Juu ya OIC na Mahakama ya Kadhi

Mawando,
Nakupongeza kwa kuwa umegusa sababu ya msingi sana.Kuna wengine sisi ni wapagani.Kwanini kodi yangu ikaendeshe mahakama ya dini fulani.Goog point!!
 
Serikali imeamua "kupoza mambo"...
Mchakato Mahakama ya Kadhi kukamilika Oktoba
Na Theodatus Muchunguzi, Dodoma

WIZARA ya Katiba na Sheria inalishughulikia suala la kuanzishwa Mahakama ya Kadhi na sasa litakuwa tayari Oktoba mwaka huu.

Akizungumza kwenye majumuisho ya Katiba na Sheria, Waziri Mary Nagu alisema Wizara yake ililikabidhi suala hilo kwa Tume ya Kurekebisha Sheria Oktoba mwaka jana na kwamba inatarajia kukabidhiwa ripoti ya suala hilo kabla ya Oktoba mwaka huu.

"Tunayo miezi miwili kuanzia sasa tu kabla ya kukamilisha suala hilo, hivyo kwa kuzingatia maslahi ya taifa na ya watu wetu wa imani zote nina imani Tume italishughulikia.. tuvute subira, suala hili limo katika ilani ya Chama cha Mapinduzi (CCM), "alisema.

Awali suala hilo la kuanzishwa mahakama ya kadhi liliibuliwa tena bungeni na kambi ya upinzani kwa kuihoji serikali sababu za kushindwa kutekeleza ahadi yake.

Hoja hiyo iliibuliwa jana na Waziri Kivuli wa Wizara ya Katiba na Sheria, Fatma Maghimbi (CUF), wakati akiwasilisha hotuba yake ya makadirio na mapato ya wizara hiyo kwa mwaka 2007/08.

Maghimbi alisema muda mrefu umepita tangu serikali ilipotoa tamko kuhusiana na suala la mahakama za Kiislamu na kwamba kambi

ya upinzani haijaona nia ya dhati ya serikali kutatua suala hilo, ambalo linagusa mustakabali wa taifa.

Aliyataja mambo makuu mawili yaliyotolewa katika tamko la serikali lililowasilishwa na Waziri wa Sheria kuwa ni kuwataka wananchi wafunge mjadala kuhusiana na suala hilo na pili, serikali iliahidi kuendesha mchakato wa kukusanya maoni kutoka kwa wananchi.

Maghimbi alisema: "Tamko la serikali lilikuwa

likijipinga lenyewe kwa maana huwezi kufunga mjadala wa wananchi kuhusiana na suala la mahakama ya kadhi na wakati huo huo ukaahidi kukusanya maoni kutoka kwao."

"Je maoni yatapatikana bila mjadala? Lengo la serikali kuutaka umma wa Watanzania kutojadili suala hili. Au nia ya serikali ni kuzima ili lisisikike?" alihoji. Maghimbi, ambaye ni Mbunge wa Chakechake.

Maghimbi alisema ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2005 iliahidi kulitafutia ufumbuzi suala hilo lakini hadi leo, hakuna jambo la msingi lililofanyika zaidi ya kuitishwa kwa kongamano moja kujadili suala hilo.

Shoka Khamis Juma (Micheweni-CUF), alisema suala la mahakama ya kadhi limesubiriwa muda mrefu bila kutekelezwa na kwamba sasa ni wakati muafaka.

Alisema kamati mbili za Bunge ziliwahi kuundwa kufuatilia suala hilo, moja ikiongozwa na aliyekuwa Mbunge wa Muhambwe, Alicardo Ntagazwa na Mbunge wa Kisarawe, Athumani Janguo kwa kutembelea nchi za Kenya, Uganda, Afrika Kusini na Msumbiji, kuona zinavyoendesha mahakama hizo.
 
jamani mimi sijui kitu kuhusu mirathi ktk uisilam huwa inakuwaje,Hiki ni kipengele muhimu ktk kudai hii mahakama ya kadhi
 
KWA HILI JF SIO WAJUZI LAKINI MWAWEZA KUENDELEA NA UMASAKU WENU KAMA KAWAIDA KUONGEA HAKUNA KUTOA KODI

ILANI YA CCM YA MWAKA 2005 INASEMA JE?

