwa na mbaya zaidi huyo anatishia hata uhuru, utawala wa sheria na zaidi ulinzi wa amani.

Mkuu FDR,

Heshima mbele kaka, maneno yako mazito sana na ubarikiwe.

Ingawa sasa wengi tuna swali moja muhimu nalo ni nani anamtuma Membe maana kuna somebody behind hii kitu kuna mtu amemtuma ni nani huyo?
 


............Ni lazima tuelewe kuwa kujiunga katika chombo chochote si lazima ukubaliane na YOTE yaliyomo katika katiba yake. As long as unakubaliana na mwelekeo wake in general basi kuna sehemu unaweza kuzimezea. Mimi ninavyoelewa ni kuwa lengo kuu la OIC ni kuleta maendeleo na mshikamano kwa waislamu na si ku proselytize wasio waislamu kujiunga na dini hiyo. Wenzangu mmeona hiyo ya pili zaidi wakati mimi nimeona ya kwanza. Sasa kwa nini nimpinge mtu anayetaka kuwainua ndugu zangu waislamu?.................................

Mkuu Fundi............usigeneralise kwa kusema si lazima kukubalina na mambo YOTE............hapo ndipo unapofanya kosa la kiufundi............. specifically kuna issue za IMANI ndio zilizopelekea uanzishwaji wa umoja huo and nothing else.................na huwezi kulinganisha masuala ya imani na mambo ya FIFA na sijui Kriketi...........mambo ya imani ni beyond michezo Mkuu wangu..........i know you know better than what you just presented..............

pili hakuna chombo chenye Calibre ya OIC kitakachosema ktk moja ya objectives zake kuwa ni ku-proselytize watu to dini ya aina yeyote............kama vipo basi ni mufilis......na havifai.........however people are reading the objectives of any organisation with deeper eyes.......kuna mtu aliweka hizo objectives na ku-highlight vipengele ambavyo nafikiri most of wapinzani wa OIC wanahitaji clarifications.......and yet no one came across to enlighten those doubts...........and trust me those doubts, you and me, Membe and his crew or someone from OIC............need to come forward and enlighten the people of this country...........
 
Vipi mzee Mwanakijiji mbona unaegemea upande mmoja. Kuna makala kadhaa sizioni hapa katika string hii imekuwaje. Au ndio tayari kuna mtu analipwa na kanisa na Vatican?????
 
Mzee wa PHD kama ninavyosema kila wakati, ukitaka mjadala wa ksitaarabu nitakupa na ukitaka hizi nyepesi nyepesi pia sina noma

Malecela hayumo infact anajitayarisha kwa ziara ndefu ya mwezi mmoja na nusu Europe na USA, ambako pamoja na mengine atashirki sana kutoa speech katika midahalo mbali mbali kwenye vyuo vikuu huko, na pia kushirki kwenye sherehe za kusimiwka kwa rais mpya huko USA.


sijakuuliza mahali ulipo maana ninapajua, pukipsi sio Dodoma mzee wa PHD, hakuna watu wenye PHD huko unakosema jaribu kua mtu mzima

sasa na wewe utagomeba wapi ndugu yangu huko kwenu Moshi watu wote wana akili huwezi danganya mtu ndio maana mnakimbilia Vijana maana mnajua kua kule kwa Ndesamburo hakuna kitu, pole sana bro lakini ukweli lazima usemwe hata kama mnatumwa na mafisadi kuja kutuvuruga hapa JF hatuwaogopi!

na OIC hatuingii never, toka majuzi Membe anahangaika ndio matatizo ya kukurupuka, mmepigwa Tarime na huku kwenye OIC nako tutawapiga tena kama watoto, mafisadi wakubwa wa taifa hili.

Kaka kwanza napenda kukutaarifu rasmi kuwa mimi sio huyo unayemdhania...Ukweli ni kuwa tunajuana na mimi na wewe tukiwa nje ya Jamboforum tunaelewana vizuri. NAKUSHAURI UFANYE UCHUNGUZI WAKO WA NGUVU ILI USIJE UKASHANGAA HIVI KARIBUNI NITAKAPOJITAMBULISHA KWAKO RASMI.

Beno ni mdogo wangu na namchukulia hivyo na wala sio mgombea wangu kwani hadi leo hii sijawahi kuwa na uanachama wa chama chochote nchini. Actually ninaamini kuwa CCM ni tatizo kwa mustkabali wa Tanzania na hivyo kinapaswa kupumzishwa kijikoshe uozo wa utamaduni wa kifisadi na kiweze kujisafisha kifalsafa. Tofauti yangu na wewe ni kuwa mimi namjua Beno wakati wewe humjui. Ndugu yangu huwezi ukakwepa kuwa taarifa zako kuhusu BENO ni nyepesinyepesi mno na zinategemea vibomu vya ndugu yetu SAIDI KUBENEA na wafuasi wa Mzee wetu MALECELA ambao wanamuona BENO kama kikwazo cha kuirudisha mikononi CCM kupitia kwa kijana wao NAPE NNAUYE. Ni wazi hata mimi nisingeweza kuacha kumuunga mkono NAPE ukitilia maanani siasa za kimakundi CCM na loyalty yake kwa Mzee Malecela. Na katika kufanya hivyo ni wazi nitakuwa vulnerable na siasa chafu dhidi ya Beno hata kumhusisha na MAFISADI MAARUFU kina LOWASSA and Co. UNLIMITED.

Kuhusu Mzee Malecela mimi namheshimu kwa hekima na upeo wake mkubwa wa siasa na masuala ya kidunia na pia natambua utumishi wake uliotukuka kwa Taifa letu. Tatizo mimi ni wale unaweza kuwaita Nyerereist (naamini katika ujamaa) hivyo natofautiana naye kimtazamo na sio yeye kama Mzee wetu. Ofcourse i cant take his current family partner....

Kuhusu kugombea kaka mimi bado naamini kuitumikia Tanzania kivulini na sio lazima niwe fulani. What matters ni mchango gani natoa na sio nina uheshimiwa gani. Kama nitagombea na hili bado ni wazo legelege tu, nitaanzia ngazi ya chini...labda UDIWANI na sio kukimbilia UBUNGE kama tunavyodhani vijana wengi wa kizazi cha MTANDAO...

Kuhusu hili la OIC nashindwa kutambua kama unapinga kama MTANZANIA ama MKRISTU. Na hili nadhani ndio tatizo kubwa tulilonalo ingawa wengi tunapenda kukimbilia kuwashutumu wao (Waislamu) kuwa wanaunga mkono kwa kutilia maanani maslahi yao kama waislamu tu. Nadhani tofauti na wananchi walivyo, msimamo wa serikali, ndio unaangalia zaidi maslahi ya nchi.

