Juu ya OIC na Mahakama ya Kadhi

Juu ya OIC na Mahakama ya Kadhi

Lakini Zanzibar Makadhi wapo na wanaye Kadhi Mkuu na hilo si kinyume na Katiba ya Muungano...?

kama mahakama zinachochea Ukuaji wa uchumi...basi acheni ziwe nyingi...
Mahakama ya matusi...Mahakama ya bangi...mahakama ya ndoa...Mahakama ya siasa..mahakana ya jinsia...
 
Hii issue ni lazima imeletwa na wanasiasa wenye nia mbaya na nchi yetu...

Mimi maoni yangu ni kwamba serikali na dini viwe mbali mbali....Inanishangaza sana kwa ndugu zetu waislam jinsi ambavyo wamekuwa wakitumika vibaya kisiasa na kupelekea migogoro isiyokwisha.

Hatataki kabisa serikali yetu iiingiliwe....Waislam wale SUNNI...Hao wanasikiliza Mekka huko Saudi....Na Shiite wao wanasikiliza huko kutoka kwa Imam Hussein....Huko IRAN.

Kama vile ilivyo Roman Catholic na VATICAN et etc...Ni wazi kuna chimbuko la taratibu za ku govern hizo congregations zao.

Hapo Tanzania Waislam wanahaki za kutosha kabisa kama Raia wengine wa dini nyingine...Tena wao ndio MATAJIRI WAKUBWA TANZANIA...Lakini hawaridhiki na wanataka ku SILIMISHA na SERIKALI.

Hapo Tanzania kuowa mke zaidi ya mmoja ni rhuksa na watu wanalimana talaka rejea nk huko mahakamani mbele za mahakimu na ama majaji....Sasa ndugu zangu waislam ni wapi hapo ambapo hamna haki?

Mnakumbuka mlipojaribu kuvunja mabucha ya nguruwe na kusababisha patashika nguo kuchanika hapo jijini?

Sasa kama ni wazi kuwa maagizo yenu mnatowa Saudi na Iran.....Je wao ndio wamewatuma muiambie serikali iwe na mahakama zenu?

Kwenye nchi nyingine duniani ni kinyume cha sheria kuoa mke zaidi ya mmoja...Sasa nyie mnataka hizo sheria zianze na nchini mwetu?
 
Mkamap,
Mkuu hapana anayekosea ni wewe na nitakueleza sababu zangu..
Serikali ya Tanzania kama serikali imeikuta dini ya kiislaam na hawa waislaam walikuwa na mfumo wao wa dini jinsi ya kuchagua viongozi wao na kadhalika. Nyerere ndiye aliyeanzisha Bakwata akilindwa na baadhi ya hao Masheikh...Sababu kubwa i kwamba Uinslaam wakati huo ulikuwa ni ndio nguvu ya Uhuru wa nchi za Kiafrika na walikuwa wakipigania haki za binadamu hasa ktk bara hili. kwa kufuata Ujamaa ambao hauna tofauti na Ukomunisti, Nyerere aliona haja ya kuwaweka waislaam ndani ya mkoba. Warusi na Wachina wao waliona dini zote ni hatari kwa sababu ilani za dini zote zilikuwa zinapingana na Udikteta!..Kwa hiyo toka hapo tulikuwa chini ya serikali na ilifahamika, pengine hata mimi ilikubaliana na mfumo huo kutokana na kwamba waislaam walikuwa ndio mstari wa mbele kugombea Uhuru wa nchi hii na tulipopata Uhuru they (Muslim leaders) expected to get something out of it - Kama binadamu.
Na kulikuwa na hatari ya kuwepo utengano wa nani kashiriki na nani alikuwa upande wa pili yaani ule wa mkoloni pamoja na kwamba Uhuru wetu ulikuwa kwa Watanzania wote bila kujali imani ama rangi zao hata kama ulipiganiwa na wachache.. Hiyo ndio imani yangu hivyo niliona umuhimu wa kuwekwa vikwazo fulani kwa wakati ule.. Baada ya hapo leo hii sioni sababu hizo tena isipokuwa naona domination ya wanasiasa ndani ya dini hiyo badala ya dini kuwa ni ibada ya kiislaam. na ndio maana swala hili limekwenda kwa Kaizar - Mkuu unauliza kitu ambacho hufahamu nani ameshikilia ule mkuki wa eagle..Yesu alihukumiwa Jerusalem na Kaizar hakuwepo, haina maana Kaizar hakuhusika..

Uhuru wa kuabudu ni lazima uzingatie taratibu z dini zetu iwe Wakatoliki, Lutheran au Waislaam kama zilivyokutwa na sio lazima kabisa kila dini ifuate utaratibu kama wa Katoliki wanavyofanya. Mbona Lutheran, Sabato na hata Budha hawachagui viongozi wao toka Vatican na hakuna mkono wa serikali?. Iweje leo serikali ikitambue chombo kimoja tu cha waislaam wote. chombo ambacho kilianzishwa na serikali yetu kwa kuwapachika baadhi ya watu ndani..Waulize hao Bakwata kama wanamtambua Sheikh mkuu anayeheshimika Ukerewe!..Kuna Politicians ndani ya Bakwata zaidi ya viongozi wa dini...

Na kama unaifahamu vizuri historia ya dini zetu na madhehebu yake ni tofauti kama hizi ndizo zilisababisha madhehebu kujikata toka dini iliyoanzishwa.. kwa hiyo unaposema Waislaam waige katoliki unakuwa unakwenda nje ya mada kujaribu kuwapatia waislaam solution inayotokana na makosa ya serikali hali ndani ya Ukiristu wenyewe yapo wadhehebu yasiyokubali kiongozi kuchaguliwa toka Vatican.
Kisha sisi waislaam hatuamini kabisa kuwa huko Makka ama sijui Teheran ndiko kuna viongozi ama waumini wa kweli wenye sifa za Uongozi.. Kiongozi bora wa dini ya kiislaam anaweza toka hata Ukerewe maadam anazo sifa za kuongoza dini..Huko Makka ndiko wamejaa mafuska wakubwa wenye upinzani mkubwa na dini yenyewe ya kiislaam kama unaielewa vizuri historia ya dini hii wapinzani wakubwa walikuwa waaarabu wenyewe -Makoreish! kwa hiyo Uislaam mkuu sio huo mnaopigiwa makampeni kila siku na Western world kujaribu kuuvunja.. lakini nakwambia hawataweza na hata siku moja hawatafanikiwa...

