Juu ya OIC na Mahakama ya Kadhi

Juu ya OIC na Mahakama ya Kadhi

Huyu Kikwete kashajua hachaguliwi tena 2010 hivyo muacheni tu asafiri muda ukifika ndio atajua kwamba alikuwa anacheza kama rais.
 
Jamani jana usiku kwa bahati usingizi uliinishia nikaamua kuwasha Tv, bahati nzuri sijui mbaya nikakuta documentary Iliyokuwa inahusu suala la nyuklia la Iran.Amabalo liliongelewa kwa takribani 1hr.
Mmoja wa waliohusika katika mahojiano hayo ni aliyekuwa anapokea pesa za Mr Khan,Khan mwenyewe na wawili toka Iran kati ya waliotumwa na Yatola kutafuta hiyo technojia.Mtu wa Khan alikuwa ni Mwindonesia.Madili yote yalifanyikia Dubai,baada ya vita kati ya Iraq na Iran ambayo inasemekana raia na askari wengi wa Iran waliuawa na hivyo Yatola akamua Iran itafute ultimate weapon(Nyuklia bom).Baada ya kuhangaika kutafuta ndipo Dr. Khan akajitokeza na kuwaelekeza kwenda Dubai ambako alikuwa tayari amefungua ofisi iliyokuwa inaendeashwa na huyo kijna wa Indonesia.Yeye hakwenda kwa kuwa CIA walikuwa wanamfuatia.Walipewa dili kwa kulipa Dola 8 milion.wakapewa tech hiyo ila wakapigwa mzinga kwenye vifaa,vilikuwa vimechoka.Hivyo dili lilibidi lifungwe kwa mara ingine baada ya Khan kuwatengenezea vifaa vipya na wakatoa Dola 32mil.Baada ya pesa kuwa tam Khan akauza tech hiyo North Korea na Libya.Ila mtu wa kwanza kuuziwa alikuwa Sadam kabla ya Iran.
 
Nimefurahi kusikia kuwa Vatican wamechukua hatua ya kumkaribisha JK Vatican. Sababu ni kuwa hivi karibuni kulikuwa na minong'ono kuwa kuna jamaa wanaomini kuwa watu wa aina yao tu ndio wana haki ya kuongoza tanzania wanajipanga kuhakikisha kuwa JK anakuwa rais wa miaka mitano tu na hiyo inategemea kama ataruka vigini. Hawa ni walewale watokao katika timu ya nyumbani (CCM and System) lakini wanaona kuwa vibweka vya wanamtandao na Ari mpya vinapita kiwango cha wao kuvumili na inasemekana kuhusisha hata wanamtandao nyeti.

Bahati mbaya kama ilivyo kawaida kwa wanasiasa mufilisi, "inasadikiwa" wanapanga mipango yao china ya kivuli cha ukanisa. Ninavyosikia wapenda nchi wakamtonya JK naye akazipokea habari hizo kwa utafiti zaidi.

Kitendo cha kanisa kutoa tamko kali hivi karibuni lenye kusisitima loyality kwa serikali nilikichukulia kama njia mojawapo ya kuondoa kawingu haka kabaya. Ni wazi hili la mwaliko ni zuri sana na nampongeza Askofu Kilaini kwa juhudi na busara zake.

Wale wanaodhani kuwa ni wajibu wa JK kupeleka malalamiko ya watanzania kuhusu misisimamo ya kanisa sidhani kama wanamfanyia haki. Hiyo ni kazi ya waumini wenyewe na si dhani kama serikali yetu ina asasi imara za kulishughulikia suala hilo zaid ya mifumo ya kanisa hapa nchini na duniani.

Tanzanianjema
 
Nyerere si wa kumlinganisha na hawa vimada ambao wao kikubwa ni pesa.Nyerere alikuwa na msimamo na alijua alichokuwa anafanya.Hawa hawana msimamo.Wewe subiri utaona tu watabadili msimamo,kwani issue ya Iran haoko mbali.Mie naamini Mmarekani hatopiga ila Israel itashambulia.
 
pamoja na Ukatoliki wake wote, Nyerere aliwahi kumtimua Padre toka Bongo...!!
 
