Joshua Nassari MB.

Joshua Nassari MB.

Fredrick Sanga.
Dogo Nassari anaropoka sana muwekeni chini mfahamisheni siasa za Tanzania zilivyo.

Wewe ndio inaelekea unatumia makamasi katika kuchambua haya maswala, kwani wewe kwa upeo wako mfupi unafikiri siasa ya Tanzania ipo vipi yaani kwa mfano niki kuliza...?
 
Last edited by a moderator:
Habari zenu wana JF...!

Nimesikitishwa na suala la Joshua Nassari kushambuliwa kama mpira wa kona bila sababu ya msingi..,kisa tu aliimwaga CCM kwenye uchaguzi arumeru na pia kukataa mamilioni ya CCM kuisaliti CHADEMA..!

Hao wanaoshambulia Nasari wapo makundi mawili, kuna CCM, ambao wanajubu mapigo ya kushindwa, huku wakiwatumia wahariri wa Magazeti ya MWANANCHI na NIPASHE, vile vile na baadhi ya watu ambao hawajui nini maana ya Siasa, wanafuata tu mkumbo..,maanak siku hizi imezuka kasumba kila mtu mwanasiasa!

Wanaosema NASSARI msaliti nia yao ni moja tu.,,kuibomoa CHADEMA..! na sasa wanahakikisha wanamgombinisha NASSARI na baadhi ya wabunge na Viongozi CHADEMA, mfano wa habari ya leo iliyoandikwa kwenye gazeti la MTANZANIA chini ya BASHE..,"ETI KWAMBA MBOWE AMEZIMA UASI CHADEMA" hii kauli ni ya uchochezi dhidi ya CHADEMA..,

Wanaosema NASSARI ni msaliti, hawataishia tu hapo watasema vincet msaliti,Godbless lema msaliti, na mwisho hata Dk.Slaa msaliti..,

Kama Nassari angekuwa pandikizi..,Lazima angewezesha CCM ishinde uchaguzi wa Arumeru, kwani LOWASSA NA BEN MKAPA wasingekubali kudhalilika, na hata kukubali mamilioni waliotumia kuteketea bila kushinda..kwakuwa CCM wanajulikana kwa kulaziimisha matokeo na kuchakachua kura
 
Kwa kweli naanza kupata wasiwasi kuhusu kijana mzalendo mwana Demokrasia kwa kuanza anavyofanya katika uwanja wa Siasa hapa Tanzania,... ''Kuhusu kwamba Sehemu ya Kaskazini Ijitenge, Iwe Jamuhuri yake''. Inawezekana ni wazo au ni mojawapo ya sera Lakini SI WAKATI HUU kwa sasa, Kwani Chama Tawala kinaweza kutumia kama njia ya Kukiharibu Chadema kwa Wananchi ambao tayari walishaanza kuweka matumaini na Kumshukuru MUNGU kuwa wamepata Chama cha kuwakomboa na cha Chama cha kupeleka Sauti zao Bungeni na kwenye Serikali.

NAJIULIZA,..
1. Inawezekana huyu kijana Alisha kuwa SETUP (Kuwekwa Pandikizi) toka yupo Chuoni kama wengine walivyofanywa?
2. Au Ameshaongwa hela Ili aje Aharibu chadema?

Sielewi lakini naamini MUNGU Atasimama kwa Raia zake,....!

Sikia usiwe na hofu wala usi mm underestimate Dogo Janja kumbuka mweshimiwa mwenyewe mku wa anga alisema hiyo ilikuwa ni hamasa tuuu....... usijali hakitengwi kitu hapa...!
 
"Mimi ni mdogo,kama ninauwezo wa kuigawa nchi hii basi nchi hii haikupaswa kuwepo"

Nini tatizo la kauli hii, mbona kuna kauli mbaya kuliko hii zimewahi kutolewa tena na viongozi wakuu wa nchi? Zanzibar ni nchi, Kimbau (Mafia iwe nchi), Kigoma ijiunge na Burundi, Kanda ya kusini ijitenge nk nk. Binafsi nilisikitishwa sana na kauli zake za mwanzo alipomtisha rais asifike Arusha, zilinisikitisha lakini zinafundisha. Funzo ni kwamba wananchi wanataka maendeleo ni sawa na mtoto anaposema leo baba usiponiletea kitabu nakufungia mlango, kimatendo ni mbaya lakini kiuhalisia yuko sahihi.