Kwa hiyo kifupi ni kwa serikali kuachia kabisa kujihusisha na uongozi wa dini hii wawaache huru na maswala ya kadhi yatakuwa hayawezi kufanya kazi kwa sababu Tanzania ya leo waislaam wanaishi nje ya maadili ya kidini..Waislaam jina ni wengi kiasi kwamba hata Kusali, kufunga mwezi wa Ramadhani, kutoa zaka na nguzo nyinginezo imekuwa ni HIARI ya mtu...Hivyo huwezi kuweka korti ya kadhi against watu ambao wanahiari ya kuchagua ibada zao kutokana na kutokuwepo sheria in the first place..
Korti za Kadhi haziwezi kufanya kazi wala mimi binafsi siwezi kukubali kuhukumiwa na korti hizi kwa sababu hakuna sheria ya Kiislaam inayofuatwa hivi, iwe bara ama Zanzibar sote tunapuyanga tu mradi siku inakwenda na status yetu imebakia palepale...
 
Mkamap,
Mkuu hapana anayekosea ni wewe na nitakueleza sababu zangu..
Serikali ya Tanzania kama serikali imeikuta dini ya kiislaam na hawa waislaam walikuwa na mfumo wao wa dini jinsi ya kuchagua viongozi wao na kadhalika. Nyerere ndiye aliyeanzisha Bakwata akilindwa na baadhi ya hao Masheikh...Sababu kubwa i kwamba Uinslaam wakati huo ulikuwa ni ndio nguvu ya Uhuru wa nchi za Kiafrika na walikuwa wakipigania haki za binadamu hasa ktk bara hili. kwa kufuata Ujamaa ambao hauna tofauti na Ukomunisti, Nyerere aliona haja ya kuwaweka waislaam ndani ya mkoba. Warusi na Wachina wao waliona dini zote ni hatari kwa sababu ilani za dini zote zilikuwa zinapingana na Udikteta!..Kwa hiyo toka hapo tulikuwa chini ya serikali na ilifahamika, pengine hata mimi ilikubaliana na mfumo huo kutokana na kwamba waislaam walikuwa ndio mstari wa mbele kugombea Uhuru wa nchi hii na tulipopata Uhuru they (Muslim leaders) expected to get something out of it - Kama binadamu.
Na kulikuwa na hatari ya kuwepo utengano wa nani kashiriki na nani alikuwa upande wa pili yaani ule wa mkoloni pamoja na kwamba Uhuru wetu ulikuwa kwa Watanzania wote bila kujali imani ama rangi zao hata kama ulipiganiwa na wachache.. Hiyo ndio imani yangu hivyo niliona umuhimu wa kuwekwa vikwazo fulani kwa wakati ule.. Baada ya hapo leo hii sioni sababu hizo tena isipokuwa naona domination ya wanasiasa ndani ya dini hiyo badala ya dini kuwa ni ibada ya kiislaam. na ndio maana swala hili limekwenda kwa Kaizar - Mkuu unauliza kitu ambacho hufahamu nani ameshikilia ule mkuki wa eagle..Yesu alihukumiwa Jerusalem na Kaizar hakuwepo, haina maana Kaizar hakuhusika..

Uhuru wa kuabudu ni lazima uzingatie taratibu z dini zetu iwe Wakatoliki, Lutheran au Waislaam kama zilivyokutwa na sio lazima kabisa kila dini ifuate utaratibu kama wa Katoliki wanavyofanya. Mbona Lutheran, Sabato na hata Budha hawachagui viongozi wao toka Vatican na hakuna mkono wa serikali?. Iweje leo serikali ikitambue chombo kimoja tu cha waislaam wote. chombo ambacho kilianzishwa na serikali yetu kwa kuwapachika baadhi ya watu ndani..Waulize hao Bakwata kama wanamtambua Sheikh mkuu anayeheshimika Ukerewe!..Kuna Politicians ndani ya Bakwata zaidi ya viongozi wa dini...

Na kama unaifahamu vizuri historia ya dini zetu na madhehebu yake ni tofauti kama hizi ndizo zilisababisha madhehebu kujikata toka dini iliyoanzishwa.. kwa hiyo unaposema Waislaam waige katoliki unakuwa unakwenda nje ya mada kujaribu kuwapatia waislaam solution inayotokana na makosa ya serikali hali ndani ya Ukiristu wenyewe yapo wadhehebu yasiyokubali kiongozi kuchaguliwa toka Vatican.
Kisha sisi waislaam hatuamini kabisa kuwa huko Makka ama sijui Teheran ndiko kuna viongozi ama waumini wa kweli wenye sifa za Uongozi.. Kiongozi bora wa dini ya kiislaam anaweza toka hata Ukerewe maadam anazo sifa za kuongoza dini..Huko Makka ndiko wamejaa mafuska wakubwa wenye upinzani mkubwa na dini yenyewe ya kiislaam kama unaielewa vizuri historia ya dini hii wapinzani wakubwa walikuwa waaarabu wenyewe -Makoreish! kwa hiyo Uislaam mkuu sio huo mnaopigiwa makampeni kila siku na Western world kujaribu kuuvunja.. lakini nakwambia hawataweza na hata siku moja hawatafanikiwa...

Kwa hiyo kifupi ni kwa serikali kuachia kabisa kujihusisha na uongozi wa dini hii wawaache huru na maswala ya kadhi yatakuwa hayawezi kufanya kazi kwa sababu Tanzania ya leo waislaam wanaishi nje ya maadili ya kidini..Waislaam jina ni wengi kiasi kwamba hata Kusali, kufunga mwezi wa Ramadhani, kutoa zaka na nguzo nyinginezo imekuwa ni HIARI ya mtu...Hivyo huwezi kuweka korti ya kadhi against watu ambao wanahiari ya kuchagua ibada zao kutokana na kutokuwepo sheria in the first place..
Korti za Kadhi haziwezi kufanya kazi wala mimi binafsi siwezi kukubali kuhukumiwa na korti hizi kwa sababu hakuna sheria ya Kiislaam inayofuatwa hivi, iwe bara ama Zanzibar sote tunapuyanga tu mradi siku inakwenda na status yetu imebakia palepale...

Mkuu Mkandara
Kuhusu hii historia ya kwamba waislamu ndio walikua mstari wa mbele kupigania uhuru wa tz na afrika kwa ujumla Hii ni mpya kabisa kwangu labda niwaachie watu waliokwenda chumvi kidogo wanisaidie maana sijawahi kuisikia wala kuisoma.