Julius siku zote alikuwa anasimamia maamuzi yake hata alipokuwa Wrong,alikuwa hakubali mpaka aone mwisho wake.Hawa viongozi wa sasa wana tabia za Uchangudoa,wataondoka Jolly club wakisikia Billicanas kuna mashefa!,wanachoangalia , watapata wapi mlo wao wa siku!
 
Mzee MKJJ yule alikuwa ni Askofu si Padre . Hawa mapade ambao wengi ni ma CIA ama FBI kila mara Mwalimu aliwaondoa maana imani ama mbingu unaweza kufika bila kupitia kanisa wala msikiti .
Issue ya Iran JK atajuta nayo mimi sina wasi wasi . Matamshi yake ya kurudia yanammaliza sana Migiro kwenye UN. Ndoa za JK na US na EU sasa hivi zinakufa tutaishia kuomba msaada toka Iran. I hope mimi sitazuiliwa kuingia US kwa JK kufuata upuuzi . JK anaweza kukaa kimya si lazima kutoa matamko ya aina hii na bado akawa ana support why kununua mbuzi kwenye gunia ? Lakini analazimika kusena haya kumpa nguvu Muiran Rostam Aziz ambaye ndiye big connection yake wakati anapata mapesa ya Ucahguzi.
 
Hivi ni vijimambo vya watanzania.

Kiongozi akikubali kuburuzwa na wakubwa tunamdhihaki kuwa hana dira, changudoa na kilakitu. Akitoa msimamo usioendana na wakubwa wa dunia tunamlaani ati anatuharibia.

Ndio maana mwenzenu naamini kuwa tatizo la uongozi kwetu sio viongozi tu bali zaidi sisi tunaongozwa(tatizo ni utanzania).

Hata kama JK anaonyesha kutokuwa na dira iliyonyooka kuhusiana na mahusiano ya kimataifa, Lazima tutambue kuwa katika nchi zetu za dunia ya tatu na haswa katika enzi hizi za Unilateral global power posture, ni mazingira zaidi ya utashi ndio yanaelekeza misimamo ya viongozi katika masuala ya kimataifa.

Wakati bado unaruhusu kutafuta "some grounds" kujenga msingi wa urais wake katika siasa za kimataifa.

Msimamo wa JK kuhusiana na Iran ni moja ya dalili kuwa anajaribu kuchukua mwelekeo wa Mwalimu huku akitambua mazingira ya sasa ambayo hayampi uwezo wa kutosha kuwa na msimamo ambao angependa yeye.

Vilevile ni wazi kuwa amegundua kuwa jitihada zake za kuwaonyesha jamaa wa New York and London kuwa anaweza kuwa a "man to do bussiness with" hazijazaa matunda yoyote zaidi ya kumdharau. Hivyo sasa anachukua "Notice me" approach ambayo ingawa ina price kubwa lakini ndiyo itakayoweza kumfanya hawa jamaa wamnotice ili nao wamkaribie kabla hajawatoka na kuenda kivyake katika anga za diplomasia duniani.

Uwongo mbaya, naanza kuona taratibuTanzania ya zamani inarudi ingawa nina wasiwasi kama tuna laverages za kutusukuma tunapotaka kuelekea katika ulimwengu wa siaisa za kimataifa.

Tanzanianjema
 
hivi rostam ni muiran ,du basi kumbe kila jambo lina chanzo afteral nyumbani ni nyumbani hata kama ni kwa babu....tujiweke mbali na contravertial global politics..kama hatuna msimamo kwenye jambo itatosha kukaa kimya..
 
Julius Nyerere (R.I.P.) siku zote alikuwa na msimamo na wazungu alikuwa anawafahamu inside-out siyo hawa vizwezwe wa siku hizi.

