Juu ya OIC na Mahakama ya Kadhi

Juu ya OIC na Mahakama ya Kadhi

hivi oic na vatican ni sawa kimuundo na kitaratibu?
kama vipo sawa basi na oic ifungue "ubalozi" nchini tanzania
au serikali ya tanzania "ijiunge" uanachama vatican. kama haiwezekani
basi nadhani hoja za kulinganisha vatican na oic inapotosha.

nadhani ni muhimu kuzungumzia na kushawishiana kwamba uanachama oic ni muhimu na kusiwe na dalili za kuonekana ni suala la kulazimisha.
 
Mkamap,
Mkuu vunja uhusiano na Iran hakuna Muislaam atakaye piga kelele kwa sababu Iran ni nchi haina Uhusiano wowote na Uislaam...hakuna kiomngozi wao yetote anayeheshimika tanzania kama kiongozi wa dini aliyechaguliwa ama kuteuliwa...Iran ni nchi Inayotawaliwa kidini na Rais anayechaguliwa na watu kwa kura nje ya dini na baraza la mawaziri wake wanatumikia wizara kama za nchi zote dunniani..
Kutumia kwao Katiba iwe Kuran haina maana yoyote ile zaidi ya kuwa sawa na Tanzania kuamua kuwa WaKomunist haitufanyi sisi kuwa Warussia au Wachina. Pili, hakuna kiongozi yeyote wa Kiislaam nchini ambaye anajibu kwa ayatollah ama anawakilisha Iran duniani kote..Zaidi ya hapo Komein ndiye aliyeongoza mapinduzi wakati asidhani kama hali hiyo inawezekana kutokokea Vatican..
Mkuu acha ubishi soma vizuri maandiko yangu kihs pima acha ushabiki utaona nilichozungumza hakika Ubishi kabisa..

Hauwezi kusema Iran haina uhusiano wowote na Uislaam. Kutofautiana kwa dhehebu si sababu tosha. Kiongozi Mkuu wa Iran ni Ayatolla na si Rais. Ayatolla ni kiongozi wa dhehebu ya Shia. Kwa watu wa dhehebu hilo, Ayatollah ana nafasi kubwa katika dini yao ambayo ni dhehebu la kiislamu. Sasa labda kama unataka kutuambia kuwa washia si waislamu? Kama ni hivyo, mbona mshia, Aga Khan ( Ismaili ni sehemu ya washia) mlimkubali alipopiga push chama cha waislamu?

Sisi hatujawahi kuwa wakommunisti bali tuliwahi kuwa wajamaa(socialists). Kwa maneno mengine tulikuwa na rangi ya pink na si nyekundu kama wenzetu.
 
kama tayari masheikh wamekubaliana nadhani ingekuwa vyema wangetoa tamko lao kabla ya ijumaa. naamini kulitoa siku ya ijumaa kutaamsha zaidi hisia za kidini badala ya hoja za umuhimu wa uanachama huo kwa taifa. hii ni sawa na maaskofu wangetoa tamko lao jumapili. chonde chonde viongozi wetu wa dini na wanasiasa wetu hili suala lawaeza peleka nchi sehemu ambayo itakuwa vigumu kurudi katika tanzania tuijuayo sasa.
 
Bakwata yapingana na maaskofu kuhusu OIC
Basil Msongo
Daily News; Saturday,October 25, 2008 @19:01

Baraza Kuu la Waislamu wa Tanzania (BAKWATA), limesikitishwa na kauli ya Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT) na kuwataka maaskofu waache kupotosha lengo sahihi la serikali la kujiunga katika Taasisi ya Kimataifa ya Kiislamu (OIC) kwa kuwa taasisi hiyo si ya kidini.

Bakwata imeeleza kuwa ilichokisema maaskofu ni dhana na wasiwasi usio na msingi kwa kuwa hadi sasa wameshindwa kuthibitisha kuwa OIC imeleta mtafaruku wa kidini katika nchi zilizojiunga na jumuiya hiyo. Katibu Mkuu wa Baraza hilo, Ally Mzee alisema jumamosi Dar es Salaam kuwa maaskofu hao hawana mamlaka au uhalali wa kuzuia jamii moja au nyingine isizungumzie jambo ambalo wao wanaliona ni muhimu.

"Bakwata inawataka maaskofu hawa waache tabia ya kuonyesha kuwa wao pekee ndio wana mamlaka ya kuiendesha serikali na viongozi wake kwani serikali na viongozi wamewekwa madarakani na Katiba ya nchi," Mzee aliwaambia wanahabari katika ofisi za Makao Makuu ya Bakwata, Kinondoni. Alisema Waislamu hawana tatizo na Wakristo na wamekuwa wakishirikiana, lakini kauli ya maaskofu inaleta hisia kuwa huenda kuna jambo limejificha.