Ila siwezi acha hivi hivi tu mimi nitaunganisha pointi zangu ili niukaribie ukweli ,
Mkandara nikiangalia kwa haraka haraka naona majina karibu yote ya wapigania uhuru AFRIKA ni ya Kikristu ,ndiyo pamoja jina linaweza kua la kiislamu harafu mtu husika ni mkristu ni kwa kiwango kidogo sana kwa wakati huo,natambua haya majina yalianza kujichanganya miaka ya 80 baada ya watu kuanza kutumia majina ya watu kurudia ama kukalili shule za misingi.

Pia nikiangalia kwa haraka haraka historia naona wakoloni walikutana na upinzani mkali kutoka Bara kama akina Mkwawa,Mirambo,Isike akina Meli na walipata mteremko pwani ambako ilikua eneo la waislamu,ktk kuunganisha points zangu naona hawa wajukuu wa mkwawa ,meli nafikiri walikua na machungu zaidi ya kupigania uhuru kuliko wapwani.

Bado nikijaribu kuunganisha vijipoints naona kabisa kama hiyo ndiyo ingekua case basi ZANZIBAR ingepata uhuru wake mapema

Sikatai ni mtazamo wangu tu mkuu wa kua WAISLAMU wakati huo nadhani ilikua ni vigumu kupigania haki maana walikua hawajaenda shule.Tena enzi hizo mpaka za juzijuzi zilikua ni MADRASA tu ,walioleta dini ya kiislamu yani waarabu walijenga ama hawakujenga shule kabisa zaidi ya MADRASA tofauti na shule nyingi za kikristu na wakristu wengi wakati huo kwenda shule.

Tujikumbushe tu baada ya uhuru kulikua na middle school ngapi za waislaamu??
Huo ni mtazamo wangu tu ngoja niwaachie wazee wazima waje watupe ukweli.

Kuhusu wakatolik ,katolik ni dhehebu ktk ukristu na hivyo huyo anayepinga maaskofu na makadinal kuteuliwa kutoka VATICAN na yeye si mkatolik ni munafiki tu.
kumbuka VATICAN ni makao makuu ya katolik na si ya wakristu nadhani umenielewa.
 
Hoja za Makakama ya Kadhi ni Dhaifu - (Makala ya Gazeti la Kulikoni)

Mchungaji/Mwanasiasa Christopher Mtikila amefungua kesi mahakamani kupinga rasmi uanzishwaji wa Mahakama ya Kadhi nchini kwa madai kuwa ni kinyume na Katiba. Mjadala huu siyo mgeni na umekuwepo katika jamii yetu kwa muda mrefu na bila ya shaka ni lazima ufikie wakati ambapo unamalizwa kwa kuanzisha mahakama hiyo kama ndugu zetu Waislamu wanavyotaka au kutoanzishwa mahakama hiyo kama baadhi ya watu wengine wanavyotaka (wawe Wakristu au vinginevyo). Kama Taifa, lazima tujifunze kuanzisha mijadala na kuihitimisha ili tuendelee na mambo mengine. Ni kutotumia muda vizuri kama tutakuwa tunaendelea kuzungumzia jambo lile lile miaka nenda, miaka rudi badala ya kuamua kuzungumza jambo na kulimaliza, hasa linaloweza kumalizika kiungwana, kitaalam, na kidugu kama suala la Kadhi.

Binafsi naamini kuwa hoja ambazo zinatolewa hadi hivi sasa kuhusu haja, ulazima, na haraka ya kuanzishwa kwa mahakama hiyo Tanzania bara ni hoja dhaifu ambazo bado hazina nguvu. Ni mpaka pale watetezi wa uanzishwaji upya wa mahakama ya Kadhi watakapojenga hoja zenye nguvu, ambazo zinaweza kusimama siyo katika kuvutia hisia za watu, bali katika kushawishi akili zao na kuona kuwa ni hoja za msingi na zisizopingika kirahisi, basi kuanzishwa kwa mahakama hiyo nchini kutaendelea kuchelewa na kwa hakika kunapaswa kuchelewa.

Kabla ya kuziangalia hoja hizi na kuonesha udhaifu wake, naomba kwanza niseme mambo machache ambayo ni muhimu kuyazingatia katika mjadala huu. Kwanza kabisa, kesi iliyofunguliwa na Mch. Mtikila kuhusu kupinga uanzishwaji wa mahakama hiyo ni suala la kwake kama raia wa nchi hii. Isichukuliwe hata kidogo kuwa Mtikila anawakilishwa Wakristu wa Tanzania katika kesi hii. Hivyo basi kauli zake zenye kuumiza hisia za Waislamu zichukuliwe kama ni kauli zake na zisichukuliwe kama ni maneno ya Wakristu dhidi ya ndugu zao waislamu. Na kama ilivyokawaida ya viongozi wetu wa Kikristu hakuna aliyetokea hadharani na kupinga kauli za Mtikila kuwa haziwakilishi mawazo au misimamo ya makanisa nchini. Ingekuwa jambo la kupendeza kusikia TEC, CCT, na Muungano wa Makanisa mengine kutoa kauli zao kupinga madai ya Mtikila kuwa kuanzishwa mahakama ya kadhi kutachochea Ugaidi na kuleta vurugu.

Jambo la pili ni kuwa, binafsi sina tatizo na uanzishwaji wa mahakama ya Kadhi Tanzania bara, na sina sababu ya kuwa na hofu ya kuwepo kwake. Nimebahatika siyo tu kuishi na Waislamu bali pia kukulia na kusoma kati yao na kuwa na marafiki wa karibu na wengine imefikia familia zetu kuoleana n.k Siwezi kuamini hata kidogo kuwa Watanzania wenzetu hawa ambao ni Waislamu watageuka na kuwa Afghanistani au Iraq na kuanza kututendea vibaya kisa tu ati mahakama ya kadhi imeanzishwa. Waislamu wa Tanzania ni mfano bora kabisa katika ulimwengu wa mahusiano mazuri kati ya watu wa imani tofauti katika nchi. Ni lazima tujivunie tofauti yetu na hasa pale ambapo tofauti hiyo inatufanya tuzungumze kwa uhuru, kwa heshima, na kwa upendo kati yetu.