Nassari ni Nassari kamwe hatuwezi kumbadilisha. Kwa akili yake alipoona kauli zake za mwanzo zimechukuliwa tofauti akadhani kujutia aliyoyasema ni kusema 'kwani mimi ni nani mbona ni mdogo sana?' Sisi tunaweza kumshangaa lakini bado na yeye atazidi kutushangaa, na tukiendelea kumshangaa tusione ajabu akaja na kauli itakayotushangaza zaidi.

Hakuna kauli inayokuja kwa bahati mbaya, kauli za bwana 'mdogo' si za bahati mbaya is a wakeup note kwa utawala wetu ujue kumbe kuna watu wanamawazo ya kujitenga. Kinachotakiwa kwa serikali ni kujiuliza tatizo ni nini, ni 'kitabu' watu wanataka maendeleo. Kama serikali ina mwona Nassari ni mwehu na inakimbizana naye inaweza kuaibika zaidi. Kumbuka amesema yeye 'mdogo' hana hata platoon wao wana kikosi cha jeshi, ni aibu iliyoje kwa mkuu wa nchi mwenye maximum security kuogopa kwenda Arusha eti ametishwa na matamko ya Nassari.

Zanzibar kuna kikundi kiitwacho 'UAMSHO' hiki si kikundi cha siasa, wao si tu wanatoa matamko kama alivyofanya Nassari bali wanafanya kwa vitendo. Hivi sasa kuna watu wanakusanya sahihi za kuuvunja muungano na rais anajua, nafikiri hilo ndilo serious zaidi. Tutakuwa wanafiki kumzuia mtu mmoja anayetoa kauli huku tukiacha kundi cha watu mia likiendelea. Narudia tena sikufurahishwa na kauli za Nassari hasa zile za kwanza lakini nafarijika zimetoa somo fulani kwa jamii na watawala.
 
Wewe ndio inaelekea unatumia makamasi katika kuchambua haya maswala, kwani wewe kwa upeo wako mfupi unafikiri siasa ya Tanzania ipo vipi yaani kwa mfano niki kuliza...?

Pro-Chadema JF wengi ni wachanga kwenye siasa hivi hunaweza kumpiga marufuku Rais wa Tanzania kwenda Arusha? Akili za kitoto kabisa hizi
 
Haya ni baadhi tu maneno machache ya Mbunge Joshua Nassary ktk mahojiano yake na polisi baada ya kujisalimisha.
Kasema hivi" Mimi sikuwa na nia mbaya juu ya kauli yangu bali ilikuwa ni kutoa hamasa ya mabadiliko kwa mikoa mingine iige Arusha,Mbeya,Musoma,Manyara, kwa mabadiliko walioonyesha pia Mimi ni mtu mdogo sana ktk nchi hii so sina mamlaka ya kumzuia Rais kuja Arusha wala sina uwezo wa kuigawanya nchi kwani kama ni kweli mm ninaweza kuigawanya nchi na kumzuia Rais basi HIYO ITAKUWA SIYO NCHI WALA HAIPASWI KUWEPO maana mi ni mtu mdogo sana"
Kweli huyu dogo anahitaji semina elekezi. Wewe tayari ni mbunge, maana yake wanachi wote katika jimbo lako wanawakilishwa na wewe. Ukisema wanaona Jimbo lako limesema. Sasa ukija na sababu za udogo wakati wewe ni mbunge naona kama hujui unachoongea. Nafikiri jifunze kujifunza kwanza, na kukaa kimya ni busara.
 