108. CCM itazitaka Serikali ziendelee na hatua zilizoanza kuchukuliwa ili kuiboresha Sekta ya Sheria kusudi nayo itoe huduma bora zaidi kwa jamii. Yatakayosisitizwa katika kipindi hiki ni pamoja na yafuatayo:-
(a) Kuzifanyia marekebisho sheria za mirathi na zile zinazoonekana kuwakandamiza wanawake.
(b) Kulipatia ufumbuzi suala la kuanzishwa kwa Mahakama ya Kadhi Tanzania Bara.
(c) Kuanzisha na kutekeleza mpango maalumu wa kuanzisha Ofisi za Mahakama Kuu katika kila Mkoa.
(d) Kukamilisha mchakato wa kutenganisha shughuli za upelelezi na uendeshaji mashitaka.
(e) Kuziimarisha na kuzioanisha sheria zinazohusiana na mapambano dhidi ya rushwa.
(f) Kutekeleza Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Sheria hususani ujenzi wa majengo ya mahakama ya ngazi zote na kuajiri majaji na mahakimu wa kutosha.
(a) Kuweka mfumo wa kuwasaidia wananchi wasiojiweza kupata msaada wa kisheria.
(b) Kuweka mfumo utakaowezesha kutumika kwa wanasheria wa awali (para-legals) katika mahakama za mwanzo.
Demokrasia na Madaraka ya Umma
109. Katika jitihada za kukuza demokrasia na kuimarisha

Ikumbukwe kwamba KENYA na ZANZIBAR kuna Kadhi lakini masuala ya Mgongano wa dini hayapo?

Ikumbukwe kwamba Mbunge alisema kwamba Zanzibar waislamu ni wengi kuliko wakristo na sio Bara!

Mambo ya Kadhi ni Mambo ambayo yataifanyia kazi kwenye mambo ya ndoa na miradhi tu, mambo ya mahakama zingine yataendelea kama kawaida...

Wakuu kama huna hoja kuwa observer tu, hoja zingine zitakuja utachangia
 
Niulize- as a Lay Person!
Kwani kesi za ndoa na mirathi haziwezi kutatuliwa na mahakama zilizopo? Kuna advantages gani za Kadhi over Mahakama za sasa? Je pia tuna haja ya Chombo kushuhulikia ndoa na mirathi ya Wakristo, Wasio na Dini, Kalasinga, Ithnashari?
 
Ndio kwa kuwa Quran inaeleza namna ya kutatua mambo ya ndoa na mirathi na sheria zetu za kutumia akili zetu hazijatumia vitabu vya Mungu.

In short it is a Belief... so please I'm sure you can convince one... to change his/her belief...

Na kumbukeni nchi hii ilikuwa na Kadhi enzi za Ukoloni ikaondoka hivihivi tu...

Kwa maoni yangu hakuna ambalo dini zingine zitapata shida kwa hili...
 
Kumbukeni ni Haki ya Waislam kuwa na Mazingira ya kumwabudu Mungu wao provided hawavunji sheria zingine au katiba itakayokuwepo.

Haki hii ni ya Kikatiba: naomba kuwasilisha kutoka ibara ya 19, Ya katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania toleo la 2000.

19.-(1) Kila mtu anastahili kuwa na uhuru wa mawazo, imani na uchaguzi katika mambo ya dini, pamoja na uhuru wa mtu kubadilisha dini au imani yake.
(2) Bila ya kuathiri sheria zinazohusika za Jamhuri ya Muungano, kazi ya kutangaza dini, kufanya ibada na kueneza dini itakuwa ni huru na jambo la hiari ya mtu ya binafsi, na shughuli na uendeshaji wa jumuiya za dini zitakuwa nje ya shughuli za mamlaka ya nchi.
(3) Kila palipotajwa neno "dini" katika ibara hii ifahamike kwamba maana yake ni pamoja na madhehebu ya dini, na maneno mengineyo yanayofanana au kuambatana na neno hilo nayo yatatafsiriwa kwa maana hiyo.
Hivyo mnavyochangia hakikisheni mnalifahamu hili.
 
Mzee Mwanakijiji,

Nafahamu ndio maana naomba na wewe uangalie nukuu hii kwenye post yangu.

Kumbukeni ni Haki ya Waislam kuwa na Mazingira ya kumwabudu Mungu wao provided hawavunji sheria zingine au katiba itakayokuwepo.
 