JK aende huko vatican alikoalikwa lakini ajiandae kwenda kuweka heshima ya taifa hawa wapambe wake nao wajifunze sio kumwaibisha kila wakati. Kweli anafanya makosa lakini sasa haya makosa yakiwa mengi yanatia kinyaa, kama hawezi kuwa up front kwenye hizi press conference ambazo zitamuuliza maswali magumu. Na hili la sheria ya waandishi wa habari atapambana nalo and I wonder what the hell where they thinking? and then analivalia njuga hili la Iran, litamtokea puani. Lets put our house in order and forget about other peoples problems.
 
Mbunge mmoja amedai kuwa wakati umefika CCM itekeleze ilani yake kwa kuwatimizia waislamu haja yao ya kuwa na Kadhi Mkuu. Amesema kwa vile waislamu ndio wengi nchini Tanzania, kwanini suala la kadhi linacheleweshwa?
 
I don't know. yeye kasema ana uhakika wa Kitakwimu kuwa waislamu ndio wengi. Kasema Bungeni so it must be true.
 
Mwkjj,
Just because limesemwa bungeni does not make it true.
 
Mbunge mmoja amedai kuwa wakati umefika CCM itekeleze ilani yake kwa kuwatimizia waislamu haja yao ya kuwa na Kadhi Mkuu. Amesema kwa vile waislamu ndio wengi nchini Tanzania, kwanini suala la kadhi linacheleweshwa?

Kazi imeanza sasa. Mbunge gani huyo aliyetumbua jipu ambalo kwa hakika mimi naona limeiva.

Ila kitu kimoja ambacho amesahau ni kuwa, ikiwa hoja ni wingi wao(SIJUI KWA SENSA GANI?)basi wawatuletee sharia kabisa waanze kutukata mikono.

Huyo mbunge mimi amenifurahisha kuwa walichikuwa wakikitaka si kashi bali ni kuleta utawala wa kidini TANZANIA.

Kwa kuwa hoja kama ni kadhi sijui kama kuna mtu alikuwa analikataa, kilichokuwa kinagomna ni jinsi serikali ianzishe chombo cha waislamu badala ya waislamu wenyewe kuanzisha.

Serikali ni ya wote, Kadhi niwa waislamu, sasa serikali ndio ndio inaanzisha au waislamu wenyewe waanzishe.

Ngoja tusubiri ila naomba jina la mbunge husika.
 
sasa kama lilikuwa la waislamu wenyewe kuanzishwa ilikuwaje kutiwa kwenye ilani ya CCM ktk kugombea kura, na kuinadi kwa waislamu kuwa watafanyia ?

tuweni wakweli, hii ni moja ya sera ya chama tawala na waislamu wanahaki kudai utekelezwaji wa ahadi hiyo
 
Mimi pia zijaona sensa ya dini. Ila ukiangalia kwenye makabila yote makubwa TZ yana waislam wachache. Sasa inakuwaje leo wawe wengi. Haiingi akilini. Its true mijini na pwani wako wengi. lakini jaribu kwenda usukumani huko, msikiti wenyewe ni wa kutafuta!!!!!!
 
Huyo mbunge akasema kuwa kuwa kwa vile waislamu ni wengi basi wapewe watakacho. Akasema wangeweza kuomba kama sheria zile kali za kukatana mikono lakin wao wanachoomba ni kuwa mahakama hiyo ya kadhi ishughulikie mambo ya ndoa, mirathi n.k yasiyohusiana ya uhalifu. Jasusi, huko nyuma mbunge akisema kitu ambacho kina utata alitakiwa kuleta ushahidi lakini katika hili Mwenyekiti wa kikao aliliacha lipite tu hivyo nimeassume kuwa wamekubali kuwa huo ni ukweli.
 
sasa kama lilikuwa la waislamu wenyewe kuanzishwa ilikuwaje kutiwa kwenye ilani ya CCM ktk kugombea kura, na kuinadi kwa waislamu kuwa watafanyia ?

Mtumwitu,
So they want their own republic? What will happen if the Christians and other sects would ask for their tradidonal laws? Hii nchi itatawalika kweli.

Kuingiza kwenye Ilani ilikuwa ni kutafuta kura za Waislam and nothing else.
 
Back
Top Bottom