Leo baada ya mahojiano na polisi Arusha mjini zaidi ya masaa sita,Nassari akiongea na waandishi wa habari alisema "Mimi ni mdogo,kama ninauwezo wa kuigawa nchi hii basi nchi hii haikupaswa kuwepo"

Source;ITV News 2000hrs*
Mdogo ki umri au ki akili,kama ni yote mawili,nawahurumia wananchi wa Arumeru.
 
Mwanakijiji kidogo huwa tunakuheshimu lakini naona una mwelekeo wa kukuza hili jambo tena kwa tafsiri ya hatari kuliko hao mapolisi.Wewe mtu anayesema eti Rais ajaye hatatoka kaskazini ya Tanzania na kwamba jina lake analo JK, na kwa siku zote hizi Kurugenzi ya Mawasiliano ya Ikulu haijakanusha(ikiwa imejitahidi kukataa habari za JK kupewa hongo ya suti,kupikwa kwa hukumu ya kesi ya Lema na matukio mengine) unaelewa uzito wa maneno yake kwa sisi watanzania wa kaskazini au hata mtanzania asiye wa kaskazini mwenye akili kidogo?
Kwa kweli kama POLISI wameshapoteza RELEVANCE ushahidi upo Arusha.Mbeya jamaa walimrushia mawe JK kweupee mkasema ni walevi wale?Wale ni watu walioonesha kutokuridhishwa na mfumo na wanajua hata risasi za moto zingeliweza kuwapitia lakini wakajitolea.
Naomba usiwe mwoga kiasi hiki ndugu mwanakijiji tena muunge mkono NASSARI na wewe usimame uwe tayari kuhesabiwa,kwa risasi,virungu,tindikali,ama powder za Russia/Ukraine!
 
Inavyoonesha bado Nasari anasumbuliwa na bangi alizovuta sekondari.
 
Pro-Chadema JF wengi ni wachanga kwenye siasa hivi hunaweza kumpiga marufuku Rais wa Tanzania kwenda Arusha? Akili za kitoto kabisa hizi
Wewe unayeshangaa hayo ndiye mchanga kwenye siasa kuwa uyaone, kuna nchi zimewahi kujitenga kwa sababu ya serikali kutojali matatizo ya sehemu moja. Halafu mkuu uko addicted sana na 'H'.
 
I doubt the mental ability politically of Nassari on issues...
he talks cheaply & lightly ..... kuanzia sasa kumbe JJ Mnyika ni very matured, huyu kwa CDM wamchunge naona atachafua CDM kwa maneno....

You might be out of your senses 4sure kwani wewe una vipimo vya I.Q ya mtuu kwa kutumia your own selfishness point of view n thinking capacity ama ni vipi yaani? Dont ever under estimate a person kwa mtazamo wako duni wa siku moja2, keep in mind whenever your right no one remembers while when you wrong no one forgets.... dont act like a layman if u dont happen to be one....!
 
Msemo wa mgema akisifiwa TEMBO hulitia maji, dalili zaonyesha CDM wamelewa misifa HIVYO wamefikia kuongea pasipo tafiti wala busara. Imefikia hatua viongozi kutoa matamko tofauti wakiwa majukwaani. Moja kwa moja UONGOZI WA KITIMU NDANI HIKI CHAMA HAUPO.

Imethibitika katika mkutano wa UNGA LTD, mbunge Nasari katoa tamko la UBAGUZI na kuthibitika hiki chama ni cha Kanda ya Kaskazini tu, wengine ni abiria.

Watanzania tutumie vichwa vyetu tufikiri kwa makini, CDM ni kwa ajili wa KANDA MOJA!!!!

Kuna matukio mengi yanayoonyesha CDM hawana utashi wa kuongoza TZ, kwani walianza kutoutaka muungano, na sasa wanataka kujitenga. tuwahurumie ndugu zetu toka kanda ya Ziwa, Kusini Nyanda za Juu waliovutwa na upepo wa msimu wa CDM pasipo kujua undani wa wamiliki wa CDM; ambao ni Mbowe & Mtei Co.

Najua wafuasi wa CDM toka kanda husika mtasema sana kwa vile nimewagundua ujanja unaotumia kutaka kutugawa watanzania kwa misingi ya ukanda.

