MwanakijijiKwa mfano Lema angekuwa makini na kauli zake wala asingevuliwa Ubunge! HEKIMA, HEKIMA, HEKIMA!!
Mwanakijiji
Sidhani kipimo unachotumia kuwapimia kina Nassari na Lema kiko sahihi, ukizipima kauli za Lema na Nassari kwa kutumia kipimo cha CCM definitely hazitakuwa njema. Leo hii Slaa amefunguliwa kesi zaidi ya kumi na bado tunasikia anatafutwa na polisi sidhani kama naye hayuko makini. Ndiyo maana nasema kwa kipimo chako wapinzani karibu wote hawatakuwa na Hekima. Hadi sasa karibu wabunge wote wa upinzani (CDM) wana kesi mahakamani siyo kwamba hawana hekima.
Kauli ya Nassari ni sahihi kabisa, kama polisi na serikali nzima inapoteza muda kuhangaika na mtu mmoja 'mdogo' kama Nassari basi itakapovamiwa na Al shaabab itabidi tuombe polisi wa ziada kutoka Kenya. Nassari anakuwa victim si kwa kauli zake bali kwa upande aliko na msimamo wa chama chake.
Si serikali wala polisi inaweza kushinda iwapo itashindana na mtu mmoja mmoja, inatakiwa ijikite kurekebisha mfumo mzima wa utendaji kazi (double standard) na mambo mengine, ijiulize kwa nini mtu 'mdogo' kama huyu amtishie rais wa nchi asikanyage sehemu moja ya nchi yake, what is wrong? Lakini ikiendelea kukimbizana na kina Lema kamwe haitashinda. Tumeona na wewe umeona, walifikiri wakimvua Lema ubunge watapumzika na Arusha itatawalika, katokea Nassari, hata wakimdhibiti Nassari lazima atatokea mwingine.
Inchi kama inchi inagawanywa na nani? Or nini? Namuunga mkono mangi marialle aliyetaka kuwe na nchi ya kaskazini. Ukweli ingawa mchungu niambie tafadhali usinifiche! Nakiri hapa na nasema wazi wazi kwamba sisi watu wa kaskazini tunacheleweshwa kimaendeleo kutokana na kuongozwa na viongozi vilaza wanaoegemea udini bila elimu. Ukihoji wanakujibu hawawezi chagua ama kutawaliwa na mchagga! Kama mchagga hawezi chaguliwa kuwa rais wa inchi ili kuharakisha maendeleo kutokana na itikadi za ukanda ukabila na udini? Haina budi kaskazini kujigawa na kujitawala wenyewe na kuiacha hilo eneo lililobakia la kati na kusini kuendelea kuongozwa na vilaza wenye misimamo ya kidini. Nasema kama kweli tunataka inchi yetu iendelee kuwa moja basi tuwe na misimamo katika katiba kwamba rais anaweza toka popote pale katika nchi na sio kusema eti mchaga hawezi kuwa rais, kwani mchaga sio mtanzania? Katiba yasemaje kuhusu haya? Je mchaga ana kasoro gani? Piga uwa kwa misingi na misimamo hii ya chama cha magamba, haina budi kaskazini tujigaweni tuwe nchi kama sudani kusini.