Na suala hili haliihitaji uhusika wa baraza la mawaziri wakati Wizara ya Mambo ya Nje ndiyo iliyokabishiwa ba katiba ya jamhuri ya muungano jukumu la kuandaa, kutekeleza na kusimamimia utekelezaji wa Sera Ya Mambo ya Nje ambayo ilipitishwa na Baraza la mawaziri. Kusema kuwa hili lnahitaji baraka za wananchi ama bunge ni kumpokonya madaraka halali Waziri wa Mambo ya Nje. Ni rais tu ndiye anayepaswa kuingilia utekelezaji huo kwa kushauriana na waziri husika ambaye kwa hivi sasa tupende tusipende ni Bernard Membe.

Siamini kama ni busara kuachia religious sentiments za wananchi kudetermine utendaji kazi wa serikali. Nadhani kama kuna mtu anaona kuwa serikali iliyopo madarakani haiheshimu MASLAHI YAKE YA KIDINI (na hapa sio imani) basi asubiri wakati wa uchaguzi na achague serikali nyingine ambayo ana uhakika itaendesha nchi bila ya kukandamiza RELIGIOUS INTERESTS zake...nadhani with that utang'amua ni Tanzania gani tutakayokuwa tunaitengeza (KUIBOMOA)...

Tanzanianjema
 
Kithuku.

Nimeisoma charter ya OIC (pengine kabla yako) na nilikuwa mmoja wa waliobandika link humu mapema tu. Muulize Mkandara.

Hayo ya Membe siyajui wala mimi si mshabiki wake.

Kuhusu maswali yako:

1. Nani anayeweza kuzungumzia utashi wa taifa la Tanzania? Kwani hao waislamu wanaokubaliana na malengo yote katika OIC hawamo katika taifa letu? Hatuwezi kujidai kuwa tu wazungumzaji wa taifa lilo diverse kama la kwetu. Ndiyo maana tumechagua wawakilishi kutuzungumzia. Lakini wao ni binadamu, na kunasema wanakosea. Hilo linaeleweka.

Ni lazima tuelewe kuwa kujiunga katika chombo chochote si lazima ukubaliane na YOTE yaliyomo katika katiba yake. As long as unakubaliana na mwelekeo wake in general basi kuna sehemu unaweza kuzimezea. Mimi ninavyoelewa ni kuwa lengo kuu la OIC ni kuleta maendeleo na mshikamano kwa waislamu na si ku proselytize wasio waislamu kujiunga na dini hiyo. Wenzangu mmeona hiyo ya pili zaidi wakati mimi nimeona ya kwanza. Sasa kwa nini nimpinge mtu anayetaka kuwainua ndugu zangu waislamu?

2. Kwani watanzania wote tunakubali kutekeleza malengo yote yaliyo kwenye FIFA? Hata sisi wapenzi wa kriketi! Kama hautaki hautalazimishwa. Ni haki yako kama mtanzania kukataa kupeleka watoto wako kusoma katika shule iliyojengwa na pesa kuto OIC:


3. Nani amesema kuwa wasio waislamu watafungwa na maazimio ya OIC? Kama nilivyosema hapo awali, mbona sisi wapenzi wa kriketi hatufungwi na maazimio ya FIFA?

Sasa wewe nijibu mimi:

Niambie kama usie muislamu utaathirika vipi kwa kujiunga kwetu na chombo hicho? Unipe mifano rahisi.

Amandla.................................

Ili kujiunga na chama au umoja wowote, ni lazima ukubaliane na malengo yake YOTE, maana umoja huo haujagawanyika kusema malengo mengine atatekeleza mwingine. Huwezi kujiunga kwenye umoja fulani ati kwenda "kuchuja" unayoyataka tu, huo sio umoja. Ndio maana kuna charter, na wanaokubaliana na charter hiyo ndiyo wanaojiunga.

Halafu ulinganisho wako wa FIFA na mambo ya kriketi hauna uhusiano hata kidogo na OIC, hivi ni vyombo vya michezo, vya burudani, starehe, hakuna siasa za nchi na nchi, havina vikao vya wakuu wa dola, ama mabaraza ya mawaziri. Maamuzi ya FIFA hayawajibishi serikali, yanavihusu vyama vya mchezo huo na si dola au serikali. Hata hivyo katika taifa letu kuna sera ya michezo, na moja ya malengo yake ni kuendeleza michezo kama ilivyo kwenye hiyo FIFA. Katika sera za taifa letu, hakuna sera ya kuendeleza dini yoyote.

Nchi inapojiunga na taasisi ya muungano wa kiserikali ama kidola inawajibika kutekeleza maamuzi ya muungano huo kwa kipindi chote ambacho ni mwanachama, na ni kwa njia hiyo maamuzi ya OIC yatakavyowaathiri wasio waislamu ama wasiokubaliana nayo. Mfano, AU ilipoamua kuvamia Comoro kumtoa Kanali Mohamed Baccar, nchi zote wanachama ziliwajibika kuchangia ikiwa ni pamoja na kodi yangu na yako, na wengine ndugu zetu walikwenda vitani. Siku OIC wakiamua kutenda jambo lolote kulinda maslahi yao kwa mujibu wa charter yao, nchi zote wanachama zitawajibika kuheshimu na kushiriki uamuzi huo, ikiwamo wananchi kama mimi ambaye sikubaliani na charter hiyo. Kwa hiyo tusirefushe maneno bila sababu, kitu kinachowaunganisha wanaokuwa kwenye umoja wowote ni MALENGO ya umoja huo, anayejiunga na umoja wowote kwa kufuata tu mkumbo huyo nitamwita punguani na sitaomba radhi.

Hivi kama taasisi fulani ina malengo A na B, unakubaliana na A lakini hukubaliani na B, utajiunga tu? Sasa muda wa kuanza kutekeleza hiyo B ukifika utajitoa? Unadhani wenzako watakukubalia baada ya kumaliza rasilimali zao kwenye lengo A ulilolitaka? Haya ni yaleyale ya wanaotaka kula vya wenzao, ikifika muda wa vyao kuliwa wanaleta ubishi, sasa ikifikia hapo huwa "hapatoshi" na tumeona mifano mingi. Tukiwa na viongozi wenye msimamo kama wako Fundi Mchundo tutaishia kama Chifu Mangungo wa Msovero tuliyemsoma kwenye historia. Chifu Mangungo aliingia mkataba na wajerumani kuwa watakuwa marafiki, watampa ulinzi dhidi ya adui zake, naye atawapa ardhi yote iliyo chini ya milki yake. Kumbe yeye urafiki aliutaka, ulinzi pia aliutaka, lakini kipengele cha kugawa ardhi yote hakukitaka, lakini akasaini mkataba! Yaliyofuata ni historia hadi leo. Sasa unataka kutudanganya ati tujiunge kwenye OIC maana ndani ya charter yao kuna tunayokubaliana nayo, yale tusiyokubali "tuyamezee", nani atakubali hii, unadhani hao wenye OIC yao ni mazuzu? Wana akili sana na kamwe huwezi kuja kuwaletea "za kitoto" mwishoni kuwa ati licha ya kujiunga baadhi ya malengo huyakubali! Ni kula na kulipa, dunia nzima iko hivyo. Sasa kabla hujala, pima uwezo wako wa kulipa.