Kwa taarifa yako mimi mrdash1 nimezaliwa na kukulia kanda ya ziwa, kata yangu ya kiriba, musoma (V) imezungukwa na ziwa Victoria lakini hakuna hata kijiji kimoja chenye maji ya bomba, bado mama na dada zetu wanabeba ndoo za maji vichwani kutoka ziwani hadi majumani mwao, wanatembea km 0 - 5 kulingana na mahala makazi yao yalipo kutoka ufukwe wa ziwahalafu wewe lofa wa fikara ndo unataka kutuambia nini hapa?? Kwamba ccm ni ya kitaifa na inaliendeleza taifa???? kwa taarifa yako ccm ni kampuni ya mafisadi na wahujumu uchumi inayomiliki nguvu za dola
 
Wewe unayeshangaa hayo ndiye mchanga kwenye siasa kuwa uyaone, kuna nchi zimewahi kujitenga kwa sababu ya serikali kutojali matatizo ya sehemu moja. Halafu mkuu uko addicted sana na 'H'.

Kumbe ni kweli Chadema mnataka kujitenga...
 
Kumbe ni kweli Chadema mnataka kujitenga...

Tumia akili wewe, usiwe kama pimbi wa madoadoa wacha kuropoka kama umekalia *****. Wewe una uwakika gani na unayo yasema....?
 
Pro-Chadema JF wengi ni wachanga kwenye siasa hivi hunaweza kumpiga marufuku Rais wa Tanzania kwenda Arusha? Akili za kitoto kabisa hizi

Listen bwana being pro haijalishi unadhania utajifunzaje bila kukosea, isitoshe kuwa pro ama senior jf haitoshi kupima uchanga na uelewa wa mtuu. Mbona wazee wazima wa CCM hawana jipya mfano mtu kama Wasira na Chenge wao unavyo hisi hadi leo hii wamekomaaa kisiasa kweli.? Haimanishi unaweza kumpiga marufuku raisi kwenda arusha, besides mwenyekiti Mbowe alishawaeleza yakuwa ile ilikuwa ni hamasa ilio jaa shahuku2 ya kuonyesha kuchoshwa na ushenzi wa chama tawala CCM kinachongozwa na huyo aitwaye raisi wa Tanzania. Na jibu la swali lako nadhani nimekujibu....!
 
Ngoja niweke wazi kabisa; sina tatizo na kauli ya 'kujitenga'. Ni kauli ya kisiasa na imeshawahi kutolewa mara nyingi na watu wa Kigoma, watu wa Mtwara/Lindi, na hata watu wa Pemba.Binafsi hilo halinisumbui sana. Na mtu yeyote anajua aliitoa kauli hiyo kwa maana ya kuweka point ya utani ndio maana alisema "kama Sudan". Haina maana nzito ya kihivyo kwani na wengine wameshatoa kauli kama hizo.

Lakini huwezi kutoa kauli yenye kumtishia Rais na ukabakia hivihivi. Mtagundua kwamba kauli zenye kutishia maisha au usalama wa kiongozi yeyote wa umma huwa hatuzivumilii hapa kwa sababu moja kubwa - siyo watu wote wana akili zilizotulia na huwezi kujua nani akisikia anasukumwa vipi.

Nassari ni kiongozi maarufu sana sasa hivi na ameshinda kwa kishindo kikubwa sana. Kule Arusha ana mvuto mkubwa sana na ni mvuto wa watu kukesha na kumlinda hadi dakika ya mwisho. Chuki dhidi ya CCM ni chuki ya kweli (real hate) na siyo watu wote wanaweza kudumu kwenye chuki hiyo na wakiacha kwenye mambo ya kisiasa tu. Sasa, mbunge maarufu, tena kijana anaposimama na kusema anaweza kumpiga mkwara rais asikanyage Arusha siyo jambo dogo kwa sababu siyo wasikilizaji wake wote wanamuona 'mdogo hivyo'. Nassari ana ushawishi na anamvuto.

