Joshua Nassari MB.

Joshua Nassari MB.

Kwa kweli naanza kupata wasiwasi kuhusu kijana mzalendo mwana Demokrasia kwa kuanza anavyofanya katika uwanja wa Siasa hapa Tanzania,... ''Kuhusu kwamba Sehemu ya Kaskazini Ijitenge, Iwe Jamuhuri yake''. Inawezekana ni wazo au ni mojawapo ya sera Lakini SI WAKATI HUU kwa sasa, Kwani Chama Tawala kinaweza kutumia kama njia ya Kukiharibu Chadema kwa Wananchi ambao tayari walishaanza kuweka matumaini na Kumshukuru MUNGU kuwa wamepata Chama cha kuwakomboa na cha Chama cha kupeleka Sauti zao Bungeni na kwenye Serikali.

NAJIULIZA,..
1. Inawezekana huyu kijana Alisha kuwa SETUP (Kuwekwa Pandikizi) toka yupo Chuoni kama wengine walivyofanywa?
2. Au Ameshaongwa hela Ili aje Aharibu chadema?

Sielewi lakini naamini MUNGU Atasimama kwa Raia zake,....!

Si kosa lako bali ni kosa la uwezo wako mdogo wa kufikiria uliosababishwa na utawala mbovu wa nchi yako
 
I doubt the mental ability politically of Nassari on issues...
he talks cheaply & lightly ..... kuanzia sasa kumbe JJ Mnyika ni very matured, huyu kwa CDM wamchunge naona atachafua CDM kwa maneno....
 
Kitu kinachoniacha hoi mimi ni kuwa kama kauli ya Mh. Nassari inaweza kugawa nchi basi tuna kila sababu ya kuamini kuwa tayari nchi ilishaanza kuelekea huko na Mh. Nassari anataka kumalizia tu. Nadhani pamoja na ukweli uliopo kuwa kauli ya Mh. Nassari ilikuwa na harufu ya uchochezi, kama ilivyonukuliwa kauli ya Dr. Slaa huko nyuma kuwa nchi haitatawalika, lakini kitu ambacho kitafanya nchi yetu kugawanyika au kutotawalika wala haitakuwa kauli za namna hiyo bali wizi na ufisadi unaoendeshwa na kuratibiwa na genge la wajanja ambao serikali inashindwa kuwachukulia hatua.

Kama waziri mkuu wa nchi hii alisema kuwa mafisadi wakichukuliwa hatua nchi itayumba, basi hiyo hali ya mafisadi kuogopwa ndiyo cha kuogopa zaidi kuliko kauli ya Nassari au ya Dr. Slaa. Watu wanao'capitalize' kauli ya Mh. Nassari wanataka kutufanya kuwa hatuna akili kiasi kuwa kinachosemwa na kila mwanasiasa kitakuwa hivyo eti tu kwa sababu wana ushawishi. Ukweli ni kuwa jambo ambalo wananchi watakubaliana nalo hasa baada ya kusemwa na mwanasiasa kitakuwa kile ambacho wao wanaliamini na wanalitaka. Wananchi siyo roboti ya kuendeshwa na wanasiasa kama watu wengine wanavyotaka kutuaminisha.

Nassari licha ya kuwa Mbunge tuelewe bado mchanga katika masuala ya kutoa matamko jukwaani ndio maana si kitu cha kawaida Mbowe kusimama mara na kusahihisha kauli hiyo pale pale mbele ya umma, maana hake Mbowe aliona akiacha hivyo hivyo ni tamko ambalo si la kawaida kutamkwa na mwanasiasa mwa manufaa ya nchi na kichama.

Nassari akiachwa hivyo hivyo na kuendelea na matamko kama hayo ni dhahiri wengi wetu tunaojenga utetezi tutajuta kutokuwa wa wazi. Hata maelezo ya polisi ni hisani na uungwana vinginevyo wangekuwa serious yangefika mbali.
 
Usiwe kama inzi kuzungukia uchafu all times, haya maneno yameshasikika kila kona na wahusika wanayafanyia kazi now we are in development feedback so shut..! Waliosema rais hatatoka kaskazini umewaambia nini..
 
jmushi1 Verbatim? Tangu lini tukaanza kudaiana ushahidi wa namna hiyo?Hebu tujadili hoja hapa.Kama Nassari alikuwa sahihi ni kwa nini Mbowe alimkanusha on the spot??
 
Last edited by a moderator:
Mbunge wa Arumeru Mashariki (Chadema), Joshua Nassari, jana alijisalimisha kwa Jeshi la Polisi akiwa na wakili wake Albert Msando, ambako alihojiwa kwa zaidi ya saa nne kuhusu tuhuma za kutoa maneno yanayodaiwa kuwa ya uchochezi.

Hata hivyo, baada ya mahojiano hayo majira ya jioni, Nassari alipata dhamana ya Polisi kwa kudhaminiwa na James Ole Millya, lakini anatakiwa kuripoti tena polisi leo.

KAULI YA WAKILI WAKE
Akizungumza na waandishi wa habari baada ya kutoka kufanya mahojiano na makachero wa Polisi, Wakili Msando, alisema kila kitu kilikwenda sawa na aliwashukuru polisi kwa kumpokea mteja wake kwa heshima zote.