Narudia. Malengo ya taasisi husika yapimwe kwanza kwa ufananisho na malengo na mwelekeo wa taifa letu, ili tunapojiunga na taasisi yoyote tujiunge na ile ambayo inatuwezesha kutekeleza malengo ambayo tunayo, tunayaamini, na kuyakubali kama taifa, nasema malengo ya taifa, siyo ya kikundi kimoja tu.
 
Kwani watanzania wote tunakubali kutekeleza malengo yote yaliyo kwenye FIFA? Hata sisi wapenzi wa kriketi! Kama hautaki hautalazimishwa. Ni haki yako kama mtanzania kukataa kupeleka watoto wako kusoma katika shule iliyojengwa na pesa kuto OIC:


Ndiyo, Tanzania kama nchi mwanachama wa FIFA tunakubaliana na malengo yote yaliyo kwenye FIFA. Hivyo hivyo Tanzania kama nchi tukiingia OIC itabidi tukubaliane na malengo ya OIC na kama hatuko tayari kwa hilo, kwa nini tujiunge ?


Nani amesema kuwa wasio waislamu watafungwa na maazimio ya OIC? Kama nilivyosema hapo awali, mbona sisi wapenzi wa kriketi hatufungwi na maazimio ya FIFA?


Tanzania ikiwa mwanachama wa OIC itafungwa na maazimio ya OIC - sasa swala la wasio waislamu linatoka wapi. Halafu dini na michezo au imani na burudani unaviweka kwa mtizamo sawa kweli ?
 
Kithuku,

Mkuu samahani nimewaingilia ktk mada hii...
Umeandika mengi ambayo ni kama vile sinema yaani mambo ambayo hayapo ila unafikiria kama ikiwa litatokea!
Sasa ni vizuri tukatazama kama mifano hiyo inaonekana mahala popote ktk historia ya OIC kwa mfano uliozungumzia Comoro,
Je, OIC imewahi kutoa maagizo kama hayo kwa nchi wanachama au kuingilia imani za dini tofauti kuharibu uhusiano wa wananchi wake?..Hapana! then, hizi habari za uzushi zinatoka wapi?...Hivi kinachowatisha zaidi ni kipi.. kuangalia maendeleo na maslahi ya Waislaam?..Hivi vyombo vya dini nyinginezo havifanyi hivyo? na ni wakati gani wameweza kuingilia maslahi ya nchi hizo kwa kutumia dini ama Uanachama wake.
Muundo wa chombo chochote duniani sio lazima uwe sawa na wala haiwezekani Waislaam wawe na mpangilio sawa na Wakristu ndio sababu kubwa iliyotufanya sisi sote tuwe na dini tofauti...
Mwisho wa hoja hii ni pale utakapo amini kwamba ni mambo kama haya ndio yamekufanya wewe uwe mkristu kwa sababu hukubaliani nayo lakini wakati huo huo huwazuii Waislaam kufannya mambo yao pamoja na kwamba sio mapendekezo yako.
Unapo heshimu na kupokea matakwa ya mwenzako maadam hayana madhara kwao ndio unapojenga jamii hata iwe ktk ndoa zetu..Mwanamke atafanya ya kike na wewe utafanya ya kiume maadam tu hayana madhara na ndoa nzima!... lakini huwezi kumkataza mkeo kucheza Upatu ati kwa nini asiwe kama wewe ku bet mpirani!..
Ni bora sana kutoa ushauri ktk maswala ya kike kuliko kutoa AMRI kuwa haiwezekani! Utaonekana Dikteta! na ndicho nachokiona ktk hoja hii ya OIC.
 
Tusisambaze sumu ya udini kwa kivuli cha Membe na OIC


NCHI inakwenda kubaya na tunaitengezea bomu la maangamizi.
Udini utaangamiza taifa, utaleta vita, maafa na hakuna atakayepona, utatuondoa katika mstari wa utaifa wa kupambana na ufisadi na kukuza uchumi.

Mada yangu ya leo ni udini, ambao naona sasa unatupeleka kubaya na hata kutishia kulipasua taifa letu katika mapande mawili.

Nimekuwa nikifutilia vizuri sana malumbano ya kidini nchini kimya kimya. Ukimya wangu unatokana na hofu kubwa kutokana na unyeti wa suala lenyewe. Baada aya kimya cha muda mrefu, nimeona leo nizungumzie suala hili.

Huko nyuma niliwahi kuonya katika safu hii kwamba tunatengeneza bomu la aangamizi katika nchi. Nilichobaini ni kile alichoonya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere, miaka 13 iyopita, watu sasa wanazungumza na kujivunia udini hadharani kama alama yao ya utaifa.

Hili limejitokeza kwa kasi sana tangu kuingia madarakani serikali awamu ya nne ya Rais Jakaya Kikwete, watu wamekuwa wakizungumza udini kama wendawazimu.

Mjadala huu sasa umepamba moto kufuatia kauli ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernad Membe, kwamba Watanzania hawapaswi kuogopa kujiunga na Jumuiya ya Nchi Kiislam Duniani (OIC).

Binafsi, nilikuwapo katika mkutano wa Membe na waandishi wa habari, huyu mtu amefafanua vizuri sana hatma ya Tanzania kujiunga au kutojiunga na OIC.

Kwanza, Membe hakusema kwamba ni lazima Tanzania ijiunge na OIC licha ya kusema hakuna haja ya kuogopa.

Pili, alisema Tanzania haikujiunga na OIC kama watu wanavyovumisha.

Tatu, aliweka bayana kwamba, Watanzania katika maamuzi yao, watapaswa kuangalia mambo mbalimbali katika kufanya maamuzi ya kujiunga au kutojiunga na OIC ikiwezekana hata kuangalia nchi kama Uganda.

Akifafanua hilo, alisema Uganda ambayo asilimia 66 ya wananchi wake ni Wakristo, asilimia 10 Waislam na waliobaki wapagani, ni mwanachama wa OIC.

Lakini, msisitizo mkubwa wa waziri huyo ni kwamba uamuzi huo utakuwa chini ya mamlaka ya wananchi na si vinginevyo.

Baada ya kauli hiyo, mbivu na mbichi zikabainika, wenye kusambaza sumu ya udini katika nchi wakajitokeza, hawa baadhi yao ni wale wanaoitwa viongozi wa dini.

Mstuko unatokana na kuona viongozi wa dini kuwa wenye kuendekeza udini kwa kutoa matamshi makali ambayo hajengi taifa.

Tumesikia na kuona, viongozi wanakaza misuli ya shingo, kuzungumzia OIC kidini badala ya kuzungumzia kitaifa.