Jambo la tatu hapa ni kuwa, utakapofika mwisho wa mjadala huu ni lazima tubakie na heshima na hisia yetu ya Utanzania. Itakuwa jambo baya na la hatari kama tutafikia mwisho wa mjadala huu na kujikuta ni “watanzania wapenda Kadhi” na “Watanzania wapinga Kadhi”. Tofauti ya maoni na mitazamo ni kiini cha utawala wa demokrasia kwani kwa kutofautiana ndipo tunapata nafasi ya kupata mawazo mazuri na yenye nguvu zaidi. Kwa sababu hiyo basi, kusiwe na Mtanzania yeyote yule mwenye hofu ya mjadala huu. Wale Mashehe waliozungumza kwenye kipindi cha “Jenerali on Monday” wasitupe sababu ya kuwa na hisia ya vurugu au uvunjifu wa amani. Katika maneno yao ya mwisho siku ile, ndugu zetu hawa “waliwasihi” Waislamu nchini kuwa “wawe watulivu na kutoleta vurugu”. Ni nani kawaambia kuwa Waislamu ni watu wa shari au wanataka kuleta vurugu kwa sababu tu Mtikila kafungua kesi Mahakamani? Ni lazima wao viongozi wa dini waoneshe imani kwa Waislamu wenzao kuwa wanafahamu umuhimu wa utulivu na amani, na wao si chanzo cha uvunjifu wa amani kisa tu ya mjadala wa Kadhi. Na katika hili, ningependa kuona viongozi wengine wa Kiislamu wakiwaweka sawa hawa wenzao ambao waliashiria kuwa Waislamu si watu wa amani na utulivu. Kama vile maaskofu walivyokaa kimya kuhusu Mtikila, vivyo hivyo Maimamu na Mashehe wengine nao wamekaa kimya katika hili.


Baada ya kusema hayo turudi kwenye kichwa cha habari cha hoja ya leo kuwa hoja zinatolewa ili Mahakama ya Kadhi irudishwe Tanzania Bara ni hoja dhaifu. Naomba nieleweke sisemi kuwa hoja hizi ni za kupuuzia (kama watu wengine wafanyavyo wasipoweza kujibu hoja), bali ni hoja zenye kujibiwa. Udhaifu wake unatokana na ukweli kuwa zikiangaliwa moja baada ya nyingine tena kwa karibu zaidi bila hata ya kutumia darubini utaona kuwa zimepotoka ndani kwa ndani (inherently flawed). Kwa muda mrefu sasa nimesubiri kuona kama kuna mtu ambaye atathubutu kuzijibu hoja hizi na kuzionesha kuwa hazifai. Mtu huyo hajatokea na badala yake yupo mtu aliyekimbilia mahakamani. Hetu tuziangalie hizi hoja ambazo hutajwa sana kuwa kwanini Mahakama ya Kadhi ianzishwe tena kwa sheria ya Bunge na uwepo wake uunganishwe katika utaratibu wa mahakama za Tanzania. Kwa maneno mengine, kwanini Waislamu wanataka serikali ianzishe mahakama ya Kadhi Tanzania Bara.

Hoja ya 1: Mahakama ya Kadhi imeahidiwa na serikali ya CCM, hivyo Chama cha Mapinduzi kitimize ahadi yake ama sivyo watakiona 2010.

Nimepata nafasi ya kuangalia Ilani ya Uchaguzi ya CCM, na kuhusu suala la kadhi ahadi waliyoitoa inasema hivi “CCM itazitaka Serikali ziendelee na hatua zilizoanza kuchukuliwa ili kuiboresha Sekta ya Sheria kusudi nayo itoe huduma bora zaidi kwa jamii. Yatakayosisitizwa katika kipindi hiki ni pamoja na yafuatayo…. Kulipatia ufumbuzi suala la kuanzishwa kwa Mahakama ya Kadhi Tanzania Bara”

Hivyo utaona kuwa CCM haijatoa ahadi ya kuanzisha mahakama ya Kadhi Tanzania bara, bali “kulipatia ufumbuzi suala la kuanzishwa” kwa mahakama hiyo. Hii ina maana ya kuwa CCM inaweza kabisa kushiriki kwa namna fulani (kwa sera au utunzi wa sheria) kuhakikisha kuwa mahakama ya kadhi inapokuwepo Tanzania bara. Hilo bila ya shaka limechukuliwa kumaanisha kuwa CCM itarudisha Mahakama ya Kadhi kwa kuitungia sheria ya kuianzisha, kuitengea bajeti, na kuiendesha mahakama hiyo. Hii si tafsiri sawa sawa au ya pekee (inawezekana kuwa ni tafsiri mojawapo ya ahadi hiyo) kama nitakavyoonesha baadaye.

Hata hivyo mtu anaweza kusema ahadi hiyo ina maana ya kurudisha mahakama ya kadhi na mimi nimeielewa vibaya. Katika hotuba yake ya bajeti ya mwaka 2005/2006 aliyekuwa Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. H. Bakari Mwapachu alisema hivi kuhusu sehemu hiyo ya Ilani, “aidha, (kuhusu) suala kadhi, litafanyikwa kazi”. Na hata katika bajeti ya wizara hiyo chini ya Waziri Mpya Bi. Mary Nagu na yeye hakutoa ahadi mpya ila iliyokuwemo kwenye ilani ya CCM kuwa katika mwaka huu Wizara yake kwa kutumia Tume ya Kurekebisha Sheria itapitia mambo mengi miongoni mwake ni “kulipatia ufumbuzi suala la Uanzishwaji wa Mahakama ya Kadhi, Tanzania Bara”.

Kwa kifupi, serikali ya CCM haikuwaahidi waislamu kuanzisha Mahakama ya Kadhi. Ilichoahidi ni kutafuta ufumbuzi jinsi gani inaweza kuanzishwa pasipo kupingana na sheria au kutengeneza sheria itakayowezesha kuanzishwa kwake. Kilichofanyika ni sawa na mtu kuahidi kuwa kwa vile una matatizo ya mahali pa kuishi basi “atafanya kila jitihada kukutafuta ufumbuzi wa tatizo lako la makazi ili na wewe uweze kujisitiri na famili yako”. Itakuwa ni jambo la kuchekesha kama mtu atatoka na kuanza kudai nyumba kutoka kwa aliyetoa ahadi!!

Sasa haina maana kuwa serikali haitarudisha mahakama ya kadhi bali ina maana katika kutafuta ufumbuzi wa suala la kadhi, kurudisha kwa kutunga sheria inayounda Mahakama ya Kadhi kama zilivyo sheria za Mahakama ya Biashara kwa mfano, ni mojawapo tu ya vitu vinavyowezekana, na kwa hakika siyo jambo pekee.

Hivyo ili hoja hii iwe na nguvu kidogo, ndugu zetu Waislamu wawabane CCM na kuwauliza walichowaahidi hasa ni nini? Je wameahidiwa Kurudishwa kwa Mahakama ya Kadhi au kutafutiwa ufumbuzi wa kurudishwa kwa mahakama hiyo? Baadhi ya Wabunge wa CCM wameoneshwa kukerwa na utata huu wa makusudi na wamehoji iweje ahadi ya kushughulikia suala la kadhi inachukua zaidi ya miaka kumi sasa?