Mwanakijiji,
Nadhani Kilitime aliandika bila kusoma.Tehehehee


Ngangumi,

Hapa naona umekurupuka ndugu yangu; kwa kuwa waislamu hawajavunja sheria yoyote ndio maana wanadai haki yao kihalali, na kwa kuwa kwa sasa hawa-practice Kadhi... hakuna sheria yoyote wanayovunja

Quote hii hapa narudia kwa niaba yako.

Kumbukeni ni Haki ya Waislam kuwa na Mazingira ya kumwabudu Mungu wao provided hawavunji sheria zingine au katiba itakayokuwepo.

Note; dhumuni la kuweka katiba itakayokuwepo nilimaanisha katiba ya sasa hairuhusu ndio maana waislamu wanaomba ibadilishwe itambue hilo,,, kwa hiyo katiba itakayokuja (future tense) na kwa mujibu wa ibara 19. (1)
 
Suala ni kuwa kwa wanaotaka kulazimisha hii mahakama ambayo itakuwa niya kidini.Waangalie hicho kipengele no 2 ambacho kinakataa serikali kuhusika.
 
But I think Sharia or Khadii Courts is where Muslim men can nyosha their women.

Mazee! are you serious about this? looks like men will be favoured more than women, gender imbalance? what about muslim women "nyoshering" their men?
 
Hili ni suala la kisheria ni lichambuliwe katika sura hiyo sio prejudices zilizotujaa watanzania ambao tunapenda kudanganyana kuwa tunapendana na kuheshimiana...

Moderator naomba kuwakilisha malalamiko yangu kuhusu mwenendo wa huyu mtu anayejiita KGM. Tusisubiri hii sumu ilete madhara halafu ndio tujifanye tunashtuka..kama wafanyavyo hao tunaojidai tunawakomalia...

Tanzanianjema
 
Mwanakijiji.
Kuna tatizo gani mahakama si ya waislamu.kama wewe si muislam unaumia nini?
 
wapi umeniona mimi ninalalamika? Na kama suala ni la waislamu kwanini walilete kwenye Bunge lenye wakristu na wahindu? ingebidi wawatake wabunge wakristu na wasio waislamu watoke kwanza...
 
Wenzetu wanaanzisha hadi digrii za Uislam. itakuwaje Udsm waseme wanaanzisha LLM Islamic Law, kelele sijui zitakuwaje. haya mambo yanapoteza maendeleo.

University of Wales Cardif wanatoa Islamic digrii, University oFlondon wanafanya , East London nao wanasoma Islamic studies na wao wako kwenye kitivo cha ukristu.

hizi ni course za kiislam zinazotolewa na East London university.
http://www.uel.ac.uk/programmes/law/postgraduate/imes.htm

Waislam ni wengi kwa takwimu na kwa factor nyingi. mfano wa karibu jiulize Mkapa ana watoto wa ngapi na mzee Kawawa ana watoto wangapi? MKAPA ana wawili. Mzee Kawawa anao zaidi ya 27

.Sababu mkapa kachukua muda mwingi shuleni. KAWAWA kaanza maisha muda mrefu hakuwa na commitment za masomo akawahi kuona. na dini yake ina mruhusu kuwa na wake wanne.

Masheikh wanaruhusiwa kuoa wake zaidi ya mmoja wakati mapadri na masisiter ni watawa hiyo population itaongezeka vipi?

JK ana watoto nane,na anaruhusiwa kuwa na mke mwingine tena, Lowassa ana wangapi?

zipo sababu nyingi sana kuthibitisha waislam wengi kwa idadi.
 
wapi umeniona mimi ninalalamika? Na kama suala ni la waislamu kwanini walilete kwenye Bunge lenye wakristu na wahindu? ingebidi wawatake wabunge wakristu na wasio waislamu watoke kwanza...

Waislam walipotaka kuleta OIC bila kurishikisha bunge waliambiwa wamevunja katiba unataka wavunje katiba tena? na G55 ianze upya?
kwani PENGO amepata wapi haki ya kuwa na pasipoti mbili huku wengine haturuhusiwi?

Jumuiya ya Commonwealth ni ya kikritu na katiba yake inaleza wazi. lakini hakuna muislam anayelalamika kuwa kuna wahindu au waislam.
 
Back
Top Bottom