Suala la OIC si la Waislamu pekee bali hata Wakristo, hivyo kama linajadiliwa iwe katika misingi ya utaifa, huu ndiyo uzalendo na hata Mungu anapenda.

Hapa hatuko katika vita ya Jihadi au vita ya Msalaba, tuko katika kujadili jambo nyeti linalohusu nchi, hivyo tunapaswa kujadili kama Watanzania wenye akili na utaifa wao.

Kwa mtu mwenye akili timamu, asiye na fikra au chembe za udini kamwe hawezi kujadili jambo nyeti kama hili la kujiunga na OIC akijiita mimi: "Mkristo au Mwislamu"

Hebu tujiulize, Wakristo wakikaza misuli ya shingo kupinga Tanzania kujiunga na OIC, na Waislam nao wakafanya hivyo, matokeo yake ni nini?

Matokeo yake ni kwamba tutatengeneza bomu la maangamizi, na taifa litakuwa kama la Ivory Coast, ambalo limegawanyika kaskazini ya Waislam na kusini ya Wakristo.

Kinachoonekana ni kwamba katika nchi hii kuna watu ambao wanaomba mijadala ya kidini iibuke ili wapate nafasi ya kuonyesha udini wao.

Leo hii baadhi ya watu wenye fikra za udini wanaweza kuhoji uhusiano kati ya Tanzania na Iran, wakisema eti nchi inataka kuingizwa OIC.

Wengine wanaohoji uhusiano na Vatican hadi ubalozi wake kuwa hapa nchini, hizi ni fikra za kimaskini na kijima, nani rafiki mzuri duniani asiye na doa?

Hivi hiyo Marekani inayotoa misaada duniani na hapa kwetu, ina mazuri gani inafanya duniani?

Mbona yenyewe ina madhambi mengi tu, mbona tunakula mabilioni ya dola zao, sasa kwanini Iran iwe kituko na kuanza kuzusha fikra za udini eti tunaingia OIC na Membe ajiuzulu.

Hivi hao wanadhani wankemea udini, wanajua ambayo yamekuwa yakifanywa na Shirika la Ujasusi la Marekani (CIA) tangu kuanzishwa na hadi sasa?

Au hivi Ufaransa ina lipi zuri, mbona inaongoza kusaidia mapinduzi ya kijeshi katika makoloni yake, ilidaiwa kuhusika katika mauaji ya kimbari ya Rwanda mwaka 1994 na mbona tunapokea misaada yake?

Tuache fikra za kijima, fikra za kuigawa nchi, hizi ni fikra za hatari ambazo kamwe zikiachiwa haziwezi kumbakisha mtu.

Ukiona mtu ameishiwa sera, ataanza kujitambulisha kwa udini au ukabila, sasa hivi watu wamekosa mambo ya msingi ya kufanya wanasambaza sumu ya udini katika nchi.

Kwa maana, siku zote sipendi kabisa kuona sura au kusikia mawazo ya watu wenye kutaka kuvuruga amani na usalama wa nchi kwa kivuli cha udini.

Hawa ni watu hatari sana. Hivi Watanzania watoto wa taifa moja tunashindwaje kukaa na kutatua mambo yetu kwa amani na utulivu?

Tunaipeleka wapi sifa yetu hii, watu wanakaa na kujivunia umaskini wa mawazo kwa kujiita eti sisi Waislam au Wakristo.

Wengine wanadikiri kuzungumza uchochezi eti Rais Kikwete ni mdini, ukiuliza hupati majibu zaidi ya kuona ni watu wenye hisia tu za kichochezi, hisia za hatari na fikra za kimaskini na kipuuzi.

Leo hii badala kukaa kuzungumza mambo ya msingi kwa pamoja, tunakaa na kutoa matamshi makali yatakayoyumbisha mustakabali wa taifa.

Baadhi ya Wakristo wanasahau kwamba, kutoa matamshi makali kuhusu Tanzania kujiunga na OIC hakuwezi kujenga taifa huku baadhi ya Waislam nao wakisahau kuwa kudai jambo hilo kwa nguvu hakuwezi kufanikiwa.

Nchi hii si ya Waislam wala ya Wakristo kama alivyosema Mwalimu Nyerere, bali wapo wenye fikra za udini wanaofanya mbinu za kuigawa, na ole wao, watakumbana na mkono wa dola!

Halafu cha ajabu baadhi ya wanaojiita viongozi wa dini wenye misimamo mikali kwa kuwa na fikra za kijima, ndiyo wenye kutunza majini nyumbani kwao, wengine wakiwajihusiaha na matukio ya ajabu.

Ndugu zangu Watanzania tusicheze wala tusiruhusu sumu hii ya udini kusambaa, hii itaangamiza taifa na wala hakuna ufundi katika kucheza na jambo hili.

Watanzania tunapaswa kukaa kama taifa moja, kudumisha umoja, utaifa na amani yetu, tusiruhusu watu wachache wenye fikra hatari kuzisambaza katika taifa, tuwakatae, tuwadhibiti na uwezo wa kuwadhibiti tunao.

Aluta Continua!






Ramadhan Semtawa ni mwandishi wa mwananchi:0782-528229:mwanamapinduzi@yahoo.com
 
Kaka kwanza napenda kukutaarifu rasmi kuwa mimi sio huyo unayemdhania...Ukweli ni kuwa tunajuana na mimi na wewe tukiwa nje ya Jamboforum tunaelewana vizuri. NAKUSHAURI UFANYE UCHUNGUZI WAKO WA NGUVU ILI USIJE UKASHANGAA HIVI KARIBUNI NITAKAPOJITAMBULISHA KWAKO RASMI.

Uchunguzi nilishafanya, the minute uliposema ninajitayarisha kugombea , uliniambia mwenyewe kuwa wewe ni nani, kwa hiyo hakuna noma kwenye hilo.

Beno ni mdogo wangu na namchukulia hivyo na wala sio mgombea wangu kwani hadi leo hii sijawahi kuwa na uanachama wa chama chochote nchini. Actually ninaamini kuwa CCM ni tatizo kwa mustkabali wa Tanzania na hivyo kinapaswa kupumzishwa kijikoshe uozo wa utamaduni wa kifisadi na kiweze kujisafisha kifalsafa.

Ohhh ahsante kumbe ni mdogo wako, ahsante sana kwa kukubali hilo.

Tofauti yangu na wewe ni kuwa mimi namjua Beno wakati wewe humjui.
Ndugu yangu huwezi ukakwepa kuwa taarifa zako kuhusu BENO ni nyepesinyepesi mno na zinategemea vibomu vya ndugu yetu SAIDI KUBENEA na wafuasi wa Mzee wetu MALECELA ambao wanamuona BENO kama kikwazo cha kuirudisha mikononi CCM kupitia kwa kijana wao NAPE NNAUYE. Ni wazi hata mimi nisingeweza kuacha kumuunga mkono NAPE ukitilia maanani siasa za kimakundi CCM na loyalty yake kwa Mzee Malecela. Na katika kufanya hivyo ni wazi nitakuwa vulnerable na siasa chafu dhidi ya Beno hata kumhusisha na MAFISADI MAARUFU kina LOWASSA and Co. UNLIMITED.