"Tunachohitaji kukiangalia ni maslahi ya taifa na sio vinginevyo na sisi wakati wote tumekuwa tukiwasihi Waislamu wawe wavumilivu," alisema na kutoa mwito kwa viongozi wa dini wamrudie Mwenyezi Mungu, wahubiri umoja na mshikamano. Kwa mujibu wa Mzee, zipo nchi ambazo si za Kiislamu, zimejiunga na OIC na hazijageuzwa kuwa za Kiislamu hivyo maaskofu waache kupotosha kwa misingi ya kidini.

"Sasa tusiingize suala la udini kwenye maslahi ya taifa, sisi ni viongozi wa kiroho, tusiwafanye waumini wetu wakawa na wasiwasi badala ya kuwaondoa wasiwasi," alisema kiongozi huyo wa Bakwata. Kwa mujibu wa Mzee, OIC ni taasisi ya kimataifa kama taasisi nyingine na si taasisi ya kidini na akahoji kwa nini wanaopinga kujiunga na jumuiya hiyo hawapingi ushirikiano wa Serikali ya Tanzania na Benki ya Maendeleo ya Waislamu (IDB).

"Kauli ya maaskofu hawa inapotosha lengo sahihi la serikali la kuletea wananchi wake maendeleo, na kuligeuza kuwa suala la kidini. Katika kufanya hivyo maaskofu hawa wanaweza kuamsha hisia za mtafaruku wa kijamii na kidini," alisema Mzee wakati akisoma tamko la Bakwata.

Baraza hilo limeiomba serikali iendelee na mpango wa kuwaletea wananchi maendeleo kwa kuendelea na mchakato wa kujiunga na OIC na limemshauri Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe asijiuzulu.

"Bakwata inaipongeza serikali kwa kufuata taratibu za kikatiba na utawala bora, hivyo baraza linamshauri Mheshimiwa Membe asijiuzulu kwa shinikizo la maaskofu hao kwa kisingizio cha udini kwani kujiuzulu kwake kutaigawa nchi," ilisema sehemu ya tamko la baraza hilo.

Katika tamko hilo, Bakwata pia imepinga msimamo wa maaskofu kuhusu suala la Mahakama ya Kadhi kwa kusema kuwa mahakama hiyo ni suala la ibada kwa Waislamu na wala halina mjadala. Juzi, CCT ilimtaka Membe aache kuzungumzia suala la OIC na endapo anataka kuendelea kulipigia debe ajiuzulu. Maaskofu hao walidai kuwa pingamizi lao si la chuki ila wanazuia uwezekano wa taifa kugawanyika endapo Tanzania itajiunga na OIC na kwamba hilo likifanyika, pia Katiba ya nchi itavunjwa.
 
Wanaotaka tufuate mfano wa uganda napingana nao, hatuna cha kujifunza kuhusu amani toka uganda, kila kukicha uganda ni nchi ilyoko vitani, tutajifunza nini kule, tungejifunza kwenye zile nci zilizokataa kujiunga na kwa nini? Zimepoteza nini kwa kukataa kujiunga
 
Mkuu nakujua sana unavyoweza kubeba mzigo kama huu ukajaribu kutuvika sote msalaba... Unapounga maneno kama haya:- Waislamiu wote wahamie zanzibar na tuvunje muungano ili Zanzibar ingine OIC na Tanganyika ibaki secular..

Mkuu kweli unaweza kunambia ni serikali gani hiyo ya secular ambayo kwanza inawataka waislaam wote wahamie Zanzibar as if Tanganyika ni ya Wakristu.. Hii habari mnaitoa wapi haswa!..Hivi kweli huoni kuwa maneno haya yamebeba Udini zaidi hata ya hiyo OIC..

Mkuu Bob,

Heshima yako bro, kwanza naomba kuweka one thing clear kwamba hayo maneno unayojaribu kunipachika sio yangu, ni haki yangu kama ilivyo na yako hapa JF kuunga mkono au kutounga mkono anything bila au na maelezo.

Msimamo wangu kuhusu hii ishu uko wazi na nimeuweka bila kuchanganya maneno, sidhani kama ninahitajhi kuurudia maana nimeuweka wazi, lakini ukitaka ninaweza kuurudia tena anytime!
 
Jambo lolote lenye kuhusiana na uislamu lazima hutafutiwa njia ya kupingwa na kupotoshwa na Maskofu. Tabia hii imeendelea kwa muda mrefu tu kiasi kwamba wanasahau kabisa mchango waliotoa waislamu katika kuupigania UHURU wa tanganyika. Inasikitisha sana kuona heshima wanayoinyesha viongozi wa KIKRISTO juu ya UISLAMU na WAISLAMU. Hii habari ya serikali haina dini ila watu wana dini ni maneno yaliyokuwa na malengo fulani katika jamii. Ni kiasi gani yamefanikiwa, tunayaona sasa. Masuala ya OIC tuna yaangalia kwa makini sana.
 