Hoja ya 2. Mahakama ya Kadhi ilikuwepo wakati wa Ukoloni, hivyo kama ilikuwepo wakati wa Ukoloni kwanini isiwepo sasa?

Hoja hii ina nguvu kidogo lakini msingi wake unamashaka. Jambo kufanywa na wakoloni au kuruhusiwa na wakoloni hakulifanyi jambo hilo kuwa jambo sahihi au ambalo tuliendeleze jinsi ile ile. Wakoloni katika nchi mbalimbali walifanya mambo mbalimbali kwa malengo tofauti tofauti. Kuna mambo ambayo wakoloni waliyafanya au taasisi walizozianzisha ambazo sisi kama nchi huru tuliamua kuachana nazo.

Zaidi ya yote, tangu lini tumeanza kutukuza wakoloni? Hivi kweli hoja haiwezi kujenga ikasimama wenyewe hadi tupige magoti na kuonesha kile “walichofanya wakoloni”. Huku ni kujidhalilisha kusiko kwa lazima. Na kama jambo lilifanywa na wakoloni haina maana jambo hilo lilikuwa sawa. Si hawa hawa wakoloni wanaolalamikiwa na Waislamu kuwa ndio walioweka misingi ya kuwapendelea Wakristu? (soma kitabu cha Hamza Njozi na kile cha Mohammed Said). Si ndiyo hawa wakoloni waliowatenda vibaya waislamu kwa mambo yao kama yanavyosimuliwa katika nyaraka mbalimbali za kihistoria? Ni lazima tukubaliane kuwa kutumia Wakoloni kama msingi wa kujenga hoja ya kadhi ni mkakati mbovu.

Hoja ya 3. Nchi nyingine majirani na za kiafrika zina mahakama ya kadhi kwanini sisi tuogope?

Hoja hii ukiingalia kwa haraka ina nguvu ya “kufanana” na ushawishi wa “ukaribu”. Mara nyingi katika hoja hii kauli inayofuatia ni “mbona hata Zanzibar Mahakama ya Kadhi ipo kwanini isiwepo hapa Bara?” Hoja hii nayo ina msingi lakini haina nguvu ukiingalia kwa karibu. Kwa kuzihusu nchi nyingine hoja hii ina udhaifu mkubwa ufuatao, Tanzania ni nchi huru inayojiamulia mambo yake yenyewe na haishinikizwi kwa namna yoyote ile kufuata kile ambacho nchi nyingine inafanya.

Kuna mambo ambayo nchi nyingine zinafanya na sisi hatufuati. Kuna nchi ambazo zinatambua uwepo wa mahakama ya Kadhi lakini zina mambo mengine ambayo hatuambiwi tuyafuate pia. Afrika ya Kusini inayo Kadhi lakini hao hao wanaruhusu mashoga kuoana. Sasa kama vinavyofanya na sheria za nje ni mambo ya kufuata kwanini tufuate la kadhi tu na tusifuate la kuruhusu mashoga kuoana?

India ambako tuna ukaribu zaidi wa kisheria labda kuliko sehemu nyingine yoyote katika jumuiya ya Madola, wao wanazo mahakama za kadhi lakini hazitambuliki na sheria ya India lakini hazipingwi na maamuzi yake yanakuwa ni ushauri tu usio na nguvu ya kisheria na uamuzi huo hamzuii Muislamu kwenda katika mahakama za serikali. Kwanini tuchague kufuata ya Kenya na siyo ya India? Nchi kama Uturuku ambazo zina Waislamu wengi kuliko Tanzania hazina Mahakama ya Kadhi jinsi zinavyotakwa hapa Tanzania. Wao (Waturuki) ingawa mahakimu wao wanaitwa “Makadhi” kutokana na sababu za kihistoria lakini hawahukumu kwa sheria za Kiislamu.

Kwa kifupi ni kuwa, suala la kadhi linawahusu Watanzania na ni Watanzania ambao wagonganishe vichwa vyao wakikusanya mang’amuzi ya utaalamu wao mbalimbali na kutafuta suluhisho ambalo ni la Watanzania na la Kitanzania.

Itaendelea wiki ijayo kwa kuangalia hoja nyingine zilizosalia na zile hoja zenye nguvu.

Ndugu Mzee Mwanakijiji, asante sana kwa mchango wako mzuri. Nakushauri mchango huu ikiwezekana uuchapishe gazetini ili watu wasioweza kuusoma hapa wausome gazetini. Umechambua hoja vizuri sana.

Nionavyo mimi, kuna vitu vinachanganywa na haviongelewi kabisa na wanaotaka Mahakama ya Kadhi ianzishwe hapa Tanzania.


1. Mahakama ya Kadhi ni haki ya Waislamu na Katiba ya Tanzania inaheshimu uhuru wa kuabudu na inasema kuendesha mambo ya kiimani kwa dini au madhehebu husika SIYO jukumu la serikali bali dini au dhehebu husika. Rejea Katiba ya Tanzania (1977), [Article 19(2)].

2.Waislamu wanataka liwe jukumu la serikali kuanzisha Mahakama hii.

3. Tatizo ni kwamba kwa vile serikali haina dini ila wananchi wake ndio wenye dini, ombi la Waislamu linakuwa na maana kuwa serikali ina dini (yaani, hili likitekelezwa kama linavyodaiwa na waumini wa Kiislamu) basi dini na madhehebu mengine nayo yatapenda iwe hivyo kwa imani zao.

4. Serikali ikibadilisha Katiba na kuanza kutoa upendeleo kwa dini moja, ambayo mahakama zake zitafadhiliwa na walipa kodi wegine, basi uhuru wa dini utakuwa umeingiliwa au serikali itaonekana inapendelea dini moja.

5. Kanisa Katoliki lina mahakama zake (ecclestiastical tribunalas) - mbona haziendeshwi na kodi ya walipa kodi bali waumini tu wa Kikatoliki?

6. Hoja kwamba Kenya, Uganda na nchi nyingine mbona zina mahakama hizi, haina uzito kama alivyosema Mzee wa Kijiji kwa sababu hatufanyi kitu Tanzania kwa vile kinafanyika sehemu nyingine. Tunafanya au hatufanyi kwa vile tunaona ama kitu hicho kinatufaa sisi kulingana na utamaduni na mahitaji yetu na hatufanyi kama tunaona hatuna sababu bado ya kufanya hivyo.

