Habari zenu wana JF...!
Nimesikitishwa na suala la Joshua Nassari kushambuliwa kama mpira wa kona bila sababu ya msingi..,kisa tu aliimwaga CCM kwenye uchaguzi arumeru na pia kukataa mamilioni ya CCM kuisaliti CHADEMA..!
Hao wanaoshambulia Nasari wapo makundi mawili, kuna CCM, ambao wanajubu mapigo ya kushindwa, huku wakiwatumia wahariri wa Magazeti ya MWANANCHI na NIPASHE, vile vile na baadhi ya watu ambao hawajui nini maana ya Siasa, wanafuata tu mkumbo..,maanak siku hizi imezuka kasumba kila mtu mwanasiasa!
Wanaosema NASSARI msaliti nia yao ni moja tu.,,kuibomoa CHADEMA..! na sasa wanahakikisha wanamgombinisha NASSARI na baadhi ya wabunge na Viongozi CHADEMA, mfano wa habari ya leo iliyoandikwa kwenye gazeti la MTANZANIA chini ya BASHE..,"ETI KWAMBA MBOWE AMEZIMA UASI CHADEMA" hii kauli ni ya uchochezi dhidi ya CHADEMA..,
Wanaosema NASSARI ni msaliti, hawataishia tu hapo watasema vincet msaliti,Godbless lema msaliti, na mwisho hata Dk.Slaa msaliti..,
Kama Nassari angekuwa pandikizi..,Lazima angewezesha CCM ishinde uchaguzi wa Arumeru, kwani LOWASSA NA BEN MKAPA wasingekubali kudhalilika, na hata kukubali mamilioni waliotumia kuteketea bila kushinda..kwakuwa CCM wanajulikana kwa kulaziimisha matokeo na kuchakachua kura