kaka naomba uelewe mahakama ya kadhi ni haki kamili ya waislamu. Walioshinikiza serikali kuondoa kodi katika ngos walikuwa maaskofu na serikali ikasalimu amri na kuondoa kodi katika institution za kidini na sisi tutaishinikiza serikali itupe mahakama ya kadhi.
Ama kuhusu kugharimiwa mahakama ya kadhi itagharimiwa kwa pesa ya serikali kwani waislamu pia tunalipa kodi serikalini hivyo basi na hela zetu zijulikane zinaenda wapi serikalini na sio kutufanya sio watu hatuelewi kinachoendelea. Ikishindakana basi tusiione serikali ikitoa michango katika shule za seminari, hospitali za seminari eti kwa kisingizio cha kusambaza huduma ya jamii. Mnasambaza huduma ya jamii wakati vilevile mnaenezo neno, mnatoa kazi kwa wakristo kufanya kazi katika hizo institution this is total unfair na waislamu hatutakubali iendelee.
Kwamba maaskofu waliishinikiza serikali na ikasalimu amri ya kurejesha msamaha wa kodi kwa mashirika ya dini na NGOs Good! waliifanya kazi yao kikamilifu kumbuka suala hili kwa hakika watanzania wote bila kujali tofauti zetu zozote ziwazo, Na kwamba ni kazi ya mashekhe kwa niaba ya waislamu wote kuhakikisha kuwa tunapata mahakama ya kadhi hilo halina mjadala. Ila kulinganisha hoja ya kurejesha misamaha ya kodi na kunazishwa kwa mahakama ya kadhi aah mi hapo sijakuelewa.
Hili la kodi za waislamu zinakokwenda sina hakika kama TRA inafanya kazi ya kibaguzi namna hiyo. Wala sina shida ya kuhangaika juu ya hilo, wasiwasi wangu ni kwamba iko siku utauliza fedha za kodi ya watu wa kabila lako zinaenda wapi, baadae ukoo wako n.k. Kaka unakoenda sio kuzuri tafakari tena hoja yako.