7. Mimi nashauri Mahakama za Kadhi zianzishwe na Waislamu wenyewe na wasisubiri serikali iwafanyie kwa vile Katiba yetu imeshatoa uhuru huo wa kuendesha mambo ya dini kuwa jukumu la dini au dhehebu husika. Kwani Waumini wa Kiislamu hawawezi kufanya hivyo?

8. Wanaosema kama Mahakama ya Kadhi haianzishwi basi kutaweza kutokea vurugu nadhani ni wao wenyewe watakaoanzisha vurugu hizo. Kwa kawaida Waislamu wa kawaida huko mitaani kwetu hawana shida hiyo. Kukitokea msiba tunashirikiana hata kwa ujenzi wa msikikiti au kanisa. Ni waumini baadhi tu kwa pande zote mbili - Waislamu na Wakristo - wenye ubaguzi kwa sababu ya dini.
 
Kwani; naomba kuuliza. Unajua tena sisi wengine hatujaenda shule.

WAISLAMU WAMEKATAZWA KUANZISHA MAHAKAMA YAO WENYEWE KUPITIA BAKWATA?

Kwani mpaka hela yangu mie mlokole ikalipie kesi za kiislamu? (ikianzishwa na serikali)

Ka swali tu naomba jibu jamani
 
MANENO HAYA ULIYOYASEMA NI KWELI TUPU NA YANAONYESHA BUSARA NA KUTOFUNGAMANA NA UPANDE WOWOTE!WAARABU NA WAZUNGU WALILETA DINI ZAO AFRIKA ZIKATUTENGANISHA,NDUGU KATI YA NDUGU,KIJIJI KATI YA KIJIJI AND SO ON..MWANAKIJI ANADAI KUWA MAHAKAMA YA KADHI ILIKUWEPO WAKATI WA UKOLONI KWA HIYO TUIKUBALI!?NANI KASEMA MFUMO WA UKOLONI ULIKUWA NI WA MANUFAA YA WATAWALIWA?NANI ASIYEJUA KUWA KWA UMBUMBUMBU WETU WATANZANIA CCM NA SERIKALI AKE BADO WANATUMIA KATIBA ILE ILE YA KIKOLONI YENYE KUWANYIMA HAKI WATAWALIWA?NI HIVI KARIBUNI TU WAISLAM WAMEUNDA KAMATI YA KUPINGA UBALOZI WA VATICAN NCHINI KWA MADAI KWAMBA NI YA KIKRISTO NA SERIKALI HAITAKIWI KUWA NA UHUSIANA NA SERIKALI YENYE MWELEKEO WA KIDINI,JE WAKRISTO NAO WAKIZIPINGA BALOZI ZA IRAN NA SAUDI WATAKUWA WAMEKOSEA?JE HIZI ISSUE ZINATUGAWA AMA KUTULETA PAMOJA?NA NI KWELI KUWA AHADI WALIZOTOA CCM ZINAWEZA KUWATOKEA PUANI KWASABABU WALITOA AHADI HIZO ILI WAENDELLE KUKAA MADARAKANI,SASA THIS TIME MAMBO ITAKUWA MSHIKE MSHIKE,NA UPINZANI NAO LAZIMA WATAKOMAA NAO!HIVI KWELI TUNAKOELEKEA KUNA USALAMA?

Asante sana kwa mchango wako JMushi. Unajua tatizo letu kubwa ni kwamba tunayumbishwayumbishwa na watu wachache. Hatuna kitu kinachoitwa INDEPENDEDNT JUDGEMENT. We are not yet transformed by our core values.

Mimi ni Mkristo, lakini kwa imani yangu naheshimu dini zote kama njia zinazotupeleka kwa Mungu. Of course, njia nyingine ni fupi na nyingine ndefu - lakini cha msingi njia zote zinatupeleka kwa Mungu.

Kwa imani yangu hii naheshimu kuanzishwa Mahakama ya Kadhi kwani Waislamu wana haki na uhuru wa kuanzisha Mahakama hii na Katiba yetu imewapa waumini wa dini zote uhuru wa kuabudu na kuendesha mambo yao ya kiroho bila kuvunja sheria za nchi.

Tatizo langu ni kuona kwa nini Waislamu wanaona uhuru huo hautoshi na bado wanashinikiza mpaka isemwe waziwazi kwenye katiba kuwa kutakuwa na Mahakama ya Kadhi. Mbona dini au madhebu mengine wanafanya mambo yeo bila ya lazima kurekodiwa kwenye katiba.

Halafu kampeni za kupinga uwepo wa ubalozi wa Vatican nchini si kutasababisha Wakristo nao waanze kuchokonoachonoa mambo na hatimaye watu wengine wataanza kubuni mfumo mbadala utakaoondoa dini zote kama ule wa kikomunisti ambao hauruhusu hata kuabudu katika imani fulani zaidi ya ukomunisti?
 
Kigarama,
Bakwata ni chombo cha serikali kilichowekwa kwa ajili ya Waislaam na ndicho nilichokizungumzia hapo nyuma...Nimesema Kiongozi Sheikh mkuu na chombo kinachowaongoza..
Kama unakumbuka waislaam chini marehemu Sheikh Kassim bin Jumaa walianzisha chombo cha waislaam, viongozi wake wakichaguliwa na waislaam na ilileta mgogoro mkubwa hata kufikia Sheikh huyo kuitwa gaidi na alikamatwa kisha waka Mkolimba!...

Kwa hiyo, jibu swali langu kama unaelewa nachouliza badala ya kusema Bakwata ni chombo cha waislaam hali serikali ndiyo inayokiongoza kwa kodi za wananchi!.. Muslims don't want that! kwa nini nyie nyote msipige makelele kuwepo kwa Bakwata ambayo inatumia mifuko yenu (kodi), kitu ambacho waislaam hawakihitaji kama dini nyinginezo. KKK haikuanzishwa na serikali wala kiongozi wake kuchaguliwa na chombo cha serikali.. Hilo ndio swali langu..
Mkuu mimi nafahamu vizuri historia ya Bakwata na ilieleweka wakati wa Nyerere kwa baadhi yetu lakini leo hii sioni sababu ya serikali kuendelea kusimamia maswala ya dini hii...Uislaam bado uko controlled na serikali hili ni wazi kabisa.
Tofauti ya kufuata udaku na kufanya utafiti hujionyesha kwenye misimamo, hata kama una misimamo ya kuichukia serikali au kwa wazo lako linalozungumza likiwa limenyamaza, kwamba BAKWATA ilianzishwa na wakristo (Nyerere na wenzake) lakini ukweli ulio wazi ni kwamba BAKWATA si mali ya serikali wala haiendeshwi kwa kodi za watanzania

kama unakumbukumbu yoyote ile inayothibitisha kwamba serikali imewahi kuchagua viongozi wa BAKWATA tafadhali sana tukumbushe wenzio!
 