Kuhusu mdogo wako, ni media zote za bongo ndio zilizosema kwanza, you got it right simjui kabisa maana ni small fish anayejaribu kusimama kwa kutumiwa na mafisadi, Nape ni mjumbe wa NEC na ana nafasi kubwa sana ya kuongoza taifa sio lazima iwe UV-CCM, ambayo Kikwete hawezi kuiruhusu tena kua na nguvu ndani ya CCM, ndio maana alimtaka Nape aandike Rufaa na sasa iko mezani kwake, Malecela has nothing to do na hizi siasa uchwara tena ndio maana hakuwepo Tarime na kumewashidna mafisadi, Mkamba hakujua hilo kuwa wananchi wamechoshwa na wenzako, poleni sana!

Kuhusu Mzee Malecela mimi namheshimu kwa hekima na upeo wake mkubwa wa siasa na masuala ya kidunia na pia natambua utumishi wake uliotukuka kwa Taifa letu. Tatizo mimi ni wale unaweza kuwaita Nyerereist (naamini katika ujamaa) hivyo natofautiana naye kimtazamo na sio yeye kama Mzee wetu. Ofcourse i cant take his current family partner....

Yale yale ya mjamaa kwenda kutibiwa UK, bwa! ha! ha! ha!

Kuhusu kugombea kaka mimi bado naamini kuitumikia Tanzania kivulini na sio lazima niwe fulani. What matters ni mchango gani natoa na sio nina uheshimiwa gani. Kama nitagombea na hili bado ni wazo legelege tu, nitaanzia ngazi ya chini...labda UDIWANI na sio kukimbilia UBUNGE kama tunavyodhani vijana wengi wa kizazi cha MTANDAO...

Ahsante tena mkuu kama vile na mimi ninavyolisaidia sana taifa langu nikiwa hapa JF sio lazima nigombee anything.

Kuhusu hili la OIC nashindwa kutambua kama unapinga kama MTANZANIA ama MKRISTU. Na hili nadhani ndio tatizo kubwa tulilonalo ingawa wengi tunapenda kukimbilia kuwashutumu wao (Waislamu) kuwa wanaunga mkono kwa kutilia maanani maslahi yao kama waislamu tu. Nadhani tofauti na wananchi walivyo, msimamo wa serikali, ndio unaangalia zaidi maslahi ya nchi.

La OIC ninalikataa kama Mwnanchi Mtanzania, na pia kama Mkristo, na pia siwaamini viongozxi waliopewa hela za uchaguzi na Iran ambako ndiko majuzi Membe alikokuwa kabla ya kuja na hizi nonesense!

Na suala hili haliihitaji uhusika wa baraza la mawaziri wakati Wizara ya Mambo ya Nje ndiyo iliyokabishiwa ba katiba ya jamhuri ya muungano jukumu la kuandaa, kutekeleza na kusimamimia utekelezaji wa Sera Ya Mambo ya Nje ambayo ilipitishwa na Baraza la mawaziri. Kusema kuwa hili lnahitaji baraka za wananchi ama bunge ni kumpokonya madaraka halali Waziri wa Mambo ya Nje. Ni rais tu ndiye anayepaswa kuingilia utekelezaji huo kwa kushauriana na waziri husika ambaye kwa hivi sasa tupende tusipende ni Bernard Membe.

Hapa unajinasa mwenyewe, kwa sababu Mwalimu shujaa wako ndiye aliyetuambia kuwa hili la OIC ni letu wananchi, sio la waziri wa nje na hakuna aliyebisha, Zanzibar ilipoamua kujiunga na kujitoa, haikuwa suala la waziri wa nje

Siamini kama ni busara kuachia religious sentiments za wananchi kudetermine utendaji kazi wa serikali. Nadhani kama kuna mtu anaona kuwa serikali iliyopo madarakani haiheshimu MASLAHI YAKE YA KIDINI (na hapa sio imani) basi asubiri wakati wa uchaguzi na achague serikali nyingine ambayo ana uhakika itaendesha nchi bila ya kukandamiza RELIGIOUS INTERESTS zake...nadhani with that utang'amua ni Tanzania gani tutakayokuwa tunaitengeza (KUIBOMOA)...

Mkuu tumeliachia taifa letu limefikia hapa tulipo kwa maneno kama yako, enough, hatuwezi kukaa pembeni na kuwaacha hawa viongozi watupeleke shimoni zaidi kwa visingiiizo vya kuogopa dini,

infact you got it backwards, ni kwamba kiongozi yoyote siyekua na uwezo wa kuelewa kuwa OIC ni Jumuiya ya Wa-Isilamu na kwamba kujiunga nayo ni lazima uwe taifa la Kiisilamu, na kwamba Tanzania sio taifa la Kiii-Isilamu, huenda hawezi uongozi wa taifa letu, sasa dawa ni kujitoa mapema!

Otherwise, ahsante mkuu and I am out!
 
Tanzania ikiwa mwanachama wa OIC itafungwa na maazimio ya OIC - sasa swala la wasio waislamu linatoka wapi. Halafu dini na michezo au imani na burudani unaviweka kwa mtizamo sawa kweli ?

Kwa nini nisilinganishe? Vyote hivi si vinafanya wafuasi wake wapandishe mori vinapoguswa? Hakuna logic katika upenzi wetu wa kimoja dhidi ya kingine lakini tuko tayari kufa kukitetea!

Mnaposema kuwa tukiwa wanachama wa chombo fulani kuwa tutafungwa na maazimio yake yote ndipo mnapokosea. Kama alivyosema Kithuku, AU iliazimia kuvamia Comoro. Tanzania tukaitikia wito. Afrika Kusini ikagoma. Hakuna kilichofanywa kuifukuza Afrika ya Kusini kwenye uanachama. Nchi ngapi za A.U. zimepeleka majeshi Somalia pamoja na maazimio ya chombo chao? Si moja tu! Mbona wengine hatujafukuzwa uanachama?

Sisi ni wanachama wa IOC lakini tulisusia michezo ya Olimpiki LA na wenzetu Moscow! Mbona mado tunapeta katika chombo hicho? Mauritius walikuwa ni wanachama wa O.A.U lakini haikuwahi kuisusia serikali ya makaburu kibiashara. Nchi ambayo O.A.U ilikuwa katika hali ya kivita nayo! Misri na Jordan zina ushirikiano na Israel wakati wako mstari wa mbele katika umoja wa nchi za kiarabu. Mbona hatusikii wakifukuzwa huko?