wote wanaotetea ujinga kumtetea nasary kuona alichokisema ni sawa,ni wajinga wa fikra na wamezidi kushikiwa akili na wanasiasa ni kweli tunaitaji mabadiliko tuwe wakweli na tutende haki kwa maslahi ya nchi hii,sio kulinganisha ujinga aliofanza lusinde,hata tukimtathimin lusinde alishambulia mtu binafsi xio kutugawa
Ndugu yangu, mimi siwezi kusema lolote kuhusu uwezo au ujinga wako kiakili hasa kwa vile umehitimisha kuwa watu wasiokubaliana nawe kuhusu jambo hili ni wajinga; hata hivyo ninaona wazi kuwa swala hili unaliangalia kwa kiwango cha mtu mwenye akili finyu sana, na nadhani ndiyo maana unaona kuwa polisi kumtisha Nasari ni sawa kabisa badala ya kutafakari kwa kina uhalali wa kufanya hivyo na standard inayotumiwa na polisi. Kwa bahati mbaya inaonekana watu wa akili ya aina yako ni wengi sana miongoni mwetu, na ndiyo maana polisi watakuwa wanatuonea kila siku. Fahamu kuwa, hata kama maneno aliyosema Nassari wakati wa kampeini hayakuwa mazuri, bado haya-warrant hatua aliyochukuliwa na polisi leo. Kuna sababu kadhaa kuonyesha kwa nini polisi hawakumtendea haki Nassari leo hata kama kweli alisema maneno yale. Kama wanadhani maneno hayo yalivuruga uchaguzi, kuna njia za kufanya bila kumtisha. Bila kuwa na proof kuwa maneno hayo yaliathiri matokeo ya Uchaguzi, hawana sababu ya kudai uchochezi kwa vile walishachelewa kumshika na imeshonekana kuwa hakuchochea fujo zozote; na kama wanadai ni uhaini, watakuwa pia wameshachelewa sana kumkamata kwani sasa hivi hakuna ushaidi wowote wa kama kweli Nassari alikuwa anataka kufanya uhaini. Iwapo wangemkamata on the spot wangekuwa na kisingizio kuwa walikuwa wanazuia asifanye uchochezi kwani wajibu wa kwanza wa polisi ni kuzuia uvunjaji wa sheria, siyo kuvizia watu wavunje sheria ili wakamatwe. Na hata hivyo, kabla ya kumkamata walitakiwa kwanza wampe onyo kuwa maneno yake yalikuwa yanatishia amani na kumtaka aachane naye, iwapo asingesikiliza ndipo wangemkamata.
Inchi kama inchi inagawanywa na nani? Or nini? Namuunga mkono mangi marialle aliyetaka kuwe na nchi ya kaskazini. Ukweli ingawa mchungu niambie tafadhali usinifiche! Nakiri hapa na nasema wazi wazi kwamba sisi watu wa kaskazini tunacheleweshwa kimaendeleo kutokana na kuongozwa na viongozi vilaza wanaoegemea udini bila elimu. Ukihoji wanakujibu hawawezi chagua ama kutawaliwa na mchagga! Kama mchagga hawezi chaguliwa kuwa rais wa inchi ili kuharakisha maendeleo kutokana na itikadi za ukanda ukabila na udini? Haina budi kaskazini kujigawa na kujitawala wenyewe na kuiacha hilo eneo lililobakia la kati na kusini kuendelea kuongozwa na vilaza wenye misimamo ya kidini. Nasema kama kweli tunataka inchi yetu iendelee kuwa moja basi tuwe na misimamo katika katiba kwamba rais anaweza toka popote pale katika nchi na sio kusema eti mchaga hawezi kuwa rais, kwani mchaga sio mtanzania? Katiba yasemaje kuhusu haya? Je mchaga ana kasoro gani? Piga uwa kwa misingi na misimamo hii ya chama cha magamba, haina budi kaskazini tujigaweni tuwe nchi kama sudani kusini.
wote wanaotetea ujinga kumtetea nasary kuona alichokisema ni sawa,ni wajinga wa fikra na wamezidi kushikiwa akili na wanasiasa ni kweli tunaitaji mabadiliko tuwe wakweli na tutende haki kwa maslahi ya nchi hii,sio kulinganisha ujinga aliofanza lusinde,hata tukimtathimin lusinde alishambulia mtu binafsi xio kutugawa
Kuna watu humu ni vinara wa ushabiki hadi unawafanya kuwa vipofu wa kuuona Ukweli. Kama wewe unadhani hoja ya Mzee Mwanakijiji si kwa maslahi ya nchi hii basi jijue kwamba uwezo wako wa kufikiri uko chini sana. Hebu fikiria kidogo, CHADEMA imeshika nchi kwa kupata kura nyingi sana mikoa ya Pwani, kusini, nyanda za Juu kusini, Arusha na Kilimanjaro kwenye uchaguzi wa mwaka 2015.
Itokee Mikoa ya Kanda ya ziwa imeshikiliwa na CCM na mmoja wa wabunge wa CCM anasema "nitaigawa mikoa hii na tuwe na Rais wetu na serikali yetu". Unatarajia Rais aliyeko madarakani wa CHADEMA atafanya nini? Acheni ushabiki usio na tija.
Mwanakijiji ameongea vema kuhusu kauli za baadhi ya viongozi wa Chadema akitolea mfano wa Lema kupoteza ubunge ni sababu ya kauli si vitendo. Hali kadhalika Slaa baadhi ya kesi ni lugha si vitendo. Kinachomsumbua leo Nasari ni lugha si vitendo. Nimeongea hili jana hapa jf lakini mdau mmoja alivyoniporomoshea matusi namsamehe kwa kuwa hajui kuwa najua hajui alitetealo.