Labda watu wengi hawajui historia. Martin Luther King hakuwa na cheo chochote cha kisiasa zaidi ya kuwa mhamasishi mwanaharakati. Lakini mauaji yake yalisababisha miji ya Wamarekani kuingia katika machafuko makali sana. Ni kwa sababu watu walijua ameuawa na mikono ya watu wenye nguvu. Hata Nassari pamoja na "udogo" wake wote hakuna mtu Arusha atapenda anatendewa vibaya au kuonewa na wapo watu wanaoweza kufanya lolote kwa ajili ya utii wao. Nadhani watu wengi wameshasahu kuwa mauaji ya Arusha ya 2011 kwa kiasi kikubwa yalisababishwa na polisi kutumia nguvu dhidi ya watu ambao waliona wanaonewa.

Sasa mbunge anaposimama na kutoa kauli ambayo vyombo vya usalama vinaiona ni ya vitisho dhidi ya Rais ni kutokuwa makini kudhania tu ni jambo dogo. Alichotakiwa kusema Nassari ni hiyo kauli yake ya kwanza tu kuwa hakumaanisha ubaya wowote na kama mtu yeyote amekwazwa anaomba radhi. Lakini siyo kusema kuwa ati yeye ni mtu mdogo na asingeweza kugawa nchi; well hilil ni zaidi ya kugawa nchi. Hivi akisema kuwa Rais asikanyage na Kikwete akaamua kukanyaga na mwehu mmoja akaamua kufanya kitu kibaya kwa msafara wa rais watu watamlaumu mwehu kwa vile ni mwehu siyo? Lakini, yule mwehu ukimuuliza atasema "rais wetu" alitoa amri Kikwete asikanyage Arusha na akakanyaga!

Hii ni sababu moja ambayo inanifanya miye nisiwe shabiki sana ya hoja ya 'uongozi bora ni ujana' kwani tayari tumeshaona mengi yasiyo ya lazima ambayo vijana wameyafanya na kuthibitisha ukosefu mkubwa wa hekima na utulivu unaotokana na busara. Siyo lazima useme kila kinachoingia kichwani hata kama unaamini ni sahiihi. Kuna vingine unaweza kuvisema ila kwa namna tofauti. Hili huwezi kufundishwa shuleni au chuoni!

Ni matumaini yangu Polisi hawatoliendeleza hili na Nassari atakuwa amegundua (sidhani kwa sababu arrogance ya madaraka nayo nimbaya sana!) makosa yake. Sitaki ajisikie ameonewa bali ajue genuinely hakupaswa kutoa kauli hiyo na ni unfortunate. Kwa mfano Lema angekuwa makini na kauli zake wala asingevuliwa Ubunge! HEKIMA, HEKIMA, HEKIMA!!

Acha kujikomba kwa Mzee Mwanakiji amechemka sana. Sidhani kama ni yeye ama kaibiwa password.
Siungi na sikubaliani na kauli ya Dogo Janja, lakini pia sikubaliani na pumba alizoongea MMK. Suala la msingi ni kwamba ile kauli haikuwa kauli ya chama, ndiyo maana ilikanushwa pale pale uwanjani na Mbowe, na hili Mzee Mwanakijiji alijua mapema siku hiyo. Jambo alilotakiwa kulijadili Mzee Mwanakijiji kama nguli humu Jf ilitakiwa iwe ni nini kilisababisha Dogo Janja afikie hatua ya kutamka yale manen, nini kiliwaudhi au kilimuudhi. Hii ndiyo ilitakiwa iwe pakuanzia.
Tusiwe kama wapumbavu wanaopiga vita uvutaji wa sigara wakati huo huo wanasimamia uzalishaji wa sigara.
Hii kauli ya Kaskazini kujitenga mnaona kama kauli mbaya ya kibaguzi kuliko kauli ya uvccm mkoa wa pwani ambayo hadi leo hakuna kiongozi wa ccm aliyethubutu kanusha kwa kumwogopa Riz1! Shame on you guys!
Ni afadhali ya CHADEMA waliothubutu kukanusha kauli ya Dogo Janja pale pale.

