Huyu Slaa alipokuwa Mayor wa jiji la Dar es Salaam, alipingana sana na Magufuli. Wakati magufuli akiwa waziri wa ujenzi walikuwa wanabishana kuhusu kung'oa mabango ya biashara kutoka barabara za Tanroad. Alimshutumu magufuli kwamba anaendesha wizara kwa mihemko na hafuati sheria.
Sasa Leo tena Slaa naye kawa Magufuli?
Tuendelee kumsikiliza
 
Promota wa Tamasha la Pasaka, Mtangazaji wa vipindi vya kwaya na Mgombea wa nafasi mbalimbali za uongozi huko CCM, Bwana Alex Msama ametajwa kuwemo kwenye 3 bora ya Matapeli Papa wa Viwanja DSM.

Taarifa kamili hii hapa

====



Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Jerry Silaa amemtaka Mkurugenzi wa Msama Promotions, Alex Msama kujisalimisha kwa Kamishna wa Ardhi Msaidizi mkoa wa Dar es salaam akiwa na baadhi ya watu waliouziwa eneo la viwanja namba 1 kitalu 22 lililopo Kibada Manispaa ya Kigamboni jijini Dar es salaam ili kurejesha kwa wananchi eneo hilo lijengwa shule ya sekondari.

Silaa ametoa maagizo hayo alipofanya ziara katika eneo hilo Manispaa ya Kigamboni baada ya mgogoro huo kuwa wa muda mrefu kati ya wananchi wa eneo hilo na baadhi ya watu walionunua eneo la shule akiwemo Allex Msama.

Aidha, Waziri Silaa amemtaja Alex Msama kuwa ni tapeli namba 3 wa viwanja jijini Dar es salaam na tayari ameishaagiza baadhi ya maeneo anayoyamiliki kinyemela kunyang’anywa ikiwemo eneo la wazi na eneo la fukwe lililopo Mbweni Manispaa ya Kinondoni jijini Dar es salaam.

Mwanahalisi Digital
Wakimalizana nae kwenye ardhi wamkabe kwenye ishu ya kumdhulumu Rose Mhando
 
Kupishana kupo katika utendaji, mbona huyo huyo Magufuli hakung'oa mabango alipoingia madarakani??? Hapa narudi kwenye uhalali wa kauli yako

Ila all in all, Magufuli alimpigia kampeni katika chaguzi zotebili na alimtaja kwa majina kuhusiana na utendaji wake

Rejea hotuba zake wakati anatambulisha mbunge mmoja mmoja katika kampeni za 2015& 2020
Huyu Slaa alipokuwa Mayor wa jiji la Dar es Salaam, alipingana sana na Magufuli. Wakati magufuli akiwa waziri wa ujenzi walikuwa wanabishana kuhusu kung'oa mabango ya biashara kutoka barabara za Tanroad. Alimshutumu magufuli kwamba anaendesha wizara kwa mihemko na hafuati sheria.
Sasa Leo tena Slaa naye kawa Magufuli?
 
Mkimalizana nae kstika hili Mamlaka nyingine imkamate kwa Kosa la Kudhulumu Mishahara na Stahiki za Wafanyakazi ( Waandishi wa Habari ) wa iliyokuwa Media ( hasa Gazeti ) akiongozwa na Marehemu Dada Yamola.
'
 
Msichokifahamu ni kwamba waziri SLAA ni MAGUFULI namba mbili, anapita kwenye njia ambayo viongozi wengi hawawezi kupita
Mlinganisho uliofanya hauwezi kuwa sahihi katika mambo mengi. Lakini ninakubaliana nawe kinamna fulani, na inanifanya nianze kumtizama kwa jicho la kipekee zaidi kwa maana anajipambanua na makondoo wengi tunaowaona katika baraza lile la mawaziri. Hatari inayomkabili ni kuwa anafanya kazi katika mazingira magumu zaidi, huku anaowafanyia kazi (wateuzi wake) wakiwa upande tofauti na alipo yeye.
Kwa hiyo itabidi achunge sana namba, asije akajikuta anagusa waya inayounga moja kwa moja na maslahi ya wakubwa wake.
 
Mjinga wewe kinacho takuwa ni kuweka mifumo dhabiti sana ya uwajbikaj, swala sio kuwapata mawaziri watatu kama Slaaa, hizi ni hadaaa za kuwahadaa wapumbavu type yako.
Huo mfumo wako dhabiti upo wapi sasa, mjinga ni yule anayekurupuka kujibu bila kuelewa btn the lines.... Sisi tunasema tunataka utendaji ndio wenye matokeo kwa hali uliyonayo sasa wewe unaleta ujinga wako wa mfumo ambao umeshindwa hata kushauri unataka uweje huo mfumo wako
 
Waziri wa Ardhi Mheshimiwa Jerry Slaa amemtaja Alex Msama wa Msama Promotions kwamba ni mojawapo ya matapeli wakubwa 7 wa viwanja mkoa wa Dar es Salaam aliowahi kutamka kwamba atawashug
hulikia.

Msama amekua akitapeli watu viwanja, kuuza viwanja vya wazi, kuuza viwanja vya wajane, kutumia majina ya viongozi waliostaafu kutapeli viwanja na kujifanya mtoto wa mjini.

Msama amekua akiandaa matamasha ya kusifia viongozi kila mwaka kumbe ni coverup tu ya matukio yake ya utapeli wa viwanja.

View attachment 2946528
Apigwe huyu Mutu tapeli anayependa vya bure))
 
Back
Top Bottom