Ati mtu akibadilisha dini, mahakama ya kadhi itafanya nini?...kwani mahakama ya serikali itafanya nini!.. again Mbona pumba zinazidi humu... haya kweli ni maswali ya mtu mwenye akili timamu?

utimamu huja kwa tafakuri,hivi unadhani vichaa wanatuona sisi tuna akili timamu? lakini swali langu lina mantiki unayotakiwa kuiona na kuijibu. kwenye nchi nyingi zenye mahakama ya kadhi kubadili dini ni dhambi kubwa sana kama uhaini kwenye dola.

watu wanaobadili dini kwa mujibu wa imani za kiislamu wamemuasi mungu na adhabu yao inapaswa kuwa kubwa. sasa kwa kuwa katika nchi yetu imekuwa kawaida mtu kutoka uislamu na kwenda kwenye ukristo au ukristo kwenda uislamu na kuwa hakuna tatizo katika hilo, sawali langu ni kwamba mahakama ya kadhi itavumilia uasi wa waislamu dhidi ya dini yao?
 
Kwani; naomba kuuliza. Unajua tena sisi wengine hatujaenda shule.

WAISLAMU WAMEKATAZWA KUANZISHA MAHAKAMA YAO WENYEWE KUPITIA BAKWATA?

Kwani mpaka hela yangu mie mlokole ikalipie kesi za kiislamu? (ikianzishwa na serikali)

Ka swali tu naomba jibu jamani

Hapa ndipo kwenye tatizo kwani hiyo BAKWATA nani kaipa mandate ya kuwakilisha maslahi ya waislamu.....

Na pia kama ikianzishwa na Bakwata itatambulikaje, kukubalika na kuheshimika katika mfumo wa kisheria wa nchi yetu?

je kuwa chini ya BAKWATA ndio kutaondoa uwezekano wa mahakama hizi kutumika kwa masuala mengine kuliko yale yaliokusudiwa?

Je ni vipi tutaweza kuhakiki athari za matumizi mabaya ya mahakama hiyo ambazo zinaweza kuhatarisha amani, usalama na haki za watanzania waislamu? Hudhani kuwa ikianzishwa na serikali ndio rahisi kuzicontain zisivuke mipaka yake?

Vilevile kumbuka kuwa kuharibikiwa kwa waislamu ni kuharibikiwa kwa watanzania hivyo tusiliangalie suala hili kwa muono wa maslahi ya waislamu pekee.....


Naomba ufikirie maswali haya na uangalie kama ni busara ama sio busara kuanzishwa ama kutoanzishwa na kusimamiwa na serikali yetu wote...
 
Tofauti ya kufuata udaku na kufanya utafiti hujionyesha kwenye misimamo, hata kama una misimamo ya kuichukia serikali au kwa wazo lako linalozungumza likiwa limenyamaza, kwamba BAKWATA ilianzishwa na wakristo (Nyerere na wenzake) lakini ukweli ulio wazi ni kwamba BAKWATA si mali ya serikali wala haiendeshwi kwa kodi za watanzania

kama unakumbukumbu yoyote ile inayothibitisha kwamba serikali imewahi kuchagua viongozi wa BAKWATA tafadhali sana tukumbushe wenzio!

Kama nadhani wewe ndiye unapaswa kupitia facts zako kwanza kuhusu kuanzishwa na mahusiano ya BAKWATA na serikali.....

Tanzanianjema
 
Hii issue ni lazima imeletwa na wanasiasa wenye nia mbaya na nchi yetu...

Mimi maoni yangu ni kwamba serikali na dini viwe mbali mbali....Inanishangaza sana kwa ndugu zetu waislam jinsi ambavyo wamekuwa wakitumika vibaya kisiasa na kupelekea migogoro isiyokwisha.

Hatataki kabisa serikali yetu iiingiliwe....Waislam wale SUNNI...Hao wanasikiliza Mekka huko Saudi....Na Shiite wao wanasikiliza huko kutoka kwa Imam Hussein....Huko IRAN.

Kama vile ilivyo Roman Catholic na VATICAN et etc...Ni wazi kuna chimbuko la taratibu za ku govern hizo congregations zao.

Hapo Tanzania Waislam wanahaki za kutosha kabisa kama Raia wengine wa dini nyingine...Tena wao ndio MATAJIRI WAKUBWA TANZANIA...Lakini hawaridhiki na wanataka ku SILIMISHA na SERIKALI.

Hapo Tanzania kuowa mke zaidi ya mmoja ni rhuksa na watu wanalimana talaka rejea nk huko mahakamani mbele za mahakimu na ama majaji....Sasa ndugu zangu waislam ni wapi hapo ambapo hamna haki?

Mnakumbuka mlipojaribu kuvunja mabucha ya nguruwe na kusababisha patashika nguo kuchanika hapo jijini?

Sasa kama ni wazi kuwa maagizo yenu mnatowa Saudi na Iran.....Je wao ndio wamewatuma muiambie serikali iwe na mahakama zenu?

Kwenye nchi nyingine duniani ni kinyume cha sheria kuoa mke zaidi ya mmoja...Sasa nyie mnataka hizo sheria zianze na nchini mwetu?


prejudice, prejudice, prejudice....and we dare to call ourselves PATRIOTS to our nation.....

Tanzanianjema
 
Kama nadhani wewe ndiye unapaswa kupitia facts zako kwanza kuhusu kuanzishwa na mahusiano ya BAKWATA na serikali.....

Tanzanianjema
hoja yangu iko pale pale kwamba Mufti sheikh mkuu hachaguliwi na seriikali wala BAKWATA haiendeshwi kwa kodi za watanzania. na mimi sijadai hizi ni fact zoote kuhusu uhusiano wa BAKWATA na serikali,bali katika hili la kuchagua Sheikh mkuu,serikali haimo wala haitoi kodi za wananchi kuiendesha BAKWATA.

KAMA KUNA KODI INATUMIKA KUIENDESHA BAKWATA HUTOLEWA NA WIZARA GANI NA KUPITIA FUNGU GANI?
 
hoja yangu iko pale pale kwamba Mufti sheikh mkuu hachaguliwi na seriikali wala BAKWATA haiendeshwi kwa kodi za watanzania. na mimi sijadai hizi ni fact zoote kuhusu uhusiano wa BAKWATA na serikali,bali katika hili la kuchagua Sheikh mkuu,serikali haimo wala haitoi kodi za wananchi kuiendesha BAKWATA.