Jambo lolote lenye kuhusiana na uislamu lazima hutafutiwa njia ya kupingwa na kupotoshwa na Maskofu. Tabia hii imeendelea kwa muda mrefu tu kiasi kwamba wanasahau kabisa mchango waliotoa waislamu katika kuupigania UHURU wa tanganyika. Inasikitisha sana kuona heshima wanayoinyesha viongozi wa KIKRISTO juu ya UISLAMU na WAISLAMU. Hii habari ya serikali haina dini ila watu wana dini ni maneno yaliyokuwa na malengo fulani katika jamii. Ni kiasi gani yamefanikiwa, tunayaona sasa. Masuala ya OIC tuna yaangalia kwa makini sana.

Suala ni nyeti hapa ni uvunjaji wa katiba, haya mengine ni maoni yako kutokana na propaganda mnazodanganyana misilkitini kwenu. Peleka hukuhuko tafadhali.
 
Katika hili tunaomba busara itumike ikizingatia katiba inasemaje na sio JAZBA, kwasababu uamuzi huu unagusa kila mtanzania bila kujali dini yake.Tanzania ni yetu sote uwe mkristo, muislamu au mpagani kwahiyo maamuzi kama haya yasielemee upande mmoja na kuufumbia macho upande mwingine kwa manufaa ya watu wachache! Rais awe makini na maamuzi kama haya na utafiti wa kina inabidi uzingatiwe na si kukurupuka, who knows for whom benefit?.
Huu sio mvutano kati ya mashehe na maaskofu ni jambo ambalo maaskofu wameliongelea kama viongozi wanaowakilisha kundi fulani katika jamii. Jambo hili ni kero yetu sote na wao ni wasemaji tu, hivyo serikali ndio mlengwa na sio imani fulani ya dini tusitumie udini katika kila jambo hautatufikisha popote; again tutumie busara Vs Jazba.
 
Maoni yangu...

We should have a referendum throughout the whole country tuone kama
wananchi wanataka kujiunga au la. Iwapo kama viongozi wa kisiasa na kidini
wataamua hili swala I don't think the voice of the people will be heard.

Mfano mzuri ni wa Uganda.They simply joined the organisation because Idi Amin said so na sio kama katiba ya OIC isemavyo...

Article 3 (2) "Any State, member of the United Nations, having Muslim majority...."
 
Hahaaa
Hapa tumefikia sehemu tamu mnooo!!!
Walidhani ukimya wa wakristo juu ya kadhi na OIC ni wajinga.
Maaskofu,Wakristo wote shime tulipinge hili na mengine yote kwa maslahi ya Taifa letu.
Hata kama ni vita tupigane tuuu,kwani vp?
Tutawakola bakora hadi mukione cha moto.
Big up kakobe,mtikila,gamanwa,n.k
 
Hahaaa
Hapa tumefikia sehemu tamu mnooo!!!
Walidhani ukimya wa wakristo juu ya kadhi na OIC ni wajinga.
Maaskofu,Wakristo wote shime tulipinge hili na mengine yote kwa maslahi ya Taifa letu.
Hata kama ni vita tupigane tuuu,kwani vp?
Tutawakola bakora hadi mukione cha moto.
Big up kakobe,mtikila,gamanwa,n.k

Mi naona hamna haja ya kupigana ..tupiganie nini?

Narudia kupendekeza, 'nchi iuzwe na kila raia apewe chake' halafu tuone huu upumbavu wa mkusanyiko wa watu wasiotaka kufikiri na serikali isio-deliver itakula wapi?
 
Wakulaumiwa hapa ni Mwinyi,wakati wa uongozi wake ndie alietaka kuibadili nchi hii kuwa "The United Islamic Republic Of Tz",wasomi wa mlimani walimjia juu,jamaa akawafukuza woooote.

Mwalimu nae alimpa dongo lile lile kwamba anaedhani nchi hii itakuwa ya kiislamu au kikristo ni mjinga,alivyo bwege akushtukia deal.

Aibu inamsuta sasa amekaa kimya,watz wanalumbana kukicha.

Madawa ya kulevya,kwa kiasi kikubwa yalichangiwa na mkewe,....hafu yuko kimya.

Kaingia JK muislamu mwenzake,wameona waanzishe yaleyale,waliumia sana Mkapa alipshinda.

Mkapa hakutaka hata kiduchu JK atinge ikulu,nyeti zinasema alipigwa mkwara mzito wa karne.....
 