Mkuu Mungii, wewe ni mojawapo ya watu ninao waheshimu sana katika jukaa hili ila unaanza kunipa wasiwasi.
1. Kwamba hukubaliana na kauli ya 'Dogo Janja' na pia "pumba" za MMK nikujikanganya maana hoja ya msingi ya Mzee Mwanakijiji inapinga kauli ambayo unasema hukubaliana nayo.

2. Hizi tabia za kutenganisha chama na viongozi wake ni tabia za CCM, " chama ni kizuri ila viongozi ndo wabovu" na si Chadema. NASARI NI KIONGOZI NA KIONGOZI NI TASWIRA. Anabeba sura ya taasisi/watu anaowaogoza na Nasari anapaswa kuwa hivyo. Kujaribu kumtenganisha Nasari na Chadema unakosea

3. Kinachobishaniwa hapa si sababu zilizomplekea Nasari kusema aliyo yasema. Kinacho jadiliwa/bishaniwa nikwamba Nasari alikosa hekima kueleza alichokikusudia. Moja ya Sifa kuu za kiongozi ni kuwa na hekima/busara. Kwa lugha nyepesi uwezo wa kutambua kitu gani unapaswa kufanya/kusemea na kwa wakati gani. Wakati huo uwe wa furaha au huzuni, sherehe au majonzi. Maranyingi uwezo wa kiongozi unajidhihilisha katika kutatua matatizo kwenye complex situations.

4. Ni utamaduni humu janvini kwa wanajanvi hukubaliana na kupongeza ama kupinga hoja za wenzao. Katika kuonyesha kuikubali hoja wengine hutumia "LIKE" na wengine hueleza hisia zao kwa kuandika na umekuwa ukifanya ama kufanyiwa hivyo karibia kila siko. Nadhani hauko sahihi kumbwambia mwenzio anajikomba kwa Mwanakijiji.

5. Hii tabia ya kulinganisha uovu kwa uovu sio nzuri na bora tukaizika.

6. Ninaanza kupata hisia kuwa baadhi ya vijana wa kasikazini wamenasa kwenye mtego wa CCM. Mtego wa kutumia ukanda/ukabila kuigawa CDM. Kuweni makini makini tena makini. Siku mkianza kujiona zaidi wanaarusha kuliko wanachadema, huo ndo utakuwa mwanzo wa kudidimia kwa harakati hizi ambazo sote ni wadau.


MKUU MUNGI MIMI NA WEWE TU WAPENZI WA CHADEMA LAKINI USIPENDE KUWA MPENZI KIPOFU
 
Suala la udogo na kugawa nchi haviingiliani kabisa!!! Hapa kikubwa ni nguvu ya ushawishi, kwani wakina Martin Luther walivokuwa wanafanya movement walikuwa watu wazima????

Nafikiri CDM ni kuwa makini na zaidi ni kumrudisha dogo Nasari jikoni apikwe upya kabla yakupewa mic na kuingia Majukwaani. Maana kunawatu wapo tayari na makini kunote makosa ili watokee humo. Nasari uwe makini na Kauli zako, wewe ni Mbunge ni Public figure maneno unayoyasema sisi tunayapa uzito!! Usijifanye hamnazo...
 
Amesema jambo ambalo kwa haraka linaonekana lina mantiki lakini linapuuzia uzito wa alichokisema. Kama ni mtu mdogo hivyo aligombea ubunge wa nini? Kama anakosa hekima ya kupima madhara ya maneno yake - watu wanaweza kuumia kwa kauli moja tu ya mtu mwenye ushawishi - kwa sababu yeye ni 'mtu mdogo' ananitisha. Yeye anaweza kuwa na umri mdogo lakini nguvu ya ushawishi wake inashinda baruti na siyo watu wote wanaomsikiiliza wanamchukulia kuwa ni mtu 'mdogo'. grrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrr

umeniwahi mzee mwanakijiji! .... nilitaka kuliongea hili ...
 
Back
Top Bottom