KAMA KUNA KODI INATUMIKA KUIENDESHA BAKWATA HUTOLEWA NA WIZARA GANI NA KUPITIA FUNGU GANI?

Una uhakika kuwa serikali huwa haichangii kuendeshwa kwa BAKWATA?

Haya yamefanyika mara nyingi tu, wkati mwingi ni kwa siri na wakati mwengine ni waziwazi. Mfano hai ni enzi zile Mrema alipokuwa naibu waziri mkuu katika uchaguzi wa uongozi wa BAKWATA uliofanyika Dodoma. Enzi za chama kimoja hilo lilikuwa ni suala la kawaida.......

Suala ni kwa manufaa ya nani?

Tanzanianjema
 
Kuwapo Kwa Mahakama Ya Kadhi Popote Duniani Huwa Ni Kwa Misingi Ifuatayo

I) Ni Kwa Ajili Ya Waislamu
2) Tena Waislamu Wenye Imani Ya Dhati Na Dini Yao
3) Amboa Kwa Hiari Yao Wenyewe Wataamua Kutatua Matatizo\migongano
Yao Kupitia Mahakama Hizo
4) Na Mambo Ambayo Yatapelekwa Huko Kwa Kiasi Kikubwa Yanahusu; Mirathi,
Ndoa\talaka Na Mambo Madogo Madogo Ya Kimaisha.

Ukiangalia Kwa Makini Nia Kubwa Ni Kutatua Masuala Tajwa Hapo Juu Kwa Misingi Ya Imani, Hivyo Kuokoa Muda Na Haki, Kwani Sual La Kukata\kutokukubali Na Hukumu Litakuwa Halipo.

Suala La Uendeshaji Wake Ndiyo Naona Issue Hapa, Basi Ni Bora Tuchangie Kwa Umakini Ni Njia Ipi Bora Ya Kulifanya Hili Jambo Litimie Bila Ya Kuathiri Fikra Na Maslahi Ya Makundi Mengine Katika Jamii Yetu.
 
Kuwapo Kwa Mahakama Ya Kadhi Popote Duniani Huwa Ni Kwa Misingi Ifuatayo

I) Ni Kwa Ajili Ya Waislamu
2) Tena Waislamu Wenye Imani Ya Dhati Na Dini Yao
3) Amboa Kwa Hiari Yao Wenyewe Wataamua Kutatua Matatizo\migongano
Yao Kupitia Mahakama Hizo
4) Na Mambo Ambayo Yatapelekwa Huko Kwa Kiasi Kikubwa Yanahusu; Mirathi,
Ndoa\talaka Na Mambo Madogo Madogo Ya Kimaisha.

Ukiangalia Kwa Makini Nia Kubwa Ni Kutatua Masuala Tajwa Hapo Juu Kwa Misingi Ya Imani, Hivyo Kuokoa Muda Na Haki, Kwani Sual La Kukata\kutokukubali Na Hukumu Litakuwa Halipo.

Suala La Uendeshaji Wake Ndiyo Naona Issue Hapa, Basi Ni Bora Tuchangie Kwa Umakini Ni Njia Ipi Bora Ya Kulifanya Hili Jambo Litimie Bila Ya Kuathiri Fikra Na Maslahi Ya Makundi Mengine Katika Jamii Yetu.


..sawa kama ipo kwa masilahi ya waislamu na kwa ridhaa yao ..halihitaji seal ya kikatiba in first place....nadhani waislamu waandae kongamano lao na kuamua KUANZISHA HII MAHAKAMA MUDA WOWOTE......

...MUHIMU NA WALA BILA MJADALA NI KUWA GHARAMA ZOTE ZA UENDESHAJI ZIWE JUU YA JUMUIA ZA KIISLAMU.....SERIKALI HAITANGILIA..UNLESS OTHERWISE...
 
Kuwapo Kwa Mahakama Ya Kadhi Popote Duniani Huwa Ni Kwa Misingi Ifuatayo

I) Ni Kwa Ajili Ya Waislamu
2) Tena Waislamu Wenye Imani Ya Dhati Na Dini Yao
3) Amboa Kwa Hiari Yao Wenyewe Wataamua Kutatua Matatizo\migongano
Yao Kupitia Mahakama Hizo
4) Na Mambo Ambayo Yatapelekwa Huko Kwa Kiasi Kikubwa Yanahusu; Mirathi,
Ndoa\talaka Na Mambo Madogo Madogo Ya Kimaisha.

Ukiangalia Kwa Makini Nia Kubwa Ni Kutatua Masuala Tajwa Hapo Juu Kwa Misingi Ya Imani, Hivyo Kuokoa Muda Na Haki, Kwani Sual La Kukata\kutokukubali Na Hukumu Litakuwa Halipo.

Suala La Uendeshaji Wake Ndiyo Naona Issue Hapa, Basi Ni Bora Tuchangie Kwa Umakini Ni Njia Ipi Bora Ya Kulifanya Hili Jambo Litimie Bila Ya Kuathiri Fikra Na Maslahi Ya Makundi Mengine Katika Jamii Yetu.

Waleed karibu sana jamvini, umeyaweka wazi mambo ambayo wenzako wanayaficha. Watu tunaopinga suala la kadhi, hatupingi kuwepo kwake ila kuingizwa kwenye katiba ya nchi, Serikali kuhusika katika uendeshaji yaani kuteua viongozi na kugharimia uendeshaji. Umetoa option nzuri kwa wanaotaka hiyo mahakama kujadili namna ya kuiendesha. Na mjadala huo haupaswi kuwa bungeni wala katika vyombo vya Serikali bali uwe wa Waislam au mtu mwingine mwenye interest.
 
Muslims watapata urahisi wa kuendeleza sheria zao kama hii nchi ya tz itakuwa nchi ya kiislam tu, na kama itaweka kwenye katiba kuwa hakuna mtu kuhama dini. lakini kama tunaishi kwenye secular country kama hii, huu mpango wao hautakuwa mzuri na utaleta fujo tu. Tena washindwe na walegee kwa Jina la Yesu. uingize uislam kwenye katiba ya dini zote kwasababu wao wana nini haswa, tunawaogopa hata tuaabudu kiasi hiki? mbona wanataka kutuendesha? au kwasababu rais ni mwislam mwenzao?
 
Back
Top Bottom