Jambo lolote lenye kuhusiana na uislamu lazima hutafutiwa njia ya kupingwa na kupotoshwa na Maskofu. Tabia hii imeendelea kwa muda mrefu tu kiasi kwamba wanasahau kabisa mchango waliotoa waislamu katika kuupigania UHURU wa tanganyika. Inasikitisha sana kuona heshima wanayoinyesha viongozi wa KIKRISTO juu ya UISLAMU na WAISLAMU. Hii habari ya serikali haina dini ila watu wana dini ni maneno yaliyokuwa na malengo fulani katika jamii. Ni kiasi gani yamefanikiwa, tunayaona sasa. Masuala ya OIC tuna yaangalia kwa makini sana.

Kuu, jambo hili linahusu uisilamu ay Tanzania? Inayotaka kujiunga ni Tanzania na si Uisilamu. Maoni yako haya yananifanya kwa mara ya kwanza nianze kuhisi kuwa kweli kuna element ya udini katika suala hili.
Unapozungumzia mchango aliotoa waislamu katika kutafuta uhuru na kulihusisha na kujiunga OIC, inaonyesha kupotosha malengo yaliyotajwa kwa tanzania kujiunga na OIC. Serikali inasema inataka kunufaika na misaada na si kuwalipawaislamu fadhila kutokana na kushiriki kudai uhuru.
Unaweza kuona kuwa suala la 'serikali haina dini' kuwa ni la kipuuzi lakini jaribu kujifunza kutoka kwa nchi ambazo zinafuata sheria za kidini na utagundua hili maana yake ni nini
 
Yeah umenena
Nchi iuzwe tuuu,
Kila Mkoa ujitegemee kama nchi,au siyo?
Hahahhahah.
 
Yeah umenena
Nchi iuzwe tuuu,
Kila Mkoa ujitegemee kama nchi,au siyo?
Hahahhahah.

Kisha wale wa Masih walio wasafi tutajikusanya kuunda taifa letu huru (wale 'wengine' pia tutawakaribisha ila itabidi walipe JIZYA na kuwa ktk dhimmi ..LOL!)..Hii ndo theory nzima..halafu tuone nani wa kutuonea donge mwingine..
 
GAME THEORY upo wapi na hili unalionaje kwa sisi tuso na dini?
 
Naomba + nina hamu vita itokee Tanzania,tufundishane adabu,kama Rwanda,nidhamu iko ya kutosha kule sasa.

Yeah,tunazichapa,hadi kieleweke.

Vita vita ya udini Christian vs waislamu,nakukaribisha kwa hamu,hahahahah,tutazichapa chapa chapaaaa tuuuuu.

Huku jeshini tuna hamu sana ya kupasha,so ako kavita ka dini katasaidia sana,hahahah.

Membe,kuwa makini JK si mtu mzuri hata kidogo,anakutumia kama KAFARA,hahaha,yeah kafaraaaa.
 
Wakulaumiwa hapa ni Mwinyi,wakati wa uongozi wake ndie alietaka kuibadili nchi hii kuwa "The United Islamic Republic Of Tz",wasomi wa mlimani walimjia juu,jamaa akawafukuza woooote.

Mwalimu nae alimpa dongo lile lile kwamba anaedhani nchi hii itakuwa ya kiislamu au kikristo ni mjinga,alivyo bwege akushtukia deal.

Aibu inamsuta sasa amekaa kimya,watz wanalumbana kukicha.

Madawa ya kulevya,kwa kiasi kikubwa yalichangiwa na mkewe,....hafu yuko kimya.

Kaingia JK muislamu mwenzake,wameona waanzishe yaleyale,waliumia sana Mkapa alipshinda.

Mkapa hakutaka hata kiduchu JK atinge ikulu,nyeti zinasema alipigwa mkwara mzito wa karne.....


Hizi ni allegations zinazotolewa bila umakini wala uthibitisho. Imefika wakati watu wakawekewa "luku" kwenye keyboard zao.

Swali dogo, have u got anything to back up ur story or u just throw allegations for the sake of it?
 
Yeah Nchi iuzwe
Jk nchi imemshinda(mbowe said),ni kweli,imemshinda,lazima ajifunze,anamweka mtu kama Mama Simba,n.k watamsadia nini wale?zaidi ya kuimba mipasho!!!!!???Kaacha kina mama walio kamilika na wene uwezo wa kuongoza nchi hii,akihofu watampa challenge,hahahahah

Angalia hata mawaziri wake,waziri akiwa muislamu naibu mkristo and vice versa,anafikiria kukwepa kero za kidini badala ya kutuwekea watu safi na wenye uzalendo na nchi yetu.

Tazama balaza la kapa lilitulia,na maujinga kama ya sasa hayakuwepo.

Hahah,Munajua Wazenj and waislamu wanamchukia sana Mkapa,kwakuwa alikuwa serious,na hakupendelea upande wowowte,alikuwa fair,hahhaah

I miss u Mkapa,we need another Mkapa,2010.
 
Back
Top Bottom