Wengi (sio wote) mnaopinga uanachama katika O.I.C ni kutokana na hisia zilizojikita kuwa hakuna chema kitakachotokana na chombo cha Kiislamu. Hawa lazima watakuwa na kiji-ajenda ya kutushughulikia sisi wote wanaotuita makafir! Hakuna mahali ambapo mmeeleza bayana kuwa sisi tusio waislamu tutaathirika vipi na uanachama huo. Badala yake mnatuletea chimera kuwa tutafungwa na maazimio yao yote! Bila shaka mkimaanisha kuwa iko siku watataka nchi zote zitawaliwe kwa sharia! Hamuangalii kuwa Katibu Wake Mkuu ni mturuki. Nchi yenye waislamu ambayo haielewi kabisa mambo ya sharia! Nchi ambayo wamepiga marufuku uvaaji wa hijab katika bunge lao! Unadhani hawa watakubali nchi yao kugeuzwa ya kiislamu? Hata kama ina waislamu wengi? Thubutu!

Kutaka kukubaliana na kila kitu katika chombo ni kuwa naive. Wote kama wanachama tuna haki ya ku-pick and choose. Tofauti ikizidi tunajitoa. Lakini kama tunaona mzani unaelemea kwenye kufaidika tunabaki! Bila shaka ndiyo maana waganda na wengine kama hao bado ni wanachama.

Ni hayo tu.
 
Ndiyo, Tanzania kama nchi mwanachama wa FIFA tunakubaliana na malengo yote yaliyo kwenye FIFA. Hivyo hivyo Tanzania kama nchi tukiingia OIC itabidi tukubaliane na malengo ya OIC na kama hatuko tayari kwa hilo, kwa nini tujiunge ?

Pamoja na kwamba Tanzania inakubaliana na malengo (sidhani kama ni yote) ya uanachama FIFA haimaanishi kuwa watanzania wote wanaunga mkono. Sasa nyinyi mnataka kutuambia kuwa ni lazima watanzania WOTE ( si Tanzania) wakubaliane na malengo ya OIC ndiyo iwe muafaka? Tutafika kweli?
 
Kithuku,

Mkuu samahani nimewaingilia ktk mada hii...
Umeandika mengi ambayo ni kama vile sinema yaani mambo ambayo hayapo ila unafikiria kama ikiwa litatokea!
Sasa ni vizuri tukatazama kama mifano hiyo inaonekana mahala popote ktk historia ya OIC kwa mfano uliozungumzia Comoro,
Je, OIC imewahi kutoa maagizo kama hayo kwa nchi wanachama au kuingilia imani za dini tofauti kuharibu uhusiano wa wananchi wake?..Hapana! then, hizi habari za uzushi zinatoka wapi?...Hivi kinachowatisha zaidi ni kipi.. kuangalia maendeleo na maslahi ya Waislaam?..Hivi vyombo vya dini nyinginezo havifanyi hivyo? na ni wakati gani wameweza kuingilia maslahi ya nchi hizo kwa kutumia dini ama Uanachama wake.
Muundo wa chombo chochote duniani sio lazima uwe sawa na wala haiwezekani Waislaam wawe na mpangilio sawa na Wakristu ndio sababu kubwa iliyotufanya sisi sote tuwe na dini tofauti...
Mwisho wa hoja hii ni pale utakapo amini kwamba ni mambo kama haya ndio yamekufanya wewe uwe mkristu kwa sababu hukubaliani nayo lakini wakati huo huo huwazuii Waislaam kufannya mambo yao pamoja na kwamba sio mapendekezo yako.
Unapo heshimu na kupokea matakwa ya mwenzako maadam hayana madhara kwao ndio unapojenga jamii hata iwe ktk ndoa zetu..Mwanamke atafanya ya kike na wewe utafanya ya kiume maadam tu hayana madhara na ndoa nzima!... lakini huwezi kumkataza mkeo kucheza Upatu ati kwa nini asiwe kama wewe ku bet mpirani!..
Ni bora sana kutoa ushauri ktk maswala ya kike kuliko kutoa AMRI kuwa haiwezekani! Utaonekana Dikteta! na ndicho nachokiona ktk hoja hii ya OIC.

Mukandara,

Mimi nakataa kwamba hakuna madhara, yapo na nilishayasema huko nyuma ya kujiunga na OIC. Nilipomaliza ukasema sasa hapo weka wanawake. Kuna national consensus katika baadhi ya mambo, kwamba hayo yapewe special treatment. Mojawapo ni makundi kama wanawake na walemavu. Kuingia OIC na kuingia kwa mahakama za Kadhi ni kuwapa Waislam special treatment ndani ya Serikali. Itabidi kuwe na national consensus, badala ya kusema tu haya mambo yanawahusu waislam peke yao. Kwa nini basi mnataka yaingie Ndani ya serikali isiyokuwa ya waislam peke yao? Hapo mnataka special treatment kwa waislam na kukishakuwa na special treatement ambayo msingi wake ni Dini, ambayo hakuna consensus ya kitaifa, ni tatizo.


Tatizo namba moja ni hili hapa: Look at BAKWATA AND THE MESS IT IS. You want to move this mess in a government. Itakuwa moto zaidi. Nilishasema huko nyumba tutahitaji kuwa na special department ndani ya serikali kushughulikia mambo ya waislam, hii itakuwa bakwata iliyohamia serikalini. Wapo wanaosema Bakwata ilianzishwa na mwalimu kwa nia ya kuwa opress waislam. Well and good. Sasa tiba ni kuzihamishia kazi zake serikalini au kuirekebisha na sasa mwalimu hayupo? Hapo sasa mwingiliano na serikali utakuwa rasmi, na akiwa rais asiye mwislam this will be a nightmare. Fikiria unfair blames zinazopelekwa kwa mwalimu. Waislam kukosa institution katika mfumo wao wa uendeshaji wa dini ni suala ambalo inatakiwa walishughulikie siyo kulihamishia serikalini. Serikali tayali ina matatizo ya kutosha.

Tatizo la pili ni hili hapa: Fikiria Judge wa Mahakama ambaye ni mwislam, mambo yake anayapeleka Mahakama ya Kadhi na yanaamuliwa kwa mujibu wa sharia na huku yeye anatumia sheria za kawaida kuwahukumu watu wengine. Will it be fair? (I'm sorry hili la kadhi na la OIC naona ni kitu kile kile - Kuwapa waislam special treatment ndani ya serikali).

Tatizo la tatu: OIC ni jumuiya ya kimataifa (wanachama ni mataifa). Sasa fikiria hii misaada tunayoikimbilia. Serikali itawezaje kuhakikisha kuwa misaada hii inawanufaisha waislam tu? OK mtasema misaada itakuwa ni kwa ajili ya wote, na hili tayari litakuwa mgogoro, vipaumbele vitakuwa vipi? ... Mambo ya waislam.

