108. CCM itazitaka Serikali ziendelee na hatua zilizoanza kuchukuliwa ili kuiboresha Sekta ya Sheria kusudi nayo itoe huduma bora zaidi kwa jamii. Yatakayosisitizwa katika kipindi hiki ni pamoja na yafuatayo:-
(a) Kuzifanyia marekebisho sheria za mirathi na zile zinazoonekana kuwakandamiza wanawake.
(b) Kulipatia ufumbuzi suala la kuanzishwa kwa Mahakama ya Kadhi Tanzania Bara.
(c) Kuanzisha na kutekeleza mpango maalumu wa kuanzisha Ofisi za Mahakama Kuu katika kila Mkoa.
(d) Kukamilisha mchakato wa kutenganisha shughuli za upelelezi na uendeshaji mashitaka.
(e) Kuziimarisha na kuzioanisha sheria zinazohusiana na mapambano dhidi ya rushwa.
(f) Kutekeleza Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Sheria hususani ujenzi wa majengo ya mahakama ya ngazi zote na kuajiri majaji na mahakimu wa kutosha.
(a) Kuweka mfumo wa kuwasaidia wananchi wasiojiweza kupata msaada wa kisheria.
(b) Kuweka mfumo utakaowezesha kutumika kwa wanasheria wa awali (para-legals) katika mahakama za mwanzo.
Demokrasia na Madaraka ya Umma
109. Katika jitihada za kukuza demokrasia na kuimarisha
Kumbukeni ni Haki ya Waislam kuwa na Mazingira ya kumwabudu Mungu wao provided hawavunji sheria zingine au katiba itakayokuwepo.
Mwanakijiji,
Nadhani Kilitime aliandika bila kusoma.Tehehehee
Kumbukeni ni Haki ya Waislam kuwa na Mazingira ya kumwabudu Mungu wao provided hawavunji sheria zingine au katiba itakayokuwepo.
But I think Sharia or Khadii Courts is where Muslim men can nyosha their women.
wapi umeniona mimi ninalalamika? Na kama suala ni la waislamu kwanini walilete kwenye Bunge lenye wakristu na wahindu? ingebidi wawatake wabunge wakristu na wasio waislamu watoke kwanza...