Alisema katika mazungumzo, polisi walisema kosa analodaiwa kufanya Nassari linaangukia katika kifungu namba 63 cha Sheria ya Kanuni za Adhabu, cha kutoa kauli ambayo inaweza kuleta uchochezi dhidi ya Jamhuri.
Kwa mujibu wa kosa hilo, adhabu anayoweza kupewa mtu anayedaiwa kutoa maneno hayo ni faini ya Sh. 1,000 au kifungo cha miezi 12 au vyote kwa pamoja.
 
Hapana siyo CCM, yeye ni kielelezo tosha namna viongozi wa CDM walivyokosa BUSARA hivyo huwaza namna ya kutugawa watanzania kwa misingi ya ukanda
 
Chadema ni Chama kizuri sana, kina Muelekeo na Sera nzuri. Lakini ninapenda kuwashauri MUWE makini sana na UTEUZI wenu, Msikurupuke Tu kuchagua Wagombea katika nafasi za Uongozi kama wabunge na Madiwani na Hata kwenye Ngazi za Ndani za Chama, Kwani Vijana wengi wenye Tamaa na Wanaopenda UFISADI Walishakubali kununuliwa na kupandikizwa ndani ya Chadema ili Waje Waiharibu na Kuwachanganya Wananchi kuhusu Chadema.

TAFADHALI KUWENI MAKINI, TUMIENI HEKIMA na MUOMBE MUNGU SANA VIONGOZI WENYE DHAMANA NDANI YA CHADEMA MNAOTEUA VIONGOZI.

MUNGU IBARIKI TANZANIA.
 
huna lolote kwanza nasar keshatoa ufafanuz wa yale aliyotamka.Na ukae ukijua nasar kama nasar wala si chadema! So muiache chadema ifanye mambo yake.
 
Mini naamini ubovu wa kitu unatokana na viungio vyake. Gari bovu litakuwa na engine mbovu, bodi chakavu na kadhalika. Mh. Nassari ni aina ya viongozi wabovu wanaoweza kuamka na kuanzisha hoja ya kijinga kama kuitenga kaskazini na maeneo mengine. Mbowe alifanya vizuri sana kumuita Mh. kuwa anamawazo ya kitoto. Ila cha kushangaza hakuspecify ni lini Mh. atakuwa maana tayari yupo katika game.
 
kuhusuhu muungano waulize wazanzibar je anautaka au hawautaki,usinipe jibu.kuhusu ukanda Nasari alisema kuanzia Mwanza,Musoma,singida,babati mpaka arusha sasa niambie ukanda uko wapi hapo?mwanza ni kaskazini?au jingrafia inakupiga chenga?nipo bukoba kwa sasa alakini ukiongea kuhusu chadema watu wanaona kama vile chadema inawachelewesha,kwanini hawaendi huko kuvalishwa magwanda?magamba yamewachosha.unaumia sana kuona chadema wanavyopendwa,nabado mpaka mfe kabisa
 
Amesema jambo ambalo kwa haraka linaonekana lina mantiki lakini linapuuzia uzito wa alichokisema. Kama ni mtu mdogo hivyo aligombea ubunge wa nini? Kama anakosa hekima ya kupima madhara ya maneno yake - watu wanaweza kuumia kwa kauli moja tu ya mtu mwenye ushawishi - kwa sababu yeye ni 'mtu mdogo' ananitisha. Yeye anaweza kuwa na umri mdogo lakini nguvu ya ushawishi wake inashinda baruti na siyo watu wote wanaomsikiiliza wanamchukulia kuwa ni mtu 'mdogo'. grrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrr

mh nassari amefanya jambo jema kutumia kauli hiyo maana ukiingalia vizuri hii ni spiritual comment, “humble yourself under the mighty hands of God and at the right time he will lift you up in honor” (1Peter 5:6). ukijishusha MUNGU atakuinua ukijiinua MUNGU atakushusha(kama nebkadneza), nimeipenda sana kauli hii.
 
Hamasa za kisiasa hizo haswa pindi unaposhuhudia mauaji ya watu wasio hatia,unapoona haki za wananchi uliokuwa nao wengine wazazi wako wengine viongozi wako wakihangaikia ardhi ,ukiona umaskini ulikithiri na wa kutupwa kati ya wananchi unaowaoongoza huko jeshi la polisi likijifanya kufumba macho kwa wauaji tumeona hapo Arusha wale walioua wananchi tareke 5 hakuna kitu kimefanya ,Polisi wamechagiza wabunge wa chadema wacharangwe mapanga hawajachukua hatua yeyote,wameua bila ajizi wananchi kule songea,mbeya,mwanza,geita,nyamongo kweli roho inauma,hata mimi ningekuwa mwanasiasa ningesema vivyo
 
kwa hiyo mnaleta mauzi ili watu wakasirike waseme mbovu mkimbilie polisi. sasa tunabadilisha kibao mkituuzi tunawakong'oli na idadi ya wanachama 1000 kuhamia cdm.
 
Wewe kimeo kweli hivi aliloongea mheshimiwa ni dogo kiasi hivyo. Acha uppppp wako. CDM ni hatar kama ukoma
 
Dogo anatakiwa ajiepushe na siasa za Lema ha ha ha ha ha.
 
Kikwetu, Mafilili ni yale matapishi ya mlevi. Huyu mleta hoja mwenye jina hili nashawishika kuamini anaendana na jina lake.

Napita tu makamanda...
 
Back
Top Bottom