Tatizo la nne: Gharama. OIC na mahakama ya kadhi vitaingia katika mfumo rasmi was serikali. kwa hiyo bajeti ya serikali itakwenda kwenye masuala yanayohusu kundi fulani tu la kidini na mainly kwa masuala yao ya kidini tu. Hii ni special treatment. Wapo wanaosema kwa kuwa serikali ni ya wote na hao (waislam) ni sehemu ya walipa kodi. Lakini kwa nini mambo yao ya kiimani wachotewe kwenye mfuko wa pamoja wakati wengine wanachangia mambo yao moja kwa moja? Wawakilishi wa Tanzania kwenye mikutano ya OIC ambao lazima watakuwa waislam watalipwa posho na marupurupu kutoka serikalini. Hata Makadhi na gharama za kuendesha mahakama zao. Siku maaskofu wakitaka kusafiri kwenye mikutano yao nje wakaomba na wao funds serikalini, itakuwa fair kuwanyima? Na wao si wanakwenda kwenye masuala yao ya kidini kama wanavyoenda waislam?

Tatizo la tano: OIC inajitambulisha kuwa ni kwa ajili ya waislam. Matamko wanayoyatoa au maamuzi ya vikao, yakiridhiwa na serikali hayatakuwa sheria? Nani atakayelinda maslahi ya watu wasiokuwa waislam (ambao hawawakilishwi kwenye mikutano yao)?

Ni kweli tuna tatizo la dini hizi zetu, na hasa hasa waislam na wakristo. Tatizo si kutopendana au kutoheshimiana. No. Watu wanaoana na kuishi pamoja. Tatizo ni kutoaminiana. Na hili tumelishwa, ni la kihistoria. Huko dini hizi zilikotoka. Lingine, waislam sasa hivi ni kundi kubwa ndani ya jamii. Kuwapa special treatement wakati tayari wananguvu kubwa tunayoiona kutazidi kuyaweka pembeni makundi mengine, na I'm sorry kwa nitakalolisema hapa. Unfortunately katika nchi ambazo waislam ni Majority groups, makundi mengine ya kidini yanawakati mgumu zaidi. Katika Nchi za kiislam kuacha uislam ni offense ambayo punishment yake ni death. Waislam sauti zao zinasikika huko Ulaya, ingawa wanalalamikia islamaphobia (ambayo siyo institutionalized). Umeshawasikia wakristo au wapagani wa Libya? Wa Saudia? Wa-Iran? May be this is a source of contention! Ubaguzi wa kiimani huko ni institutionalized!
 
The OIC Charter

The Representatives of:

The Kingdom of Afghanistan, the People's Democratic Republic of Algeria, the State of the United Arab Emirates, the State of Bahrain, the Republic of Chad, the Arab Republic of Egypt, The Republic of Guinea, the Republic of Indonesia, the Islamic Republic of Iran, the Hashemite Kingdom of Jordan, the State of Kuwait, the Republic of Lebanon, the Libyan Arab Republic, Malaysia, the Republic of Mali, the Islamic Republic of Mauritania, the Kingdom of Morocco, the Republic of Niger, the Sultanate of Oman, the Islamic Republic of Pakistan, the State of Qatar, the Kingdom of Saudi Arabia, the Republic of Senegal, the Republic of Sierra Leone, the Somali Republic, the Democratic Republic of Sudan, the Syrian Arab Republic, the Republic of Tunisia, the Republic of Turkey, and the Yemen Arab Republic, meeting in Jeddah from 14 to 18 Muharram, 1392H (29 February - 4 March, 1972); (30 members).

REFERRING to the Conference of the Kings and Heads of State and Government of Islamic countries held in Rabat, 9 - 12 Rajab, 1389 (22 - 25 September 1969);

RECALLING the First Islamic Conference of Foreign Ministers held in Jeddah, 15 - 17 Muharram 1390 (23 - 25 March, 1970), and the Second Islamic Conference of Foreign Ministers held in Karachi, 27 - 29 Shawal 1390 (26 - 28 December, 1970);

Hii ni preamble tu na sioni tatizo lake kwangu kama mmisheni.

CONVINCED that their common belief constitutes a strong factor for rapprochement and solidarity among Islamic people;

Ni haki yao kutaka kushikamana. Bado sioni tatizo kwangu mmisheni.


RESOLVED to preserve Islamic spiritual, ethical, social and economic values, which will remain one of the important factors of achieving progress for mankind;

Hii tena ina tatizo gani kwangu? Muislamu kutaka kudumisha misingi ya imani yao?

REAFFIRMING their commitment to the United Nations Charter and fundamental Human Rights , the purposes and principles of which provide the basis for fruitful cooperation among all people;

Hawa wanakubaliana na mmisingi ya haki za binadamu na Charter ya Umoja wa Mataifa. Tatizo liko wapi?

DETERMINED to consolidate the bonds of the prevailing brotherly and spiritual friendship among their people, and to protect their freedom, and the common legacy of their civilization restoring particularly on the principles of justice, tolerance and non-discrimination;

Wanataka kudumisha undugu na urafiki wa kiimani baina yaorudisha misingi ya haki, kuvumiliana na kutokubagua ya tamaduni yao. malengo ninayoyaafik kabisa.

IN THEIR ENDEAVOR to enhance human well-being, progress and freedom everywhere and resolved to unite their efforts in order to secure universal peace which ensures security, freedom and justice for their people and all people throughout the world.

Katika jitihada zao wanataka amani duniani kote itakayohakikisha usalama, uhuru na haki kwa watu wao na watu wengine wote duniani. Tatizo liko wapi?

APPROVES the present Charter of the Islamic Conference:-


ARTICLE I: The Islamic Conference:
The Member States do hereby establish the Organization of "The Islamic Conference".

ARTICLE II: Objectives and Principles:

A) Objectives:
The objectives of the Islamic Conference shall be:

* to promote Islamic solidarity among Member States;

Ushirikiano wa waislamu katika nchi wanachama. Tatizo bado sioni. Au tunaogopa kuwa wakishirikiana watatutosa sisi ambao sio waislamu?

* to consolidate cooperation among Member States in the economic, social, cultural, scientific and other vital fields of activities, and to carry out consultations among Member States in international organizations;

Kudumisha ushirikiano katika nyanja za kiuchumi, jamii, tamaduni, sayansi na nyanja nyingine muhimu na kufanya mazungumzo baina ya nchi wanachama katika vyombo vya kimataifa. Mazungumzo na si kushurutisha.

* to endeavor to eliminate racial segregation, discrimination and to eradicate colonialism in all its forms;

Kupinga kutengwa katika jamii kwa misingi ya rangi, ubaguzi wa kila aina na kila aina ya ukoloni. Hapa napo tunapinga?

* to take necessary measures to support international peace and security founded on justice;

Kuchukua hatua zinazotakiwa kuhakikisha kuwa kuna amani baina ya mataifa na usalama kwa isingi ya haki. Tunapinga nini hapa?