Elimu ya usemaji ni muhimu sana katika majukwaa, si kupanda na kuropoka kikutokacho kichwani, licha ya kujiandaa namna gani uwepo jukwaani kama alivyotokea mbunge wa Tabora wakati wa Kampeni Igunga kupanda jukwaani na trigger. Profesa moja alituambia chuoni, kama huweze kuwa msetirivu katika mada yako na kushtukia unayumba kutoka nje ya mada jitahidi kuandika na uyasome uliyoyaandaa hadi utakakuwa mzoefu wa kudadafula dhamira inayokusudia bila kutoka nje ya dhamira.
Ni nadharia ya kawaida upandapo jukwaani utakuwa umejiandaa vya kutosha nini utaenda kuongea hadharani. Ni bora uandike na uanze kusoma tangu mwanzo mpaka mwishi kama unaona unashindwa kuzuia ulimi wako kuropoka kila kikutokacho kwani uliyojiandaa huwa umeshayachuja yapi yanafaa kwa watu utakaokutana nao badala ya kuongea tu kukujiacho uwapo jukwaani ndio matokeo yake mbunge anafikia hatua ya kumwekea mipaka Rais wa nchi asigusi ndani ya mipaka ya jimbo au ukanda wake, ni kitu kisichoingia akilini mwa wengi wenye upeo wa kuelewa nini dhamana ya viogozi wetu watarajiwa.
Uongozi bora haupimwi kwa usemaji mwingi jukwaani, bali busara hekima na maoni ya umoja kitaifa ndiyo kigezo cha kujenga nchi kwa amani na utulivu. Siasa inaweza kukugeukia upande mbaya mara moja kutokana na kosa moja tu hata kama umefanya mengi mazuri.
Kesi karibu zote zilizopo mahamakani ni za maneno ya uchochezi, hilo ni jambo ambalo Viongozi wa Chadema wanapaswa kuwa waangalifu sana. Viongozi wa Chadema wasidanganywe na uwingi wa watu kuona kwamba ndio kigezo cha kuongea watakavyo bila kupima nini kinatakiwa kuongelewa katika nafasi walizo nazo mikutanoni na kuonyesha umahiri wao wa kisiasa. Mvuto wa kisiasa ni uwezo wa kujenga hoja nzuri na kuzitetea na wala si kutukana au kusema kauli za kuashiria uchochezi.
MMMAmesema jambo ambalo kwa haraka linaonekana lina mantiki lakini linapuuzia uzito wa alichokisema. Kama ni mtu mdogo hivyo aligombea ubunge wa nini? Kama anakosa hekima ya kupima madhara ya maneno yake - watu wanaweza kuumia kwa kauli moja tu ya mtu mwenye ushawishi - kwa sababu yeye ni 'mtu mdogo' ananitisha. Yeye anaweza kuwa na umri mdogo lakini nguvu ya ushawishi wake inashinda baruti na siyo watu wote wanaomsikiiliza wanamchukulia kuwa ni mtu 'mdogo'. grrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrr
Tusiwe na mapenzi kwa chama kiasi kwamba tunatafuta udhuru wa tabia mbovu. Kuna mambo ambayo sasa CDM inapaswa ikemewe na wale wanaoipenda pasi ya kusita. Mambo mengine yakiachwa yaendelee yana matokeo mabovu huko mbeleni.
Kuna watu humu ni vinara wa ushabiki hadi unawafanya kuwa vipofu wa kuuona Ukweli. Kama wewe unadhani hoja ya Mzee Mwanakijiji si kwa maslahi ya nchi hii basi jijue kwamba uwezo wako wa kufikiri uko chini sana. Hebu fikiria kidogo, CHADEMA imeshika nchi kwa kupata kura nyingi sana mikoa ya Pwani, kusini, nyanda za Juu kusini, Arusha na Kilimanjaro kwenye uchaguzi wa mwaka 2015.
Itokee Mikoa ya Kanda ya ziwa imeshikiliwa na CCM na mmoja wa wabunge wa CCM anasema "nitaigawa mikoa hii na tuwe na Rais wetu na serikali yetu". Unatarajia Rais aliyeko madarakani wa CHADEMA atafanya nini? Acheni ushabiki usio na tija.