* to coordinate efforts for the safeguarding of the Holy Places and support of the struggle of the people of Palestine, to help them regain their rights and liberate their land;

Kushirikiana kutetea maeneo matakatifu na kuhakiksha kuwa wapalestina wanatendewa haki na wanakomboa nchi yao. Kwa imani hii ya pili, Julius alivunja uhusiano na Israel. Mpaka leo nchi yetu ina balozi wa PLO na tuko mstari wa mbele kudai nchi huru ya Palestina. Hapa kuna kitu gani cha kututisha?

* to back the struggle of all Muslim people with a view to preserving their dignity, independence and national rights;

Kutetea mapambano ya waislamu wote kwa nia ya kudumisha heshima, uhuru na haki zao kitaifa. Hili linaweza kutusumbua kidogo hasa hilo la mwisho. Lakini kama nchi yenye waislamu wengi tuu hatuwezi kupinga waislamu hao kudai kutambuliwa katika jamii. Lakini hawa wanazungumzia kudumisha uhuru wao na haki zao kitaifa. Kwa vile unadumisha kilichokuwepo basi bila shaka hii inalenga yale mataifa yanayojitambua kama ya kiislamu na si mengine.

* to create a suitable atmosphere for the promotion of cooperation and understanding among Member States and other countries.

Kuweka mazingira mazuri ya kujenga ushirikiano baina ya nchi wanachama na mataifa mengine. Hapa bado sijamuona Osama.

B) Principles:

The Member States decide and undertake that, in order to realize the objectives mentioned in the previous paragraph, they shall be inspired and guided by the following principles:

* total equality between Member States;

Utekelezaji wa yale yalio juu yatakuwa kwa msingi wa usawa kamili baina ya nchi wanachama. Hamna security council humu!

* respect of the right of self-determination, and non-interference in the domestic affairs of Member States;

kuheshimu haki ya kujiamulia na kutokuingiliwa kwa masuala ya ndani kwa nchi wanachama. Uhusiano baina yetu ( waislamu na wamisheni) ndani ya nchi yetu bado utabaki ni jukumu letu na si la OIC. OIC hawana mamlaka ya kutuambia tuanzishe Mahakama ya Kadhi kwa mfano. Hilo tutaamua wenyewe.

* respect of the sovereignty, independence and territorial integrity of each Member States;

Kuheshimu utaifa, uhuru na mipaka ya kila nchi mwanachama. Kipi cha kupinga hapa?

* settlement of any conflict that may arise by peaceful means such as negotiation, mediation, reconciliation or arbitration;

Kutatua migogoro yote kwa njia za amani. Sisi ni wanachama wa Umoja wa mataifa ambao kihistoria haujachelea kutumia nguvu kutatua migogoro. Kuanzia Korea hadi vita ya kwanza ya Persian Gulf. AU imetumia mabavu Comoro. Hawa wanasema watatumia njia za amani nasi tunaogopa!

* abstention from the threat or use of force against the territorial integrity, national unity or political independence of any Member States.

Kujitoa katika kutumia vitisho vya nguvu dhidi ya uhalali wa mipaka, UMOJA WA KITAIFA, au uhuru wa kisiasa wa nchi yeyote mwanachama. Umoja wa kitaifa unajumuisha umoja baina ya watu wa imani tofauti.

Mengine kwenye Charter yanahusu mfumo wa sekretariet na kadhalika.

Haya, Kithuku usie punguani, nieleze katka haya lipi linakutoa mapovu kinywani?

Unayefuata mkumbo si wewe? Umerukia bandwagon kumhukumu Membe aliyedai majadiliano tu kuhusu suala hili!

Kukimbilia matusi ni kupungukiwa na hoja. Pamoja na hayo sitegemei uniombe radhi. Wewe si wa kwanza kuniona punguani na wala hautakuwa wa mwisho. Kama wasemavyo wenzetu. Inshaallah.

Amandla........
 
Kipimambele,
Mkuu bado hujanijibu kitu kabisa... kisha swala la OIC halihusiani na Mahakama ya kadhi kwani tunaweza kubaliana moja na jingine tusikubaliane...Jaribu kutenganisha laa sivyo unazungumza kwa nguvu ya Udini..
Unapozungumzia special treatment ni ipi hiyo, Kujiunga kwa Taifa letu ni special treatment kwa waislaam?... Je, mimi naweza kusema kufungua Ubalozi Vatican ni special treatment kwa wakristu?..Wanawake wetu kutuwakilisha ktk chombo cha kimataifa ni special treatment kwao au ni haki yao kimsingi..
Mkuu, nimekwisha sema hivi kuwa KUKATAZA kundi fulani wasifanye mambo yao ni moja ya sababu kubwa za vita, utengano na kadhalika, historia imeonyesha hivyo na hakuna nchi hatya moja imepata matatizo kwa sababu kundi moja limepewa haki yake ya kimsingi..
Pili, nilishasema haiwezekani culture na mipangilio ya kiislaam iwe sawa na wakristu, Tamaduni za dini hizi mbuili ni tofauti kabisa kiasi kwamba huwezi kusema wakristu wanachombo kimoja kama waislaam kimataifa. sasa kwa sababu wakristu hawana basi kila dini lazima iwe kama Wakristu. Afrika kuna makabila mengi ndani ya nchi moja ni lazima kuwepo na mfumo wa kujenga uhusiano kati ya makabila hayo tofauti na Ulaya ambako unaweza kukuta Wafaransa ni wafaransa, Waswedish ni kabila moja.. Hivyo hatuwezi kuiga Ulaya wakati watu na mazingira yetu ni tofauti. Tuitazame tanzania kama ilivyo na watu wanaojumuisha Taifa hilo kuweza kuunda misingi ambayo inaweza kuboresha uhusiano kati ya watu hao...
Ni matatizo kama haya siku hizi hata huku nje tumeanza kujenga makundi makundi ya Ukabila, Udini,na kadhalika wakati Mataifa mengine jumuiya zao zinakwenda mbele... hakuna nchi hata moja jumuiya ya Kitanzania imesimama imara kwa sababu kila siku tunatazamana sisi wenyewe na kuanza kuchambuana..Mwisho wa yote hakuna kinachofanyika, Na kwa akili hiyo leo hii tunafungua matawi ya CCM kesho utasikia Chadema na kadhalika. Yote hii inatokana na fikra mbaya kuwa CCM ni adui wa Chadema na Chadema ni Adui wa CCM..hivyo misingi ya jumuiya hizi inatanguliwa na Identity kama wewe sio CCM hukaribishwi ktk mikutano yao hata kama wewe ni Mtanzania...
Huu ni ULIMBUKENI mkuu wangu, tunashindwa kuona nje ya kabati na matokeo yake yatakuja wala sii muda mrefu. Utakuja kubali maneno yangu..
 
Back
Top Bottom